Nani Atasikiliza Ujumbe Wetu?
1 Kamwe kuliko wakati mwingine wowote, watu wanafurikwa na habari, ambazo kati yazo ni za juu juu tu, huenda hata za udanganyifu. Kwa hiyo, wengi ni wenye kufurikwa na mambo, na inakuwa vigumu kwetu kuwafanya kusikiliza ujumbe wa Ufalme wa Mungu. Hawatambui matokeo mazuri ambayo kusikiliza Neno la Mungu yanaweza kuwa nayo juu yao.—Lu. 11:28.
2 Tunafurahi kuona kwamba katika sehemu nyingi za ulimwengu makumi ya maelfu ya watu wanasikiliza ujumbe huo na wanakubali kujifunza Biblia. Hata hivyo, katika maeneo mengine hakika hakuna kuitikia huko. Mazungumzo mengi ambayo tunayo katika huduma hayazai matunda, na labda tunajiuliza nani atasikiliza ujumbe wetu.
3 Tunapaswa kujihadhari tusivunjike moyo. Paulo alisema ifuatayo: “ ‘Kila mtu aitiaye jina la Yehova ataokolewa.’ Hata hivyo, watamwitiaje . . . yeye ambaye hawajasikia? Nao watasikiaje bila mtu fulani kuhubiri? . . . Kama vile imeandikwa: “Jinsi ilivyo yenye kupendeza miguu ya wale watangazao habari njema ya mambo mema!” (Rom. 10:13-15, TUM) Ikiwa tunapanda kwa bidii mbegu ya Ufalme, Mungu ataikuza kwa watu wanyofu.—1 Cor. 3:6.
4 Ufunguo wa Kufanikiwa ni Kufanya Kila Siku Ziara za Kurudia: Katika maeneo ambako inaonekana kwamba ni watu wadogo wanaosikiliza ujumbe wetu, tunapasa kuwa wangalifu ili kukomaza kila kupendezwa tunakokuta, iwe tuliacha kichapo au hapana. Kwa nini kuwa haraka kukata shauri kwamba hakuna matokeo yoyote yatakayopatikana? Tunapopanda mbegu fulani, hatujui ni ya wapi itakayofanikiwa. (Muh. 11:6) Ikiwa tunarudi baada ya sisi kujitayarisha katika kusudi la kutoa wazo fulani linalotokana na Maandiko, hata kwa kusema kwa kifupi, labda tutafanikiwa kugusa moyo wa mtu. Tunaweza kuacha trakti au kutolea magazeti ya mwisho mwisho. Siku nenda, itawezekana kwetu labda kuonyesha jinsi funzo la Biblia linavyoendeshwa. Tutashangazwa kwa furaha kuona kwa kiasi gani Yehova atabariki bidii yetu. —Zab. 126:5, 6.
5 Trakti moja iliachwa kwa mwanamume fulani aliyeonyesha kupendezwa. Ni miezi miwili baadaye tu ndipo aliweza kukutwa nyumbani kwake, lakini alikuwa mwenye shughuli nyingi kwa kuzungumza. Aliweza kuachiwa trakti ileile tena. Ijapokuwa udumilifu wa mhubiri huyo wa kike ili kukutana naye, aliweza kuonana naye tena baada ya miezi mitatu, akitambua sasa kwamba alikuwa mgonjwa. Dada alirudi juma lifuatalo, na mazungumzo mafupi yalianzishwa kulingana na trakti. Dada aliporudi juma la baadaye, mwanamke huyo alionyesha kupendezwa kwa kweli kuelekea ujumbe wa Ufalme. Mabadiliko katika maisha yake yalimfanya atambue mahitaji yake ya kiroho. Funzo la Biblia lilianzishwa, na mwanamke huyo alijifunza kwa shauku muda wa majuma yaliyofuata.
6 Iwe ni maua, majani mboga au kupendezwa na ujumbe wa Ufalme, yote ambayo tunapenda kuona yanakomaa yanapaswa kukuzwa. Hilo linaomba wakati, jitihada, uangalifu na azimio ili kutokuacha. Mwaka jana, watu karibu 400,000 ambao ndani yao mbegu ya Ufalme iliota mizizi walibatizwa! Ikiwa tunaendelea kuhubiri, tunaweza kuwa na uhakika wa kwamba tutawapata watu wengi watakaosikiliza ujumbe wetu.—Ona Wagalatia 6:9.