Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 1/97 uku. 8
  • Neno La Mungu Linatuongoza

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Neno La Mungu Linatuongoza
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Biblia: Kiongozi Kilichotolewa Na Mungu Kwa Watu Wote
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Utoaji Mbalimbali Uliopendekezwa kwa Ajili ya Utumishi wa Shambani
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Ujuzi Utokao Kwa Mungu Unajibu Kwa Maulizo Mengi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • “Hii Yamaanisha Uhai Udumuo Milele”
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 1/97 uku. 8

Neno La Mungu Linatuongoza

1 “Twaishi katika ulimwengu wenye matatizo mengi mno na majibu machache mno. Mamilioni wengi hukosa chakula kwa ukawaida. Hesabu zenye kuongezeka ni wazoevu wa dawa za kulevya. Familia zaidi na zaidi zinavunjika. Daima katika habari ni ngono ya watu wa ukoo na jeuri ya familia. Hewa tunayopumua na maji tunayokunywa vinatiwa sumu polepole. Wakati uo huo, zaidi na zaidi kati yetu wanaathiriwa na uhalifu.”

2 Ndivyo kinavyoanza kitabu Biblia​—Neno la Mungu au la Binadamu? Utangulizi wacho ni wa maana hata leo kama wakati kitabu hicho kilipochapishwa kumepita hivi miaka saba. Watu wanahitaji kujua kwamba Neno la Mungu linatuongoza na kwamba lina suluhisho kwa matatizo yetu yote yanayotusumbua. Mnamo Januari, tutajikaza kuwasaidia kwa kuwatolea Tafsiri ya Ulimwengu Mpya na kitabu Biblia​—Neno la Mungu au la Binadamu? Ni wazi kwamba jambo tu la kuacha kichapo kwa mtu halitoi uhakikisho wa kwamba atakubali uongozi wa kimungu. Imetupasa kurudi kuwaona watu tukiwa na kusudi la kuanzisha mafunzo ya Biblia. Tunao uhakika wa kwamba tutasaidiwa ikiwa tunafanya juhudi hiyo. (Mt. 28:​19, 20) Tazama vielelezo ambavyo tunakudokezea:

 3 Ikiwa tunakuta mtu mzee-mzee, tunaweza kujaribu utangulizi huu:

◼ “Je! ninaweza kukuuliza ulizo moja: Ulipokuwa bado kijana, watu walikuwa wakijiongoza namna gani wamoja kwa wengine? [Tuache mtu ajibu.] Hali ni tofauti sana leo, je! hauoni hivyo? Kwa maoni yako, kwa nini mambo yamebadilika? [Acha mtu ajibu.] Kwa kweli, tunaona utimizo wa unabii wa Biblia. [Tusome 2 Timotheo 3:​1-5.] Biblia hairidhiki tu na kuonyesha kwa usahihi ulimwengu kama ulivyo leo; inaahidi ulimwengu bora katika wakati ujao ulio karibu. Ni kwa sababu hiyo tunamtia kila mtu moyo kuisoma. Je! ulipata kutambua kwamba Biblia niliyotumia, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya, inatumia usemi ulio kamili?” Tuongeze kwamba imeaandikwa katika Kiswahili cha siku hizi, jambo ambalo linafanya maandishi yawe rahisi zaidi kueleweka. Tuonyeshe kitabu Biblia​—Neno la Mungu au la Binadamu? na tukazie sura ya 10, ambayo inaeleza kwa urefu unabii mwingine ambao tunaona utimizo. Tutolee Biblia na kitabu.

 4 Tunaporudi kumwona mtu mzee-mzee ambaye tuliachia Biblia na kitabu, tungeweza kusema:

◼ “Mara ya mwisho, tulikubaliana kwamba jamii ya leo imeharibika zaidi na zaidi katika hali nyingi mbalimbali, tunapochunguza maisha kama yalivyokuwa kumepita tu hivi miaka fulani. Hata hivyo, nimerudi tena ili kukuonyesha kwamba Biblia inaahidi ulimwengu bora zaidi kwa wakati ujao. [Tusome Ufunuo 21:​3, 4.] Jambo la kujua kwamba Neno la Mungu linasema hivyo lingepaswa kutusukuma kuangalia jambo la ziada lililo nalo tena la kututangazia.” Tufungue kitabu Neno la Mungu kwenye sura 14 na tusome mafungu 3-4. Tutolee funzo la Biblia la bure.

 5 Ikiwa tunaanzisha mazungumzo pamoja na kijana, tunaweza kusema:

◼ “Ningependa kukuuliza ulizo moja: Wewe ambaye ni kijana, je! unafikiri kwamba tunayo sababu ya kuona wakati ujao kwa matazamio mema? Jinsi gani unatazamia mambo? [Tumuache kijana ajibu.] Kwa furaha, tunayo sababu yenye nguvu ya kutazamia mambo mazuri. [Tusome Zaburi 37:​10, 11.] Kwa kuwa watu wana maoni yenye kutofautiana juu ya Biblia na mambo yaliyomo, tulichapa kitabu hiki, Biblia​—Neno la Mungu au la Binadamu? Angalia sababu zinazofanya kitabu hiki kitutie moyo kuisoma Biblia. [Kusoma mafungu 16-17, kur. 10-11.] Tangu wakati tunapokuwa hakika kwamba Biblia inasema kweli, tunafikia hivyo kuwa na tumaini lililo hakika kwa wakati ujao. Ikiwa ungependa kuisoma Biblia, ningefurahi kukuachia yenyewe kwa mchango mdogo.”

 6 Tunaporudi kumuona kijana aliyekubali kitabu “Neno la Mungu,” tunaweza kuanza kwa kusema:

◼ “Nilithamini kuona kwamba unashughulikia wakati ujao. Unakumbuka, nilikuonyesha andiko moja la Biblia ambalo linatuahidi wakati ujao wenye furaha na uliyo hakika. Tazama andiko lingine. [Tusome Ufunuo 21:​3, 4.] Kitabu nilichokuachia kinatoa shuhuda zenye kuaminika kwamba Biblia ni Neno la Mungu na si la mwanadamu. Jambo hilo ni la maana kubwa. Tuone jinsi hilo linavyomaanisha. [Tusome mafungu 1-2, uku. 184-5.] Ikiwa unataka hilo, ningefurahi kujifunza Biblia kwa bure pamoja nawe.” Ikiwa kijana anakubali funzo, tumuulize ikiwa ana Biblia. Ikiwa sivyo, tumtolee Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.

 7  Mtu ambaye hajui atageukia wapi kwa kupata msaada ili kushindana na magumu yake labda ataitikia hili:

◼ “Kwa wakati wetu, karibu kila mtu anapaswa kukabiliana na matatizo makubwa. Wengi wanawaendea washauri katika hali zote. Wamoja wanawaendea wafumu. Kwa maoni yako, wapi tunaweza kupata mashauri ambayo ni yenye manufaa kabisa kwetu? [Tuache mtu ajibu.] Biblia inaonyesha jambo lililo la maana ambalo kila mmoja anapaswa kutambua.” Tusome Yeremia 10:23. Tufungue kitabu Biblia​—Neno la Mungu au la Binadamu? kwenye ukurasa 187 na tusome fungu la 9. “Kitabu hiki kitakusaidia kuelewa jinsi magumu yetu yote yatatoeka kupitia Ufalme wa Mungu. Je! ungependa kulisoma?”

 8 Ikiwa wakati wa mazungumzo ya kwanza tulisema kwamba mwanadamu anahitaji kiongozi, wakati wa ziara ya kurudia, tunaweza kuendeleza mazungumzo kwa namna hii:

◼ “Mara ya mwisho, tulikubaliana kwa kusema tuna lazima ya uongozi wa Mungu ikiwa tunataka kuyashinda magumu ya maisha. Kwa habari hiyo, ninafikiri kwamba utathamini mashauri ya umalizio ambayo unaweza kusoma katika kitabu nilichokuachia. [Tusome mafungu 12-13, uku. 189 wa kitabu Neno la Mungu.] Ninafurahi kukutolea funzo la Biblia la nyumbani la bure na ningependa kukuonyesha tangu sasa jinsi linavyofanyika.”

 9 Yehova atabariki bidii ambayo tutafanya ili kuwasaidia vijana na watu wazee-wazee kutambua thamani ya Neno la Mungu, ambalo ni kiongozi katika maisha yetu.​—Zab. 119:105.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine