WIMBO 120
Tukuwe Wapole Kama Kristo
Maandishi
1. Yesu Kristo alikuwa mukubwa,
Lakini hakukuwa na kiburi.
Hata kama alikuwa na cheo,
Alijishushaka mu mambo yote.
2. Wale wenye wako wanateseka,
Watupie Yesu mizigo yao.
Na wakitafuta kwanza Ufalme,
Atawasaidia kwa upole.
3. Yesu alisema: ‘tuko wandugu,’
Tusikuwe watu wa kujivuna.
Yehova anapendaka wapole,
Na njo wenye watariti dunia.
(Ona pia Mez. 3:34; Mt. 5:5; 23:8; Ro. 12:16.)