-
Namna Gayo Alisaidia Ndugu ZakeMunara wa Mulinzi (Gazeti la Funzo)—2017 | Mwezi wa 5
-
-
Pengine wageni hao walikuwa wamisionere, watu wenye Yohana alituma, ao waangalizi wenye kusafiri. Iwe ni hivyo ao hapana, walisafiri kwa ajili ya habari njema. Yohana alisema hivi: “Kwa maana wao walisafiri kwa ajili ya jina lake.” (3 Yohana 7) Yohana alikuwa amezungumuzia Mungu (ona mustari wa 6), kwa hiyo maneno “kwa ajili ya jina lake” yanaonekana kuwa yanazungumuzia jina la Yehova. Kwa hiyo, ndugu walikuwa sehemu ya kutaniko la Kikristo na walipaswa kukaribishwa kwa furaha. Ndiyo sababu Yohana aliandika hivi: “Sisi tuna wajibu wa kuwakaribisha watu wa namna hiyo, ili tuwe wafanyakazi wenzi katika kweli.”—3 Yohana 8.
-
-
Namna Gayo Alisaidia Ndugu ZakeMunara wa Mulinzi (Gazeti la Funzo)—2017 | Mwezi wa 5
-
-
Kwanza, kwa kiasi fulani, wengi kati yetu tulijifunza kweli kupitia Wakristo waaminifu wenye walikuwa tayari kusafiri ili kutujulisha kweli hiyo. Kwa kweli, haiko Wakristo wote wa kutaniko la Kikristo leo ndio wanafanya safari ya mbali sana kwa sababu ya habari njema. Hata hivyo, kama vile Gayo, katika njia fulani tunaweza kutegemeza na kutia moyo wale wenye kusafiri, kama vile mwangalizi wa muzunguko na bibi yake. Ao tunaweza kuwa na uwezo wa kutoa musaada wenye kufaa kwa ndugu na dada wenye wamehamia katika maeneo mengine katika inchi yao, ao katika inchi ingine, ili kutumikia mahali kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri. Kwa hiyo, tuendelee basi “kufuata mwendo wa ukaribishaji-wageni.”—Waroma 12:13; 1 Timotheo 5:9, 10.
-