Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
TAREHE 3-9/05
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | HESABU 27-29
“Umuige Yehova kwa Kuepuka Ubaguzi”
Tupendezwe Sana na Sifa za Yehova
14 Binti hao watano walimukaribia Musa na kumuuliza hivi: “Kwa nini jina la baba yetu liondolewe kutoka katikati ya familia yake kwa sababu hakuwa na mwana [mutoto mwanaume]?” Na walimusihi hivi: “Tupe miliki katikati ya ndugu za baba yetu.” Je, Musa aliwajibu hivi: ‘Sheria imesema, sina jambo lingine la kufanya’? Hapana, ‘aliweka kesi yao mbele za Yehova.’ (Hes. 27:2-5) Yehova alimujibu namna gani? Yehova alimuambia Musa hivi: ‘Binti za Selofehadi wanasema jambo lililo sawa. Wape miliki ya uriti katikati ya ndugu za baba yao, nawe utaupitisha uriti wa baba yao kwao.’ Yehova hakusimamia hapo. Alimuagiza Musa aongeze maneno haya katika Sheria: ‘Ikiwa mutu yeyote atakufa bila kuwa na mwana, mutaupitisha uriti wake kwa binti yake.’ (Hes. 27:6-8; Yos. 17:1-6) Kuanzia wakati huo na kuendelea, wanawake wote Waisraeli ambao wangepatwa na tatizo hilo wangepaswa kutendewa kama binti za Selofehadi.
Tupendezwe Sana na Sifa za Yehova
15 Huo ulikuwa uamuzi muzuri na usio na ubaguzi kabisa. Yehova aliwatendea kwa heshima binti hao ambao hawakuwa na mutu wa kuwasemea kama vile alivyowatendea Waisraeli wote. (Zab. 68:5) Habari hii ni moja ya masimulizi mengi ya Biblia yanayotufundisha jambo hili lenye kuchangamusha moyo: Yehova anawatendea watumishi wake wote bila ubaguzi.—1 Sam. 16:1-13; Mdo. 10:30-35, 44-48.
Tupendezwe Sana na Sifa za Yehova
16 Namna gani tunaweza kumuiga Yehova? Kumbuka kwamba tutatendea wengine bila ubaguzi ikiwa tu tunaamini katika moyo wetu kwamba kila mutu anastahili kutendewa kwa haki. Kwa kweli, sisi wote tunafikiri kwamba tuna maoni yanayofaa juu ya watu wengine na kwamba hatuna ubaguzi. Lakini, labda utakubali kwamba si rahisi siku zote kujijua vizuri. Kwa hiyo, tunaweza kufanya nini ili kujua kwamba hatuna ubaguzi? Yesu alipotaka kujua maoni ambayo watu walikuwa nayo kumuhusu, aliwauliza hivi rafiki zake wenye kutumainika: “Watu wanasema Mwana wa binadamu ni nani?” (Mt. 16:13, 14) Je, hauwezi kufanya kama Yesu? Unaweza kumuuliza rafiki yako ambaye hawezi kukuficha jambo lolote ili akuambie ikiwa wewe una ubaguzi ao hapana. Utafanya nini ikiwa anakuambia kwamba wewe una muelekeo wa kupendelea tu watu wa rangi, jamii fulani, ao walio na feza? Sali Yehova kwa bidii kuhusu hali yako, umulilie akusaidie kubadili muelekeo wako ili uachane kabisa na tabia ya kuwabagua wengine.—Mt. 7:7; Kol. 3:10, 11.
Mali ya Kiroho
it-2-F uku. 850 fu. 1
Matoleo
Matoleo ya kinywaji. Waisraeli walikuwa wanatoa matoleo ya kinywaji pamoja na matoleo ingine, zaidi sana wakati walifika mu Inchi ya Ahadi. (Hes 15:2, 5, 8-10) Matoleo ya kinywaji ilikuwa divai (“pombe”) na ilimwangwa ku mazabahu. (Hes 28:7, 14; linganisha na Kut 30:9; Hes 15:10.) Mutume Paulo aliandikia hivi Wakristo wenye waliishi Filipi: “Kama ninamwangwa kama toleo la kinywaji juu ya zabihu na utumishi mutakatifu kwenye imani yenu imewaongoza, ninafurahi.” Hapa, mutume Paulo anatumia maneno toleo la kinywaji juu ya kuonyesha namna anapenda kujitolea kwa ajili ya Wakristo wenzake. (Flp 2:17) Wakati kidogo mbele akufe, alimuandikia hivi Timoteo: “Mimi tayari ninamwangwa kama toleo la kinywaji, na wakati wangu wa kufunguliwa umekaribia sana.”—2Ti 4:6.
Hotuba
w07-SW 1/4 uku. 17-18
“UHAI ulitokana na kifo, ndivyo walivyoamini Waazteki ambao waliwadhabihu wanadamu kwa kiwango kisicho na kifani huko Mesoamerika,” kinasema kitabu kimoja (The Mighty Aztecs). Kitabu hicho kinaendelea kusema hivi: “Kadiri milki hiyo ilivyopanuka, ndivyo wanadamu wengi zaidi walivyotolewa dhabihu ili kujenga imani katika milki hiyo.” Kitabu kingine kinasema kwamba Waazteki waliwadhabihu wanadamu 20 000 kwa mwaka.
Katika historia yote, wanadamu wametoa dhabihu tofauti-tofauti kwa miungu yao labda kwa sababu ya woga na wasiwasi au kwa sababu ya hatia na majuto. Kwa upande mwingine, Biblia inaonyesha kwamba dhabihu fulani zilianzishwa na Mungu mweza-yote, Yehova. Kwa hiyo, inafaa kuuliza hivi: Ni dhabihu gani zinazompendeza Mungu? Na je, matoleo na dhabihu zinapaswa kuwa sehemu ya ibada leo?
Matoleo na Dhabihu Katika Ibada ya Kweli
Taifa la Israeli lilipoanzishwa, Yehova alitoa maagizo yaliyo wazi kuhusu njia ambayo alitaka Waisraeli watumie kumwabudu, na ilitia ndani dhabihu na matoleo. (Hesabu, sura ya 28 na 29) Matoleo fulani yalikuwa mazao ya nchi; mengine yalihusu kudhabihu wanyama kama vile, ng’ombe-dume, kondoo, mbuzi, hua, na njiwa-tetere. (Mambo ya Walawi 1:3, 5, 10, 14; 23:10-18; Hesabu 15:1-7; 28:7) Kulikuwa na matoleo mazima ya kuteketezwa ambayo yalipasa kuteketezwa kabisa katika moto. (Kutoka 29:38-42) Kulikuwa pia na dhabihu za ushirika. Wale waliotoa dhabihu hizo walishiriki kwa kula kutokana na kile kilichotolewa dhabihu kwa Mungu.—Mambo ya Walawi 19:5-8.
Matoleo na dhabihu zote ambazo zilitolewa kwa Mungu chini ya Sheria ya Musa zilikuwa njia ya kumwabudu Mungu na kumtambua kuwa Mwenye Enzi Kuu ya ulimwengu wote. Kupitia dhabihu hizo, Waisraeli walionyesha shukrani zao kwa Yehova kwa sababu ya kuwabariki na kuwalinda, na pia walisamehewa dhambi zao. Walibarikiwa sana kadiri walivyoendelea kufuata kwa uaminifu matakwa ya Yehova ya ibada.—Methali 3:9, 10.
Jambo muhimu zaidi kwa Yehova lilikuwa mtazamo wa wale waliotoa dhabihu. Kupitia nabii wake Hosea, Yehova alisema hivi: “Mimi ninapendezwa na fadhili zenye upendo, na si dhabihu; ninapendezwa na kumjua Mungu kuliko matoleo mazima ya kuteketezwa.” (Hosea 6:6) Kwa hiyo, watu walipoacha ibada ya kweli na kuwa na mwenendo mpotovu na kumwaga damu isiyo na hatia, dhabihu ambazo walikuwa wakitoa kwenye madhabahu ya Yehova hazikuwa na thamani yoyote. Ndiyo sababu Yehova aliliambia hivi taifa la Israeli kupitia Isaya: “Dhabihu zenu nyingi zina faida gani kwangu? . . . Nimetosheka na matoleo mazima ya kuteketezwa ya kondoo-dume na mafuta ya wanyama waliolishwa vizuri; nami sikupendezwa na damu ya ng’ombe-dume wachanga na wana-kondoo na mbuzi-dume.”—Isaya 1:11.
“Jambo Ambalo Sikuamuru”
Tofauti kabisa na Waisraeli, wakaaji wa Kanaani waliwatoa watoto wao kuwa dhabihu kwa miungu yao, kutia ndani mungu wa Waamoni aliyeitwa Moleki, pia aliitwa Milkomu au Moloki. (1 Wafalme 11:5, 7, 33; Matendo 7:43) Kitabu kimoja (Halley’s Bible Handbook) kinasema: “Wakanaani walikuwa na desturi ya kidini ya kuabudu kwa kujihusisha na ukosefu wa adili katika ngono mbele za miungu yao; kisha, waliwaua na kuwatoa watoto wao wazaliwa wa kwanza kuwa dhabihu kwa miungu hiyo.”
Je, mazoea hayo yalimpendeza Yehova Mungu? Bila shaka hapana. Waisraeli walipokuwa karibu kuingia katika nchi ya Kanaani, Yehova aliwapa amri iliyoandikwa katika andiko la Mambo ya Walawi 20:2, 3: “Utawaambia wana wa Israeli, ‘Mtu yeyote wa wana wa Israeli, na mkaaji mgeni yeyote anayekaa akiwa mgeni katika Israeli, anayempa Moleki yeyote kati ya uzao wake, lazima auawe. Watu wa nchi watampiga kwa mawe mpaka afe. Mimi nami, nitauweka uso wangu juu ya mtu huyo, nami nitamkatilia mbali kutoka katikati ya watu wake, kwa sababu amempa Moleki baadhi ya uzao wake kwa kusudi la kupatia unajisi mahali pangu patakatifu na kulitia unajisi jina langu takatifu.’”
Ingawa huenda likaonekana kuwa jambo lisiloaminika, Waisraeli fulani walioacha ibada ya kweli walifuata zoea hilo lililoongozwa na roho waovu la kuwadhabihu watoto wao kwa miungu ya uwongo. Kuhusu hilo, Zaburi 106:35-38 inasema hivi: “Wakachangamana na hayo mataifa na kuanza kujifunza matendo yao. Nao waliendelea kutumikia sanamu zao, nazo zikawa mtego kwao. Nao wakawa wakiwatoa dhabihu wana wao na binti zao kwa roho waovu. Kwa hiyo wakaendelea kumwaga damu isiyo na hatia, damu ya wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani; na nchi ikachafuliwa na umwagaji wa damu.”
TAREHE 10-16/05
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | HESABU 30-31
“Timiza Naziri”
it-2-F uku. 1164
Naziri
Ya Kujipendea, Lakini Mutu Akiifanya Alipaswa Kuitimiza. Kila mutu alikuwa anafanya naziri kwa kujipendea. Lakini, kulingana na sheria ya Mungu, kama mutu anafanya naziri alipaswa kuitimiza. Kwa hiyo, ilisemwa kama ‘alijifunga naziri,’ maana yake, mu maisha yake yote alipaswa kuwa tayari kufanya mambo yote yenye aliapa. (Hes 30:2; ona pia Ro 1:31, 32.) Juu ni mambo yenye ilihusu maisha ya mutu, tunaelewa juu ya nini Maandiko inaonyesha kama mbele mutu afanye naziri, alipaswa kuwa mwangalifu kwa kufikiri kwa uzito juu ya mambo yenye mutu alipaswa kutimiza kama anafanya naziri. Sheria ilisema hivi: “Kama unafanya naziri kwa Yehova . . . Mungu hakika atakudai naziri hiyo, kama sivyo, utakuwa umetenda zambi. Lakini kama unajizuia kufanya naziri, hautakuwa na hatia ya zambi.”—Kum 23:21, 22.
it-2-F uku. 1164
Naziri
Naziri ni ahadi nzito yenye mutu anafanya mbele ya Mungu ya kama atafanya jambo fulani, atamutolea matoleo ao zawadi fulani, atafanya kazi fulani, ao atajiepusha na mambo fulani yenye sheria haikataze. Kila mutu alikuwa anafanya naziri kwa kujipendea. Juu naziri ni ahadi nzito, ilikuwa tu sawasawa na kufanya kiapo. Njo maana, wakati fulani ile maneno mbili inatumiwa pamoja mu Biblia. (Hes 30:2; Mt 5:33) “Naziri” inakazia zaidi sana nia ya mutu ya kufanya jambo fulani, lakini “kiapo” wakati mutu anaambia mwenye kuwa na mamlaka makubwa kama jambo lenye amesema ni la kweli na kama atalifanya. Mara mingi kisha kufanya viapo watu walikuwa wanafanya agano.—Mwa 26:28; 31:44, 53.
w04-SW 1/8 uku. 27 fu. 3
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Hesabu
30:6-8—Je, mwanamume Mkristo anaweza kuvunja nadhiri za mke wake? Kuhusu nadhiri, sasa Yehova anashughulika na watumishi wake wakiwa mtu mmoja-mmoja. Kwa mfano, kujiweka wakfu kwa Yehova ni nadhiri ya kibinafsi. (Wagalatia 6:5) Mume hana mamlaka ya kuvunja nadhiri kama hiyo. Hata hivyo, mke anapaswa kuepuka kuweka nadhiri inayopingana na Neno la Mungu au wajibu wake kwa mume wake.
Mali ya Kiroho
it-2-F 1203 fu. 4
Yefta
Zamani watu walikuwa wanatolewa kwa Yehova ili kumufanyia utumishi wa pekee wenye ulikuwa unafanywa patakatifu. Wazazi njo walikuwa na haki ya kufanya vile. Kwa mufano, mbele ya kumuzaa Samweli, Hana alifanya naziri ya kama angemutoa ili atumikie ku tabenakulo. Elkana, bwana yake, njo mwenye aliitika ile naziri. Wakati tu Samweli aliachishwa kunyonya, Hana alimutoa ili atumikie patakatifu. Na wakati uleule alitoa pia zabihu ya munyama. (1Sa 1:11, 22-28; 2:11) Samsoni naye alitolewa ili amutumikie Mungu mu njia ya pekee, alikuwa Munaziri.—Amu 13:2-5, 11-14; linganisha na mamlaka yenye baba alikuwa nayo juu ya mutoto wake mwanamuke vile inaonyeshwa mu Hes 30:3-5, 16.
TAREHE 17-23/05
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | HESABU 32-33
‘Mufukuze Wakaaji Wote wa Inchi’
w10-SW 1/8 uku. 23
Je, Wajua?
Ni nini kilichomaanishwa na “mahali pa juu” ambapo panatajwa mara kwa mara katika Maandiko ya Kiebrania?
Wakati wana wa Israeli walipokuwa karibu kuingia katika Nchi ya Ahadi, Yehova aliwaambia waondolee mbali mahali pote pa ibada ya Wakanaani ambao waliishi huko. Aliwaamuru hivi: “Mutaharibu mawe yao yote ya kuchorwa sanamu, na kuharibu sanamu zao zote za kuyeyusha, na kuharibu pahali pao pa juu [au, mahali pa juu] pote.” (Hesabu 33:52, Zaire Swahili Bible) Vituo hivyo vya ibada ya uwongo vilikuwa juu ya milima katika sehemu zilizo wazi au jukwaa zilizojengwa mahali penginepo kama vile chini ya miti au kwenye majiji. (1 Wafalme 14:23; 2 Wafalme 17:29; Ezekieli 6:3) Vituo hivyo vilikuwa na madhabahu, nguzo takatifu, sanamu, vinara vya uvumba, au vitu vingine vilivyotumiwa katika ibada ya uwongo.
w08-SW 15/2 uku. 27 fu. 5-6
Jifunze Kutokana na Makosa ya Waisraeli
Leo, tunakabili matatizo mengi kama ya Waisraeli. Katika jamii ya leo, kuna vitu vingi na watu ambao wanaabudiwa kama sanamu. Wanaabudu pesa, watu mashuhuri katika burudani, wanamichezo, mifumo ya kisiasa, viongozi fulani wa kidini, na hata washiriki wa familia. Chochote ambacho mtu anaabudu kinaweza kuwa jambo kuu katika maisha yetu. Kusitawisha urafiki wa karibu pamoja na wale ambao hawampendi Yehova kunaweza kutudhuru kiroho.
Ngono haramu ilikuwa sehemu kuu ya ibada ya Baali na iliwavutia na kuwashawishi Waisraeli wengi. Watu wengi wa Mungu bado wananaswa na mitego kama hiyo. Kwa mfano, mtu mwenye hamu ya kujua mambo au asiye mwangalifu anaweza kuchafua dhamiri yake safi kwa kuangalia ponografia (picha au habari za ngono) kwenye Intaneti nyumbani mwake. Ingehuzunisha sana ikiwa Mkristo angeshawishiwa na ponografia kwenye Intaneti!
it-1-F uku. 392 fu. 4
Kanaani
Yoshua alionyesha kama iko na hekima juu “hakukosa kufanya jambo lolote kati ya mambo yote yenye Yehova alikuwa amemuamuru Musa” kuhusu kuharibiwa kwa Wakanaani. (Yos 11:15) Lakini Waisraeli hawakufuata uongozi wa Yoshua na hawakuweza kumaliza kabisa watu wenye walifanya inchi ikuwe na uchafu. Kuendelea kuishi na Wakanaani kulifanya Waisraeli waambukizwe. Na ile ilifanya watu mingi sana wakufe (bila kutaja wenye walikufa juu ya kuvunja sheria, uasherati, na kuabudu sanamu). Ile haingetokeaka kama Waisraeli walifuataka ile maagizo ya Yehova ya kuua Wakanaani wote. (Hes 33:55, 56; Amu 2:1-3, 11-23; Zb 106:34-43) Yehova alionya Waisraeli kama haki na maamuzi yake haiko na upendeleo. Tena aliwaonya kama ikiwa wanajiunga na Wakanaani, kuoana nao, kuchanga imani, kufuata desturi zao za dini, na kufanya matendo yao ya mubaya, wangejiletea wao wenyewe uharibifu sawasawa na ule wa Wakanaani. Na ku mwisho ‘inchi ingewatapika.’—Kut 23:32, 33; 34:12-17; Law 18:26-30; Kum 7:2-5, 25, 26.
Mali ya Kiroho
it-1-F uku. 933 fu. 6
Mupaka
Kisha kura kuonyesha fasi yenye kabila fulani itariti, iliomba sasa kufikiria ukubwa wa kabila ili kujua ukubwa wa eneo yenye ile kabila ilipaswa kupewa. “Munapaswa kugawanya inchi hiyo kwa kura ili kuwa uriti kati ya familia zenu. Kwa kikundi kikubwa mutaongeza uriti wake, na kwa kikundi kidogo mutapunguza uriti wake. Uriti wa kila mutu utakuwa mahali kwenye kura yake itaangukia.” (Hes 33:54) Uamuzi wa kupiga kura ili kuonyesha fasi yenye kabila fulani ilipaswa kuriti haukuwa unabadilika, lakini kulikuwa kunafanywa mabadiliko fulani kuhusu ukubwa wa uriti. Kwa mufano, wakati ilionekana kama eneo ya Yuda ilikuwa kubwa sana, sehemu fulani za ile eneo zilipunguzwa na zikapewa kabila la Simeoni.—Yos 19:9.
Hotuba
w09-SW 1/10 uku. 30, kisanduku
Israeli la kale, taifa ambalo Mungu alichagua kwa njia ya pekee karne nyingi kabla ya Ukristo kuanzishwa, liliruhusiwa nyakati nyingine kukusanya jeshi na kupigana. Kabla ya kuingia Kanaani, nchi ambayo Mungu alikuwa amemwahidi Abrahamu, Waisraeli waliambiwa hivi: ‘Yehova Mungu wako hakika atayatia hayo mataifa saba mkononi mwako, nawe utayashinda. Unapaswa kuyaangamiza. Usifanye agano lolote pamoja nayo wala kuyaonyesha kibali chochote.’ (Kumbukumbu la Torati 7:1, 2) Hivyo, Yoshua, Jenerali Mwisraeli, aliyashinda mataifa hayo ya maadui “kama vile Yehova Mungu wa Israeli alivyokuwa ameamuru.”—Yoshua 10:40.
Je, Waisraeli walipigana vita hivyo kwa ukatili ili kunyakua ardhi ya mataifa mengine kwa pupa? Sivyo hata kidogo. Mataifa hayo yalikuwa yamejaa ibada ya sanamu, umwagaji wa damu, na matendo mengine ya ngono yaliyopotoka. Hata watoto walitolewa dhabihu kwa kutupwa motoni. (Hesabu 33:52; Yeremia 7:31) Utakatifu, haki, na upendo wa Mungu kuelekea watu wake ulimchochea kuondoa mazoea yote machafu katika nchi. Hata hivyo, Yehova alichunguza mioyo ya kila mtu, jambo ambalo hakuna kamanda wa jeshi anayeweza kufanya leo, na hivyo hakuwaua wale waliokuwa tayari kuacha njia zao mbaya na kumtumikia.
TAREHE 24-30/05
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | HESABU 34-36
‘Umukimbilie Yehova’
Unamukimbilia Yehova?
4 Lakini, namna gani Waisraeli walishugulikia mutu mwenye aliua, lakini hakufanya hivyo kwa makusudi? Hata kama hakufanya hivyo kwa makusudi, mutu mwenye aliua mwenzake alikuwa na kosa la kumwanga damu yenye haina kosa. (Mwa. 9:5) Hata hivyo, kwa rehema, aliruhusiwa kukimbia kutoka kwa mutu mwenye kulipiza kisasi cha damu na kuenda katika muji moja kati ya miji sita ya makimbilio. Angepata ulinzi huko. Mutu mwenye aliua mwenzake bila kukusudia alipaswa kubakia katika muji wa makimbilio mupaka kifo cha kuhani mukubwa.— Hes. 35:15, 28.
Unamukimbilia Yehova?
6 Kisha kumuua mwenzake bila kukusudia, kwanza mukimbizi alipaswa ‘kusema maneno yake masikioni mwa wanaume wazee’ kwenye mulango wa muji wa makimbilio ambamo alikimbilia. Alipaswa kukaribishwa muzuri. (Yos. 20:4) Kisha wakati fulani, alitumwa kwenye wazee wa muji ambamo mauaji yalitendeka, na wazee hao walipaswa kuhukumu jambo hilo. (Soma Hesabu 35:24, 25.) Mukimbizi angeweza kurudia katika muji wa makimbilio kisha tu wazee kuonyesha kuwa hakuua kwa makusudi.
Unamukimbilia Yehova?
13 Kisha kufika katika muji wa makimbilio, mukimbizi alipata usalama. Juu ya miji hiyo, Yehova alisema hivi: ‘Itakuwa kwenu makimbilio.’ (Yos. 20:2, 3) Yehova hakuomba mutu mwenye aliua mwenzake bila kukusudia ahukumiwe mara ya pili kwa ajili ya kosa lilelile; na hakuruhusu mutu mwenye kulipiza kisasi cha damu aingie katika muji ili kuua mukimbizi huyo. Kwa hiyo, mukimbizi hakupaswa kuogopa hata kidogo kuwa atauawa. Wakati alikuwa katika muji, alikuwa salama chini ya ulinzi wa Yehova. Muji huo haukukuwa gereza kwa mukimbizi. Katika muji huo, angeweza kufanya kazi, kusaidia wengine, na kumutumikia Yehova katika amani. Ndiyo, angeweza kuwa na maisha ya muzuri na yenye furaha!
Mali ya Kiroho
w91-SW 15/2 uku. 13 fu. 13
Ukombozi Unaolingana Kwa Ajili Ya Wote
13 Hata hivyo, wala Adamu wala Hawa, hawafaidiki na ukombozi. Sheria ya Kimusa ilitia ndani kanuni hii: “Tena hamutapokea ukombozi kwa uzima wa mwuaji anayestahili kufa.” (Hesabu 35:31, ZSB) Adamu hakudanganywa, kwa hiyo dhambi yake ilikuwa ya hiari, ya makusudi. (1 Timotheo 2:14) Ilikuwa sawa na kuwaua wazao wake, kwa ajili sasa walirithi kutokamilika kwake, kwa hiyo wakaja chini ya hukumu ya kifo. Kwa wazi, Adamu alistahili kufa, kwa kuwa akiwa mtu mkamilifu, alikuwa amechagua kwa hiari kutotii sheria ya Mungu. Ingalikuwa kinyume cha kanuni zilizo adilifu za Yehova kwa yeye kutumia ukombozi kwa ajili ya Adamu. Hata hivyo, kulipa mshahara kwa ajili ya dhambi ya Adamu, kunaandalia kubatilishwa kwa hukumu ya kifo juu ya wazao wa Adamu! (Warumi 5:16) Katika maana iliyo halali kisheria, uwezo wenye uharibifu wa dhambi unakatwa kwenye chanzo chao hasa. Mwenye kukomboa ‘aionja mauti kwa ajili ya kila mtu,’ akichukua matokeo ya dhambi kwa ajili ya watoto wote wa Adamu.—Waebrania 2:9; 2 Wakorintho 5:21; 1 Petro 2:24.
TAREHE 31/05–6/06
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | KUMBUKUMBU LA TORATI 1-2
“Hukumu Ni ya Mungu”
w96-SW 15/3 uku. 23 fu. 1
Yehova—Mpenda Uadilifu na Haki
Wazee waliowekwa rasmi wana wajibu wa kuhukumu katika kesi za kosa zito. (1 Wakorintho 5:12, 13) Wafanyapo hivyo, wao hukumbuka kwamba haki ya Mungu huonyesha rehema iwezekanapo. Ikiwa hakuna msingi wa rehema—kama katika kisa cha watenda dhambi wasiotubu—hiyo haiwezi kuonyeshwa. Lakini wazee hawafukuzi wakosaji kutoka kutanikoni kwa sababu ya kisasi. Wao hutumaini kwamba tendo la kutenga na ushirika litamfanya apate kurudia fahamu zake. (Linganisha Ezekieli 18:23.) Chini ya ukichwa wa Kristo, wazee hufuatia haki, na hilo hutia ndani kuwa kama “mahali pa kujificha na upepo.” (Isaya 32:1, 2) Hivyo ni lazima waonyeshe kutopendelea na kuwa wenye kukubali sababu.—Kumbukumbu la Torati 1:16, 17.
w02-SW 1/8 uku. 9 fu. 4
Tii kwa Uaminifu Mamlaka ya Kimungu
4 Hata hivyo, mtu hakuhitaji kujua Sheria tu ili awe mwamuzi. Kwa sababu ya hali ya kutokamilika, wazee hao walipaswa kuwa waangalifu ili waepuke maelekeo yasiyofaa—kama vile ubinafsi, upendeleo, na pupa—mambo yanayoweza kupotosha hukumu. Musa aliwaambia hivi: “Msimpendelee mtu yeyote katika kutoa hukumu; mtawasikiliza bila upendeleo, wakubwa kwa wadogo. Msiogopeshwe na sura ya mtu, maana nyinyi mtapaswa kuhukumu kwa niaba ya Mungu.” (Italiki ni zetu.) Naam, waamuzi wa Israeli walikuwa wakiamua kwa niaba ya Mungu. Hilo lilikuwa pendeleo kubwa kama nini!—Kumbukumbu la Torati 1:16, 17, Biblia Habari Njema.
Mali ya Kiroho
Vikumbusho vya Yehova Ni Vyenye Kutegemeka
9 Waisraeli walipoanza safari yao ya miaka 40 katika nyika [ao jangwa] “kubwa yenye kuogopesha,” Yehova hakuwatolea mafasirio fulani mbele ya wakati kuhusu namna ambavyo angewaongoza, kuwalinda, na kuwatunza. Hata hivyo, aliwaambia tena na tena kwamba walipaswa kumutegemea yeye na kufuata maagizo yake. Yehova alitumia nguzo ya wingu wakati wa muchana na nguzo ya moto wakati wa usiku ili kuwakumbusha Waisraeli kwamba alikuwa akiwategemeza muda wote aliokuwa akiwaongoza katika jangwa hiyo ya hatari. (Kum. 1:19; Kut. 40:36-38) Yehova aliwatimizia pia mahitaji yao ya lazima. “Mavazi yao hayakuchakaa, wala miguu yao haikuvimba.” Bila shaka, “hawakukosa chochote.”—Neh. 9:19-21.
Hotuba
Maneno yasiyofaa ya wengine yanaweza kutuathiri. (Soma Kumbukumbu la Torati 1:26-28.) Waisraeli walikuwa tu wamekombolewa kutoka utumwani huko Misri. Yehova alikuwa ameleta kimuujiza mapigo kumi juu ya taifa hilo lenye uonevu na kisha akamwangamiza Farao na jeshi lake katika Bahari Nyekundu. (Kut. 12:29-32, 51; 14:29-31; Zab. 136:15) Watu wa Mungu walikuwa karibu kuingia Nchi ya Ahadi. Hata hivyo, katika kipindi hicho muhimu, Waisraeli walianza kulalamika kumhusu Yehova. Ni nini kilichosababisha ukosefu huo wa imani? Mioyo yao iliyeyuka kwa sababu ya habari mbaya iliyoletwa na baadhi ya watu waliotumwa kuipeleleza nchi. (Hes. 14:1-4) Matokeo yakawa nini? Kizazi chote hakikuruhusiwa kuingia katika ‘nchi hiyo nzuri.’ (Kum. 1:34, 35) Je, nyakati nyingine tunaweza kuruhusu maneno yasiyofaa ya wengine yadhoofishe imani yetu na kutufanya tunung’unike kuhusu jinsi Yehova anavyoshughulika nasi?
TAREHE 7-13/06
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | KUMBUKUMBU LA TORATI 3-4
“Sheria za Yehova NI Zenye Hekima na Haki”
it-1-F uku. 1199 fu. 2
Uelewaji
Mutu mwenye anajifunza Neno la Mungu kwa bidii na kutumikisha amri na mambo yenye kuwa ndani, anaweza kuwa na ufahamu mwingi kuliko walimu wake na uelewaji mwingi kuliko wanaume wazee. (Zb 119:99, 100, 130; linganisha na Lu 2:46, 47.) Ile ni kweli, juu masharti na maagizo ya hukumu ya Yehova njo inafanyaka mutu akuwe na hekima na uelewaji; kwa hiyo, Waisraeli wangefuata kwa uaminifu masharti na maagizo ya hukumu ya Yehova, mataifa yenye ilikuwa pembeni yao ingewaona kuwa “taifa la watu wenye hekima na uelewaji.” (Kum 4:5-8; Zb 111:7, 8, 10; linganisha na 1Fa 2:3.) Mutu mwenye uelewaji anatambua kama hapaswe kutenda tofauti na Neno la Mungu, na anaomba Mungu amusaidie kufanya vile. (Zb 119:169) Anaacha Neno la Mungu liingie kabisa ndani yake (Mt 13:19-23), analiandika kwenye kibao cha moyo wake (Mez 3:3-6; 7:1-4), na anachukia kabisa “kila njia ya uongo” (Zb 119:104). Ni vile Mwana wa Mungu alifanya, wakati alikuwa ku dunia, ili kuonyesha kama alikuwa na uelewaji. Kwa mufano, hakukimbia hata kifo ku muti wa mateso, juu alijua kama Maandiko ilikuwa ilishatabiri kama ni vile alipaswa kuuawa.—Mt 26:51-54.
w99-SW 1/11 uku. 20 fu. 6-7
Ukarimu Unapokuwa Mwingi
Akiwa ameshangazwa na yale aliyosikia na kuona, malkia huyo alijibu kwa unyenyekevu hivi: “Heri watumishi hawa wako, wasimamao mbele yako siku zote, wakisikia hekima yako.” (1 Wafalme 10:4-8) Hakuwatangaza watumishi wa Solomoni kuwa wenye furaha kwa sababu walizungukwa na utajiri—ingawa ndivyo ilivyokuwa. Badala yake, watumishi wa Solomoni walibarikiwa kwa sababu wangeweza kusikiliza daima hekima ambayo Solomoni alipewa na Mungu. Malkia wa Sheba ni kielelezo kizuri kama nini kwa watu wa Yehova leo, ambao wanapata kwa wingi hekima ya Muumba mwenywe na ya Mwana wake, Yesu Kristo!
Maneno ambayo malkia alifuatisha kumwambia Solomoni yafaa pia kuangaliwa: “Na ahimidiwe BWANA, Mungu wako.” (1 Wafalme 10:9) Inaonekana kwamba aliona mkono wa Yehova katika hekima na ufanisi wa Solomoni. Jambo hilo lapatana na lile ambalo Yehova alikuwa amewaahidi Waisraeli hapo awali. ‘Kushika amri zangu,’ akasema, “ndiyo hekima yenu na akili zenu, machoni pa mataifa watakaozisikia amri hizi zote, nao watasema, Hakika taifa hili kubwa ni watu wenye hekima na akili.”—Kumbukumbu la Torati 4:5-7.
w07-SW 1/8 uku. 29 fu. 13
Je, Wewe Ni “Tajiri Kwa Mungu”?
13 Yehova anapowabariki watu wake, sikuzote anawapa vitu vilivyo bora. (Yakobo 1:17) Kwa mfano, Yehova alipowapa Waisraeli nchi, “ilikuwa nchi inayotiririka maziwa na asali.” Ingawa nchi ya Misri pia ilisemwa kuwa hivyo, nchi ambayo Yehova aliwapa Waisraeli ilikuwa tofauti angalau katika njia moja muhimu. Musa aliwaambia Waisraeli hivi: Ni “nchi ambayo Yehova Mungu wako anaitunza.” Kwa maneno mengine, wangefanikiwa kwa sababu Yehova angewatunza. Maadamu Waisraeli waliendelea kuwa waaminifu kwa Yehova, aliwabariki sana na ni wazi kwamba waliishi kwa njia bora kuliko mataifa yote yaliyowazunguka. Ndiyo, baraka ya Yehova ndiyo “hutajirisha”!—Hesabu 16:13; Kumbukumbu la Torati 4:5-8; 11:8-15.
Mali ya Kiroho
w04-SW 15/9 uku. 25 fu. 3
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Kumbukumbu la Torati
4:15-20, 23, 24—Je, katazo la kutengeneza sanamu za kuchongwa lilimaanisha kwamba ni kosa kufanya mifano ya vitu kwa ajili ya mapambo? La. Katazo hili lilihusu kufanya sanamu ili kuziabudu, yaani, ‘kuziinamia na kuzitumikia.’ Biblia haikatazi kuchonga sanamu au kuchora picha kwa ajili ya mapambo.—1 Wafalme 7:18, 25.
TAREHE 14-20/06
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | KUMBUKUMBU LA TORATI 5-6
“Mufundishe Watoto Wenu Wamupende Yehova”
w05-SW 15/6 uku. 20 fu. 11
Wazazi, Waandalieni Mahitaji Watu wa Familia Zenu
11 Kuhusu jambo hilo, labda andiko ambalo hunukuliwa mara nyingi zaidi ni Kumbukumbu la Torati 6:5-7. Tafadhali fungua Biblia yako na usome mistari hiyo. Ona kwamba wazazi wanaambiwa waboreshe kwanza uhusiano wao na Mungu, kwa kusitawisha upendo kwa Yehova na kuyaweka maneno yake moyoni. Naam, unahitaji kujifunza Neno la Mungu kwa bidii, kuisoma Biblia kwa ukawaida na kutafakari ili uweze kuzielewa vizuri na pia kuzipenda njia, kanuni, na sheria za Yehova. Kwa kufanya hivyo, moyo wako utajaa kweli nzuri za Biblia ambazo zitafanya uwe na shangwe na pia kumheshimu na kumpenda Yehova. Utakuwa na mambo mengi mazuri ya kuwafundisha watoto wako.—Luka 6:45.
w07-SW 15/5 uku. 15-16
Ninaweza Kuwasaidia Jinsi Gani Watoto Wangu Waelimike Kikweli?
Tamaa, viwango, kanuni, na mapendezi yako hayapaswi kuonekana kupitia maneno yako tu bali pia kupitia matendo yako. (Waroma 2:21, 22) Tangu wakiwa wachanga, watoto wanajifunza kwa kuwatazama wazazi wao kwa uangalifu. Watoto wanatambua mambo yaliyo ya maana kwa wazazi wao, na kwa kawaida hayo ndiyo mambo yanayokuwa ya maana kwa watoto. Ikiwa unampenda Yehova kikweli, watoto wako watatambua jambo hilo. Kwa mfano, wataona kwamba kusoma na kujifunza Biblia ni mambo muhimu kwako. Watatambua kwamba unatanguliza mambo ya Ufalme katika maisha yako. (Mathayo 6:33) Ukihudhuria mikutano kwa ukawaida na kushiriki katika kazi ya kuhubiri Ufalme utawaonyesha kwamba kumtolea Yehova utumishi mtakatifu ni jambo la maana sana kwako.—Mathayo 28:19, 20; Waebrania 10:24, 25.
w05-SW 15/6 uku. 21 fu. 14
Wazazi, Waandalieni Mahitaji Watu wa Familia Zenu
14 Kama andiko la Kumbukumbu la Torati 6:7 linavyoonyesha, kuna pindi nyingi ambapo ninyi wazazi mnaweza kuzungumzia mambo ya kiroho pamoja na watoto wenu. Mnaweza kupata nafasi za kuandaa mahitaji ya kiroho ya watoto wenu mnaposafiri pamoja, mnapofanya kazi za nyumbani, au kustarehe pamoja. Bila shaka, hamhitaji kuzungumza mfululizo na watoto wenu kuhusu kweli za Biblia. Badala yake, jaribuni kuwa na mazungumzo ya kiroho na yenye kujenga katika familia. Kwa mfano, gazeti la Amkeni! huwa na makala nyingi kuhusu mambo mbalimbali. Makala hizo zinaweza kutumiwa ili kuzungumza kuhusu wanyama, maeneo ya asili yenye kuvutia ulimwenguni, na maisha na utamaduni mbalimbali wenye kuvutia. Mazungumzo hayo yanaweza kuwachochea watoto wasome vichapo zaidi vinavyoandaliwa na jamii ya mtumwa mwaminifu na mwenye busara.—Mathayo 24:45-47.
Mali ya Kiroho
Upendo na Haki Katika Israeli ya Zamani
11 Mambo yenye tunajifunza: Yehova haone tu namna mutu anaonekana kwa inje. Anaona namna tuko kabisa ndani ya moyo wetu. (1 Sa. 16:7) Hatuwezi kumuficha wazo fulani, jambo fulani lenye kuwa mu moyo wetu, ao tendo fulani. Yehova anatafuta sifa za muzuri zenye kuwa ndani ya moyo wetu, na anapenda tukomalishe sifa hizo za muzuri. Lakini anapenda tutambue na kuzuia mawazo ya mubaya mbele ituongoze kufanya mambo ya mubaya.—2 Ny. 16:9; Mt. 5:27-30.
TAREHE 21-27/06
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | KUMBUKUMBU LA TORATI 7-8
“Haupaswe Kufanya Mapatano Yoyote ya Ndoa Pamoja nao”
wp12 1/7 uku. 29 fu. 2
Sababu gani Mungu Aliwaomba Waabudu Wake Waoane Kati yao tu?
Yehova alipenda kuwalinda Waisraeli kwa ujumla; alijua kama Shetani alitaka kuchafua ibada ya taifa lake kwa kuwachochea waabudu miungu ya uongo. Kwa hiyo, Mungu aliwaonya juu ya mataifa yaliyowazunguka kwa kusema hivi: ‘Watamugeuza mwana wako aache kunifuata, nao watatumikia miungu mingine.’ Kuoana na watu wasiomuabudu Mungu kungewaletea hatari nyingi. Waisraeli wangeabudu miungu mingine, Mungu hangewakubali tena na kuwalinda, na maadui wao wangewashinda kwa vyepesi. Basi, ikiwa mambo hayo yangewapata, namna gani wangetokeza Masiya aliyeahidiwa? Inaonekana wazi sababu gani Shetani alikuwa anawashawishi Waisraeli waoane na watu wasiomuabudu Mungu.
Amri ya Kuoa ao Kuolewa “Katika Bwana Tu” Ingali Yenye Kufaa?
Hata hivyo, katika Neno lake, Yehova ametoa muongozo wa kuoa ao kuolewa katika Bwana tu. Sababu gani? Kwa sababu anapenda watu wake wakuwe na maisha mazuri. Anapenda watumishi wake wasipatwe na maumivu yenye mutu anaweza kupata kwa sababu ya kuchukua maamuzi mabaya, lakini pia anapenda wakuwe wenye furaha. Katika siku za Nehemia Wayahudi wengi walioa wanawake wenye hawakuwa waabudu wa Yehova. Kwa hiyo, Nehemia aliwakumbusha matokeo mabaya ambayo Mufalme Sulemani alipata kwa sababu alioa wanawake wasio Waisraeli. Nehemia aliwaambia kwamba ijapokuwa Mufalme Sulemani ‘alipendwa na Mungu wake, . . . wake wa kigeni walimufanya hata yeye atende zambi.’ (Neh. 13:23-26) Ndiyo sababu Mungu amewaamuru watumishi wake waoe ao kuolewa tu na waabudu wa kweli, na kufanya hivyo ni kwa faida yao. (Zab. 19:7-10; Isa. 48:17, 18) Wakristo wa kweli wanamushukuru Mungu kwa sababu anawahangaikia kwa upendo; kwa hiyo wanategemea muongozo wake. Wanaonyesha kwamba wanamukubali Mungu kuwa Mutawala wa Ulimwengu Wote Muzima kwa kutii muongozo wake.—Met. 1:5.
Ufanye Angalisho na Marafiki Wabaya Katika Siku Hizi za Mwisho
12 Wakristo wenye wanapenda kuoa ao kuolewa, wanapaswa kuwa waangalifu sana kuhusu mutu mwenye wanachagua kuchumbia. Neno la Mungu linatuonya hivi: ‘Musifungwe nira isivyo sawa pamoja na wasio waamini. Kwa maana kuna ushirika gani kati ya uadilifu na uasi-sheria? Ao nuru ina ushirika gani na giza?’ (2 Wakorintho 6:14) Biblia inawaomba watumishi wa Mungu waoe ao kuolewa “katika Bwana tu,” ni kusema, kuoa ao kuolewa tu na mutu mwenye amekwisha kujitoa kwa Mungu na kubatizwa, na mwenye anaishi kupatana na kanuni za Yehova. (1 Wakorintho 7:39) Wakati unaoa ao kuolewa na mutu kama huyo, ni kusema, mutu mwenye kumupenda Yehova, unapata mutu mwenye atakusaidia uendelee kuwa mwaminifu kwa Mungu.
Mali ya Kiroho
w04-SW 1/2 uku. 13 fu. 4
Yehova Hutuandalia Mahitaji Yetu ya Kila Siku
4 Sala yetu ya kuomba mkate wa kila siku inapaswa pia kutukumbusha kwamba tunahitaji chakula cha kiroho kila siku. Ingawa Yesu alikuwa na njaa kali baada ya kufunga kwa muda mrefu, alikataa kishawishi cha Shetani cha kugeuza mawe yawe mkate, aliposema: “Imeandikwa, ‘Mwanadamu ataishi, si kwa mkate tu, bali kwa kila neno linalotoka katika kinywa cha Yehova.’” (Mathayo 4:4) Hapa Yesu alimnukuu nabii Musa aliyewaambia Waisraeli hivi: “[Yehova] alikunyenyekeza, akakuacha ukae na njaa, akakulisha mana, ambayo hukuwa umeijua wala baba zako hawakuwa wameijua; ili kukufanya ujue kwamba mwanadamu haishi kwa mkate tu bali mwanadamu huishi kwa kila neno la kinywa cha Yehova.” (Kumbukumbu la Torati 8:3) Njia ambayo Yehova alitumia kutoa mana iliwaandalia Waisraeli chakula cha kimwili na pia kuwafunza mambo fulani ya kiroho. Mojawapo ya mambo hayo ni kwamba walipaswa “kuokota kila mtu kiasi chake siku baada ya siku.” Iwapo wangekusanya mana nyingi kuliko mahitaji yao ya siku, mabaki yangeanza kunuka na kutokeza wadudu. (Kutoka 16:4, 20) Hata hivyo, haikuwa hivyo siku ya sita ambayo walipaswa kukusanya mana kiasi cha siku mbili kwa ajili ya siku ya Sabato. (Kutoka 16:5, 23, 24) Kwa hiyo, mana hiyo iliwakumbusha kwamba walipaswa kutii na kwamba maisha yao hayakutegemea mkate tu bali “kila neno la kinywa cha Yehova.”
Hotuba
w06-SW 1/1 uku. 28 fu. 14-15
14 Muda mfupi kabla ya Waisraeli kuingia Nchi ya Ahadi, Yehova aliwaonya wasimsahau. Alisema hivi: “Jiangalie usije ukamsahau Yehova Mungu wako kwa kutozishika amri zake na maamuzi yake ya hukumu na sheria zake ambazo ninakuamuru leo; usije ukala na kushiba kwelikweli, ukajenga nyumba nzuri na kukaa ndani yake, na mifugo yako na kundi lako likaongezeka, na fedha na dhahabu zikakuongezekea, na vyote vilivyo vyako vikaongezeka; nao moyo wako uinuke juu, na umsahau Yehova Mungu wako.”—Kumbukumbu la Torati 8:11-14.
15 Je, jambo kama hilo linawezekana leo? Ndiyo, ikiwa tunatanguliza mambo yasiyofaa. Hata hivyo, tukiutafuta kwanza uadilifu wa Mungu, ibada safi itakuwa jambo la maana zaidi maishani mwetu. Kama Paulo alivyotutia moyo, ‘tutajinunulia wakati unaofaa’ na kufanya huduma yetu tukitambua kwamba muda uliobaki ni mfupi. (Wakolosai 4:5; 2 Timotheo 4:2) Hata hivyo, ikiwa tunaona starehe au njia nyingine za kupata raha kuwa muhimu sana kuliko kuhudhuria mikutano na kuhubiri, tunaweza kumsahau Yehova kwa kumpa nafasi ya pili maishani mwetu. Paulo alisema kwamba katika hizi siku za mwisho watu ‘wangependa raha badala ya kumpenda Mungu.’ (2 Timotheo 3:4) Wakristo wanyoofu hujichunguza kwa ukawaida ili kuhakikisha kwamba hawaathiriwi na kufikiri kwa aina hiyo.—2 Wakorintho 13:5.
TAREHE 28/06–4/07
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | KUMBUKUMBU LA TORATI 9-10
“Yehova Mungu Wako Anataka Ufanye Nini?”
w09-SW 1/10 uku. 10 fu. 3-4
Yehova Anataka Nini Kutoka Kwetu?
Ni nini kinachoweza kutuchochea tumtii Mungu kwa hiari? Musa anataja sababu moja: “Kumwogopa Yehova Mungu wako.” (Mstari wa 12) Huo si woga wa kupata matokeo mabaya bali ni woga unaotokana na kumheshimu Mungu na njia zake. Ikiwa tunamwogopa Mungu kwa njia inayofaa, tutaepuka kumkasirisha.
Lakini nia yetu kuu ya kumtii Mungu inapaswa kuwa nini? Musa alisema hivi: “Kumpenda [Yehova] na kumtumikia Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote.” (Mstari wa 12) Kumpenda Mungu kunahusisha mengi kuliko hisia. Kitabu kimoja kinaeleza: “Vitenzi vya Kiebrania vinavyorejelea hisia nyakati nyingine hurejelea matokeo ya hisia hizo.” Kitabu hichohicho kinasema kwamba kumpenda Mungu kunamaanisha “kutenda kwa upendo” kumwelekea Mungu. Kwa maneno mengine, ikiwa kwa kweli tunampenda Mungu, tutatenda kwa njia ambazo tunajua zitamfurahisha.—Methali 27:11.
w09-SW 1/10 uku. 10 fu. 6
Yehova Anataka Nini Kutoka Kwetu?
Kutii kwa hiari kutatuletea baraka. Musa aliandika hivi: “Kuzishika amri . . . ninazokuamuru wewe leo, [ni] kwa faida yako.” (Mstari wa 13) Naam, kila amri ya Yehova, kila kitu anachotaka tufanye, ni kwa faida yetu. Mbona isiwe hivyo? “Mungu ni upendo,” inasema Biblia. (1 Yohana 4:8) Kwa hiyo, ametupa amri ambazo zitatuletea faida za kudumu. (Isaya 48:17) Kufanya yale ambayo Yehova anataka kutoka kwetu kutatuzuia tusikatishwe tamaa sasa na kutatuletea baraka za milele chini ya Ufalme wake.
cl-SW uku. 16 fu. 2
Je, Kweli Unaweza ‘Kumkaribia Mungu’?
2 Abrahamu aliyeishi nyakati za kale alifurahia uhusiano wa karibu na Mungu. Yehova alimwita huyo mzee wa ukoo “rafiki yangu.” (Isaya 41:8) Naam, Yehova alimwona Abrahamu kuwa rafiki yake mkubwa. Abrahamu alifurahia uhusiano huo wa karibu kwa sababu “aliweka imani katika Yehova.” (Yakobo 2:23) Hali kadhalika leo, Yehova hutafuta fursa za ‘kuwapenda kwa dhati’ wale wanaomtumikia kwa sababu wanampenda. (Kumbukumbu la Torati 10:15, Biblia Habari Njema) Neno lake linatusihi hivi: “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia.” (Yakobo 4:8) Anatualika tumkaribie na kututolea ahadi kwa maneno hayo.
Mali ya Kiroho
it-1-F uku. 115
Waanaki
Ni jamii (race) ya watu wenye walikuwa na ukubwa wa ajabu. Waliishi Kanaani, mu maeneo ya milima na mu maeneo fulani yenye ilikuwa pembeni ya bahari, zaidi sana upande wa kusini. Wakati fulani, wanaume tatu Waanaki, wenye walijulikana sana, ni kusema, Ahimani, Sheshai, na Talmai, waliishi Hebroni. (Hes 13:22) Ni kule njo kwenye wapelelezi Waebrania 12 waliona kwa mara ya kwanza Waanaki. Ile ilifanya wapelelezi 10 kati yao watoe ripoti yenye kuogopesha kwa kusema kama wale wanaume walitokana na Wanefili wenye waliishi mbele ya Garika. Tena walisema kama Waebrania ni kama “panzi” mbele ya wale wanaume. (Hes 13:28-33; Kum 1:28) Ukubwa wa Waanaki ulitumiwa ili kuzungumuzia ukubwa wa wanaume Waemi na Warefaimu. Inaonekana kama ni nguvu yenye Waanaki walikuwa nayo njo ilifanya kukuwe hii mezali: “Ni nani anaweza kusimama mbele ya wana wa Anaki?”—Kum 2:10, 11, 20, 21; 9:1-3.