Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Endelea Kubakia mu Tengenezo ya Yehova
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
    • 8 Pia, Yakobo anaonyesha mu barua yake kama ni lazima sana kuwa na uvumilivu. Aliandika hivi: “Muone yote kuwa furaha, ndugu zangu, wakati munapata majaribu mbalimbali, mukijua kama sifa yenye imejaribiwa ya imani yenu inatokeza uvumilivu. Lakini muache uvumilivu ukamilishe kazi yake, ili mukuwe kamili na bila kosa katika mambo yote, bila kukosa kitu chochote.” (Yak. 1:2-4) Yakobo anasema kama Wakristo wanapaswa kukubali majaribu na kuiona kuwa furaha juu inawasaidia kuonyesha sifa ya uvumilivu. Ulishakafikiri vile? Kisha, Yakobo alionyesha kama uvumilivu uko na kazi fulani ya kufanya, ni kusema, unatusaidia tukuwe na sifa za muzuri za Kikristo na unafanya tukubaliwe na Mungu. Ndiyo, kadiri tunaendelea kupambana na majaribu kila siku na kuishinda, ni vile tunaendelea kuwa wavumilivu zaidi. Uvumilivu unatusaidia pia kuwa na sifa zingine za muzuri zenye tuko nazo lazima.

  • Endelea Kubakia mu Tengenezo ya Yehova
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
    • 10 Kama tunapenda kuendelea kuwa wavumilivu mu hii wakati ya hatari, tunapaswa kuepuka kuwa na mawazo yenye haifae juu ya mateso yenye tunapata tukiwa Wakristo. Kumbuka, Yakobo aliandika hivi: “Muone yote kuwa furaha.” Haiko mwepesi kuwa na furaha vile, juu majaribu inaweza kufanya mutu ateseke kimwili ao kiakili. Lakini, usisahau kama ni uzima wako wa wakati wenye kuya njo uko mu hatari. Mufano wa mitume unatusaidia tuelewe muzuri namna ya kuwa na furaha wakati tunapata mateso. Ile habari inapatikana mu kitabu ya Matendo, na inasema hivi: “Wakaita mitume, wakawapiga viboko, na kuwaagiza waache kusema katika jina la Yesu, kisha wakawaacha waende. Basi wakatoka mbele ya Sanhedrini, wakiwa na furaha kwa sababu walikuwa wamehesabiwa kuwa wanastahili kuvunjiwa heshima kwa ajili ya jina lake.” (Mdo. 5:40, 41) Mitume walielewa kama ile mateso ilihakikisha kama walitii amri ya Yesu, na kama Yehova alikuwa amewakubali. Kisha miaka fulani, wakati roho ya Mungu ilisaidia mutume Petro kuandika barua yake ya kwanza, alizungumuzia faida ya kuteseka vile juu ya haki.​—1 Pe. 4:12-16.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine