Waangalizi Wanaoongoza—Mwangalizi-msimamizi
1 Kuwa mwangalizi katika kutaniko ni daraka zito. (Mdo. 20:28; 1 Tim. 3:1) Hii ni ya kwanza ya mfululizo wa makala zitakazoonyesha madaraka mbalimbali ya wazee, ili kwamba kila mmoja wetu ajue kazi ya maana wanayofanya kwa ajili yetu.
2 Sosaiti huweka mwangalizi-msimamizi kwa wakati usiowekewa mipaka. Mwangalizi-msimamizi huratibu utendaji, jambo linalosaidia wazee watoe uangalifu unaohitajika kwa kazi wanazogawiwa. (Huduma Yetu, uku. 42) Hilo humaanisha nini?
3 Mwangalizi-msimamizi hupokea barua za kutaniko na huzitoa bila kukawia kwa mwandishi ili kuzishughulikia. Wakati wa kutayarisha mkutano wa wazee, mwangalizi-msimamizi huomba madokezo ya wazee wengine juu ya mambo yanayohitaji kuzungumziwa, kisha hupanga ajenda. Yeye ndiye husimamia vilevile mkutano wa wazee. Maamuzi yanapofanywa, anahakikisha kwamba hayo yanatimizwa kwa kufaa. Yeye analo daraka katika kutayarisha Mkutano wa Utumishi na programu ya hotuba za watu wote. Anatoa kibali kwa ajili ya matangazo yote yanayofanywa kwa kutaniko, anatoa ruhusa ya kulipia gharama za kawaida na anahakikisha kwamba uchunguzi wa baada ya miezi mitatu wa akaunti za kutaniko ufanywe.
4 Ndugu huyo ndiye mwenyekiti wa Halmashauri ya Utumishi cap: see Engl na yeye huratibu kazi ya halmashauri hiyo. Mwanafunzi wa Biblia anapoomba kuwa mhubiri asiyebatizwa au mhubiri asiyebatizwa anapoomba kubatizwa, mwangalizi-msimamizi hupanga kwamba wazee wakutane naye. Mwangalizi-msimamizi ndiye hupanga ziara ya mwangalizi wa mzunguko ili kwamba kutaniko lifaidike kikamili na juma la utendaji wa pekee.
5 Kazi za mwangalizi-msimamizi ni nyingi na za namna mbalimbali. Huku cfr Rjb anapozitimiza “katika bidii halisi” na kwa unyenyekevu, kila mmoja wetu aweza kutimiza fungu lake kwa kushirikiana na wazee. (Rom. 12:8) Ikiwa sisi ni “watiifu” na “wenye kunyenyekea” wale wanaoongoza miongoni mwetuEngl. OK, wao watafanya kazi yao kwa shangwe kubwa zaidi.—Ebr. 13:17.