-
Uaminifu Ungali wa Maana Leo?Munara wa Mulinzi (Gazeti la Watu Wote)—2016 | No. 1
-
-
HABARI KUBWA | SABABU GANI NI MUZURI KUWA MUAMINIFU?
Uaminifu Ungali wa Maana Leo?
Hitoshi alitumika katika biro ya kuhesabu feza ya shirika moja la kutafutia watu kazi katika inchi ya Japani. Wakati alikuwa anachunguza hesabu ya feza pamoja na mukubwa wake wa kazi, aliambiwa kama alipaswa kufanya ripoti ya uongo. Hitoshi alifasiria kama zamiri yake haingeweza kumuruhusu akose uaminifu. Kwa hiyo, mukubwa wake wa kazi alimuogopesha kama atafukuzwa kwenye kazi na mwisho akapoteza kazi yake.
Katika miezi yenye ilifuata, Hitoshi alivunjika moyo kwa sababu ya magumu ya kupata kazi. Kwa mufano, wakati fulani alipoulizwa maulizo ili kupewa kazi, alisema kama hawezi kutumika kazi ya kumufanya akose uaminifu. Mutu mwenye alimuuliza maulizo alisema hivi: “Namna yako ya kufikiri ni ya kushangaza!” Familia ya Hitoshi na marafiki wake walimutia moyo aendelee kuwa muaminifu, lakini yeye alianza kuwa na mashaka. Kwa mufano, alisema hivi: “Nilijiuliza ikiwa kubakia muaminifu kwa sababu ya imani yangu lilikuwa wazo la muzuri.”
Mufano huo wa Hitoshi wenye kuhuzunisha unatukumbusha kama haiko kila mutu anaona uaminifu kuwa jambo la maana. Kwa kweli, watu fulani wanaweza kuona uaminifu kuwa kizuizi, zaidi sana katika mambo ya biashara. Mwanamuke mumoja mwenye kufanya kazi katika inchi ya Afrika Kusini alisema hivi: “Ninazungukwa na watu wenye hawako waaminifu, na wakati fulani ninashawishiwa sana kufuata mufano wao.”
Namna moja ya kukosa uaminifu yenye kuenea sana leo ni kusema uongo. Miaka fulani iliyopita, uchunguzi moja wa Robert Feldman, mwanasayansi wa elimu ya mambo ya akili kwenye Masomo ya Juu ya Massachusetts Amherst, ulionyesha kama watu wazima 60 juu ya 100 hivi wanasema uongo karibu mara moja katika mazungumuzo ya dakika 10. Feldman anasema hivi: “Matokeo hayo yalikuwa ya kushangaza sana. Hatukuwazia kama kusema uongo kulienea sana katika maisha ya watu ya kila siku.” Inashangaza kuona kama watu wengi hawapendi kudanganywa lakini wengi wanadanganya, hauone vile?
Sababu gani kusema uongo, kuiba na namna zingine za kukosa uaminifu zimeenea sana leo? Kukosa uaminifu kuko na matokeo gani juu ya maisha ya watu kwa ujumla? Na jambo la lazima zaidi, namna gani tunaweza kuepuka kuangukia katika matendo hayo ya kukosa uaminifu?
-
-
Kukosa Uaminifu Kunakuletea Matokeo Gani?Munara wa Mulinzi (Gazeti la Watu Wote)—2016 | No. 1
-
-
HABARI KUBWA | SABABU GANI NI MUZURI KUWA MUAMINIFU?
Kukosa Uaminifu Kunakuletea Matokeo Gani?
“Sikuzote, kuko hali ngumu zenye zinaomba kukosa uaminifu kidogo ili kuzimaliza.”—Samantha, inchi ya Afrika Kusini.
Unaitika maneno hayo? Kama Samantha, sisi wote tumekwisha kupambana na hali ngumu wakati fulani. Namna tunatenda katika hali hizo zenye kutuchochea kukosa uaminifu inaweza kufunua ni kanuni gani tunaona kuwa za maana. Kwa mufano, ikiwa tunaona kulinda heshima yetu ili tusipate haya kuwa jambo la lazima, tutaona kukosa uaminifu kuwa jambo la lazima pia. Lakini, mara nyingi wakati watu wengine wanavumbua kweli, kukosa uaminifu kunaleta matokeo ya mubaya. Ona matokeo yenye kufuata.
KUKOSA UAMINIFU KUNAVUNJA KUTUMAINIANA
Musingi wa urafiki wa kweli ni kutumainiana. Wakati watu wawili wanatumainiana, wanajisikia salama kabisa. Lakini kutumainiana hakujilete kwa muujiza. Watu wanaanza kutumainiana kwa kupitisha wakati pamoja, kuzungumuza waziwazi na kutendeana bila uchoyo. Hata hivyo, tendo moja tu la kukosa uaminifu linaweza kuvunja kutumainiana. Na wakati kutumainiana kunavunjika, inaweza kuwa nguvu sana kutumainiana tena.
Umekwisha kudanganywa na mutu fulani mwenye uliwazia kuwa rafiki wa muzuri? Kama ni vile, ulijisikia namna gani? Pengine ulijisikia kuwa mwenye kuumizwa, ao hata kusalitiwa. Jambo hilo linaeleweka kabisa. Kwa kweli, kukosa uaminifu kunaweza kuvunja musingi wa urafiki wa kweli.
KUKOSA UAMINIFU KUNAAMBUKIZA
Katika uchunguzi moja, Robert Innes, profesa wa mambo ya feza kwenye Masomo ya Juu ya Kalifornia, alivumbua kama, “kwa kweli, kukosa uaminifu kunaambukiza.” Kwa hiyo, kukosa uaminifu kunaweza kufananishwa na ugonjwa wenye kuambukiza. Ikiwa unazoea kujiunga na mutu mwenye tabia ya kudanganya, uko katika hatari kubwa ya “kuambukizwa” na tabia hiyo.
Namna gani unaweza kuepuka kuangukia katika mutego wa kukosa uaminifu? Biblia inaweza kukusaidia. Tafazali, chunguza kanuni fulani za Biblia..
-
-
Kuwa Muaminifu Kuko na Faida?Munara wa Mulinzi (Gazeti la Watu Wote)—2016 | No. 1
-
-
HABARI KUBWA | SABABU GANI NI MUZURI KUWA MUAMINIFU?
Kuwa Muaminifu Kuko na Faida?
‘Tuna uhakika kwamba tuna zamiri nyoofu, kwa kuwa tunataka kujiendesha kwa unyoofu [uaminifu] katika mambo yote.’—Waebrania 13:18..
Katika Biblia, neno la Kigiriki lenye kutafsiriwa wakati fulani “unyoofu” linamaanisha moja kwa moja “jambo fulani lenye kuwa muzuri kabisa.” Linaweza pia kumaanisha jambo fulani lenye kuonwa kuwa la muzuri kuhusu mwenendo.
Wakristo wanachukua kwa uzito maneno haya ya mutume Paulo yenye yaliongozwa na roho ya Mungu: “Tunataka kujiendesha kwa unyoofu katika mambo yote.” Kufanya hivyo kunaomba nini?
VITA NDANI YETU
Watu wengi wanajiangalia katika kioo kila asubui mbele ya kutoka nyumbani. Sababu gani? Kwa sababu wanataka waonekane muzuri. Lakini kuko jambo lingine la maana zaidi kuliko kuwa na nywele zenye kukatwa muzuri ao kuvalia nguo za mutindo wa leo. Kwa kweli, namna tuko ndani inaweza kufanya hali yetu ya inje ikuwe ya muzuri ao ya mubaya.
Neno la Mungu linaonyesha waziwazi kama tuko na tamaa ya kufanya mambo ya mubaya. Andiko la Mwanzo 8:21 linasema kama, ‘muelekeo wa moyo wa mwanadamu ni mubaya tangu ujana wake.’ Kwa hiyo, ili tukuwe waaminifu, tunapaswa kupiganisha tamaa zetu za kizalikio za kufanya zambi. Mutume Paulo alifasiria waziwazi namna yeye mwenyewe alikuwa anapiganisha zambi. Alisema hivi: ‘Kwa kweli ninaipenda sheria ya Mungu kulingana na mutu niliye kwa ndani, lakini mimi ninaona ndani ya viungo vyangu sheria nyingine ikipigana na sheria ya akili yangu na kunichukua mateka kwa sheria ya zambi iliyo ndani ya viungo vyangu.’—Waroma 7:22, 23.
Kwa mufano, wakati moyo wetu unatusukuma kufanya mambo ya mubaya na tuko na tamaa ya nguvu sana ya kutenda bila uaminifu, hatulazimishwe kufuata tamaa hiyo. Uamuzi ni wetu. Wakati tunachagua kukataa mawazo ya mubaya, tunaweza kubakia waaminifu hata kama tunazungukwa na ukosefu wa uaminifu.
NAMNA YA KUPATA USHINDI
Ili kuwa waaminifu, kuko ulazima wa kanuni za juu za mwenendo. Inahuzunisha kuona kama watu wengi wanapitisha wakati mwingi ili kuamua juu ya ‘kanuni za mavazi’ zenye wanajiwekea wao wenyewe, kuliko wakati wanapitisha ili kufikiri juu ya kanuni zao za mwenendo. Jambo hilo linafanya wajitetee kwa kusema kama haiko mubaya kukosa kuonyesha uaminifu katika hali fulani. Kitabu kimoja kinasema hivi: “Kwa kweli, tunadanganya kwa kiasi chenye kinaturuhusu tulinde heshima yetu na kuonekana kama watu waaminifu.” [The (Honest) Truth About Dishonesty] Lakini, kuko kanuni yenye kutegemeka yenye inaweza kutusaidia kuamua ikiwa kukosa uaminifu, hata kwa kiasi kidogo, kunakubalika ao hapana? Jambo la kufurahisha ni hili: kuko kanuni hiyo.
Mamilioni ya watu katika dunia wameona kama Biblia inatimiza kabisa ulazima huo. Biblia iko na kanuni za mwenendo zenye haziwezi kulinganishwa na kanuni zingine. (Zaburi 19:7) Inatoa muongozo wenye kutumainika juu ya mambo kama vile maisha ya familia, kazi, mwenendo, na urafiki wetu pamoja na Mungu. Biblia inaendelea kutumika mupaka leo. Sheria na kanuni zake zinahusu watu wa inchi zote, rangi zote, na makabila yote. Kwa kuchunguza Biblia, kuwaza sana juu ya mambo inasema, na kutumikisha mashauri yake, tunaweza kuzoeza moyo wetu ukuwe muaminifu.
Lakini, zaidi ya kuwa na ujuzi wa kweli wa Biblia, kuko jambo lingine la kufanya ili tupate ushindi juu ya tabia ya kukosa uaminifu. Tunaishi katika dunia yenye mwenendo muchafu. Dunia hii inatuchochea kukubali kanuni zake za mubaya. Ndiyo sababu tuko na lazima ya kusali kwa Mungu ili atusaidie na kututegemeza. (Wafilipi 4:6, 7, 13) Kama tunafanya vile, tunaweza kuwa na ujasiri wa kufanya mambo ya muzuri na kuwa waaminifu katika mambo yote.
FAIDA ZA UAMINIFU
Hitoshi mwenye tulitaja kwenye mwanzo wa habari hii alipata faida kwa sababu ya kujulikana kuwa mufanyakazi muaminifu. Sasa anatumikia mukubwa mumoja wa kazi mwenye kupendezwa na uaminifu wake. Hitoshi anasema hivi: “Niko na shukrani, kwa sababu niliweza kupata kazi yenye inaniruhusu kuendelea kuwa na zamiri safi.”
Watu wengine wameona pia kama uaminifu unaleta faida. Ona mifano fulani ya watu wenye walipata faida kwa sababu ya kutumikisha kanuni ya Biblia ya “kujiendesha kwa unyoofu katika mambo yote.”
Zamiri Safi
“Niliacha masomo wakati nilikuwa na miaka 13 ili kutumika na watu wenye kuiba. Kwa hiyo, karibu feza zangu zote (95 juu ya 100) zenye nilikuwa nazo nilizipata kwa kutumia njia za mubaya. Kisha, niliolewa, na mimi na bwana yangu tulianza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Tulijifunza kama Yehovaa Mungu anachukia matendo ya kukosa uaminifu, kwa hiyo, tuliamua kubadilisha maisha yetu. Katika mwaka wa 1990, tulitoa maisha yetu kwa Yehova na tukabatizwa na kuwa Mashahidi wa Yehova.”—Methali 6:16-19.
“Zamani, nyumba yangu ilikuwa inajaa vitu vya wizi, lakini sasa haina vitu kama hivyo; na hilo linanifanya nikuwe na zamiri safi. Ninamushukuru Yehova kwa sababu ya rehema yake wakati ninakumbuka miaka mingi yenye sikukuwa muaminifu. Ni jambo la kufurahisha kulala kila siku kwa kujua kama Yehova ananipenda sasa.”—Cheryl, inchi ya Irelandi.
“Wakati mukubwa wangu wa kazi alivumbua kama nilikataa rushwa (hongo, kata-midomo) ya mutu fulani mwenye alikuja kuuza, aliniambia hivi: ‘Mungu wako anakufanya ukuwe mutu mwenye kutumainika! Kusema kweli, ni baraka kuwa na wewe katika kompanyi yetu.’ Kuwa muaminifu katika mambo yote kunaniwezesha kuwa na zamiri safi mbele ya Yehova Mungu. Tena, kunaniwezesha kusaidia familia yangu na watu wengine wafanye hivyo pia.”—Sonny, inchi ya Hong Kong.
Amani ya Akili
“Niko musaidizi wa musimamizi wa benki moja ya kimataifa. Katika kazi yetu, kupata feza nyingi sana ni jambo la maana zaidi kuliko kuwa muaminifu. Watu wengi wanawaza kama ‘haiko mubaya kukosa uaminifu kidogo ili kuwa tajiri ao kusaidia katika mambo ya feza.’ Lakini, kuwa muaminifu kunaniletea amani ya akili. Nimeamua kuendelea kuwa muaminifu na kuvumilia mambo yote yenye yanaweza kutokea kwa sababu ya kuwa muaminifu. Wakubwa wangu wa kazi wanajua kama siwezi kuwadanganya ao kudanganya kwa ajili yao.”—Tom, inchi ya Amerika.
Kujiheshimia
“Musimamizi wangu wa kazi alinichochea niseme uongo juu ya vitu fulani vyenye vilipotea kwenye kazi, lakini nilikataa. Wakati watu wenye waliiba walivumbuliwa, mukubwa wangu wa kazi alinishukuru kwa sababu ya kuwa muaminifu. Inaomba ujasiri ili kuwa muaminifu katika dunia yenye kukosa uaminifu. Lakini, mwisho watu wanaweza kututumainia na kutuheshimia.”—Kaori, inchi ya Japani.
Zamiri safi, amani ya akili, na kujiheshimia, ni faida zenye kuonyesha kama ni muzuri kuwa muaminifu. Unaitika jambo hilo?
a Biblia inaonyesha kama jina la Mungu ni Yehova.
-