Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w14 1/5 uku. 16
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ni nani atakayemaliza magumu ya watu?
  • Juu ya Nini Mungu Anaacha Mambo ya Mubaya na Mateso Iendelee?
    Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
  • Kwa Nini Mungu Anaruhusu Uovu na Kuteseka?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Ni Nani Mwenye Anatawala Dunia?
    Ni Nani Mwenye Anatawala Dunia?
  • Juu ya Nini Kuko Mateso Mingi Sana?
    Biblia Inatufundisha Nini?
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 1/5 uku. 16

MAULIZO JUU YA HABARI ZA BIBLIA YANAJIBIWA

Kwa kweli, ni nani mwenye kuitawala dunia hii?

Picha ya vita, uuaji, jeuri, na misiba ya asili

Ikiwa Mungu ndiye mwenye kutawala dunia, sababu gani inajaa mateso?

Watu wengi wanaamini kwamba Mungu wa kweli ndiye mutawala wa dunia hii. Lakini ingekuwa hivyo, je, dunia ingejaa mateso? (Kumbukumbu la Torati 32:4, 5) Kulingana na Biblia, dunia inatawaliwa na mutu fulani muovu.—Soma 1 Yohana 5:19.

Namna gani mutu muovu alifikia kuwa mutawala wa wanadamu? Kwenye mwanzo wa historia ya wanadamu, malaika mumoja alimuasi Mungu na akamuchochea mwanaume na mwanamuke wa kwanza wamuasi pia Mungu. (Mwanzo 3:1-6) Mwanaume na mwanamuke huyo walichagua kumutii malaika huyo muasi, Shetani, na kumufanya kuwa mutawala wao. Mungu Mweza-Yote ndiye peke yake Mutawala anayefaa, lakini anataka watu wachague utawala wake kwa sababu wanamupenda. (Kumbukumbu la Torati 6:6; 30:16, 19) Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, watu wengi wamedanganywa na wamechagua vibaya kama mwanaume na mwanamuke wa kwanza.—Soma Ufunuo 12:9.

Ni nani atakayemaliza magumu ya watu?

Je, Mungu atamuacha Shetani aendelee na utawala wake muovu? Hapana! Mungu atamutumia Yesu ili kuondoa uovu wote ambao Shetani ametokeza.—Soma 1 Yohana 3:8.

Kwa nguvu za Mungu, Yesu atamuharibu Shetani. (Waroma 16:20) Kisha, Mungu atatawala wanadamu na kuwarudishia maisha ya furaha na amani yenye alikusudia wawe nayo tangu mwanzoni.—Soma Ufunuo 21:3-5.

Ili kupata habari zingine, soma sura ya 3 ya kitabu hiki, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

Unaweza pia kupata kitabu hiki kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine