Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Wachungaji, Muige Wachungaji Wakubwa Zaidi
    Munara wa Mulinzi—2013 | Mwezi wa 11 15
    • 4. Habari hii itajibu ulizo gani?

      4 Kwa hiyo basi, namna gani wachungaji Wakristo wanapaswa kutendea kondoo? Washiriki wa kutaniko wanaombwa ‘kutii wale wanaowaongoza.’ Kwa upande mwingine, wazee wanashauriwa kwamba waepuke ‘kupiga ubwana juu ya wale ambao ni uriti wa Mungu.’ (Ebr. 13:17; soma 1 Petro 5:2, 3.) Namna gani basi, wazee wanaweza kuongoza bila kupiga ubwana juu ya kutaniko, ao namna gani wanaweza kuepuka kutumia vibaya mamlaka ambayo Mungu amewatolea wanaposhugulikia kondoo?

  • Wachungaji, Muige Wachungaji Wakubwa Zaidi
    Munara wa Mulinzi—2013 | Mwezi wa 11 15
    • 9. Yesu aliomba wanafunzi waepuke muelekeo gani?

      9 Maoni ya Yesu kuhusu daraka la kuwa muchungaji yalitofautiana na yale ambayo Yakobo na Yohana walikuwa nayo. Mitume hao wawili walitafuta vyeo vya juu katika Ufalme wa Mungu. Lakini Yesu alisahihisha maoni yao, aliposema hivi: ‘Munajua kwamba watawala wa mataifa wanatawala watu wao kwa nguvu na wakubwa wao wanamiliki watu wao. Lakini kwenu isiwe hivyo, ila yeyote anayetaka kuwa mukubwa kati yenu sharti awe mutumishi wa wote.’ (Mt. 20:25, 26, Habari Njema Kwa Watu Wote) Mitume walipaswa kuepuka muelekeo wa kutaka “kupiga ubwana” juu ya ndugu zao, ao ‘kuwatawala kwa nguvu.’

      10. Yesu anapenda wazee watendee kundi namna gani, na ni mufano gani ambao mutume Paulo aliwaachia wazee?

      10 Yesu anatazamia wazee watendee kundi namna yeye mwenyewe alivyolitendea. Wanapaswa kuwa tayari kutumikia ndugu na dada zao, wala si kuwatawala. Mutume Paulo alikuwa munyenyekevu, kwa kuwa aliwaambia hivi wanaume wazee wa kutaniko la Efeso: ‘Ninyi munajua vema jinsi tangu siku ya kwanza niliyokanyaga wilaya ya Asia nilivyokuwa pamoja nanyi wakati wote, nikimutumikia Bwana nikiwa na unyenyekevu mukubwa zaidi wa akili.’ Mutume Paulo alipenda wazee hao wawe wanyenyekevu na watumike kwa bidii ili kuwasaidia wengine katika kutaniko. Alisema hivi: ‘Nimewaonyesha ninyi wazi katika mambo yote kwamba kwa kufanya kazi kwa bidii hivyo ni lazima muwasaidie wale walio zaifu.’ (Mdo. 20:18, 19, 35) Mutume Paulo aliwaambia Wakorintho kwamba yeye hakuwa bwana juu ya imani yao. Lakini, alikuwa mufanyakazi munyenyekevu kama wao, na alitaka kuwasaidia wamutumikie Yehova kwa furaha. (2 Kor. 1:24) Mutume Paulo aliwaachia wazee wa leo mufano muzuri wa unyenyekevu na wa kutumika kwa bidii.

  • Wachungaji, Muige Wachungaji Wakubwa Zaidi
    Munara wa Mulinzi—2013 | Mwezi wa 11 15
    • “VIELELEZO KWA KUNDI”

      Wazee wanasaidia familia zao kujitayarisha kwa ajili ya mahubiri (Ona fungu la 13)

      13, 14. Wazee wanapaswa kuwa mifano kwa kundi katika mambo gani?

      13 Kisha kuwashauria wanaume wazee katika kutaniko ‘wasipige ubwana juu ya wale waliokabiziwa,’ Mutume Petro aliwatia moyo ‘wawe vielelezo [mifano] kwa kundi.’ (1 Pet. 5:3) Namna gani muzee anaweza kuwa kielelezo ao mufano kwa kundi? Tufikirie sifa mbili ambazo yule ‘anayejitahidi kufikia cheo cha [daraka la] mwangalizi’ anapaswa kuonyesha. Anapaswa kuwa mwenye “utimamu wa akili” na “mwanamume anayeisimamia nyumba yake mwenyewe kwa njia nzuri.” Ikiwa muzee ana familia, anapaswa kuisimamia vizuri, kwa kuwa, ‘ikiwa mutu yeyote hajue jinsi ya kusimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje kutaniko la Mungu?’ (1 Tim. 3:1, 2, 4, 5) Ili kustahili kuwa mwangalizi, mutu anapaswa kuwa na akili timamu ao akili nzuri, ni kusema, anapaswa kuelewa vizuri kanuni za Mungu na kujua namna ya kuzitumia katika maisha yake mwenyewe. Hilo litamusaidia awe mutulivu na asiyeamua mambo haraka​-haraka. Wazee wanapoonyesha sifa hizo, ndugu na dada katika kutaniko wanawatumainia.

      14 Wazee wanaonyesha mufano muzuri pia wanapokuwa kwenye mustari wa mbele katika kazi ya kuhubiri. Kuhusiana na hilo, Yesu aliwaachia wazee mufano. Kuhubiri habari njema ya Ufalme kulikuwa sehemu ya maana sana ya utendaji wa Yesu duniani. Alionyesha wanafunzi wake namna kazi hiyo inapaswa kufanywa. (Mk. 1:38; Lu. 8:1) Katika siku zetu, ni jambo lenye kutia-moyo kuona ndugu na dada wakihubiri pamoja na wazee, kuona bidii ya wazee katika kazi hiyo inayookoa maisha ya watu, na kujifunza kutokana na njia zao mbalimbali za kufundisha! Wazee wanapotumia wakati wao ili kuhubiri habari njema kwa bidii ijapokuwa wana programe yenye kujaa mambo mengi, hilo linatia moyo kutaniko nzima kuhubiri kwa bidii. Wazee wanaweza pia kutolea ndugu na dada mufano muzuri kwa kutayarisha mikutano na kutoa majibu na kwa kushiriki katika mambo mengine kama vile kufanya usafi na kutunza Jumba la Ufalme.​—Efe. 5:15, 16; soma Waebrania 13:7.

      Wazee wanapaswa kuwa mifano katika mahubiri (Ona fungu la 14)

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine