KISANDUKU CHA KUFUNDISHIA 9E
“Wakati wa Kurudishwa kwa Mambo Yote”
MATENDO 3:21
Wakati mutume Petro alitaja “wakati wa kurudishwa kwa mambo yote,” alikuwa anazungumuza mu njia ya unabii kuhusu kipindi kizuri sana chenye kingeanza wakati Yesu angewekwa kuwa Mufalme na chenye kingeendelea mupaka mwisho wa Utawala wa Miaka Elfu.
1914—Yesu Kristo anawekwa kuwa Mufalme mbinguni. Watu wa Mungu wanaanza kurudishwa mu hali ya muzuri ya kiroho mu mwaka wa 1919
Siku za Mwisho
ARMAGEDONI—Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo unaanza, na “wakati wa kurudishwa kwa mambo yote” unapanuka na unaletea wanadamu waaminifu wenye kuwa mu dunia baraka za kimwili
Utawala wa Miaka Elfu
MWISHO WA UTAWALA WA MIAKA ELFU—Yesu anamaliza kazi ya kurudisha mambo yote mu hali ya muzuri na anamurudishia Baba yake Ufalme
Paradiso ya Milele
UTAWALA WA YESU . . .
utarudishia jina la Mungu utukufu
utarudishia wagonjwa afya ya muzuri
utarudishia wazee ujana
utarudishia wafu uzima
utarudishia wanadamu waaminifu ukamilifu
utarudisha Paradiso juu ya dunia