Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/96 uku. 7
  • Programu ya Kusanyiko Lipya la Pekee la Siku Moja

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Programu ya Kusanyiko Lipya la Pekee la Siku Moja
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Programu ya Kusanyiko la Pekee la Siku Moja Lijalo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Programu Ya Kusanyiko La Pekee La Siku Moja Lijalo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Programu Ya Kusanyiko Lipya La Mzunguko
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Kusanyiko Lipya La Pekee La Siku Moja
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 3/96 uku. 7

Programu ya Kusanyiko Lipya la Pekee la Siku Moja

1 Kwa nini tunapaswa kutangaza habari njema bila kuacha? Ni matakwa gani inafaa kutimiza ili kuwa mhubiri wa habari njema? Namna gani hata watu wenye haya na waoga wanaweza kuchukua hatua ya kwanza ili kupasha habari njema kwa majirani zao? Maulizo hayo yanayofanya mtu kufikiri na mengine mengi yatajibiwa kwenye kusanyiko lipya la pekee la siku moja lililoanza mnamo Septemba iliyopita. Lina kichwa “Wenye Sifa za Kustahili Ili Kuwa Wahudumu wa Habari Njema.”—Tazama 2 Kor. 3:​5, NW.

2 Sisi ni watumishi wa Yehova; ndiyo sababu tunapaswa kuangalia sana mwenendo wetu. Walio vijana wataeleza mambo yaliyoonwa ili kuonyesha namna gani walipingana na uvutano wa marafiki zao. Wazazi wanatiwa moyo kuelewa ulazima wa kuzoeza watoto wao ili wawe wahudumu wa Mungu. Sisi sote tunapokea mashauri yatakayotusaidia tuwe wenye kutambua ulazima wa kuhubiri, na pia baraka ambazo tunapata, na vivyo hivyo wale wanaotusikiliza.— 1 Tim. 4:16.

3 Sherehe ya ubatizo bila shaka inakuwa wakati wa lazima katika siku hiyo. Lakini kabla ya hilo; hotuba ya kibiblia itatolewa hasa kwa ajili ya watu waliojiweka wakf kwa Mungu hivi karibuni. Kwa kawaida, watu wote wanaohudhuria wanaalikwa kusikiliza kwa uangalifu hotuba hiyo inayofasiria kwa wazi maana ya ubatizo. Wote wale wanaotamani kubatizwa wakati wa kusanyiko la pekee la siku moja wanapaswa kumjulisha mapema vya kutosha mwangalizi-msimamizi, ili achukue mipango ili kwamba wazee wachunguze pamoja na wale wanaotaka kubatizwa maulizo yaliyotayarishwa kwa ajili yao.

4 Siku hiyo inatiwa pia alama na hotuba ya maana, inayotolewa na msemaji-mgeni. Hotuba hiyo, yenye kichwa “Wenye Sifa za Kustahili Ili Kuwa Wahudumu wa Mungu,” inatoa ile mipango mine mikubwa inayotuwezesha kuwa wenye kustahili kama wahudumu. Mambo yaliyoonwa yenye kujenga yataelezwa pia.

5 Tutengeneze mambo yetu tangu sasa ili kuhudhuria kwenye hotuba zote (isipokuwa kwamba tumekwisha kuhudhuria mahali pengine). Tusikose kualika watu wanaopendezwa na Biblia ili wao pia waweze kufaidika na siku hiyo yenye mafundisho ya kitheokrasi. Tutapata hivyo kuwa na uhakika wa kuwa wenye “sifa za kustahili” kama wahudumu wa habari njema.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine