“Msaada Katika Wakati Ufaao”
1 Ni jambo lenye kuburudisha kama nini kupokea msaada kwa wakati hasa tunaouhitaji! (Ebr. 4:16) Kwenye Kusanyiko la Wilaya “Wajumbe wa Amani ya Kimungu”, tulifurahi tulipopokea kwa wakati hasa unaofaa vichapo viwili ambavyo ni misaada yenye thamani kwetu.
2 Kitabu kipya, Siri ya Furaha ya Familia, kimefika kwa wakati unaofaa. Kinatia mkazo juu ya mambo manne ya lazima kwa maisha ya familia yenye furaha: (1) kujidhibiti (kujiweza), (2) utiifu kwa kanuni ya ukichwa, (3) mawasiliano mazuri na (4) upendo. Mashauri yanayotolewa katika kitabu Furaha ya Familia yatazisaidia familia zote zinazoyatumikisha kupata amani ya kimungu. Tujiwekee wakati ili kukisoma kwa makini na kwa kujifunza chenyewe katika familia. Tufahamiane vizuri na mambo yake makubwa ili kuwa tayari kukitumia kwa matokeo tutakapokitolea kwa mara ya kwanza kwa watu, mnamo Aprili.
3 Broshua mpya, Mungu Anataka Nini Kwetu? imefika kwa wakati unaofaa ili kuchochea kazi ya kufanya wanafunzi. Ijapokuwa imekusudiwa hasa kuwasaidia watu walio na magumu ya kusoma, watu wazima wengi wanaojua kusoma na pia watoto watafaidika pia na mafasirio mepesi ya mafundisho ya msingi ya Biblia yaliyomo. Kitakuwa labda ndicho chombo tu cha muhimu ili kuanzisha funzo na kuliendeleza na kitabu Ujuzi. Bila shaka kwamba broshua hiyo itawasaidia watu wengi zaidi kutambua baraka nyingi wanazoweza kujipatia ikiwa wanafanya yale Mungu anataka kwetu.
4 Daudi alionyesha vizuri maoni yetu aliposema kwamba ‘hakupungukiwa na kitu, kwamba nafsi yake ilirudishwa na kwamba kikombe chake kilifurika.’ (Zab. 23:1, 3, 5) Sisi ni wenye shangwe kuacha misaada hiyo bora ya kibiblia kwa watu wengi wanaopenda kwa unyofu kujua Mungu wa kweli, Yehova, na kumtumikia.