Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwbr22 Mwezi wa 1 uku. 1-9
  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha (01/2022)

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha (01/2022)
  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha (2022)
  • Vichwa Vidogo
  • TAREHE 3-9/1
Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha (2022)
mwbr22 Mwezi wa 1 uku. 1-9

Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha

TAREHE 3-9/1

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | WAAMUZI 15-16

“Ni Mambo ya Haya Sana Kusaliti Wengine!”

w12 15/4 uku. 9 fu. 4

Kuwasaliti Wengine​—Alama ya Siku za Mwisho!

4 Mufano wa kwanza, tufikirie Delila mwanamuke mudanganyifu, ambaye alipendwa na Mwamuzi Samsoni. Samsoni alikusudia kupigana na Wafilisti kwa faida ya watu wa Mungu. Labda Wafilisti walijua kama Delila hamupendi kabisa Samsoni, kwa hiyo wakubwa wa tano wa Wafilisti, walimutolea Delila feza nyingi kusudi wajue siri ya nguvu za Samsoni ili wamuue. Kwa sababu Delila alikuwa mwanamuke mwenye pupa ao tamaa sana alikubali feza hizo. Alijaribu mara tatu kumufanya Samsoni amujulishe siri ya nguvu zake, lakini alishindwa. Basi Delila aliendelea kumusumbua sana Samsoni ‘kwa maneno yake wakati wote na kuendelea kumusihi.’ Mwishowe, “nafsi yake [Samsoni] ikakosa subira kufikia hatua ya kutaka kufa.” Kwa hiyo, Samsoni akamufunulia Delila siri, akamuambia kwamba hajakatwa nywele hata siku moja, akikatwa nywele atapoteza nguvu zake. Delila alipojua siri hiyo, akafanya mupango ili Samsoni akatwe nywele alipokuwa akilala kwenye mapaja yake, kisha akamuacha katika mikono ya maadui ili wamutendee wanavyotaka. (Amu. 16:4, 5, 15-21) Delila alitenda jambo mbaya sana! Kwa sababu tu ya pupa Delila alimusaliti mwanaume aliyemupenda.

w05-SW 15/1 uku. 27 fu. 3

Mambo Makuu Katika Kitabu cha Waamuzi

14:16, 17; 16:16. Kumsumbua mtu mwingine kwa kulia na kumkasirisha kunaweza kuharibu uhusiano.​—Methali 19:13; 21:19.

w12 15/4 uku. 11-12 fu. 15-16

Kuwasaliti Wengine​​—Alama ya Siku za Mwisho!

15 Namna gani wale wenye kufunga ndoa ao kuolewa wanaweza kubaki washikamanifu kwa wenzi wao? Neno la Mungu linasema: “Ushangilie pamoja na muke [ao mume] wa ujana wako” na, ‘Furahia maisha pamoja na muke [ao mume] unayemupenda.’ (Met. 5:18; Mhu. 9:9) Bwana na bibi wanapoendelea kuzeeka wanapaswa kufanya yote wawezayo ili waendelee kushikamana katika upendo wao na katika mambo mengine. Hilo linamaanisha kuhangaikia mwingine, kusaidiana, kupitisha wakati pamoja na kuzungumuza. Wanapaswa kufanya nguvu ili kulinda ndoa yao na kuwa na uhusiano muzuri pamoja na Yehova. Ili kufikia jambo hilo, bibi na bwana wanapaswa kujifunza Biblia pamoja, kuhubiri pamoja kwa ukawaida, na kusali pamoja ili kuomba baraka za Yehova.

USHIKAMANIFU KWA YEHOVA

16 Kuna ndugu na dada fulani ambao waliangukia katika zambi nzito na kwa hiyo walikaripiwa “kwa ukali ili wawe na afya katika imani.” (Tito 1:13) Wengine walitengwa na ushirika kwa kuwa iliomba watengwe. Kwa wale ambao wamekubali ‘kuzoezwa’ na nizamu ao discipline hiyo, wamesaidiwa na sasa wako tena na afya njema kiroho. (Ebr. 12:11) Itakuwa namna gani ikiwa mutu wa jamaa ao rafiki yetu anatengwa? Hapo sasa ndipo ushikamanifu wetu unajaribiwa. Je, tutabaki washikamanifu kwa Mungu ao kwa mutu? Yehova anatutazama ili kuona ikiwa tutatii amri yake inayotukataza kushirikiana na mutu yeyote anayetengwa.​—Soma 1 Wakorintho 5:11-13.

Mali ya Kiroho

w04-SW 15/10 uku. 15 fu. 7, 8

“Ondoka, Zunguka Katika Nchi”

7 Kwenye Waamuzi 16:2, unaweza kusoma kuhusu Mwamuzi Samsoni alipokuwa Gaza. Leo eneo la Gaza hutajwa mara nyingi katika vyombo vya habari, kwa hiyo huenda ikawa unajua kwa kadiri fulani mahali Samsoni alipokuwa, katika eneo la Wafilisti karibu na Pwani ya Mediterania. [gl 11] Sasa ona andiko la Waamuzi 16:3: ‘Samsoni aliendelea kulala mpaka katikati ya usiku, kisha akaamka katikati ya usiku, akakamata milango ya lango la jiji na miimo yake miwili, akaing’oa pamoja na pingo, akaiweka juu ya mabega yake, akaichukua mpaka kwenye kilele cha mlima ulio mbele ya Hebroni.’

8 Bila shaka malango na miimo ya jiji la Gaza ilikuwa mikubwa na mizito, kwa kuwa jiji hilo lilikuwa ngome. Wazia ukijaribu kubeba malango na miimo hiyo! Samsoni aliibeba, lakini aliipeleka wapi, naye alifunga safari ya aina gani? Gaza liko pwani, karibu na usawa wa bahari. Hata hivyo, Hebroni liko upande wa mashariki kwenye mwinuko wa meta 930​—eneo lililo juu kwelikweli! Hatujui mahali hususa ambapo “mlima ulio mbele ya Hebroni” ulikuwa, lakini Hebroni liko umbali wa kilometa 60 hivi kutoka Gaza! Kujua umbali uliohusika kunatusaidia kuelewa ukubwa wa tendo la ujasiri la Samsoni, sivyo? Kumbuka kwamba Samsoni aliweza kufanya mambo hayo kwa sababu ‘roho ya Yehova ilianza kutenda kazi juu yake.’ (Waamuzi 14:6, 19; 15:14) Tukiwa Wakristo leo, hatutarajii roho ya Mungu itupe nguvu za kimwili zisizo za kawaida. Hata hivyo, roho hiyohiyo yenye nguvu inaweza kuongeza utambuzi wetu wa mambo ya kiroho yenye kina na kutufanya tuwe na uwezo kulingana na mtu tuliye kwa ndani. (1 Wakorintho 2:10-16; 13:8; Waefeso 3:16; Wakolosai 1:9, 10) Naam, kuelewa masimulizi kuhusu Samsoni, hukazia uhakika kwamba roho ya Mungu inaweza kutusaidia.

TAREHE 10-16/1

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | WAAMUZI 17-19

“Kuvunja Sheria ya Mungu Kunaletaka tu Magumu”

it-2-F uku. 278

Mika

1. Mwanaume wa Efraimu. Alivunja amri ya munane kati ya Amri Kumi kwa kuiba vipande vya feza 1 100 vya mama yake. (Kut 20:15) Wakati aliungama na kuvirudisha, mama yake alisema hivi: “Hakika nitatakasa kwa ajili ya Yehova feza hiyo yenye kutoka katika mukono wangu ili mwana wangu aitumie kutengeneza sanamu ya kuchongwa na sanamu ya metali. Sasa nitarudisha feza hiyo kwako.” Kisha pale, alikamata vipande 200 vya feza na kuvipatia fundi wa feza, na ule fundi alivitumia ili ‘kutengeneza sanamu ya kuchongwa na sanamu ya metali,’ na zile sanamu ziliwekwa mu nyumba ya Mika. Mika alikuwa na “nyumba ya miungu,” alitengeneza efodi na terafimu, na akaweka mumoya wa watoto wake kuwa kuhani wake. Hata kama ile mupango ilikuwa na kusudi ya kumuletea Yehova heshima, haikufaa hata kidogo juu ilivunja amri yenye ilikataza kuabudu sanamu (Kut 20:4-6) na ilizaraulisha tabenakulo ya Yehova na ukuhani wake. (Amu 17:1-6; Kum 12:1-14) Kisha, Mika alikamata Yonatani kijana Mulawi na muzaliwa wa Gershomu, mutoto wa Musa, akamuleta mu nyumba yake na kumufanya kuwa kuhani wake. (Amu 18:4, 30) Kisha kufanya ile yote, alisema hivi kwa furaha: “Sasa ninajua kwamba Yehova atanitendea mema.” Lakini ile ilikuwa ni kujidanganya kabisa. (Amu 17:7-13) Yonatani hakustahili kuwa kuhani juu hakukuwa mu kizazi ya Haruni. Kwa hiyo, Mika alijiongezea tu makosa kwa kumufanya kuwa kuhani.​—Hes 3:10.

it-2-F uku. 278-279 fu. 6

Mika

Wakati fulani kisha pale, Mika pamoya na kikundi fulani ya wanaume, walifuata Wadani. Wakati walifika ku Wadani, Wadani waliuliza Mika kama alikuwa na shida gani. Mika alisema hivi: “Mumekamata miungu yangu yenye nilitengeneza, na mumeenda na kuhani pia. Nimebakia na nini?” Kisha kusikia vile, watoto wa Dani walimuambia kama akiendelea kuwafuata na kuwalalamikia watamushambulia. Wakati aliona vile Wadani walikuwa na nguvu kuliko yeye, aligeuka na kurudia kwake. (Amu 18:22-26) Kisha pale Wadani waliangusha na kulunguza muji wa Laishi na wakajenga pale muji wa Dani. Yonatani na watoto wake walifikia kuwa makuhani wa Wadani, wenye ‘walisimamisha ile sanamu ya kuchongwa yenye Mika alikuwa ametengeneza, na ikabakia kule sikuzote zenye nyumba ya Mungu wa kweli [tabenakulo] ilikuwa katika Shilo.’​—Amu 18:27-31.

Mali ya Kiroho

w15 15/12 uku. 11 fu. 6

Tafsiri ya Biblia Yenye Kuwa Mwepesi Kueleweka

6 Leo, kuko mambo mengi yenye kuonyesha kwamba tunapaswa kutumia jina la Yehova. Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya 2013 inatumia jina la Mungu mara 7216. Ni kusema, jina la Mungu linapatikana katika tafsiri hiyo mara sita zaidi kuliko katika tafsiri ya zamani kwa sababu jina hilo lilipatikana tena mara tano katika Vitabu vya Kukunjwa vya Bahari ya Chumvi vyenye vilipatikana hivi karibuni. (Soma maelezo ya chini.) Jina hilo lilipatikana katika maandiko haya tano: 1 Samweli 2:25; 6:3; 10:26; 23:14, 16. Kuchunguza tena zaidi maandishi ya zamani ya Biblia yenye kutegemeka kulisaidia kupata andiko la sita; andiko hilo ni Waamuzi 19:18.

TAREHE 17-23/1

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | WAAMUZI 20-21

“Endelea Kumuomba Yehova Akuongoze”

w11-SW 15/9 uku. 32 fu. 2

Je, Unaweza Kuwa Kama Finehasi Unapokabili Hali Ngumu?

Baada ya wanaume wa Gibea wa kabila la Benyamini kumlala kinguvu na kumuua suria wa Mlawi fulani, yale makabila mengine yaliamua kwenda kupigana na Wabenyamini. (Amu. 20:1-11) Kabla ya kupigana, walisali kwa Yehova ili awasaidie, lakini wakashindwa mara mbili, na kupata hasara kubwa. (Amu. 20:14-25) Je, wangekata kauli kwamba sala zao hazikujibiwa? Je, kweli Yehova alitaka kuona wakichukua hatua kwa sababu ya kosa ambalo lilikuwa limefanywa?

w05-SW 15/1 uku. 27 fu. 7

Mambo Makuu Katika Kitabu cha Waamuzi

20:17-48​—Kwa nini Yehova aliruhusu Wabenyamini washinde makabila mengine mara mbili, ingawa wao ndio waliostahili kuadhibiwa? Kwa kuruhusu makabila yenye uaminifu yashindwe kwanza, Yehova alijaribu azimio lao la kuondoa uovu katika Israeli.

w11-SW 15/9 uku. 32 fu. 4

Je, Unaweza Kuwa Kama Finehasi Unapokabili Hali Ngumu?

Tunajifunza nini kutokana na kisa hicho? Matatizo fulani yanaweza kuendelea katika kutaniko ingawa wazee wanajitahidi na kumwomba Mungu awasaidie. Jambo kama hilo linapotokea, wazee wanapaswa kukumbuka maneno haya ya Yesu: “Endeleeni kuomba [au kusali], nanyi mtapewa; endeleeni kutafuta, nanyi mtapata; endeleeni kupiga hodi, nanyi mtafunguliwa.” (Luka 11:9) Hata inapoonekana kwamba sala hazijibiwi haraka, wazee wanaweza kuwa na hakika kwamba Yehova atajibu kwa wakati wake.

Mali ya Kiroho

w14 1/5 uku. 11 fu. 4-6

JE, ULIJUA?

Kombeo zilitumiwa namna gani katika vita wakati wa zamani?

Kombeo ndiyo silaha yenye Daudi alitumia ili kumuua Goliathi, aliyekuwa mutu murefu na munene sana. Inawezekana Daudi alijifunza kutumia silaha hiyo katika miaka yake ya ujana alipokuwa muchungaji.​—1 Samweli 17:40-50

Michoro ya kombeo inaonyeshwa kati ya vitu vilivyotengenezwa na Wamisri na Waasiria katika nyakati za Biblia. Silaha hiyo ilitengenezwa kwa mufuko mudogo wa ngozi ao wa nguo ulio wazi wenye kufungwa juu ya kamba mbili. Mupigaji wa kombeo angetia katika mufuko wake jiwe lisilo na vikwaruzo ao la muviringo lililokuwa na ukubwa kama wa chungwa (ndimu-utamu) na ambalo labda lilikuwa na uzito wa gramu 250. Kisha alizungusha kombeo juu ya kichwa chake na kuachilia kamba moja, na kufanya jiwe liende kwa nguvu nyingi sana na kupiga bila kukosea mutu ao kitu kilichoviziwa.

Uchimbuaji katika eneo la Mashariki ya Kati ulifanya watu wapate majiwe mengi sana yaliyotumiwa katika kombeo kwenye vita wakati wa zamani. Labda wapiganaji wa vita wenye ufundi walitupa majiwe kwa mwendo wa kilometa 160 mupaka 240 kwa saa moja. Watu wenye elimu hawakubaliane ikiwa kombeo ilikuwa na uwezo wa upinde, lakini bila shaka kombeo ingeweza kutokeza hatari.​—Waamuzi 20:16.

TAREHE 24-30/1

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | RUTU 1-2

“Onyesha Upendo Mushikamanifu”

w16.02 uku. 10 fu. 5

Uige Marafiki wa Sana wa Yehova

5 Watu wa familia ya Ruthu waliishi Moabu. Angerudia kwa watu wa familia yake, na pengine wangeendelea kumusaidia. Alijua watu wa Moabu, luga yao, na namna yao ya kuishi. Naomi hakuahidi Ruthu kwamba angepata mambo hayo huko Bethlehemu. Pia Naomi aliogopa kwamba Ruthu hangepata mwanaume wa kumuoa ao nyumba yenye angeishi ndani. Kwa hiyo, Naomi alimuambia arudie Moabu. Kama vile tuliona, Orpa ‘alirudia kwa watu wake na kwa miungu yake.’ (Ruthu 1:9-15) Lakini Ruthu alikataa kurudia kwa watu wake na miungu yao ya uongo.

w16.02 uku. 10 fu. 6

Uige Marafiki wa Sana wa Yehova

6 Pengine Ruthu alijifunza juu ya Yehova kupitia bwana yake ao kupitia Naomi. Alijifunza kwamba Yehova haiko kama miungu ya Moabu. Alimupenda Yehova na alijua kwamba anapaswa kumupenda na kumuabudu. Kwa hiyo, Ruthu alichukua uamuzi wenye hekima. Alimuambia Naomi hivi: “Watu wako watakuwa watu wangu, na Mungu wako Mungu wangu.” (Ruthu 1:16) Tunaguswa sana moyo wakati tunafikiria namna Ruthu alimupenda Naomi. Lakini jambo lenye kushangaza sana ni namna Ruthu alimupenda Yehova. Jambo hilo lilimushangaza pia Boazi. Kisha wakati fulani, alimusifu Ruthu kwa sababu ‘alitafuta kimbilio chini ya mabawa ya Yehova.’ (Soma Ruthu 2:12.) Maneno yenye Boazi alisema yanatukumbusha namna kitoto cha ndege kinatafuta ulinzi chini ya mabawa ya wazazi wake. (Zaburi 36:7; 91:1-4) Vilevile, Yehova alimulinda Ruthu kwa upendo na alimubariki kwa sababu ya imani yake. Ruthu hakusikitika hata kidogo kwa sababu ya uamuzi wenye alichukua.

Mali ya Kiroho

w05-SW 1/3 uku. 27 fu. 1

Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ruthu

1:13, 21​—Je, Yehova alifanya maisha ya Naomi yawe machungu na kumsababishia msiba? La, na Naomi hakumlaumu Mungu kwa kosa lolote. Hata hivyo, kwa sababu ya mambo yote yaliyompata, alifikiri kwamba hakuwa na kibali cha Yehova. Alivunjika moyo na kuhisi uchungu. Isitoshe, siku hizo kuzaa kulionwa kuwa baraka kutoka kwa Mungu na kuwa tasa kulionwa kuwa laana. Kwa kuwa Naomi hakuwa na wajukuu na wana wake wawili walikuwa wamekufa, huenda alihisi kwamba alikuwa na sababu nzuri ya kufikiri kuwa Yehova alimfedhehesha.

Hotuba: Familia Ni Nini?

ia uku. 43-44 fu. 5-9

‘Mwanamuke Mwema Sana’

5 Ruthu anapomaliza kupiga​-piga mbegu zake na kuzikusanya zote, anashangaa kuona kwamba ameokota karibu efa moja ya nafaka ya shayiri, ni kusema, litre 22. Labda muzigo wake una uzito wa kilo karibu 14! Anaufunga muzigo huo labda ndani ya vazi, anaunyanyua na kuutia kwenye kichwa, na kisha anakamata njia yake mupaka Bethlehemu, wakati huo usiku unaanza kuingia.​​—Rut. 2:17.

6 Naomi anafurahi sana kumuona binti wake mukwe, na labda anashituka na kushangaa anapoona muzigo huo muzito wa nafaka ya shayiri. Ruthu analeta pia chakula chake kilichobaki kutokana na chakula walichokula wakati Boazi aliwapatia wafanyakazi chakula cha muchana, na wote wawili wanachangia chakula hicho. Sasa Naomi anamuuliza: “Uliokota masalio wapi leo, nawe ulifanya kazi wapi? Yule aliyekuona na abarikiwe.” (Rut. 2:19) Naomi ni muangalifu kabisa; anatambua kwamba Ruthu hakupata chakula kingi hivyo kwa nguvu zake mwenyewe, kunapaswa kuwa na mutu fulani aliyemuhangaikia na kumuonyesha wema.

7 Katika mazungumuzo yao, Ruthu anamuelezea Naomi wema ambao Boazi alimuonyesha. Naomi anaguswa moyo, kwa hiyo anasema: ‘Abarikiwe huyo na Yehova, ambaye hakuacha kuonyesha fazili zake zenye upendo kwa walio hai na wafu.’ (Rut. 2:20) Naomi anaona kwamba ni Yehova aliyemuchochea Boazi ili amuonyeshe Ruthu wema huo. Ni Yehova anayewachochea watumishi wake kuwa wakarimu na anaahidi kwamba atawabariki kwa sababu ya wema wanaoonyesha.​​—Soma Methali 19:17.

8 Naomi anamushauri Ruthu akubali mambo ambayo Boazi alimuambia: aendelee kuokota masalio katika shamba la Boazi na kubaki karibu na wanawake vijana wa nyumba yake ili wanaume waliokuwa wanafanya kazi ya kuvuna wasimusumbue. Ruthu anakubali shauri hilo. Pia, ‘anaendelea kukaa na mama​-mukwe wake.’ (Rut. 2:22, 23) Maneno hayo yanatusaidia tena kuona sifa kubwa ya Ruthu, ni kusema, upendo mushikamanifu. Je, sisi pia tunashikamana na watu wa familia zetu kwa kuwategemeza kwa ushikamanifu na kuwasaidia wanapohitaji musaada? Yehova hakose hata kidogo kuona upendo mushikamanifu kama huo!

9 Je, tunaweza kusema kwamba watu hao wawili tu, Ruthu na Naomi, waliunda familia? Katika sehemu zingine, ili familia iitwe kweli familia, kunapaswa kuwa bwana, bibi, mutoto mwanaume, mutoto mwanamuke, tate (nkambo) na wengine. Lakini mufano wa Ruthu na Naomi unatufundisha kwamba familia za watumishi wa Yehova zinaweza kuwa na furaha, kuonyeshana wema na upendo, hata ikiwa ni familia ndogo sana. Je, wewe unapendezwa na watu wa familia yenu, iwe ni wengi ao wachache? Yesu aliwakumbusha wafuasi wake kwamba hata wale wasio na familia kati yao wanaweza kupata familia katika kutaniko la Kikristo.​​—Mk. 10:29, 30.

TAREHE 31/1–6/2

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | RUTU 3-4

“Jifanyie Sifa ya Muzuri na Uichunge”

w12 1/10 uku. 22 fu. 5

‘Mwanamuke Bora Sana’

Sauti ya Boazi yenye upole na yenye kutuliza, ilimufariji Ruthu sana. Alisema hivi: ‘Yehova na akubariki, binti yangu. Umeonyesha fazili zako zenye upendo kwa njia bora zaidi mara hii ya mwisho kuliko mara ya kwanza. Haukuwafuata vijana, wawe ni wa hali ya chini ao matajiri.’ (Ruthu 3:10) Boazi alipotaja “mara ya kwanza” alipenda kuzungumuzia upendo mushikamanifu ambao Ruthu alimuonyesha Naomi kwa kurudi naye huko Israeli na kwa kumushugulikia. “Mara ya mwisho” ilimaanisha jambo alilofanya kwa kumufuata Boazi kuliko kuwafuata wanaume vijana. Boazi aliona kama mwanamuke kijana kama Ruthu angeweza kutafuta bwana aliye kijana, awe masikini ao tajiri. Kuliko kufanya hivyo, alitaka kufanya mema kwa Naomi na kwa bwana yake aliyekufa, ili kumuendelezea jina katika inchi yake. Ni wazi kama mwanamuke huyo kijana hakuwa mwenye kutafuta faida yake mwenyewe, ndiyo maana Boazi alivutiwa naye.

w12 1/10 uku. 23 fu. 1

‘Mwanamuke Bora Sana’

Ruthu alifurahi sana alipokuwa akiwaza juu ya jambo ambalo Boazi alimuambia​—kama alijulikana kuwa ‘mwanamuke bora sana.’ Alijulikana hivyo kwa sababu ya tamaa yake ya kutaka kumujua Yehova na kumutumikia. Pia, alikuwa ameonyesha upendo mwingi kwa Naomi na kwa watu wake, kwa sababu bila kulazimishwa, alijipatanisha na desturi ambazo hakujua katika inchi yake. Ikiwa tunaiga imani ya Ruthu, tutawaheshimu wengine na kuheshimu desturi zao. Tukifanya hivyo, sisi pia tunaweza kujulikana kuwa watu wazuri.

w12 1/10 uku. 24 fu. 2

‘Mwanamuke Bora Sana’

Boazi akamuoa Ruthu. Kisha hapo, Biblia inasema kama ‘Yehova akamuwezesha kupata mimba naye akazaa mwana.’ Wanawake wa huko Bethlehemu walimubariki Naomi na kumusifu Ruthu kwa sababu alikuwa bora kwa Naomi kuliko watoto saba. Mwishowe, mutoto wa Ruthu akawa tate ya Mufalme Daudi. (Ruthu 4:11-22) Na Daudi akaja kuwa katika vizazi ambamo Yesu alizaliwa.​—Mathayo 1:1.

Mali ya Kiroho

w05-SW 1/3 uku. 29 fu. 3

Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ruthu

4:6​—Mkombozi angewezaje ‘kuharibu’ urithi wake anapokomboa? Kwanza, ikiwa mtu aliyejikuta katika umaskini angeuza shamba lake la urithi, ingembidi mkombozi anunue shamba hilo kwa bei ambayo ingetegemea miaka iliyobaki hadi Yubile ambayo ingefuata. (Mambo ya Walawi 25:25-27) Kufanya hivyo kungepunguza thamani ya shamba lake. Isitoshe, kama Ruthu angezaa mwana, mwana huyo ndiye angerithi shamba hilo lililonunuliwa bali si mtu yeyote wa ukoo wa karibu na mkombozi.

TAREHE 7-13/2

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 1 SAMWELI 1-2

“Fungulia Yehova Moyo Wako Katika Sala”

ia uku. 55 fu. 12

Alimufungulia Mungu Moyo Katika Sala

12 Kwa hiyo, Hana ni mufano muzuri sana kwa watumishi wote wa Mungu kuhusiana na sala. Yehova anawaomba wajisikie huru kuzungumuza naye, bila kusita, wamutupie mahangaiko ya moyo wao kama vile mutoto anayemutumainia baba yake. (Soma Zaburi 62:8; 1 Wathesalonike 5:17.) Mutume Petro aliongozwa na roho ya Mungu ili kuandika maneno haya yenye kufariji kuhusu sala zetu kwa Yehova: ‘Mutupe mahangaiko yenu yote juu yake, kwa sababu yeye [anawahangaikia] ninyi.’​—1 Pet. 5:7.

w07-SW 15/3 uku. 16 fu. 4

Jinsi Hana Alivyopata Amani

Tunaweza kujifunza nini kutokana na mambo hayo yote? Tunaposali kwa Yehova kuhusu mahangaiko yetu, tunaweza kumwambia jinsi tunavyohisi na kusali kutoka moyoni kuhusu kile tunachotaka. Ikiwa hatuwezi kufanya jambo lingine lolote ili kutatua tatizo hilo, tunapaswa kuacha mambo mikononi mwake. Hakuna njia iliyo bora kuliko hiyo.​—Methali 3:5, 6.

Mali ya Kiroho

w05-SW 15/3 uku. 21 fu. 5

Mambo Makuu Katika Kitabu cha Samweli wa Kwanza

2:10​—Kwa nini Hana alisali kwamba Yehova “ampe mfalme wake nguvu” ingawa wakati huo hakukuwa na mfalme wa kibinadamu aliyetawala Israeli? Sheria ya Musa ilikuwa imetabiri kwamba Waisraeli wangekuwa na mfalme wa kibinadamu. (Kumbukumbu la Torati 17:14-18) Katika unabii aliotoa alipokuwa akikaribia kufa, Yakobo alisema hivi: “Fimbo ya enzi [ishara ya mamlaka ya kifalme] haitageuka kando kutoka kwa Yuda.” (Mwanzo 49:10) Isitoshe, kumhusu Sara, nyanya wa Waisraeli, Yehova alisema hivi: “Wafalme wa vikundi vya watu watatoka kwake.” (Mwanzo 17:16) Hivyo, Hana alikuwa akisali kuhusu mfalme wa wakati ujao.

TAREHE 14-20/2

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 1 SAMWELI 3-5

“Yehova Anafikiriaka Wengine”

w18.09 uku. 24 fu. 3

Ni Mweza-Yote Lakini Anafikiria Wengine

3 Samweli alianza kutumika mu tabenakulo wakati alikuwa kijana mudogo sana. (1 Sa. 3:1) Usiku moja, wakati alienda kulala, jambo fulani lenye halikukuwa la kawaida kabisa lilitokea. (Ona maelezo ya chini.) (Soma 1 Samweli 3:2-10.) Alisikia mutu fulani iko anaita jina lake. Samweli aliwaza kama ni Eli, Kuhani Mukubwa mwenye kuzeeka. Kwa hiyo, alionyesha utii wakati aliamuka na kukimbilia kwenye Eli alikuwa na kusema hivi: “Mimi huyu, kwa kuwa umeniita.” Lakini Eli alimuambia hivi: “Sikukuita.” Kisha jambo hilo kutokea mara mbili tena, Eli alitambua kama ni Mungu ndiye alikuwa anamuita Samweli. Kwa hiyo, Eli alimuambia Samweli jambo la kusema kama anasikia tena sauti hiyo, na Samweli alitii. Wakati Yehova alimuita Samweli kwa mara ya kwanza, juu ya nini hakumuambia kama ni yeye alikuwa anamuita? Biblia haiseme. Lakini, inawezekana Yehova alifanya mambo kwa njia hiyo juu alifikiria namna Samweli alikuwa anajisikia.

w18.09 uku. 24 fu. 4

Ni Mweza-Yote Lakini Anafikiria Wengine

4 Soma 1 Samweli 3:11-18. Sheria ya Yehova aliamuru watoto waheshimie watu wakubwa, zaidi sana wale wenye walikuwa na mamlaka. (Kut. 22:28; Law. 19:32) Kwa hiyo, ni nguvu kuwazia kama kijana mudogo kama Samweli angeenda kwa Eli asubui, na kumuambia bila woga ujumbe mukali wa hukumu kutoka kwa Mungu. Biblia inatuambia kama Samweli ‘aliogopa kumuambia Eli kuhusu maono hayo.’ Lakini, Mungu alimuonyesha Eli waziwazi kama ni Yeye alikuwa anaita Samweli. Kwa hiyo, Eli alimuomba Samweli asimufiche hata neno moja lenye Mungu alisema. Samweli alimutii Eli na “akamuambia kila jambo.”

Mali ya Kiroho

w05-SW 15/3 uku. 21 fu. 6

Mambo Makuu Katika Kitabu cha Samweli wa Kwanza

3:3​—Je, kweli Samweli alikuwa akilala katika Patakatifu Zaidi? La. Samweli alikuwa Mlawi wa familia ya Wakohathi ambayo haikuwa familia ya kikuhani. (1 Mambo ya Nyakati 6:33-38) Kwa hiyo, hakuruhusiwa “kuingia ndani ili kuviona vitu vitakatifu.” (Hesabu 4:17-20) Sehemu pekee ya patakatifu ambayo Samweli aliruhusiwa kutumia ni ua wa maskani. Lazima iwe alikuwa akilala mahali hapo. Yaonekana Eli pia alikuwa akilala mahali fulani katika ua. Kwa wazi, maneno mahali “palipokuwa sanduku la Mungu” hurejelea eneo la maskani.

TAREHE 21-27/2

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 1 SAMWELI 6-8

“Mufalme Wako Ni Nani?”

it-2-F uku. 827 fu. 1

Ufalme wa Mungu

Watu Wanaomba Mufalme Mwanadamu. Karibu miaka 400 kisha Waisraeli kutoka Misri, na zaidi ya miaka 800 kisha Mungu kufanya agano pamoya na Abrahamu, Waisraeli waliomba mufalme mwanadamu mwenye atawaongoza. Walipenda kuwa sawa vile mataifa ingine yenye ilikuwa na watawala wanadamu. Ombi yao ilionyesha kama walikatala uongozi wa Yehova. (1Sa 8:4-8) Ni kweli, kulingana na ahadi yenye Mungu alitoleaka Abrahamu na Yakobo walikuwa na sababu ya kutazamia Mungu awasimamishie mufalme. Sababu ingine yenye ilifanya wakuwe na ile tumaini ni unabii juu ya Yuda wenye Yakobo alitoaka na iko ku kitanda mbele akufe (Mwa 49:8-10), maneno yenye Yehova aliambiaka Waisraeli kisha wao kutoka Misri (Kut 19:3-6), Maneno yenye kuwa mu agano ya Sheria (Kum 17:14, 15), na hata mu sehemu fulani ya ujumbe wenye Mungu alifanya nabii Balaamu atoe (Hes 24:2-7, 17). Hana, mama muaminifu wa Samweli, alionyesha pia kama alikuwa na ile tumaini mu sala yake. (1Sa 2:7-10) Lakini, Yehova alikuwa hayafunua kabisa ‘siri yake takatifu’ na alikuwa hayaonyesha wakati yenye alikuwa alishapanga juu ya kusimamisha ule Ufalme na namna ungepangwa. Mupaka pale ilikuwa haiyajulikana kama utakuwa mbinguni ao ku dunia. Kwa hiyo, wakati watu waliomba mufalme mwanadamu ilikuwa ni kutenda kwa kimbele-mbele.

w11-SW 1/1 uku. 27 fu. 2

Alivumilia Licha ya Kuvunjwa Moyo

Ona maneno ya Yehova wakati Samweli alipomweleza jambo hilo katika sala: “Sikiliza sauti ya watu kuhusu mambo yote wanayokuambia; kwa maana hawakukukataa wewe, bali wamenikataa mimi nisiwe mfalme juu yao.” Samweli alifarijika sana, hata hivyo, watu hao walikuwa wamemkosea sana Mungu Mweza Yote! Yehova alimwambia nabii wake awaeleze Waisraeli matokeo mabaya ya kuwa na mfalme wa kibinadamu. Samweli alipowaeleza, bado walisisitiza: “Hapana, bali mfalme atakuwa juu yetu.” Kwa kuwa nyakati zote Samweli alikuwa mtiifu kwa Mungu wake, alienda na kumtia mafuta mfalme ambaye Yehova alimchagua.​—1 Samweli 8:7-19.

w10-SW 15/1 uku. 30 fu. 9

Utawala wa Yehova Umethibitika Kuwa Bora!

9 Historia ilionyesha ukweli wa onyo ambalo Yehova alitoa. Waisraeli walipata matatizo makubwa walipotawaliwa na mfalme wa kibinadamu, hasa mfalme alipokosa kuwa mwaminifu. Tukifikiria mfano huo wa Waisraeli, haishangazi kwamba katika historia yote serikali zinazoongozwa na wanadamu ambao hawamjui Yehova zimeshindwa kuleta mafanikio yenye kudumu. Ni kweli kwamba wanasiasa fulani wanamwomba Mungu abariki jitihada zao za kupata amani na usalama, lakini Mungu anaweza jinsi gani kuwabariki wale ambao hawajitiishi chini ya utawala wake?​—Zab. 2:10-12.

Mali ya Kiroho

w02-SW 1/4 uku. 12 fu. 13

Kwa Nini Ubatizwe?

13 Lazima tugeuke kwanza kabla ya kubatizwa na kuwa Mashahidi wa Yehova. Kugeuka ni hatua ya hiari inayofanywa na mtu ambaye ameamua kwa moyo wote kuwa mfuasi wa Kristo Yesu. Watu hao huacha mwenendo wao mbaya wa zamani na kuazimia kufanya mambo yanayofaa machoni pa Mungu. Katika Maandiko, kitenzi cha Kiebrania na Kigiriki kinachohusiana na neno kugeuka humaanisha kurejea. Hatua hiyo yahusisha kumgeukia Mungu na kuacha njia isiyofaa. (1 Wafalme 8:33, 34) Kugeuka kwataka “kazi zinazofaa toba.” (Matendo 26:20) Kwataka tuache ibada isiyo ya kweli, tuishi kupatana na amri za Mungu, na kumpa Yehova ujitoaji usiohusisha wengine. (Kumbukumbu la Torati 30:2, 8-10; 1 Samweli 7:3) Kugeuka hutokeza mabadiliko katika kufikiri kwetu, miradi yetu, na nyutu zetu. (Ezekieli 18:31) ‘Tunageuka kabisa’ kwa kuacha mwenendo mwovu na kuvaa utu mpya.​—Matendo 3:19; Waefeso 4:20-24; Wakolosai 3:5-14.

TAREHE 28/2–6/3

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 1 SAMWELI 9-11

“Ku Mwanzo Sauli Alikuwa Munyenyekevu na Mwenye Kiasi”

w20.08 uku. 10 fu. 11

Utembee kwa Unyenyekevu na kwa Kiasi Pamoja na Mungu Wako

11 Fikiria mufano wa Mufalme Sauli. Wakati alikuwa kijana, alikuwa na kiasi. Alijua mipaka yake na hata aliogopa kukubali madaraka. (1 Sa. 9:21; 10:20-22) Lakini, wakati fulani kisha Sauli kuwa mufalme, alianza kuwa na kimbelembele. Wakati fulani, Sauli alikuwa anangojea nabii Samweli akuje kutoa zabihu. Kuliko kuonyesha kiasi na kutumaini kama Yehova atatenda kwa ajili ya watu wake, Sauli alikosa uvumilivu na akatoa zabihu ya kuteketezwa hata kama hakukuwa na ruhusa ya kufanya vile. Kwa hiyo, Yehova hakumukubali tena na hangeendelea tena kuwa mufalme. (1 Sa. 13:8-14) Ile habari inatufundisha kama tunapaswa kuepuka kimbelembele.

w14 15/3 uku. 9 fu. 8

Endelea Kuonyesha Roho ya Kujitoa

8 Mufano wa mufalme Sauli wa Israeli unatuonyesha namna roho ya kujipenda wenyewe inavyoweza kuharibu roho yetu ya kujitoa. Sauli alipoanza kutawala, alikuwa mwenye kiasi na munyenyekevu. (1 Sam. 9:21) Alijizuia kuwaazibu wale waliosema vibaya kuhusu utawala wake, hata ikiwa angefikiri kwamba alikuwa na haki ya kutetea mamlaka ambayo Mungu alimupatia. (1 Sam. 10:27) Mufalme Sauli alikubali uongozi wa roho ya Mungu kwa kuwasaidia Waisraeli washinde vita juu ya Waamoni. Na kuliko kujitafutia sifa, alionyesha kwa unyenyekevu kwamba Yehova ndiye aliyewatolea Waisraeli ushindi.​​—1 Sam. 11:6, 11-13.

w95-SW 15/12 uku. 10 fu. 1

Waamoni​—Watu Waliorudisha Uhasama kwa Fadhili

Kwa mara nyingine tena Waamoni walikuwa wamerudisha uhasama kwa fadhili za Yehova. Yehova hakupuuza shambulizi hilo lenye jeuri. “Roho ya Mungu ikamjilia Sauli kwa nguvu, hapo alipoyasikia maneno yale [ya Nahashi], na hasira yake ikawaka sana.” Chini ya mwelekezo wa roho ya Mungu, Sauli alikusanya kikosi cha watu 330000 wenye kupigana vita ambao waliwashinda kabisa Waamoni hivi kwamba ‘hawakuachwa wawili wao pamoja.’​—1 Samweli 11:6, 11.

Mali ya Kiroho

w05-SW 15/3 uku. 22 fu. 8

Mambo Makuu Katika Kitabu cha Samweli wa Kwanza

9:9​—Maneno “nabii wa leo alikuwa akiitwa mwonaji nyakati za kale” yanamaanisha nini? Huenda maneno hayo yakamaanisha kwamba manabii walipozidi kuwa mashuhuri nyakati za Samweli na katika enzi za wafalme katika Israeli, neno “nabii” lilichukua nafasi ya neno “mwonaji.” Samweli huonwa kuwa wa kwanza katika orodha ya manabii.​—Matendo 3:24.

Hotuba: Siri ya Kuzoeza Wengine Muzuri

w15 15/4 uku. 6-7 fu. 16-20

Wazee, Munaona Namna Gani Kazi ya Kuzoeza Wengine?

16 Ukuwe tayari, lakini usisite kuzoeza wengine. Wakati nabii Samweli alisikia kwa mara ya kwanza kwamba Waisraeli walipenda wakuwe na mufalme mwanadamu, alivunjika moyo na alijisikia kuwa wamemukataa. (1 Sam. 8:4-8) Kwa hiyo, alisita kufanya jambo lenye watu walikuwa wamemuomba mupaka Yehova aliona kuwa ni lazima amuambie mara tatu kwamba asikilize sauti yao. (1 Sam. 8:7, 9, 22) Hata hivyo, Samweli hakusikia uchungu ao kumuwekea kinyongo mutu mwenye angechukua nafasi yake. Wakati Yehova alimuambia nabii Samweli amutie Sauli mafuta, nabii Samweli hakutii kwa sababu tu alipaswa kutii, lakini kwa sababu alimupenda Yehova.

17 Leo, wazee wenye uzoefu wanafuata mufano wa nabii Samweli kwa kuzoeza wengine kwa upendo. (1 Pet. 5:2) Wazee kama hao hawakatae kuzoeza wengine kwa kuogopa kwamba wanafunzi hao watachukua mapendeleo yao fulani katika kutaniko. Walimu wazuri hawaone wanafunzi wenye kufanya maendeleo kuwa ndugu wenye kufanya mashindano pamoja nao, lakini wanawaona kama ‘wafanyakazi wenzao,’ ni kusema, zawadi ya bei sana kwa ajili ya kutaniko. (2 Kor. 1:24; Ebr. 13:16) Walimu hao wenye upendo wanafurahi sana wakati wanaona namna wanafunzi hao wanatumia uwezo wao kwa faida ya ndugu na dada katika kutaniko.​—Mdo. 20:35.

18 Ukuwe rafiki, lakini usikuwe mwalimu tu. Wakati nabii Samweli alikutana na Sauli, angechukua chupa ya mafuta, na kumumwangia mbio-mbio kwenye kichwa. Sauli angeenda kuwa mufalme mwenye mamlaka bila kupewa mazoezi fulani. Lakini, kwa upendo nabii Samweli alichukua wakati ili kutayarisha pole-pole moyo wa Sauli. Kisha kula pamoja chakula kitamu, kufanya matembezi yenye kufurahisha, kuongea kwa muda murefu pamoja naye, na kupumuzika vizuri, nabii Samweli aliona kwamba wakati ulikuwa umefika ili kumutia Sauli mafuta.

19 Vilevile, leo walimu wanapaswa kuanza mazoezi kwa kuchukua wakati wa kutafuta nafasi yenye kufaa ili kufanya urafiki pamoja na mwanafunzi. Mambo mbalimbali yenye muzee anaweza kufanya ili kuwa na urafiki pamoja na mwanafunzi, inategemea hali za inchi, eneo, na tabia za watu. Lakini, iwe unaishi wapi, na hata kama uko na kazi nyingi za kufanya katika kutaniko, ikiwa unapitisha wakati pamoja na mwanafunzi, ni kama vile unamuambia hivi: “Ninakuona kuwa wa lazima.” (Soma Waroma 12:10.) Bila shaka, wanafunzi wa kila mahali watakuwa wenye shukrani sana kwa sababu munawahangaikia kwa upendo.

20 Wazee, mukumbuke kwamba, mwalimu mwenye kupata matokeo mazuri haonyeshe tu kwamba anapenda kuzoeza mwanafunzi, lakini anaonyesha pia kwamba anamupenda mwanafunzi. (Linganisha na Yohana 5:20.) Mwanafunzi anatambua haraka sifa hiyo ya lazima ya mwalimu, na hilo linamufanya afurahie sana mazoezi yenye anapewa. Kwa hiyo, wazee wapendwa, wakati munazoeza wengine, mukuwe marafiki, lakini musikuwe walimu tu.​—Met. 17:17; Yoh. 15:15.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine