Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • rr sura 18 uku. 189-199
  • “Kasirani Yangu Kali Itawaka”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Kasirani Yangu Kali Itawaka”
  • Ibada Safi ya Yehova Inarudishwa Tena!
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ni Nini Inalamushaka “Kasirani Kali” ya Yehova?
  • Yehova Ametoa Maonyo Gani?
  • Kasirani ya Yehova “Itawaka” Wakati Gani?
  • Namna Gani Yehova Ataonyesha Kasirani Yake Kali?
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Kasirani?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Ufalme wa Mungu Unaondoa Maadui Wake
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Armagedoni Ni Habari Njema!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Endelea Kuwa Muaminifu Wakati wa “Taabu Kubwa”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
Ona Habari Zaidi
Ibada Safi ya Yehova Inarudishwa Tena!
rr sura 18 uku. 189-199
Familia inasoma Biblia pamoja wakati ndugu mwingine iko anachungulia mu dirisha

SURA YA 18

“Kasirani Yangu Kali Itawaka”

EZEKIELI 38:18

WAZO KUBWA: Shambulizi la Gogu linalamusha kasirani ya Yehova; Yehova anapigania watu wake ku vita ya Armagedoni

1-3. (a) “Kasirani kali” ya Yehova itatokeza nini? (Ona picha ku mwanzo wa habari.) (b) Tutazungumuzia nini sasa?

WANAUME, wanamuke, na watoto, wote wanasimama juu ya kuimba wimbo wa Ufalme. Kisha, muzee moja anatoa sala ya kutoka mu moyo, anamulilia Yehova alinde watu wake. Ndugu na dada wa kutaniko wako hakika kama Yehova atawahangaikia, lakini, wako na lazima ya kutiwa moyo na kutiwa nguvu. Inje, kuko makelele ya watu wenye wako wanapigana. Armagedoni imeanza!​—Ufu. 16:14, 16.

2 Wakati wa vita ya Armagedoni, Yehova ataua watu mu “kasirani kali,” lakini hatafanya vile kiholela, atajua nani wa kuua, nani wa kuacha. (Soma Ezekieli 38:18.) Atamwanga kasirani yake kali, hapana juu ya jeshi ao taifa moja tu, lakini juu ya watu wengi wenye wanaishi mu dunia yote. Ile siku, wale wenye Yehova ataua “watakuwa kutoka mwisho mumoja wa dunia mupaka mwisho mwingine wa dunia.”​—Yer. 25:29, 33.

3 Ni nini itafanya Yehova, Mungu wa upendo, “mwenye rehema na huruma” na mwenye “hakasirike haraka,” akamate hatua ya vile, na “kasirani [yake] kali” iwake vile kwa kushitukia? (Kut. 34:6; 1 Yo. 4:16) Acha tuone namna jibu la ile ulizo linaweza kutufariji sana, kutupatia uhodari mingi, na kutuchochea leo mu kazi yetu ya kuhubiri.

Ni Nini Inalamushaka “Kasirani Kali” ya Yehova?

4, 5. Kuko tofauti gani kati ya kasirani ya Mungu na kasirani ya wanadamu wenye hawakamilike?

4 Kwanza, ni muzuri kujua kama kasirani ya Yehova haiko sawa kasirani ya wanadamu wenye hawakamilike. Wakati kasirani ya mutu inapanda sana na kumuchochea atende, mara mingi anashindwa kujizuia na kwa kawaida anafanya mambo ya mubaya. Kwa mufano, Kaini, mwana wa kwanza wa Adamu, ‘alikasirika sana’ sababu Yehova alikataa zabihu yake lakini akakubali zawadi yenye Abeli alitoa. Matokeo? Kaini aliua ndugu yake mwenye alikuwa mwenye haki. (Mwa. 4:3-8; Ebr. 11:4) Fikiria pia Daudi, mwenye anatajwa kuwa mutu mwenye kufurahisha moyo wa Yehova. (Mdo. 13:22) Hata kama alikuwa mutu muzuri, kulibakia kidogo tu afanye kosa kubwa wakati alisikia kama Nabali, tajiri mwenye mashamba, alimutukana yeye na watu wake. Kwa sababu ya kasirani kali, Daudi na maaskari wake ‘walijifunga panga zao,’ na nia yao ilikuwa kuua Nabali mwenye hana shukrani lakini pia kila mwanaume mu nyumba yake. Ya kufurahisha ni kwamba, Abigaili, bibi ya Nabali, aliweza kusadikisha Daudi na wanaume wake wasilipize kisasi. (1 Sa. 25:9-14, 32, 33) Yehova alikuwa na sababu ya muzuri ya kuongoza Yakobo aandike hivi: “Kasirani ya mwanadamu haitokeze haki ya Mungu.”​—Yak. 1:20.

Sikuzote Yehova anazuia kasirani yake na hakasirikake juu tu ya kukasirika

5 Tofauti na kasirani ya mwanadamu, yenye mara mingi haizuiwe, sikuzote Yehova anazuia kasirani yake na hakasirikake bure-bure tu. Hata wakati kasirani yake kali inapanda, Yehova anatenda kwa haki. Wakati anapigana na adui, hawezi hata kidogo kuharibu “mwenye haki pamoja na muovu.” (Mwa. 18:22-25) Zaidi ya ile, Yehova hakasirikake juu tu ya kukasirika, kunakuwaka sababu. Tuone sababu mbili na somo zenye tunajifunza.

6. Yehova anafanyaka nini wakati jina lake linachafuliwa?

6 Sababu ya 1: Yehova anakasirika juu jina lake limechafuliwa. Wale wenye wanasema kama wao njo watumishi wa Yehova lakini wanatenda mambo maovu wanaharibishia jina lake sifa na kwa kufanya vile wanalamusha kasirani yake. (Eze. 36:23) Kama vile tuliona mu sura zenye zilitangulia za kitabu hiki, taifa la Israeli lilifanya jina la Yehova lilaumiwe sana. Ni wazi kwamba, mutazamo na matendo ya taifa la Israeli vilimukasirisha Yehova. Lakini Yehova hakushindwa hata kidogo kuzuia kasirani yake kali​—alipatia watu wake azabu kwa kiasi chenye kufaa kabisa, hakupitisha kipimo hata kidogo. (Yer. 30:11) Na kisha kasirani ya Yehova kutimiza kusudi lake, aliacha kukasirika na hakubakia na kinyongo.​—Zb. 103:9.

7, 8. Namna Yehova alitendea Waisraeli inatupatia somo gani?

7 Somo: Namna Yehova alitendea Waisraeli inatupatia somo kubwa sana. Kama vile Waisraeli wa zamani, sisi pia tuko na pendeleo la kubeba jina la Yehova. Tuko Mashahidi wa Yehova. (Isa. 43:10) Maneno na matendo yetu inaweza kufanya watu waseme muzuri ao mubaya juu ya Mungu mwenye tunatumikia. Hatupendi hata kidogo kuwa watu wenye wanafanya makosa bila kusikia haya na kufanya jina la Yehova lilaumiwe. Matendo ya vile ya unafiki itawakisha kasirani ya Yehova, na hata kupite siku ngapi, atatenda juu ya kulinda sifa yake.​—Ebr. 3:13, 15; 2 Pe. 2:1, 2.

8 Je, kujua kama Yehova anaweza kuwa na “kasirani kali” inapaswa kutufanya tuogope kumukaribia? Hapana. Tunajua kama Yehova iko muvumilivu na mwenye kusamehe. (Isa. 55:7; Ro. 2:4) Lakini tunatambua pia kama anatoa nizamu wakati anaona ni lazima. Kwa hiyo, tunaendelea kumuheshimia mu namna yenye inafaa kwa sababu tunajua kama kasirani yake kali itawaka juu ya wale wenye wanaendelea kufanya ile yenye wanajua kama ni zambi na kwamba hataruhusu wabakie kati ya watu wake. (1 Ko. 5:11-13) Yehova ametuambia waziwazi mambo yenye inamufanyaka akasirike. Ni kwetu sasa kuepuka mitazamo na matendo yenye inaweza kumukasirisha.​—Yoh. 3:36; Ro. 1:26-32; Yak. 4:8.

9, 10. Yehova anafanyaka nini wakati watu wake waaminifu wanashambuliwa? Toa mifano.

9 Sababu ya 2: Yehova anakasirika juu watu wake waaminifu wanashambuliwa. Yehova anakasirika wakati maadui wanashambulia wale wenye wanatafuta kwa uaminifu ulinzi wake. Kwa mufano, kisha Waisraeli kutoka Misri, Farao na jeshi lake lenye nguvu walishuka juu ya kushambulia watu wenye walionekana kuwa zaifu wenye walikuwa wamesongamana pembeni-pembeni ya Bahari Nyekundu. Lakini wakati ile jeshi yenye nguvu iliwafuatilia saa walikuwa wanavuka bahari yenye ilikuwa imekauka, Yehova alifanya magurudumu ya magari yao ya vita itoke na akawakunguta Wamisri ndani ya bahari. “Hakuna hata mumoja kati ya Wamisri mwenye aliokoka.” (Kut. 14:25-28) Kasirani ya Yehova iliwaka juu ya Wamisri sababu ya “upendo mushikamanifu” wenye alikuwa nao kwa ajili ya watu wake.​—Soma Kutoka 15:9-13.

Malaika

Sawa vile malaika alilinda watu wa Mungu wasishambuliwe na Waashuru mu wakati wa Hezekia, sisi pia malaika watatulinda (Ona fungu la 10, 23)

10 Vilevile, kwa kuwa Yehova anapenda watu wake, ile ilimuchochea atende haraka wakati wa Mufalme Hezekia. Waashuru, wenye walikuwa jeshi kali na lenye nguvu zaidi mu ile wakati, walikuwa wamefika na walikuwa tayari kushambulia muji wa Yerusalemu. Walizunguka muji wa watumishi waaminifu wa Yehova, na ile ingefanya watu wakufie mu muji hatua kwa hatua. (2 Fa. 18:27) Wakati Yehova aliona vile, alituma malaika moja tu; mu usiku moja tu, ule malaika aliua maaskari adui 185 000! (2 Fa. 19:34, 35) Wazia namna mambo ilikuwa mu kambi ya Waashuru kesho yake asubui. Mikuki, ngao, panga​—yote ilikuwa imelala tu chini. Hakuna tarumbeta ya kulamusha wale maaskari. Hakuna amri za kuomba majeshi ikusanyike. Kimya kabisa, mahema na kambi imejaa tu maiti.

11. Namna gani mifano ya Biblia yenye inaonyesha mambo Yehova anafanyaka wakati watu wake wanashambuliwa inatupatia faraja na uhodari?

11 Somo: Ile mifano yenye inaonyesha mambo Yehova anafanyaka wakati watu wake wanashambuliwa inatolea maadui wetu onyo kali: “Ni jambo lenye kuogopesha kuanguka katika mikono ya Mungu mwenye kuishi” wakati kasirani yake kali inawaka. (Ebr. 10:31) Ku ngambo yetu, ileile mifano inatufariji na kutupatia uhodari zaidi. Inafariji kujua kama adui yetu mukubwa, Shetani, hataweza. Sasa hivi, “kipindi [chake] kifupi” cha kutawala kitaisha! (Ufu. 12:12) Mbele ile wakati ifike, tunapaswa kumutumikia Yehova bila woga, tukiwa na uhakika kama hakuna mutu, tengenezo, ao guvernema yenye inaweza kutuzuia kufanya mapenzi ya Mungu. (Soma Zaburi 118:6-9.) Mutume Paulo alieleza uhakikisho wenye tuko nao kwa kutumia maneno hii yenye iliongozwa na roho ya Mungu: “Kama Mungu iko upande wetu, ni nani atatushinda?”​—Ro. 8:31.

12. Wakati wa taabu kubwa, ni nini itafanya kasirani kali ya Yehova iwake?

12 Wakati wa taabu kubwa yenye iko inakuja, Yehova atatulinda sawa vile alilinda Waisraeli wakati walikuwa karibu kushambuliwa na Wamisri na sawa vile alilinda Wayahudi kule Yerusalemu wakati Waashuru waliwazunguka kwa ajili ya vita. Wakati maadui wetu watapima kutuharibu, upendo wenye Yehova iko nao kwa ajili yetu utafanya kasirani yake kali iwake. Wale wenye wataonyesha kama hawana akili na kupima kutushambulia, watakuwa sawa vile wanagusa mboni ya jicho la Yehova. Atatenda haraka na bila kukawia. (Zek. 2:8, 9) Watu watauawa mu namna yenye haiyakuwaka. Lakini maadui wa Mungu hawatakuwa na sababu kabisa ya kushangaa wakati Yehova atamwanga kasirani yake kali juu yao. Juu ya nini tunasema vile?

Yehova Ametoa Maonyo Gani?

Nabii wa Yehova

KISANDUKU CHA KUFUNDISHIA 18A: Yehova Anaonya Watu juu ya Vita Kubwa Yenye Iko Inakuja

13. Yehova ametoa maonyo gani?

13 Yehova “hakasirike haraka” na ametoa maonyo mingi ya kuonyesha kama ataharibu wale wenye wanamupinga na kutaka kushambulia watu wake. (Kut. 34:6, 7) Yehova alitumia manabii sawa vile Yeremia, Ezekieli, Danieli, Kristo Yesu, na mitume sawa vile Petro, Paulo, na Yohana juu ya kuonya watu kuhusu ile vita kubwa sana.​—Ona kisanduku “Yehova Anaonya Watu Juu ya Vita Kubwa Yenye Iko Inakuja.”

14, 15. Ni mambo gani Yehova amefanya, na juu ya nini?

14 Yehova amefanya ile maonyo iandikwe mu Neno lake. Pia, amekamata mipango juu Biblia itafsiriwe na kugawanywa sana kupita vitabu vingine. Mu dunia yote, ametokeza jeshi la wafanyakazi wa kujitolea wenye wanasaidia wengine wajifunze namna ya kufanya amani na Mungu na wenye wanaonya watu juu ya “siku kubwa ya Yehova” yenye iko inakuja. (Sef. 1:14; Zb. 2:10-12; 110:3) Amechochea watumishi wake watafsiri vitabu vya kusaidia watu kujifunza Biblia mu luga mingi na amewachochea wapitishe mamilioni ya masaa kila mwaka na wako wanaambia watu kuhusu ahadi na maonyo yenye inapatikana mu Neno lake.

15 Yehova amefanya ile yote “kwa sababu hataki mutu yeyote aharibiwe lakini anataka wote wafikie kutubu.” (2 Pe. 3:9) Tuko na pendeleo kubwa sana la kuwakilisha Mungu wetu mwenye upendo, muvumilivu, na kufanya ile kidogo tunaweza juu ya kueneza ujumbe wake! Lakini sasa hivi, wale wote wenye hawasikilize ile maonyo watakuwa wamechelewa.

Kasirani ya Yehova “Itawaka” Wakati Gani?

16, 17. Je, Yehova alishaweka siku ya vita ya mwisho? Fasiria.

16 Yehova alishaweka siku ya vita ya mwisho. Tayari anajua ni wakati gani watu wake watashambuliwa. (Mt. 24:36) Yehova anajua je wakati maadui wake watatushambulia?

17 Kama vile tuliona mu sura yenye ilitangulia ya kitabu hiki, Yehova anamuambia Gogu: ‘Nitatia . . . kulabu katika mataya yako.’ Atachochea mataifa iingie mu vita ya kukata maneno. (Eze. 38:4) Ile haimaanishe kama Yehova njo ataanzisha ile vita; wala haimaanishe kama atanyanganya wale wenye kumupinga uhuru wao wa kuchagua. Lakini, inaonyesha kama Yehova iko na uwezo wa kujua mambo yenye iko mu moyo wa mutu na anajua namna maadui wake watatenda mu hali fulani.​—Zb. 94:11; Isa. 46:9, 10; Yer. 17:10.

18. Juu ya nini wanadamu watapima kupigana na Mweza-Yote?

18 Kama haiko Yehova njo ataanzisha ile vita ao kulazimisha maadui wake waingie mu vita, juu ya nini wanadamu bure watapima kupigana na Mweza-Yote? Sababu moja ni kwamba ile wakati, inaonekana watakuwa wamejisadikisha kwamba Mungu haiko ao kwamba hahangaikie mambo ya wanadamu. Pengine watawaza vile sababu watakuwa tayari wameharibu matengenezo yote ya dini ya uongo ku dunia. Kwa hiyo watawaza kama ikiwa Mungu iko, angepaswa kupigania matengenezo yenye inasemaka kama inamutumikia. Hawatatambua kama ni Mungu njo alitia mu moyo wao wazo la kuondoa dini za uongo zenye zimefundisha mambo mingi ya uongo juu yake.​—Ufu. 17:16, 17.

19. Kunaweza kutokea nini kisha dini ya uongo kuharibiwa?

19 Wakati fulani kisha dini ya uongo kuharibiwa, Yehova anaweza kufanya watu wake watangaze ujumbe mukali sana, wenye kitabu cha Ufunuo kinalinganisha na mvua kubwa ya majiwe yenye kila jiwe liko na uzito wa kilograme 20 hivi. (Ufu. 16:21, maelezo ya chini) Ile ujumbe, inawezekana ya kuonyesha kama guvernema na mufumo wa biashara viko karibu kuharibiwa, itachoma sana wenye wataisikia kiasi ya kwamba wataanza kumutukana Mungu. Inaonekana kama ni ile ujumbe njo itafanya mataifa ishambulie kabisa watu wa Mungu, juu ya kuwafunga kinywa lote. Watawaza kama hatuna nguvu, na kama kutuharibu ni teketeke. Itakuwa kujidanganya sana!

Namna Gani Yehova Ataonyesha Kasirani Yake Kali?

20, 21. Gogu ni nani, na ni nini itamupata?

20 Kama vile tuliona mu Sura ya 17 ya kitabu hiki, Ezekieli anatumia jina la kiunabii, “Gogu wa inchi ya Magogu,” juu ya kutaja muungano wa mataifa wenye utatushambulia. (Eze. 38:2) Lakini muungano wao utakuwa wa jina tu. Hata kama itaonekana kuwa wako mu umoja, roho ya kushindana, kiburi, na roho ya kila mutu kutafuta faida za inchi yake itaendelea. Itakuwa mwepesi kwa Yehova kufanya upanga wa kila mumoja ugeukie “ndugu yake mwenyewe.” (Eze. 38:21) Lakini kuharibiwa kwa mataifa haitakuwa musiba wenye utaletwa na mwanadamu.

21 Mbele ya kuharibiwa, maadui wetu watajionea alama ya Mwana wa binadamu, inawezekana itakuwa maonyesho yenye haiko ya kawaida ya nguvu ya Yehova na Yesu. Wapinzani wetu wataona mambo yenye itawaogopesha sana. Sawa vile Yesu alitabiri, “watu watazimia kwa woga na kwa sababu ya kungojea mambo yenye yatakuja juu ya dunia yenye kuikaliwa na watu.” (Lu. 21:25-27) Watavumbua kwamba walidanganyika sana wakati walishambulia watu wa Yehova. Watalazimika kujua kama Muumbaji ni kamanda mukubwa, Yehova wa majeshi. (Zb. 46:6-11; Eze. 38:23) Yehova atatumia majeshi ya mbinguni na nguvu za asili mu njia yenye italinda watumishi wake waaminifu lakini yenye itaharibu maadui wake.​—Soma 2 Petro 2:9.

Majeshi ya mbinguni yenye iko tayari kumwanga kasirani kali ya Mungu na kulinda watu wake

Wakati watu wake watashambuliwa, Yehova atatumia majeshi ya mbinguni juu ya kumwanga kasirani yake kali (Ona fungu la 21)

22, 23. Ni nani watalinda watu wa Mungu, na watajisikia je kuhusu kazi yao?

Mambo yenye tunajua kuhusu siku ya Yehova inapaswa kutuchochea kufanya nini?

22 Fikiria namna Yesu atakuwa na hamu sana ya kuongoza shambulizi juu ya maadui wa Mungu na kulinda wale wenye wanamupenda Baba yake na kumutumikia. Fikiria pia, namna watiwa-mafuta watajisikia. Wakati fulani mbele Armagedoni ianze, wa mwisho kati yao mwenye atakuwa angali ku dunia atafufuliwa na kuenda mbinguni juu wote 144 000 waweze kusaidia Yesu mu ile vita. (Ufu. 17:12-14) Bila shaka, wengi kati ya watiwa-mafuta watakuwa wamekwisha kufanya urafiki wa karibu sana na washiriki wa kondoo wengine wakati walikuwa wanatumika nao mu siku za mwisho. Sasa watiwa-mafuta watakuwa na mamlaka na nguvu ya kupigania wale wenye walikuwa wanawategemeza kwa uaminifu mu majaribu yao.​—Mt. 25:31-40.

23 Malaika watakuwa pia mu jeshi la mbinguni la Yesu. (2 Te. 1:7; Ufu. 19:14) Walishakamusaidia Yesu kutosha Shetani na mashetani wake mbinguni. (Ufu. 12:7-9) Na wamesaidia mu kazi ya kukusanya wale wenye wanataka kumuabudu Yehova ku dunia. (Ufu. 14:6, 7) Itakuwa muzuri kabisa Yehova aache malaika walinde wale waaminifu wake! Na zaidi ya yote, wote mu jeshi la Yehova watajisikia kuwa Yehova anawaheshimia kwa kuwapatia daraka la kutakasa na kutetea jina lake, ao sifa yake, kwa kuharibu maadui wake.​—Mt. 6:9, 10.

24. Kundi kubwa la kondoo wengine litajisikia je?

24 Kwa sababu watakuwa na jeshi lenye nguvu sana, na lenye linapenda sana kuwalinda, wale wa kundi kubwa wa kondoo wengine hawatakuwa na sababu ya kuogopa. Lakini, ‘watasimama wima na kuinua vichwa vyao, kwa sababu ukombozi wao unakaribia.’ (Lu. 21:28) Kwa hiyo, mbele siku ya Yehova ifike, ni jambo la maana sana tusaidie watu wengi kadiri inawezekana wafikie kumujua na kumupenda Baba yetu mwenye rehema na mwenye kulinda watu wake!​—Soma Sefania 2:2, 3.

Malaika wanalinda washiriki wa kundi kubwa mu kipindi cha taabu kubwa wakati wenye kuwashambulia wanageukiana

Wakati wa Armagedoni, watu wa Yehova hawatapigana. Malaika watawalinda wakati wale wenye kuwashambulia watageukiana.​—Eze. 38:21 (Ona fungu la 22-24)

25. Tutazungumuzia nini mu sura ya kufuata?

25 Wakati vita za wanadamu zinaishaka, kunakuwaka tu muvurugo na huzuni. Lakini, kisha Armagedoni kutakuwa utaratibu na furaha. Mambo itakuwa je wakati kasirani kali ya Yehova inamaliza kufanya kazi yake, wakati panga za wapiganaji-vita wake zinarudishwa mu mifuko yazo, na alama za mwisho-mwisho za ile pigano kubwa zinafifia? Tutazungumuzia ile wakati ya muzuri sana mu sura ya kufuata.

UMEJIFUNZA NINI KUHUSU IBADA SAFI?

  1. Ni nini inalamushaka kasirani ya Yehova?

  2. Namna gani Yehova ataonyesha kasirani yake kali?

  3. Juu ya nini tunapaswa kuendelesha ibada safi kwa bidii leo?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine