Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwbr19 Mwezi wa 11 uku. 1-7
  • Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha (2019)
  • Vichwa Vidogo
  • TAREHE 4-10/11
  • TAREHE 11-17/11
  • TAREHE 18-24/11
  • TAREHE 25/11–1/12
Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha (2019)
mwbr19 Mwezi wa 11 uku. 1-7

Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha

TAREHE 4-10/11

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | 1 YOHANA 1-5

“Musipende Ulimwengu ao Vitu Vyenye Viko Katika Ulimwengu”

w05 1/1 uku. 10 fu. 13

Fuata Mufano Wenye Yesu Aliweka

13 Watu fulani wanaweza kuwaza kama haiko mambo yote yenye iko mu ulimwengu njo ya mubaya. Hata kama ni kweli, ulimwengu na vitu vyenye kupendeza vyenye kuwa ndani vinaweza kutukengeusha kwa vyepesi ili tuache kumutumikia Yehova. Na hakuna hata kitu moja chenye kuwa mu ulimwengu chenye kinaweza kutusaidia tumukaribie Mungu. Kwa hiyo, kama tunaanza kupenda sana vitu vyenye kuwa mu ulimwengu, hata vitu vyenye pengine haviko vya mubaya, tutakuwa mu hatari. (1 Timoteo 6:9, 10) Na tena, mambo mingi yenye kuwa mu ulimwengu ni ya mubaya na inaweza kutupotosha. Kama tunaangalia filme ao programu za televizyo zenye kuonyesha jeuri, kutafuta sana vitu vya kimwili, ao mambo ya uasherati, tunaweza kuanza kukubali ile mambo na kisha itatushawishi. Kama tunashirikiana na watu wenye wanahangaikia sana kufanya hali yao ya maisha ikuwe muzuri zaidi, ao wenye wanatafuta nafasi za kuanzisha biashara, ile mambo inaweza kuanza kuwa ya maana zaidi kwetu pia.​—Matayo 6:24; 1 Wakorinto 15:33.

w13 15/8 uku. 27 fu. 18

Tunapaswa Kuwa Watu wa Namna Gani

18 Jambo lingine linaloweza kutusaidia kupinga “vitu vilivyo katika ulimwengu” ni kuendelea kuweka katika akili maneno haya ya mutume Yohana: “Ulimwengu unapitilia mbali na pia tamaa yake, lakini yeye anayefanya mapenzi ya Mungu anadumu milele.” (1 Yoh. 2:17) Ulimwengu wa Shetani unaonekana kuwa hauwezi kuwa na mwisho. Lakini, siku moja ulimwengu huo utafikia mwisho wake. Kila kitu ambacho ulimwengu wa Shetani unaweza kututolea hakiwezi kudumu. Kukumbuka jambo hilo kutatusaidia tusidanganywe na vishawishi vya Ibilisi.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

w13 15/9 uku. 10 fu. 14

Vikumbusho vya Yehova Ni Vyenye Kutegemeka

14 Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo yanajaa vikumbusho kuhusu umaana wa kuonyeshana upendo. Yesu alisema kwamba amri ya pili iliyo kubwa zaidi ni ‘kumupenda jirani yako kama wewe mwenyewe.’ (Mt. 22:39) Vivyo hivyo, Yakobo, ndugu-nusu ya Yesu, aliuita upendo “sheria ya kifalme.” (Yak. 2:8) Mutume Yohana aliandika hivi: ‘Wapendwa, ninawaandikia ninyi, si amri mupya, bali amri ya zamani ambayo mumekuwa nayo tangu mwanzo.’ (1 Yoh. 2:7, 8) Yohana alikuwa akizungumuzia nini alipotumia maneno “amri ya zamani”? Alikuwa akizungumuzia amri hiyo ya upendo. Amri hiyo ilikuwa “ya zamani” katika maana ya kwamba Yesu alikuwa ameitoa “kutoka mwanzoni,” ni kusema, miaka mingi hapo mbele. Lakini pia amri hiyo ilikuwa ‘mupya’ katika maana ya kwamba wanafunzi walipaswa kuwa tayari kuwapenda wengine na hata kufikia kufa kwa ajili yao. Wanafunzi walipaswa kuonyesha roho hiyo ili kupambana na hali ambazo zingetokea baadaye. Kwa kuwa sisi ni wanafunzi wa Kristo, je, tunasamini mashauri yanayotusaidia tuepuke roho ya kujipenda wenyewe ambayo watu wengi katika ulimwengu wanaonyesha, na ambayo inaweza kupunguza upendo wetu kwa jirani?

it-2-F uku. 491 fu. 1

Musamaha

Ni muzuri kumuomba Yehova awasamehe watu wengine, tunaweza kufanya vile hata kwa ajili ya kutaniko lote. Musa alifanya vile kwa ajili ya taifa la Israeli, aliungama zambi za taifa lote na akaomba musamaha kwa ajili yao, na Mungu alimusikiliza. (Hes 14:19, 20) Wakati wa kumutolea Yehova hekalu, Sulemani pia alisali kwa Yehova na kumuomba asamehe watu wake wakati wangefanya zambi na kugeuka ili kuacha matendo yao ya mubaya. (1Fal 8:30, 33-40, 46-52) Ezra alikuwa musemaji wa Wayahudi wenye walirudia mu inchi yao na aliungama zambi zao mbele ya watu wote. Sala yake ya kutoka mu moyo na vitia-moyo vyake vilifanya watu watende kwa njia ya muzuri ili Yehova awasamehe. (Ezr 9:13–10:4, 10-19, 44) Yakobo alitia moyo mutu mwenye kuwa mugonjwa kiroho aite wazee wa kutaniko ili wasali kwa ajili yake, na “kama amefanya zambi, atasamehewa.” (Yak 5:14-16) Lakini, kuko “zambi yenye inaleta kifo,” zambi yenye mutu anatendea roho takatifu, ni kusema, kuzoea kutenda zambi kimakusudi; wenye kufanya vile hawawezi kusamehewa. Mukristo hapaswe kusali kwa ajili ya watu wenye kufanya zambi za vile.​—1Yo 5:16; Mt 12:31; Ebr 10:26, 27; ona ZAMBI, I; ROHO.

Hotuba

w04 1/10 uku. 29

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Wakati mutume Yohana aliandika kama “upendo mukamilifu unatupa woga inje,” alimaanisha nini kwa kusema “upendo mukamilifu,” na ni “woga” gani unatupwa inje?

Mutume Yohana aliandika kama “hakuna woga katika upendo, lakini upendo mukamilifu unatupa woga inje, kwa sababu woga unatuzuia. Kwa kweli, mutu mwenye kuwa na woga hajakamilishwa katika upendo.”​—1 Yohana 4:18.

Maneno yenye kutangulia inaonyesha kama Yohana alikuwa anazungumzia uhuru wa kusema, zaidi sana kuhusu uhusiano wenye kuwa kati ya kumupenda Mungu na uhuru wa kusema naye. Tunaweza kuona jambo hilo mu mustari wa 17: “Kwa njia hii upendo umekamilishwa ndani yetu, ili tukuwe na uhuru wa kusema katika siku ya hukumu.” Kuwa na uhuru wa kusema ao kukosa uhuru wa kusema, kunategemea namna Mukristo anamupenda Mungu na namna anajisikia kuwa Mungu anamupenda.

Maneno “upendo mukamilifu” iko na maana. Kama vile neno “kamilifu” linazoea kutumiwa katika Biblia, halimaanishe tu ukamilifu katika maana yake kamili, ni kusema, kitu chenye hakina kasoro, lakini mara mingi linamaanisha ukamilifu kwa kadiri fulani. Kwa mufano, katika Mahubiri yake ya Mulimani, Yesu alisema: “Lazima mukuwe wakamilifu, kama vile Baba yenu wa mbinguni ni mukamilifu.” Yesu alikuwa anawaambia wafuasi wake kama ikiwa wangependa tu wale wenye kuwapenda, basi upendo wao haungekuwa kamili, ungekuwa na kasoro. Walipaswa kufanya upendo wao ukuwe kamili kwa kuwapenda hata maadui wao. Vilevile, wakati Yohana aliandika kuhusu “upendo mukamilifu,” alikuwa anazungumuza kuhusu upendo kwa Mungu wenye kuwa wa moyo wote, wenye kukomaa, na wenye kuonekana katika sehemu zote za maisha ya mutu.​—Matayo 5:46-48; 19:20, 21.

Wakati Mukristo anasali kwa Mungu, anajua muzuri kama yeye ni mwenye zambi na haiko mukamilifu. Lakini, kama anamupenda Mungu kabisa na anajisikia kama Mungu anamupenda kabisa, hajizuie kusali kwa kuogopa kama Mungu atamuhukumu ao kumukataa. Kuliko kufanya vile, anafurahia uhuru wa kusema wakati anaeleza mambo yenye kuwa mu moyo wake na wakati anaomba musamaha kwa musingi wa zabihu ya bei ya ukombozi yenye Mungu ametayarisha kwa upendo kupitia Yesu Kristo. Iko hakika kama Mungu anasikiliza na kukubali maombi yake.

Namna gani mutu anaweza ‘kukamilishwa katika upendo’ mupaka afikie ‘kutupa inje’ woga wa kuhukumiwa ao kukataliwa? Mutume Yohana alisema hivi: “Yeyote mwenye anashika neno lake, kwa kweli upendo wa Mungu umekamilishwa.” (1 Yohana 2:5) Waza kidogo: Kama Mungu alitupenda wakati tulikuwa tungali watenda zambi, je, hatatupenda hata zaidi kama tunatubu kikweli na ‘kushika neno lake’ kwa bidii? (Waroma 5:8; 1 Yohana 4:10) Kwa kweli, kama tunaendelea kuwa waaminifu, tunaweza kuwa na uhakika uleule wenye mutume Paulo alikuwa nao wakati alisema hivi juu ya Mungu: “Hakujizuia kutoa hata Mwana wake mwenyewe lakini alimutoa kwa ajili yetu sisi wote, je, hatatupatia pia pamoja naye vitu vingine vyote kwa fazili?”​—Waroma 8:32.

TAREHE 11-17/11

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | 2 YOHANA 1–YUDA

“Tunapaswa Kupigana ili Kubakia Katika Kweli”

w04 15/9 uku. 11-12 fu. 8-9

“Muendelee Kujipatia Nguvu Katika Bwana”

8 Tunajua njia za ujanja za Shetani kwa sababu Maandiko inafunua njia za ujanja zenye anazoea kutumia. (2 Wakorinto 2:11) Ili kumujaribu Yobu, mwanaume mwenye haki, Ibilisi alifanya apoteze mali yake yote, aliua wapendwa wake, alitumia upinzani wa familia, alimuletea mateso ya kimwili, na alifanya marafiki wake wa uongo wamuchambue bila haki. Yobu alivunjika moyo na alijisikia kwamba Mungu alikuwa amemuacha. (Yobu 10:1, 2) Hata kama leo pengine Shetani hataleta ile mateso moja kwa moja, magumu kama ile inapataka Wakristo wengi, na Ibilisi anaweza kuitumia ili kuwajaribu.

9 Hatari za kiroho zimeongezeka sana katika wakati huu wa mwisho. Mu ulimwengu wenye tunaishi ndani watu wanaendelea kutafuta zaidi vitu vya kimwili kuliko kuwa na miradi ya kiroho. Mara mingi vyombo vya kutoa habari vinaonyesha ngono yenye haifae kuwa jambo lenye kufurahisha kuliko kuumiza. Na watu mingi wamekuwa “wenye kupenda raha kuliko kumupenda Mungu.” (2 Timoteo 3:1-5) Kuwaza vile kunaweza kufanya usawaziko wetu wa kiroho ukuwe mu hatari kama ‘hatupiganie kabisa imani.’​—Yuda 3.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

it-1-F uku. 879

Karamu za Kuonyesha Upendo

Biblia haitoe mafasirio juu ya zile karamu za kuonyesha upendo na haionyeshe zilikuwa zinafanywa mara ngapi. (Yud 12) Kwa sababu Bwana Yesu Kristo ao mitume wake hawakuomba Wakristo wafanye zile karamu, ni wazi kama hatulazimike kuzifanya ao kuona kama zilipaswa kuendelea mupaka leo. Watu fulani wanasema kama zile karamu zilitolea Wakristo wenye walikuwa matajiri nafasi ya kualika waamini wenzao wenye walikuwa maskini. Watoto wenye hawakukuwa na baba, wajane, matajiri, na wale wenye hawakukuwa na feza mingi, walichangia pamoja chakula ya mingi kama ndugu na dada.

it-2-F uku. 805 fu. 3

Mwamba

Kwa kweli, neno lingine la Kigiriki, spi·lasʹ, linamaanisha mwamba ao miamba yenye kujificha ndani ya maji. Yuda anatumia neno hilo ili kuzungumuzia watu fulani wenye walikuwa wamejiingiza katika kutaniko la Kikristo wakiwa na nia za mubaya. Kama vile miamba yenye kuwa chini ya maji ilikuwa hatari kwa ajili ya mashua, wale watu walikuwa hatari kabisa kwa wengine katika kutaniko. Anasema hivi juu ya wale watu: “Watu hao ni miamba yenye kufichwa chini ya maji kwenye karamu zenu za kuonyesha upendo wakati wanakula pamoja na ninyi.”​—Yud 12.

wp17.1 uku. 12 fu. 1

“Alimupendeza Mungu Vema”

Enoko alitoa unabii gani? Unabii huo unasema hivi: ‘Tazama! Yehova alikuja pamoja na watakatifu wake makumi ya maelfu, ili kufanya hukumu juu ya wote, na kuwasibitisha kuwa ni wenye hatia wote wasiomuogopa Mungu kuhusu matendo yao yote ya kutomuogopa Mungu ambayo walitenda kwa njia ya kutomuogopa Mungu, na kuhusu mambo yote ya kushtua ambayo watenda-zambi wasiomuogopa Mungu walisema juu yake.’ (Yuda 14, 15) Jambo la kwanza unaweza kuona ni hili: Enoko alitumia maneno yenye kuonyesha wakati uliopita, ni kama vile Mungu alikuwa amekwisha kutimiza unabii huo. Unabii mwingi wenye ulifuata uliandikwa hivyo. Wazo kubwa ni hili: Nabii anazungumuzia jambo lenye iko hakika kwamba litatokea, kwa hiyo, jambo hilo linaweza kuzungumuziwa kwa njia yenye kuonyesha kama limekwisha kutokea!​—Isaya 46:10.

wp17.1 uku. 12 fu. 3

“Alimupendeza Mungu Vema”

Imani ya Enoko inaweza kutuchochea kujiuliza ikiwa mawazo yetu juu ya ulimwengu huu yanapatana na mawazo ya Mungu. Hukumu yenye Enoko alitangaza bila woga wakati wake inahusu pia ulimwengu wa leo. Kama vile unabii wa Enoko ulisema, Yehova alileta Garika kubwa juu ya ulimwengu wa wakati wa Noa wenye ulikuwa na watu wenye hawamuogope Mungu. Hilo linaonyesha uharibifu mukubwa zaidi wenye utatokea karibuni. (Mathayo 24:38, 39; 2 Petro 2:4-6) Kama wakati huo, leo Mungu pamoja na malaika wake wengi wako tayari kuleta hukumu ya haki juu ya ulimwengu huu wenye haumuogope Mungu. Kila mumoja wetu anapaswa kukamata kwa uzito angalisho lenye Enoko alitoa na kulitangazia wengine. Watu wa familia yetu na marafiki wanaweza kuwa na musimamo wenye kuwa tofauti na wetu. Wakati fulani tunaweza kuona kama tuko peke yetu. Lakini Yehova hakumuacha Enoko; hataacha pia watumishi wake waaminifu leo!

TAREHE 18-24/11

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | UFUNUO 1-3

“Ninajua Matendo Yako”

w12 15/10 uku. 14 fu. 8

Ni Roho ya Aina Gani Unayoonyesha?

8 Ili kuepuka roho hiyo, tunapaswa kukumbuka kama Biblia inazungumuzia Yesu akiwa na ‘nyota saba’ katika mukono wake wa kuume. “Nyota” hizo zinafananisha wazee watiwa-mafuta kutia ndani wazee wengine wote katika makutaniko. Yesu anaweza kuongoza “nyota” zilizo katika mukono wake kadiri anavyopenda. (Ufu. 1:16, 20) Kwa hiyo, Yesu Kristo, aliye Kichwa cha kutaniko, anaongoza mabaraza yote ya wazee. Ikiwa muzee fulani anahitaji kukaripiwa, Yule aliye na “macho kama mwali wa moto” atashugulikia jambo hilo kwa wakati na kwa namna inayofaa. (Ufu. 1:14) Tunapongojea jambo hilo lishugulikiwe, tuendelee kuwaheshimu kabisa wale waliowekwa na roho takatifu kwa sababu Paulo aliandika hivi: ‘Watiini wale wanaoongoza katikati yenu na munyenyekee, kwa maana wanaendelea kuzilinda nafsi zenu kama wale watakaotoa hesabu; ili wafanye hivyo kwa shangwe na si kwa kuugua, kwa maana kufanya hivyo kungewazuru ninyi.’​—Ebr. 13:17.

w12 15/4 uku. 29 fu. 11

Yehova Anatulinda Ili Tupate Wokovu

11 Katika maono yaliyoandikwa katika Ufunuo sura ya 2 na ya 3, Yesu Kristo aliyetukuzwa anachunguza makutaniko saba ya Asia Ndogo. Maono hayo yanaonyesha kama Kristo anaona sifa za kila kutaniko lakini pia anaona hali moja moja katika kila kutaniko. Kwa mufano, anataja majina fulani, anataja kila jambo linalofanyika, na anapongeza na kutoa shauri kulingana na hali. Hilo linaonyesha nini? Makutaniko hayo saba yanafananisha Wakristo watiwa-mafuta kisha mwaka wa 1914, na mashauri aliyotolea makutaniko hayo saba ni kwa faida ya makutaniko yote ya watu wa Mungu duniani leo. Jambo hilo linaonyesha wazi kabisa kama Yehova anaongoza watu wake kupitia Mwana wake. Namna gani tunaweza kufaidika na mwongozo huo?

w01 15/1 uku. 20-21 fu. 20

Tembea Pamoja na Tengenezo la Yehova

20 Ili kutembea pamoja na tengenezo la Yehova lenye kusonga mbele hatua kwa hatua tunapaswa kutambua mugao wenye Mungu amepatia Yesu Kristo wa kuwa “kichwa cha kutaniko.” (Waefeso 5:22, 23) Mambo yenye tunaambiwa mu Isaya 55:4, ni ya lazima pia: “Angalia! Nilimufanya kuwa shahidi kwa mataifa, Kiongozi na kamanda kwa mataifa.” Kwa kweli, Yesu ni Kiongozi muzuri sana. Anajua pia kondoo wake na matendo yao. Kwa kweli, wakati alichunguza makutaniko saba katika Asia Ndogo, alisema hivi mara tano: “Ninajua matendo yako.” (Ufunuo 2:2, 19; 3:1, 8, 15) Yesu pia anajua kile chenye tuko nacho lazima, kama vile Baba yake, Yehova. Mbele ya kutoa Sala ya Mufano, Yesu alisema hivi: “Baba yenu anajua kile chenye muko nacho lazima hata mbele mumuombe.”​—Matayo 6:8-13.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

kr uku. 226 fu. 10

Ufalme wa Mungu Unaondoa Maadui Wake

10 Kutoa hukumu. Maadui wote wa Ufalme wa Mungu watalazimika kujionea tukio ambalo litaongeza maumivu yao. Kuhusu jambo hilo Yesu alisema hivi: ‘Watamuona Mwana wa binadamu akija katika mawingu akiwa na nguvu nyingi na utukufu.’ (Mk. 13:26) Tukio hilo la ajabu na lisilo la kawaida litaonyesha kwamba Yesu amekuja kuhukumu. Katika sehemu nyingine ya unabii huo wa Yesu kuhusu siku za mwisho, Yesu anatoa habari zaidi kuhusu hukumu ambayo itatolewa wakati huo. Habari hiyo inapatikana katika mufano wa kondoo na mbuzi. (Soma Mathayo 25:31-33, 46.) Wale ambao wanaunga mukono Ufalme wa Mungu kwa ushikamanifu watahukumiwa na kuonwa kama “Kondoo” na ‘watainua vichwa vyao,’ kwa sababu wakati huo watatambua kwamba ‘ukombozi wao unakaribia.’ (Lu. 21:28) Lakini, maadui wa Ufalme watahukumiwa na kuonwa kama “mbuzi,” na ‘watajipiga-piga wenyewe kwa kuomboleza’ kwa sababu wakati huo watatambua kwamba ‘watakatiliwa mbali milele.’​—Mt. 24:30; Ufu. 1:7.

w09 15/1 uku. 31 fu. 1

Mambo Makubwa Katika Kitabu cha Ufunuo​—I

2:7​—“Paradiso ya Mungu” ni nini? Kwa sababu ni Wakristo watiwa-mafuta njo wanaambiwa ile maneno, hapa neno paradiso inahusu paradiso ya mbinguni, fasi kabisa kwenye Mungu anakuwaka. Watiwa-mafuta waaminifu watapokea sawabu ya kula “matunda ya ule muti wa uzima.” Watapokea kutokufa.​—1 Ko. 15:53.

TAREHE 25/11–1/12

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | UFUNUO 4-6

“Wale Wenye Kupanda Farasi Ine”

wp17.3 uku. 4 fu. 3

Wale Wapanda-Farasi Ine​—Ni Nani?

Mwendeshaji wa farasi mweupe ni nani? Mambo yenye kutusaidia kumutambua yanapatikana katika kitabu hicho cha Ufunuo, chenye baadaye kinaita mupanda-farasi huyo wa mbinguni “Neno la Mungu.” (Ufunuo 19:11-13) Jina la cheo Neno, limepewa Yesu Kristo, kwa sababu anatenda kama musemaji wa Mungu. (Yohana 1:1, 14) Zaidi ya hilo, anaitwa ‘Mufalme wa wafalme na Bwana wa mabwana’ na anaitwa pia “Mwaminifu na wa Kweli.” (Ufunuo 19:16) Ni wazi kwamba, iko na mamlaka ya kutenda kama mufalme-shujaa, na hatumie mubaya mamlaka yake. Hata hivyo, maulizo fulani yanatokea.

wp17.3 uku. 4 fu. 5

Wale Wapanda-Farasi Ine​—Ni Nani?

Ni wakati gani wapanda-farasi hao walianza mwendo wao? Biblia inaonyesha kwamba Yesu, mupanda-farasi wa kwanza, alianza mwendo wake kisha kupewa taji. (Ufunuo 6:2) Ni wakati gani Yesu alivalishwa taji ili kuwa Mufalme huko mbinguni? Haikuwa wakati alirudi mbinguni kisha kifo chake. Biblia inaonyesha kwamba kipindi cha kungojea kilianza wakati huo. (Waebrania 10:12, 13) Yesu alipatia wanafunzi wake alama yenye ingewasaidia kujua mwisho wa kipindi hicho cha kungojea na mwanzo wa utawala wake huko mbinguni. Alisema kwamba wakati angeanza kutawala, hali ya ulimwengu ingeharibika sana. Kungekuwa vita, upungufu wa chakula, na magonjwa ya kuambukiza. (Mathayo 24:3, 7; Luka 21:10, 11) Kisha tu kutokea kwa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu katika mwaka wa 1914, ilionekana wazi kwamba wanadamu waliingia katika kipindi hicho cha muvurugo chenye Biblia inaita “siku za mwisho.”​—2 Timotheo 3:1-5.

wp17.3 uku. 5 fu. 2

Wale Wapanda-Farasi Ine​—Ni Nani?

Mupanda-farasi huyo anafananisha vita. Ona kwamba mupanda-farasi huyo haondoe amani katika mataifa fulani tu, lakini katika dunia yote. Katika 1914, kwa mara ya kwanza katika historia ya wanadamu, vita ilitokea katika dunia yote. Kisha, kulitokea vita ya pili ya ulimwengu yenye iliua watu wengi zaidi. Watu fulani wanakadiria kwamba hesabu ya watu wenye walikufa kwa sababu ya vita na mapambano ya watu wenye kutumia silaha tangu mwaka wa 1914 ilikuwa zaidi ya milioni 100! Tena, watu wengine wengi waliteseka kwa sababu ya matatizo makali.

wp17.3 uku. 5 fu. 4-5

Wale Wapanda-Farasi Ine​—Ni Nani?

“Nikaona, na, tazama! farasi mweusi; na yeye anayeketi juu yake alikuwa na mizani mukononi mwake. Nami nikasikia sauti kana kwamba ni katikati ya wale viumbe hai wanne ikisema: ‘Kibaba cha ngano kwa dinari moja, na vibaba vitatu vya shayiri kwa dinari moja; wala usizuru mafuta ya zeituni na divai.’”​—Ufunuo 6:5, 6.

Mupanda-farasi huyo anafananisha njaa. Tunaona kwamba kupata chakula kungekuwa nguvu sana hivi kwamba kibaba kimoja (litre 1,08) cha ngano kingekuwa na bei ya dinari moja, mushahara wa siku nzima ya mufanyakazi wakati huo! (Mathayo 20:2) Dinari hiyo moja ingetumiwa pia ili kuuza vibaba vitatu (litre 3,24) vya shayiri, yenye ilionwa kuwa ya hali ya chini kuliko ngano. Namna gani familia kubwa ingeweza kupata chakula cha kutosha katika hali hiyo? Watu wanashauriwa wasitumie ovyoovyo hata chakula kwa ajili ya siku. Jambo hilo linaonyeshwa wazi kupitia kilimo na chakula cha musingi cha wakati huo kama vile mafuta ya zeituni na muvinyo.

wp17.3 uku. 5 fu. 8-10

Wale Wapanda-Farasi Ine​—Ni Nani?

Mupanda-farasi wa ine anafananisha kifo chenye kinatokana na pigo na mambo mengine. Kisha tu 1914, homa ya Hispania iliua mamilioni ya watu. Inawezekana watu milioni 500 waliambukizwa, ni kusema, karibu mutu mumoja kati ya watu watatu duniani!

Lakini, homa ya Hispania ilikuwa mwanzo tu. Wachunguzi wanakadiria kwamba zaidi ya milioni 300 ya watu walikufa kwa sababu ya ugonjwa wa ndui (variole) katika kipindi cha kuanzia 1901 mupaka 2000. Mupaka leo, mamilioni ya watu wanakufa kwa sababu ya UKIMWI, kifua kikuu na malaria hata kama kumekuwa maendeleo mengi katika mambo ya kinganga.

Matokeo ni yaleyale, watu wanaendelea kufa, ikuwe kwa sababu ya vita, njaa, ao magonjwa. Kaburi linaendelea kukusanya watu, bila kutoa tumaini lolote.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

re uku. 77 fu. 8

Uzuri Mwingi Sana wa Kiti cha Ufalme cha Yehova cha Mbinguni

8 Yohana alijua kama makuhani waliwekwa ili watumikie katika tabenakulo ya zamani. Kwa hiyo, inawezekana alishangaa wakati aliona mambo yenye anaeleza sasa: “Kuzunguka kile kiti cha ufalme kulikuwa viti vya ufalme makumi mbili na ine (24), na kwenye vile viti vya ufalme niliona wazee makumi mbili na ine wamekaa wakiwa wamevaa nguo nyeupe, na juu ya vichwa vyao kulikuwa mataji ya zahabu.” (Ufunuo 4:4) Ndiyo, kuliko kukuwe makuhani, kuko njo wazee 24, wenye wamewekwa katika viti vya ufalme na kuvalishwa mataji kama wafalme. Wale wazee ni nani? Ni watiwa-mafuta wa kutaniko la Kikristo, wenye wamefufuliwa na kupewa cheo cha mbinguni chenye Yehova aliwaahidi. Namna gani tunajua vile?

re uku. 80 fu. 19

Uzuri Mwingi Sana wa Kiti cha Ufalme cha Yehova cha Mbinguni

19 Wale viumbe wanafananisha nini? Maono yenye Ezekieli, nabii mwingine, aliona inatusaidia kupata jibu. Ezekieli alimuona Yehova amekaa kwenye kiti cha ufalme katika gari la mbinguni, lenye lilikuwa linasindikizwa na viumbe wenye uzima wenye walikuwa na miili yenye kufanana na ile yenye Yohana alieleza. (Ezekieli 1:5-11, 22-28) Kisha, Ezekieli aliona tena lile gari la mbinguni linasindikizwa na wale viumbe wenye uzima. Lakini, wakati huu anaita wale viumbe wenye uzima kuwa makerubi. (Ezekieli 10:9-15) Wale viumbe ine wenye uzima wenye Yohana anaona wanapaswa kuwa wanawakilisha makerubi wengi wa Mungu, ni kusema, viumbe wa cheo cha juu katika tengenezo Lake la kiroho. Yohana hangewaza kama ni jambo lenye haliko la kawaida kuona makerubi wanakaa karibu sana na Yehova, kwa sababu katika mupango wa tabenakulo ya zamani, kulikuwa makerubi wawili wa zahabu juu ya kifuniko cha sanduku la agano, lenye liliwakilisha kiti cha ufalme cha Yehova. Kutoka katikati ya wale makerubi, sauti ya Yehova ilikuwa inatolea taifa amri.​—Kutoka 25:22; Zaburi 80:1

cf uku. 36 fu. 5-6

“Angalia! Simba wa Kabila la Yuda”

5 Mara mingi simba anafananisha uhodari. Ulishaka ona simba-dume mwenye kukomaa uso kwa uso? Kama ulishaka kumuona, inawezekana kabisa alikuwa amefungiwa katika nafasi ya kuchungia wanyama. Lakini, hata kama ni mwenye kufungiwa anaweza tu kuogopesha. Wakati munaangaliana uso kwa uso na ule munyama mukubwa na mwenye nguvu, utaona kama haogope kitu. Biblia inasema kama “Simba, [ni] munyama mwenye nguvu zaidi kuliko wanyama wote, mwenye hamukimbie mutu yeyote.” (Mezali 30:30) Kristo iko na uhodari kama huo.

6 Tuzungumuzie sasa namna Yesu alionyesha uhodari kama wa simba katika njia tatu: kutetea kweli, kutegemeza haki, na kupambana na upinzani. Tena, tutaona kama sisi wote, ikuwe tulizaliwa na uhodari ao hapana, tunaweza kumuiga Yesu katika kuonyesha uhodari.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine