-
Mambo Hayo Yalitokea Kabisa?Munara wa Mulinzi (Gazeti la Watu Wote)—2016 | No. 2
-
-
HABARI KUBWA | SABABU GANI YESU ALITESEKA NA KUFA?
Mambo Hayo Yalitokea Kabisa?
Katika mwaka wa 33, Yesu wa Nazarethi aliuawa. Alishitakiwa kwa uongo kama anachochea watu kupinga serikali, alipigwa kama nyama, na kutundikwa kwenye muti. Alikufa katika maumivu makali sana. Lakini Mungu alimufufua, na kisha siku 40, alipanda mbinguni.
Habari hiyo ya pekee inazungumuziwa katika vitabu ine vya Injili vya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, yenye watu wengi wanaita Agano Jipya. Mambo hayo yalitokea kabisa? Hilo ni ulizo nzito, pia lenye kufaa. Kama mambo hayo hayakutokea, imani ya Wakristo haina faida na tumaini la uzima wa milele katika Paradiso ni ndoto tu. (1 Wakorintho 15:14) Lakini kama mambo hayo yalitokea kabisa, wanadamu wako na tumaini la muzuri juu ya wakati unaokuja; wewe pia unaweza kuishi wakati huo. Kwa hiyo, habari za vitabu vya Injili ni za kweli ao ni za kuwazia tu?
MAMBO YA HAKIKA YANAONYESHA NINI?
Tofauti na habari za kuwazia, maandishi ya vitabu vya Injili yanaeleza habari za kweli kabisa na hata mambo madogo-madogo. Kwa mufano, maandishi hayo ya Injili yanajaa majina ya nafasi za kweli, na nafasi nyingi kati ya hizo zinaweza kutembelewa leo. Yanazungumuzia watu wa kweli, na wanahistoria wa ulimwengu wanahakikisha kama watu hao waliishi.—Luka 3:1, 2, 23.
Yesu mwenyewe anazungumuziwa na waandikaji wa ulimwengu wa mwaka kati ya 1 na 200.a Namna Yesu aliuawa, kama vile inaonyeshwa katika vitabu vya Injili, inapatana na namna Waroma walikuwa wanaua watu wakati huo. Tena, mambo yenye yalitokea yanaelezwa kwa uaminifu na kwa ukweli; hata makosa ya wanafunzi fulani wa Yesu yanaonyeshwa. (Mathayo 26:56; Luka 22:24-26; Yohana 18:10, 11) Mambo hayo yote yanaonyesha kabisa kama waandikaji wa vitabu vya Injili walikuwa waaminifu na hawakukosea kuhusu mambo waliandika juu ya Yesu.
TUSEME NINI JUU YA UFUFUO WA YESU?
Hata kama watu wengi wanaitika kuwa Yesu aliishi na alikufa, wengine wanaweza kuwa na mashaka juu ya ufufuo wake. Hata mitume wake hawakuamini wakati waliambiwa kwa mara ya kwanza kama Yesu alifufuka. (Luka 24:11) Lakini, mashaka yote yaliisha wakati watu fulani na wanafunzi wengine walimuona kwa wakati mbalimbali Yesu mwenye alikuwa amefufuliwa. Kwa kweli, wakati fulani kulikuwa watu zaidi ya 500 wenye walimuona.—1 Wakorintho 15:6.
Hata kama wanafunzi wa Yesu walikuwa katika hatari ya kufungwa na kuuawa, walitangaza kwa ujasiri ufufuo wa Yesu kwa watu wote, na kwa wenye walimuua. (Matendo 4:1-3, 10, 19, 20; 5:27-32) Wanafunzi hao wengi wangekuwa na ujasiri ikiwa hawakukuwa hakika kama Yesu alifufuliwa kabisa? Kusema kweli, ufufuo wa Yesu ulitokea kabisa, hilo ndilo jambo lenye lilifanya Ukristo ukuwe na matokeo makubwa wakati huo na hata leo.
Habari za vitabu vya Injili kuhusu kifo cha Yesu na ufufuo wake ziko na ushuhuda wote wenye kuonyesha kama ni habari za kihistoria za kweli kabisa. Kusoma kwa uangalifu habari hizo, kutakuhakikishia kama mambo hayo yalitokea kabisa. Tena, utakuwa hakika zaidi wakati unaelewa sababu gani mambo hayo yalitokea. Habari yenye kufuata itazungumuzia jambo hilo.
a Tasito, mwenye alizaliwa mwaka wa 55 hivi kisha kuzaliwa kwa Yesu, aliandika kama “Kristo, mwenye jina [Wakristo] lilitokana na jina lake, aliuawa katika mikono ya Pontio Pilato, mumoja kati ya magavana wetu, wakati wa utawala wa Tiberio.” Yesu anatajwa tena na mwanahistoria Suetonius (mwenye alizaliwa katika mwaka wa 69); mwanahistoria Muyahudi Joseph (mwenye alizaliwa katika mwaka wa 37 ao 38); na Plini Mudogo, gavana wa Bithinia (mwenye alizaliwa katika mwaka wa 61 ao 62).
-
-
Sababu Gani Yesu Aliteseka na Kufa?Munara wa Mulinzi (Gazeti la Watu Wote)—2016 | No. 2
-
-
HABARI KUBWA
Sababu Gani Yesu Aliteseka na Kufa?
‘Kama vile kupitia mutu mumoja [Adamu] zambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia zambi.’—Waroma 5:12
Unaweza kujibu namna gani ikiwa unaulizwa, “Unapenda kuishi milele?” Watu wengi wanaweza kusema kama wanapenda, lakini wanaona kuwa ni jambo lenye haliwezi kuwezekana. Wanasema kama, kifo ni sehemu ya kawaida ya maisha; hata kama tunaishi, mwishowe tutakufa tu.
Lakini, fikiria kama ulizo hilo lingebadilishwa na unaulizwa, “Uko tayari kufa?” Watu wengi wenye kuwa katika hali za kawaida wanaweza kujibu hapana. Hilo linaonyesha nini? Hata kama tunapatwa na magumu, tamaa yetu ya kawaida ni kuishi. Biblia inaonyesha kama Mungu aliumba wanadamu wakiwa na tamaa na nia ya kuishi. Kwa kweli, inasema kama “wakati usio na kipimo ameuweka ndani ya moyo wao.”—Mhubiri 3:11.
Kusema kweli, watu hawaishi milele. Sasa, ni nini haikuendeka? Tena, Mungu amefanya jambo fulani ili kutengeneza hali hiyo? Majibu ya Biblia ni yenye kutia moyo na yanapatana na sababu yenye ilifanya Yesu ateseke na kufa.
NI NINI HAIKUENDEKA?
Sura tatu za kwanza za kitabu cha Biblia cha Mwanzo zinaonyesha kama Mungu alipatia bibi na bwana wa kwanza, Adamu na Eva, tumaini la kuishi milele na aliwaambia nini walipaswa kufanya ili waishi milele. Kisha habari hiyo inaonyesha namna walikosa kutii Mungu na kupoteza tumaini hilo. Habari hiyo inaelezwa kwa njia nyepesi sana, na hilo linafanya watu fulani wakuwe haraka kusema kama ni habari ya kuwazia tu. Lakini, kama vile vitabu vya Injili, kitabu cha Mwanzo kinatoa ushuhuda wenye kuonyesha kama habari hiyo ni ya kweli kabisa.a
Kwa sababu Adamu hakumutii Mungu, matokeo yalikuwa gani? Biblia inajibu hivi: ‘Kama vile kupitia mutu mumoja [Adamu] zambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia zambi, na hivyo kifo kikaenea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya zambi.’ (Waroma 5:12) Kwa kukosa kutii Mungu, Adamu alifanya zambi. Wakati alifanya vile, alipoteza tumaini la kuishi milele na alifikia kufa. Tumeriti hali hiyo ya zambi kwa sababu tuko watoto wake. Ndiyo sababu tunagonjwa, tunazeeka, na tunakufa. Mafasirio hayo juu ya sababu gani tunakufa, yanapatana na mambo yenye wanasayansi wamevumbua juu ya namna watoto wanariti tabia fulani za wazazi wao. Lakini, Mungu amefanya jambo fulani juu ya kutengeneza hali hiyo?
MAMBO YENYE MUNGU AMEFANYA
Mungu alifanya mipango ya kukomboa, ao kununua tena jambo lenye Adamu alikuwa amepotezea watoto wake, ni kusema, tumaini la kuishi milele. Mungu alifanya vile namna gani?
Katika andiko la Waroma 6:23, Biblia inasema kama ‘mushahara ambao zambi inalipa ni kifo.’ Hilo linamaanisha kama matokeo ya zambi ni kifo. Adamu alikufa kwa sababu alifanya zambi. Kama Adamu, tunafanya zambi na kwa hiyo tunapata mushahara wa zambi, ni kusema, kifo. Tulizaliwa katika hali hiyo ya zambi hata kama hatukufanya makosa yoyote. Kwa hiyo, kwa sababu ya upendo wake, Mungu alituma Yesu, Mwana wake, ili aitike ‘mushahara wa zambi’ kwa ajili yetu. Hilo linawezekana namna gani?
Kifo cha Yesu kinafungua njia ya kuishi milele katika furaha
Kwa sababu Adamu, mutu mumoja mukamilifu alituletea zambi na kifo kupitia kutotii kwake, tulikuwa na lazima ya mutu mukamilifu mwenye angetii hata mupaka kifo ili kutuondolea muzigo huo. Biblia inafasiria jambo hilo hivi: ‘Kwa maana kama vile kupitia kutotii kwa mutu mumoja wengi walifanywa watenda-zambi, vivyo hivyo pia kupitia kutii kwa mutu mumoja wengi watafanywa kuwa waadilifu [wenye haki].’ (Waroma 5:19) Yesu alikuwa ‘mutu [huyo] mumoja.’ Alitoka mbinguni, akakuwa mutu mukamilifub, na akakufa kwa ajili yetu. Hilo linafanya Mungu atukubali kuwa wenye haki na tunakuwa na tumaini la kupata uzima wa milele.
SABABU GANI YESU ALITESEKA NAKUFA?
Lakini, sababu gani ilikuwa lazima Yesu akufe ili kutimiza jambo hilo? Mungu Mweza-Yote hangetoa tu sheria yenye ingeruhusu watoto wa Adamu waishi milele? Kwa kweli, alikuwa na uwezo wa kufanya vile. Lakini, hilo lingeonyesha kama anazarau sheria yake yenye ilisema kuwa mushahara wa zambi ni kifo. Sheria hiyo haiko sheria yenye haina maana yenye inaweza kuvunjwa ao kubadilishwa kwa kupenda. Ni musingi wa haki ya kweli.—Zaburi 37:28.
Kama Mungu angetia haki yake pembeni katika hali hiyo, watu wangeweza kujiuliza kama angeendelea kufanya hivyo katika hali zingine. Kwa mufano, angeamua kwa haki ni nani kati ya watoto wa Adamu mwenye anastahili kuishi milele? Tungeamini kama atatimiza ahadi zake? Kwa sababu Mungu alishikamana na haki ili kututolea nafasi ya kuokolewa, hilo linatuhakikishia kama atatenda kwa haki sikuzote.
Kupitia kifo cha Yesu cha zabihu, Mungu alifungua njia ya kupata uzima wa milele katika dunia Paradiso. Ona maneno ya Yesu yenye kuonyeshwa katika Yohana 3:16: ‘Kwa maana Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba akamutoa Mwana wake muzaliwa-pekee, ili kila mutu anayemuamini asiangamizwe bali [lakini] akuwe na uzima wa milele.’ Kwa hiyo, kifo cha Yesu kinaonyesha haki ya Mungu yenye haina mwisho, na kinaonyesha zaidi sana upendo wake mukubwa kwa wanadamu.
Lakini, sababu gani Yesu aliteseka na kufa katika maumivu makali kama vile inaonyeshwa katika vitabu vya Injili? Kwa kujiacha ajaribiwe vikali na kubakia muaminifu, Yesu alipinga kabisa shitaka la Shetani la kwamba wanadamu hawawezi kubakia waaminifu kwa Mungu wakati wanajaribiwa. (Ayubu 2:4, 5) Kisha Shetani kuchochea Adamu, mutu mukamilifu, afanye zambi, shitaka hilo lingeweza kuonekana kuwa la kweli. Lakini Yesu mwenye alikuwa mukamilifu kama Adamu, alibakia muaminifu hata kama alipatwa na mateso makali. (1 Wakorintho 15:45) Hivyo alionyesha kama Adamu pia angeweza kutii Mungu kama angechagua kufanya vile. Kwa kuvumilia mateso, Yesu alituachia mufano wenye tunaweza kufuata. (1 Petro 2:21) Mungu alibariki utii mukamilifu wenye Mwana wake alionyesha, na alimupatia uzima wenye hauwezi kufa kule mbinguni.
FAIDA YENYE UNAWEZA KUPATA
Kifo cha Yesu kilitokea kabisa. Njia ya kupata uzima wa milele iko wazi. Unapenda kuishi milele? Yesu alionyesha jambo lenye unaweza kufanya wakati alisema hivi: ‘Uzima wa milele ndio huu, waendelee kupata ujuzi juu yako wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na juu ya yule uliyemutuma, Yesu Kristo.’—Yohana 17:3.
Wachapishaji wa gazeti hili wanakuomba ujifunze mengi juu ya Yehova, Mungu wa kweli na juu ya Yesu, Mwana wake. Mashahidi wa Yehova wa eneo lenu watafurahi kukusaidia. Tena, unaweza kupata habari zingine zenye kusaidia kwenye adresi yetu ya Internete, www.pr2711.com.
a Soma habari “Historicité de la Génèse,” katika kitabu Étude Perspicaces des Écritures, volume 1, ukurasa wa 986, chenye kilichapishwa na Mashahidi wa Yehova.
b Mungu alihamisha uzima wa Mwana wake kutoka mbinguni na akautia katika tumbo la uzazi la Maria. Hilo lilifanya Maria apate mimba, lakini roho ya Mungu ilimulinda Yesu asiriti hali ya zambi kutoka kwa Maria.—Luka 1:31, 35.
-