Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 1/97 uku. 7
  • “Msaada Katika Wakati Ufaao”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Msaada Katika Wakati Ufaao”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tuwajulishe Wengine Siri Ya Kupata Furaha Ya Familia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Tusaidie Familia Kujijengea Wakati Ujao Udumuo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Toleeni Watu wa Umri Zote Kitabu Furaha ya Familia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Biblia Inafundisha— Kitabu Chetu cha Lazima cha Kujifunzia Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 1/97 uku. 7

“Msaada Katika Wakati Ufaao”

1 Ni jambo lenye kuburudisha kama nini kupokea msaada kwa wakati hasa tunaouhitaji! (Ebr. 4:16) Kwenye Kusanyiko la Wilaya “Wajumbe wa Amani ya Kimungu”, tulifurahi tulipopokea kwa wakati hasa unaofaa vichapo viwili ambavyo ni misaada yenye thamani kwetu.

2 Kitabu kipya, Siri ya Furaha ya Familia, kimefika kwa wakati unaofaa. Kinatia mkazo juu ya mambo manne ya lazima kwa maisha ya familia yenye furaha: (1) kujidhibiti (kujiweza), (2) utiifu kwa kanuni ya ukichwa, (3) mawasiliano mazuri na (4) upendo. Mashauri yanayotolewa katika kitabu Furaha ya Familia yatazisaidia familia zote zinazoyatumikisha kupata amani ya kimungu. Tujiwekee wakati ili kukisoma kwa makini na kwa kujifunza chenyewe katika familia. Tufahamiane vizuri na mambo yake makubwa ili kuwa tayari kukitumia kwa matokeo tutakapokitolea kwa mara ya kwanza kwa watu, mnamo Aprili.

3 Broshua mpya, Mungu Anataka Nini Kwetu? imefika kwa wakati unaofaa ili kuchochea kazi ya kufanya wanafunzi. Ijapokuwa imekusudiwa hasa kuwasaidia watu walio na magumu ya kusoma, watu wazima wengi wanaojua kusoma na pia watoto watafaidika pia na mafasirio mepesi ya mafundisho ya msingi ya Biblia yaliyomo. Kitakuwa labda ndicho chombo tu cha muhimu ili kuanzisha funzo na kuliendeleza na kitabu Ujuzi. Bila shaka kwamba broshua hiyo itawasaidia watu wengi zaidi kutambua baraka nyingi wanazoweza kujipatia ikiwa wanafanya yale Mungu anataka kwetu.

4 Daudi alionyesha vizuri maoni yetu aliposema kwamba ‘hakupungukiwa na kitu, kwamba nafsi yake ilirudishwa na kwamba kikombe chake kilifurika.’ (Zab. 23:1, 3, 5) Sisi ni wenye shangwe kuacha misaada hiyo bora ya kibiblia kwa watu wengi wanaopenda kwa unyofu kujua Mungu wa kweli, Yehova, na kumtumikia.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine