Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha
TAREHE 4-10/7
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 SAMWELI 18-19
“Barzilai—Mutu Mwenye Kiasi”
w07-SW 15/7 uku. 14 fu. 5
Barzilai—Mtu Aliyetambua Udhaifu Wake
Bila shaka, Daudi alithamini sana msaada wa Barzilai. Haionekani kwamba mfalme alitaka tu kuonyesha shukrani kwa kumwandalia vyakula. Barzilai aliyekuwa tajiri hakuhitaji msaada wa aina hiyo. Huenda Daudi alitaka aishi katika makao ya mfalme kwa sababu ya sifa zenye kuvutia za mzee huyo. Lingekuwa jambo la heshima kwa Barzilai kukaa katika makao hayo muda wote, kwa kuwa angeweza kufaidika kwa sababu ya pendeleo la kuwa rafiki ya mfalme.
w07-SW 15/7 uku. 14 fu. 7
Barzilai—Mtu Aliyetambua Udhaifu Wake
Huenda sababu moja iliyomfanya Barzilai aamue hivyo ni umri wake wa uzee na udhaifu wa kimwili. Labda Barzilai alihisi kwamba hangeishi muda mrefu zaidi. (Zaburi 90:10) Alikuwa amefanya yale aliyoweza ili kumsaidia Daudi, lakini pia alitambua udhaifu aliokuwa nao kwa sababu ya umri wake wa uzee. Barzilai hakuruhusu fahari na umaarufu umzuie kuchanganua kihalisi mambo ambayo angeweza kufanya. Tofauti na Absalomu mwenye tamaa ya makubwa, kwa hekima Barzilai alionyesha kiasi.—Methali 11:2.
w07-SW 15/7 uku. 15 fu. 1-2
Barzilai—Mtu Aliyetambua Udhaifu Wake
Simulizi la Barzilai linakazia uhitaji wa usawaziko. Kwa upande mmoja, hatupaswi kukataa mapendeleo ya utumishi au kukataa kujitahidi kuyafikia kwa sababu tunataka kuishi maisha ya starehe au tunahisi hatuwezi kuyatimiza. Tukimtegemea Mungu atupe nguvu na hekima, yeye anaweza kujazia upungufu wetu.—Wafilipi 4:13; Yakobo 4:17; 1 Petro 4:11.
Kwa upande mwingine, tunahitaji kutambua udhaifu wetu. Kwa mfano, huenda Mkristo tayari ni mwenye bidii katika utendaji wa kiroho. Anatambua kwamba akikubali migawo zaidi, anaweza kupuuza madaraka fulani ya Kimaandiko kama vile kuiandalia familia yake. Katika hali kama hiyo, je, hangekuwa akionyesha kiasi na usawaziko kwa kukataa mapendeleo zaidi wakati huu?—Wafilipi 4:5; 1 Timotheo 5:8.
Mali ya Kiroho
‘Kimbia Mbio Mupaka Mwisho’
19 Kama uko na matatizo ya afya na unajisikia kama wengine wanakuelewa mubaya, mufano wa Mefibosheti unaweza kukutia nguvu. (2 Sa. 4:4) Alikuwa anapambana na afya ya mubaya, na Mufalme Daudi alimuwazia mubaya. Haiko Mefibosheti njo mwenye alijileteaka ile magumu. Lakini, hakuruhusu ile magumu imufanye akuwe na kinyongo; alifurahia mambo ya muzuri yenye alikuwa nayo katika maisha yake. Alikuwa mwenye shukrani juu ya wema wenye Daudi alikuwa amemuonyesha zamani. (2 Sa. 9:6-10) Wakati Daudi alimuelewa mubaya, Mefibosheti alifikiria mambo yote yenye ilihusu ile hali. Hakuacha makosa ya Daudi imufanye akuwe na kinyongo. Na hakumulaumu Yehova juu ya mambo yenye Daudi alifanya. Mefibosheti alikaza akili yake juu ya mambo yenye angeweza kufanya ili kumutegemeza mufalme mwenye Yehova alikuwa ameweka. (2 Sa. 16:1-4; 19:24-30) Yehova aliandikisha mufano muzuri sana wa Mefibosheti katika Neno lake ili utufundishe mambo fulani.—Ro. 15:4.
TAREHE 11-17/7
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 SAMWELI 20-21
“Yehova Ni Mungu wa Haki”
it-1-F uku. 1047 fu. 3
Wagibeoni
Kwa miaka mingi, Wagibeoni waliendelea kuishi, hata kama Mufalme Sauli alikuwa anapanga kuwaangamiza. Lakini Wagibeoni walivumilia, mupaka wakati wenye Yehova atafunua ule ukosefu wa haki. Ni vile alifanyaka kupitia njala ya miaka tatu, wakati Daudi alikuwa mufalme. Kisha kumuuliza Yehova na kujua kama shida ilikuwa ni juu kulikuwa hatia ya damu, Daudi aliuliza Wagibeoni waseme ni nini yenye wangependa kufanyiwa ili kufunika zambi. Palepale Wagibeoni wakajibu na kusema haiko “jambo la feza wala zahabu,” juu kulingana na Sheria, hakuna bei ya ukombozi yenye inaweza kukubaliwa kwa ajili ya muuwaji. (Hes 35:30, 31) Walijua pia kama hawangeweza kuua mutu bila kupewa ruhusa ya kisheria. Kwa hiyo, ni wakati tu Daudi aliwaomba sana, njo walisema wawaletee “wana” saba wa Sauli. Vile hatia ya damu ilikuwa juu ya Sauli na nyumba yake, ile inaonyesha kama kata kama pengine Sauli njo aliongoza ile mauaji, inawezekana “wana” wake pia walishiriki mu ile mauwaji mu njia ya moja kwa moja ao yenye haikukuwa ya moja kwa moja. (2Sa 21:1-9) Mu ile kisa watoto hawangekufa juu ya zambi za baba zao (Kum 24:16) Lakini ilikuwa kufuata kanuni ya kupatia malipizi ya hukumu, yenye inapatana na sheria yenye inasema “uzima utakuwa kwa uzima.”—Kum 19:21.
Mali ya Kiroho
Wazee wa Kutaniko Ni ‘Wafanyakazi Wenzetu kwa Furaha Yetu’
14 Sisi watumishi wa Yehova, tunaendelea kuhubiri duniani pote ijapokuwa vizuizi ambavyo Shetani na watu wake wanatia mbele yetu. Ndugu na dada fulani wanapambana na matatizo makubwa yanayofananishwa na Goliathi, lakini wanayashinda sababu ya kumutegemea Yehova kwa moyo wote. Hata hivyo, wakati fulani tunakuwa wenye kuchoka na kuvunjika moyo katika vita hiyo. Katika hali kama hiyo, tunakuwa wazaifu na tunaweza kushindwa na magumu ambayo kwa kawaida tunavumilia. Wakati kama huo, muzee akitutia moyo, tunaweza kurudiliwa na furaha yetu na nguvu zetu. Ndugu na dada wengi wamekwisha kujionea jambo hilo. Dada mumoja painia mwenye umri wa miaka zaidi ya 60 anasema hivi: “Wakati fulani, sikuwa mwenye kujisikia vizuri, na kazi ya kuhubiri ilinichokesha. Muzee mumoja alitambua kama sikuwa na nguvu na akanitembelea. Tulikuwa na mazungumuzo yenye kutia moyo yenye kutegemea andiko fulani la Biblia. Nilitumikisha mashauri aliyonipa, na hilo lilinisaidia sana. Muzee huyo alitambua hali yangu ya kuwa muzaifu na akanitolea musaada. Huo ulikuwa upendo kabisa!” Bila shaka, inatia moyo kujua kwamba tuna wazee wanaotuhangaikia, na kama Abishai, wako tayari ‘kuja kutusaidia.’
TAREHE 18-24/7
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 SAMWELI 22
“Umutegemee Yehova”
cl-SW uku. 19 fu. 11
Je, Kweli Unaweza ‘Kumkaribia Mungu’?
11 Ni jambo moja kusoma kwamba Mungu “ni hodari kwa nguvu.” (Isaya 40:26) Na ni jambo tofauti kabisa kusoma kuhusu jinsi alivyokomboa Israeli walipovuka Bahari Nyekundu kisha akalitunza taifa hilo jangwani kwa miaka 40. Hebu ona yale maji yenye nguvu yakigawanyika. Ona taifa hilo—lenye jumla ya watu 3,000,000 hivi—likitembea katika bonde kavu la bahari, maji yakiwa yamegandamana na kusimama wima kama kuta kubwa upande huu na upande huu. (Kutoka 14:21; 15:8) Unaweza kuona uthibitisho wa kwamba Mungu aliwatunza na kuwalinda jangwani. Maji yalitiririka mwambani. Chakula kilichokuwa mfano wa punje nyeupe, kilisambaa ardhini. (Kutoka 16:31; Hesabu 20:11) Kisa hicho chaonyesha kwamba Yehova ana nguvu na yeye huzitumia kuwasaidia watu wake. Je, si jambo lenye kutia moyo kujua kwamba sala zetu humfikia Mungu mwenye nguvu ambaye ‘ni kimbilio letu na nguvu yetu, na msaada wetu daima wakati wa taabu’?—Zaburi 46:1, BHN.
w10-SW 1/6 uku. 26 fu. 4-6
“Utatenda kwa Ushikamanifu”
Na tuchunguze maneno ya Daudi kwa makini zaidi. Neno la Kiebrania linalotafsiriwa “-tenda kwa ushikamanifu” linaweza pia kutafsiriwa “-tenda kwa fadhili zenye upendo.” Ushikamanifu wa kweli unategemea upendo. Yehova ni mshikamanifu kwa wale ambao ni washikamanifu kwake kwa sababu anawapenda.
Ona pia kwamba ushikamanifu si hisia tu bali ni sifa inayomsukuma mtu atende. Daudi alijionea kwamba Yehova hutenda kwa ushikamanifu. Daudi alipokabili hali ngumu sana maishani mwake, Yehova alimlinda na kumwongoza kwa ushikamanifu mfalme huyo mwaminifu. Naye Daudi alimshukuru Yehova kwa kuwa alitambua kwamba Yeye ndiye aliyemwokoa “kutoka katika mkono wa adui zake wote.”—2 Samweli 22:1.
Maneno ya Daudi yanamaanisha nini kwetu? Yehova habadiliki-badiliki wala kugeuka-geuka. (Yakobo 1:17) Anaendelea kushikilia kanuni zake na kutimiza ahadi zake. Katika zaburi nyingine, Daudi aliandika hivi: “Yehova . . . hatawaacha washikamanifu wake.”—Zaburi 37:28.
Mali ya Kiroho
Ujiendeshe Kama Aliye Mudogo Zaidi
7 Unyenyekevu wa Mungu ulimutia moyo mutunga-zaburi Daudi. Yeye alimuimbia Yehova hivi: ‘Utanipa ngao yako ya wokovu, na unyenyekevu wako ndio hunifanya niwe mukubwa.’ (2 Sam. 22:36) Daudi alijua kama ikiwa aliweza kufanya mambo mengi makubwa katika Israeli ni kwa sababu Yehova alimutendea kwa unyenyekevu kwa kumuchagua na kumusaidia. (Zab. 113:5-7) Namna gani sisi? Tukifikiria sifa, uwezo, ao mapendeleo mbalimbali tuliyonayo, je, kuna jambo ambalo ‘hatukupokea’ kutoka kwa Yehova? (1 Kor. 4:7) Mutu anayejiendesha kama aliye mudogo zaidi ni ‘mukubwa’ kwa sababu unyenyekevu unamufanya awe na samani machoni pa Yehova. (Lu. 9:48) Namna gani? Acheni tuone.
TAREHE 25-31/7
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 SAMWELI 23-24
“Unaona Vitu Vyenye Uko Unatoa Kuwa Zabihu?”
it-1-F uku. 153
Arauna
Inaonekana Arauna alipenda kutoa fasi, ngombe na kuni kwa ajili ya zabihu kwa bure, lakini Daudi alipenda tu aviuze. 2 Samweli 24:24 inaonyesha kama Daudi aliuza kiwanja cha kupigia-pigia nafaka na ngombe kwa shekeli 50 za feza ($110). Lakini, 1 Mambo ya Nyakati 21:25 inaonyesha kama Daudi aliuza kiwanja kwa shekeli 600 za zahabu (karibu $77000). Mwandikaji wa Samweli wa pili anazungumuzia tu kuuziwa kwa kiwanja, kwenye kulijengwa mazabahu na vitu kwa ajili ya zabihu, na inaonekana kama yeye alikuwa anazungumuzia tu bei ya kuuza nayo vile vitu. Lakini mwandikaji wa Mambo ya Nyakati ya Kwanza, anazungumuzia kujengwa kwa hekalu kwenye kulikuya kufanyika mu ile kiwanja. (1Ny 22:1-6; 2Ny 3:1) Juu kiwanja ya hekalu ilikuwa kubwa sana, njo maana iliuziwa kwa shekeli 600 za zahabu; ni tofauti na ile sehemu kidogo kwenye Daudi alijengaka mazahabu kwa mara ya kwanza.
Mambo Tunayojifunza Kutokana na ‘Picha ya ile Kweli’
8 Ikiwa Mwisraeli alimutolea Yehova zabihu kwa kujipendea ili kuonyesha shukrani, ao ikiwa angetoa zabihu ya kuteketezwa ili kukubaliwa na Mungu, kwa hiyo, hangekuwa na magumu ya kumutolea Yehova munyama aliye bora zaidi. Angekuwa mwenye furaha kwa kumutolea Yehova kilicho bora zaidi. Leo, Wakristo hawaombwi kutoa zabihu kulingana na Sheria ya Musa; lakini wanatoa zabihu mbalimbali katika maana ya kwamba wanatumia wakati, nguvu, na mali yao ili kumutumikia Yehova. Mutume Paulo alisema kwamba ‘tangazo la hazarani’ ambalo Mukristo anafanya kuhusu tumaini lake na “kutenda mema na kushiriki vitu pamoja na wengine” kuwa ni zabihu zinazomupendeza Mungu. (Ebr. 13:15, 16) Maoni yetu na jinsi tunavyoshiriki katika utendaji huo vinaonyesha kwa kadiri gani tunashukuru na kupendezwa na yote ambayo Mungu ametutolea. Kwa hiyo, maoni yetu juu ya kazi ya Mungu na kile kinachotuchochea tushiriki katika kazi hiyo vinalingana na zabihu ambazo Waisraeli walimutolea Mungu kwa kujipendea.
Mali ya Kiroho
w05-SW 15/5 uku. 19 fu. 6
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Pili cha Samweli
23:15-17. Daudi aliheshimu sana sheria ya Mungu kuhusu uhai na damu hivi kwamba wakati huu aliepuka kufanya chochote kile ambacho kingevunja sheria hiyo. Tunapaswa kusitawisha mtazamo kama huo kuelekea amri zote za Mungu.
TAREHE 1-7/8
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 1 WAFALME 1-2
“Unajifunzaka Kupitia Makosa Yako?”
it-2-F uku. 870 fu. 3
Sulemani
Kisha kusikia sauti ya muziki kule Gihoni, hapana mbali sana, na makelele ya watu wako nasema: “Mufalme Sulemani aishi siku nyingi,” Adoniya na wale wenye alikuwa anafanya nao njama, wakakimbia kwa woga na katika muvurugo. Sulemani alionyesha namna utawala wake utakuwa wa amani kwa kukatala kuharibu ao kuchafua kiti yake ya ufalme kwa kulipiza kisasi. Kama Adoniya njo angekuwa pa nafasi ya Sulemani, bila shaka Sulemani angepoteza uzima wake. Adoniya alikimbilia patakatifu ili kupata ulinzi, kwa hiyo Sulemani akatuma ujumbe ili wamulete kwake. Sulemani alimuambia Adoniya kama ataendelea kuishi ikiwa hakuna mambo ya mubaya yenye itapatikana ndani yake, kisha alimuambia arudie ku nyumba yake.—1Fa 1:41-53.
it-1-F uku. 48
Adoniya
Lakini kisha kifo ya Daudi, Adoniya alishawishi Bat-sheba aende amufikishie ombi kwa Sulemani ya kuomba Abishagi, kijana mwanamuke mwenye alikuwa mutunzaji na mwandamani wa Daudi, akuwe bibi yake. Adoniya alisema “ufalme ulipaswa kuwa wangu, na Israeli wote walitazamia kwamba nitakuwa mufalme.” Kwa kusema vile, aliona kama alinyanganywa haki yake, hata kama alijua kwamba ile yote ilifanyika kupitia mukono wa Mungu. (1Fa 2:13-21) Inaonekana kama ile ombi ya Adoniya ilionyesha kama aliendelea kuwa na tamaa ya mubaya sana ya kupenda kulipwa juu alipoteza ufalme, juu kulingana na desturi ya mu mashariki ya zamani, bibi na masuria wa mufalme, walipaswa kuwa tu wa ule mwenye ataanza kutawala kisha yeye. (Linganisha na 2Sa 3:7; 16:21.) Ni vile Sulemani aliona ile ombi yenye ilifanywa kupitia mama yake na aliamuru Adoniya auwawe, Benaya alifanya vile palepale.—1Fa 2:22-25.
Mali ya Kiroho
w05-SW 1/7 uku. 30 fu. 1
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Kwanza cha Wafalme
2:37, 41-46. Ni hatari sana kufikiri kwamba tunaweza kuepuka adhabu tunapovunja sheria! Wale wanaoacha kimakusudi ‘barabara yenye nafasi ndogo inayoongoza kwenye uzima’ watapata matokeo mabaya ya uamuzi wao usio wa hekima.—Mathayo 7:14.
TAREHE 8-14/8
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 1 WAFALME 3-4
“Hekima Ni ya Maana Sana”
Yeye ni Mufano Muzuri wa Kuiga Lakini Pia ni Onyo Kwetu
4 Sulemani alipoanza kutawala, Mungu alimutokea katika ndoto na akamwambia aombe anachotaka. Sulemani aliona kwamba haelewi mambo mengi; kwa hiyo aliomba hekima. (Soma 1 Wafalme 3:5-9.) Mungu alifurahia ombi lake. Kwa hiyo akamupatia Sulemani “moyo wenye hekima na wenye uelewaji” na mali. (1 Fal. 3:10-14) Kama Yesu alivyoonyesha, hekima ya Sulemani ilikuwa kubwa sana hivi kwamba malkia wa Sheba alisikia kuhusu hekima yake na akafunga safari ndefu ili aje kumwona Sulemani na kusikiliza hekima yake.—1 Fal. 10:1, 4-9.
5 Hatutazamie kupata hekima ya kimuujiza kama ile ya Sulemani. Yeye mwenyewe alisema, “Yehova mwenyewe anatoa hekima,” lakini aliandika pia kwamba tunapaswa kujikaza ili kuipata. Aliandika hivi: “Kwa sikio lako usikilize hekima kwa makini, ili uelekeze moyo wako kwenye utambuzi.” Alitumia pia maneno kama vile ‘kuita,’ na ‘kuendelea kutafuta’ hekima. (Met. 2:1-6) Bila shaka, tunaweza kupata hekima.
6 Ni vizuri kujiuliza, ‘Je, ninaipenda kabisa hekima ya Mungu kama Sulemani?’ Kwa sababu ya matatizo ya feza watu wengi wanajitolea sana kuhusu kazi yao, wanatafuta sana feza ao wanabadili maamuzi yao kuhusu aina ya masomo na miaka wanayopaswa kusoma. Wewe na familia yako muna maoni gani juu ya mambo hayo? Je, maamuzi yenu yanaonyesha kwamba munaipenda kabisa hekima ya Mungu na munaitafuta? Je, munaweza kubadilisha mawazo yenu kuhusu feza na mambo ya masomo ili muweze kutafuta hekima zaidi? Kwa kweli, kupata hekima na kuitumia kutatuletea faida milele. Sulemani aliandika hivi: “Ndipo utakapoelewa uadilifu na hukumu na unyoofu, njia yote ya yaliyo mema.”—Met. 2:9.
Mali ya Kiroho
w98-SW 1/2 uku. 11 fu. 15
Yehova Ni Mungu wa Maagano
15 Wazao wa Abrahamu wakiwa wamepangwa kuwa taifa chini ya Sheria, Yehova aliwabariki kulingana na ahadi yake kwa huyo mzee wa ukoo. Mwaka wa 1473 K.W.K., Yoshua, mwandamizi wa Musa, aliongoza Israeli hadi Kanaani. Mgawanyo wa nchi uliofuata miongoni mwa makabila ulitimiza ahadi ya Yehova ya kuipa mbegu ya Abrahamu hiyo nchi. Israeli lilipokuwa lenye uaminifu, Yehova alitimiza ahadi yake ya kulipa ushindi juu ya adui zake. Hilo hasa lilikuwa kweli wakati wa utawala wa Mfalme Daudi. Kufikia wakati wa Solomoni mwana wa Daudi, sehemu ya tatu ya agano la Kiabrahamu ilitimizwa. “Yuda na Israeli walikuwa wengi kama mchanga wa pwani kwa wingi, wakila, na kunywa, na kufurahi.”—1 Wafalme 4:20.
TAREHE 15-21/8
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 1 WAFALME 5-6
“Walitumika kwa Nguvu Sana na kwa Moyo Wote”
w11-SW 1/2 uku. 15
Je, Wajua?
Mbao za mierezi zilizotoka Lebanoni zilikuwa maarufu hasa kwa sababu zilidumu kwa muda mrefu, zilikuwa na harufu nzuri, zilipendeza, na hazikushambuliwa na wadudu. Hivyo, Sulemani alitumia bidhaa bora kabisa katika ujenzi wa hekalu. Leo, kuna misitu michache iliyotawanyika na iliyo midogo ikilinganishwa na misitu mikubwa ambayo zamani ilifunika milima ya Lebanoni.
it-1-F uku. 411
Mwerezi
Ile matumizi ya mierezi iliomba maelfu ya wafanyakazi wa kukata miti, kuibeba na kuipeleka Tiro ao Sidoni pembeni ya Mediterania, kuifunga mafungu-mafungu, kushuka nayo pembeni-pembeni ya bahari, pengine mupaka kule Yopa. Kisha iliomba kuipeleka Yerusalemu kupitia inchi kavu. Ile yote iliwezekana kupitia mapatano yenye Sulemani na Hiramu walifanya. (1Fa 5:6-18; 2Ny 2:3-10) Ile kazi iliendelea sana kiasi ya kwamba ilifikia kusemwa kuhusu Sulemani kama, mu utawala wake alifanya mierezi kuwa mingi kama mikuyu.—1Fa 10:27; linganisha na Isa 9:9, 10.
it-2-F uku. 1047 fu. 7
Hekalu
Wakati alikuwa anapanga namna ya kufanya kazi, Sulemani aliandikisha wanaume 30,000 mu Israeli, alikuwa anawatuma Lebanoni kwa kubadilishana, ni kusema, wanaume elfu 10,000 kila mwezi, na walikuwa wanabakia ku manyumba yao kwa miezi mbili. (1Fa 5:13, 14) Aliandikisha watu elfu 70,000 wa kubeba mizigo kati ya “wakaaji wageni” wa inchi, na watu elfu 80,000 wa kuchonga majiwe. (1Fa 5:15; 9:20, 21; 2Ny 2:2) Sulemani aliweka wanaume 550 kuwa wasimamizi wa kazi, na pengine watu 3,300 kuwa wasaidizi. (1Fa 5:16; 9:22, 23) Ni wazi kwamba watu 250 kati ya wale, walikuwa Waisraeli; na watu 3,600 walikuwa “wakaaji wageni” mu Israeli.—2Ny 2:17, 18.
Mali ya Kiroho
g-SW 5/12 uku. 17, kisanduku
Biblia—Kitabu cha Unabii Sahihi, Sehemu ya 1
KUWEKA WAKATI KWA USAHIHI
Mfano unaoonyesha umuhimu wa Biblia kuweka wakati kwa usahihi unaonyeshwa katika 1 Wafalme 6:1, andiko linaloonyesha wakati ambapo Mfalme Sulemani alianza kazi ya ujenzi wa hekalu huko Yerusalemu. Tunasoma hivi: “Ikawa kwamba katika mwaka wa 480 [miaka 479 kamili] baada ya wana wa Israeli kutoka katika nchi ya Misri, katika mwaka wa nne [wa utawala wa Sulemani], katika mwezi wa Zivu, yaani, mwezi wa pili, baada ya Sulemani kuwa mfalme juu ya Israeli, akaanza kumjengea Yehova nyumba.”
Mfuatano wa matukio ya Biblia unaonyesha kwamba mwaka wa nne wa utawala wa Sulemani ulikuwa mwaka wa 1034 K.W.K. Mwaka huo unatusaidia kufahamu wakati ambapo Waisraeli walitoka Misri kwani unapohesabu kurudi nyuma miaka 479 kamili inatufikisha kwenye mwaka wa 1513 K.W.K.
TAREHE 22-28/8
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 1 WAFALME 7
“Mambo Yenye Tunaweza Kujifunza Kutokana na Nguzo Mbili”
‘Kutoka Katika Milima Utachimba Shaba’
Mufalme Sulemani alitumia kiasi kikubwa cha shaba ili kupamba hekalu la Yerusalemu. Shaba nyingi kati ya hiyo ilikusanywa na baba yake, Daudi, kutoka maeneo ya Siria ambayo alikuwa ameshinda. (1 Mambo ya Nyakati 18:6-8) “Bahari ya kuyeyushwa” yenye shaba, ni kusema, beseni kubwa iliyotumiwa na makuhani ili kunawa, ilikuwa na uwezo wa lita 66,000 za maji na uzito wa toni 30. (1 Wafalme 7:23-26, 44-46) Kisha kulikuwa na nguzo mbili kubwa za shaba ambazo zilishimikwa kwenye mwingilio wa hekalu. Nguzo hizo zilikuwa na urefu wa meta 8 na zilifunikwa na makombe yenye urefu wa meta 2.2. Zilikuwa na shimo ndani, unene wa pande za nguzo hizo ulikuwa wa sentimeta 7 na nusu, na zilikuwa na diametri ya meta 1.7. (1 Wafalme 7:15, 16; 2 Mambo ya Nyakati 4:17) Inashangaza kufikiri juu ya kiasi cha shaba kilichotumiwa ili kutengeneza vitu hivyo.
it-1-F uku. 355
Boazi, II
Moya kati ya zile nguzo kubwa mbili za shaba, kuelekea ngambo wa kaskazini, yenye ilijengwa mbele ya baraza ya hekalu yenye utukufu ya Sulemani, iliitwa Boazi, jina yenye pengine inamaanisha “Kwa Nguvu.” Nguzo yenye ilikuwa ngambo ya kusini, iliitwa Yakini, maana yake “[Yehova] Afanye Imara.” Kwa hiyo, kama tunatia yote mbili pamoya, na mutu akisoma kuanzia kuume kwenda kushoto wakati iko naangalia upande wa mashariki, ilikuwa inaleta hii wazo ‘[Yehova] afanye imara [hekalu] kwa nguvu.’—1Fa 7:15-21; ona KIFUNIKO.
Mali ya Kiroho
it-1-F uku. 257
Kuoga
Wale wenye wanamuabudu Yehova katika utakatifu na usafi, wanapaswa kuwa safi kimwili. Ni vile ilikuwa pia wakati mutu anafanya kazi mbalimbali ku tabenakulo na ku hekalu. Wakati Kuhani Mukubwa Haruni na watoto wake wanaume waliwekwa, walioga mbele ya kuvala manguo yao ya kikuhani. (Kut 29:4-9; 40:12-15; Law 8:6, 7) Juu ya kunawa mikono na migulu yao, makuhani walitumia maji yenye ilikuwa mu beseni ya kunawia ya shaba, yenye ilikuwa mu kiwanja ya tabenakulo, na kisha walinawa mu bahari kubwa ya metali yenye kuyeyushwa, ku hekalu ya Sulemani. (Kut 30:18-21; 40:30-32; 2Ny 4:2-6) Katika Siku ya Kufunika Zambi, kuhani mukubwa alioga mara mbili. (Law 16:4, 23, 24) Wale wenye walitoka mu kambi na mbuzi kwa ajili ya Azazeli na zabihu za wanyama zenye zilibakia, na ngombe mwekundu kwa ajili ya zabihu, walipaswa kuoga na kufula manguo yao mbele ya kurudia mu kambi.—Law 16:26-28; Hes 19:2-10.
TAREHE 29/8–4/9
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 1 WAFALME 8
“Sala ya Unyenyekevu Yenye Sulemani Alifanya Mbele ya Watu kwa Moyo Wote”
w09-SW 15/11 uku. 9 fu. 9-10
Boresha Sala Zako Kupitia Funzo la Biblia
9 Ili sala yetu isikiwe, ni lazima itoke moyoni. Sulemani alitoa sala ya kutoka moyoni, iliyo katika 1 Wafalme sura ya 8, mbele ya umati wa watu uliokusanyika huko Yerusalemu kwa ajili ya kuzinduliwa kwa hekalu la Yehova katika mwaka wa 1026 K.W.K. Baada ya sanduku la agano kuwekwa katika Patakatifu Zaidi na wingu la Yehova kulijaza hekalu, Sulemani alimsifu Mungu.
10 Ichunguze sala ya Sulemani na uone mambo anayotaja kuhusu moyo. Sulemani alitambua kwamba Yehova peke yake ndiye anayeujua moyo wa mwanadamu. (1 Fal. 8:38, 39) Sala hiyohiyo inaonyesha kwamba kuna tumaini kwa mtenda-dhambi ‘anayerudi kwa Mungu kwa moyo wake wote.’ Ikiwa adui angewateka nyara watu wa Mungu, maombi yao yangesikiwa ikiwa mioyo yao ilikuwa kamili kwa Yehova. (1 Fal. 8:48, 58, 61) Hivyo basi, sala zako zinapaswa kutoka moyoni.
w99-SW 15/1 uku. 17 fu. 7-8
Inueni Mikono Yenye Uaminifu-Mshikamanifu Katika Sala
7 Tuwe twasali hadharani au faraghani, kanuni muhimu ya Kimaandiko tupaswayo kukumbuka ni kwamba twapaswa kuonyesha mtazamo wa unyenyekevu katika sala zetu. (2 Mambo ya Nyakati 7:13, 14) Mfalme Solomoni alidhihirisha unyenyekevu katika sala yake ya hadharani wakati wa kuwekwa wakfu kwa hekalu la Yehova huko Yerusalemu. Solomoni alikuwa amemaliza tu mojawapo ya majengo yenye fahari zaidi kuwahi kujengwa duniani. Hata hivyo, yeye alisali kwa unyenyekevu hivi: “Mungu je! atakaa kweli kweli juu ya nchi? Tazama, mbingu hazikutoshi, wala mbingu za mbingu; sembuse nyumba hii niliyoijenga!”—1 Wafalme 8:27.
8 Kama Solomoni, twapaswa kuwa wanyenyekevu tunapowakilisha wengine katika sala ya hadharani. Ingawa twapaswa kuepuka kusikika kana kwamba tunajifanya watakatifu, unyenyekevu waweza kuonyeshwa kwa toni ya sauti yetu. Sala za unyenyekevu hazina majivuno wala unafiki. Hizo huvuta uangalifu, si kwa yule anayesali, bali kwa Yule ambaye kwake sala yatolewa. (Mathayo 6:5) Unyenyekevu pia huonyeshwa kwa yale tusemayo katika sala. Tukisali kwa unyenyekevu, hatutasikika kana kwamba tunadai kwa nguvu kwamba Mungu afanye mambo fulani jinsi tutakavyo. Badala yake, tutamwomba Yehova kwa bidii ili atende kwa njia ipatanayo na mapenzi yake matakatifu. Mtunga-zaburi alitoa kielelezo cha mtazamo ufaao alipoomba kwa bidii hivi: “Ee BWANA, utuokoe, twakusihi; Ee BWANA, utufanikishe, twakusihi.”—Zaburi 118:25; Luka 18:9-14.
Mali ya Kiroho
it-1-F uku 475 fu. 3
Mbingu
Sulemani, mwenye alijenga hekalu mu Yerusalemu alisema kama “mbingu, ndiyo, mbingu za mbingu” haziwezi kumuenea Mungu. (1Fa 8:27) Vile Yehova njo Muumbaji wa mbingu, cheo yake iko juu ya zile mbingu zote, na “jina lake peke yake liko juu sana haliwezi kufikiwa. Ukubwa wake uko juu ya dunia na mbingu.” (Zb 148:13) Yehova anapima mbingu halisi kwa wepesi sana sawa vile tu mutu anaweza kupima chombo fulani kwa kusambaza vidole vyake hivi kwamba ile chombo inakuwa kati ya ku mwisho ya kidole kikubwa na kidole kidogo. (Isa 40:12) Maneno ya Sulemani haimaanishe kama Mungu hana fasi kamili kwenye anaikala. Tena haimaanishe kama Mungu iko fasi yote, mu maana ya kwamba iko kila fasi na mu kila kitu mu njia halisi. Tunajua vile juu Sulemani alisema pia hivi kuhusu Yehova, usikie “kule mbinguni, makao yako,” maana yake makao ya viumbe vya roho.—1Fa 8:30, 39.
Hotuba: Ni Miradi Gani Yenye Tunaweza Kujiwekea Kama Hali Zetu Zinatuwekea Mipaka Fulani?
Furahia Mambo Unaweza Kufanya Kwa Ajili ya Yehova
15 Ni miradi gani unaweza kujiwekea? Umuombe Yehova akusaidie ujue ni miradi gani unaweza kufikia. (Mez. 16:3; Yak. 1:5) Unaweza kufikia moja kati ya miradi yenye ilitajwa mu fungu ya kwanza ya hii habari, ni kusema, kufikia kuwa painia musaidizi ao wa kawaida, kutumika ku Beteli, ao kusaidia mu kazi ya ujenzi? Ao pengine unaweza kujifunza luga ya mupya juu ya kuhubiri habari njema ao hata kuhubiri mu eneo ya kigeni. Unaweza kujifunza mengi zaidi kuhusu ile miradi kwa kusoma sura ya 10 ya kitabu Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova na kwa kuzungumuza na wazee wa kutaniko yenu.* Wakati unajikaza kufikia ile miradi, maendeleo yako itakuwa wazi na furaha yako itaongezeka.
16 Lakini, tusema nini kama hauwezi kufikia moja kati ya miradi yenye tumetoka kuona? Siri ni kutafuta muradi ingine yenye unaweza kufikia. Fikiria kwa mufano hii yenye tunataka kuona sasa.
17 Soma 1Timoteo 4:13, 15. Kama uko ndugu mwenye alishabatizwa, pengine unaweza kujikaza kufikia kuwa musemaji muzuri na mwalimu muzuri. Juu ya nini? Ni juu ‘utazama’ katika kusoma, kusema, na kufundisha muzuri na ile itasaidia wale wenye wanakusikiliza. Ujitilie muradi wa kujifunza na kutumikisha kila somo ya broshua Fanya Bidii Katika Kusoma na Kufundisha. Ujifunze somo moja, kisha ufanye mazoezi ku nyumba, na upime kutumikisha mambo yenye umejifunza wakati unatoa hotuba. Omba mashauri kwa mushauri musaidizi ao kwa wazee wengine “wenye wanafanya kazi kwa bidii katika kusema na kufundisha.” (1 Ti. 5:17) Kazia kwa uangalifu namna ya kutumikisha somo yenye kuwa mu ile broshua lakini pia namna ya kusaidia wasikilizaji wako watie nguvu imani yao ao uwachochee watumikishe mambo yenye wanajifunza. Wakati unafanya vile, utaongeza furaha yako na yao pia.
18 Siye wote tuko na daraka ya kuhubiri na ya kufanya wanafunzi. (Mt. 28:19, 20; Ro. 10:14) Utafurahia kupata ufundi zaidi mu hii kazi ya maana? Ujiwekee miradi fulani yenye kuwa wazi wakati uko unajifunza na kutumikisha mambo yenye umepata mu broshua Kufundisha. Unaweza pia kupata mashauri ingine mu Buku la Mukutano—Utumishi na Maisha ya Mukristo na mu video zenye kuonyesha namna ya kuanzisha mazungumuzo, zenye tunaonaka ku mukutano wa katikati ya juma. Tumia mawazo mbalimbali yenye utapata na uone ni ya wapi inaweza kufaa. Kwa kufuata ile mashauri mbalimbali, bila shaka utapata furaha kubwa sana ya kuwa muhubiri mwenye ufundi kabisa.—2 Ti. 4:5.
19 Haupaswe kusahau muradi moja wa maana sana kuliko miradi yote yenye unaweza kujiwekea, ni kusema, kukomalisha sifa zenye zinamupendeza Mungu. (Gal. 5:22, 23; Kol. 3:12; 2 Pe. 1:5-8) Namna gani unaweza kufikia ile muradi? Waza kwa mufano, unapenda kufanya imani yako ikuwe nguvu zaidi. Unaweza kusoma habari mbalimbali zenye kuwa katika vichapo vyetu, vyenye vinatoa mashauri ya muzuri kuhusu namna ya kutia nguvu imani yako. Bila shaka, utapata faida wakati unaangalia sehemu mbalimbali za JW Télédiffusion zenye zinafasiria namna ndugu na dada zetu walionyesha imani mu magumu mbalimbali. Kisha, unaweza kuona ni mu njia gani unaweza kuiga imani yao mu maisha yako.
Hotuba: Shetani Njo Anatuleteaka Magumu Yote?
w06-SW 15/8 uku. 21 fu. 7-8
Ayubu—Mtu Mvumilivu na Mtimilifu
7 Ingawa Wakristo wengi leo hawateseki kama Ayubu, wanakabili dhiki za aina mbalimbali. Wengi wao hukabili mateso au matatizo ya familia. Pia, matatizo ya kiuchumi au magonjwa yanaweza kulemea. Baadhi yao wamekufa kwa sababu ya imani yao. Bila shaka, hatupaswi kufikiri kwamba kila tatizo tunalokabili husababishwa na Shetani. Huenda matatizo mengine yakasababishwa na makosa yetu au hali tuliyorithi. (Wagalatia 6:7) Sisi sote huathiriwa na uzee na misiba ya asili. Biblia inaeleza waziwazi kwamba leo Yehova hawalindi kimuujiza watumishi wake wasipatwe na matatizo hayo.—Muhubiri 9:11.
8 Hata hivyo, huenda Shetani akatumia matatizo tunayokabili ili kudhoofisha imani yetu. Mtume Paulo alitaja kwamba alisumbuliwa na “mwiba katika mwili, malaika wa Shetani,” aliyeendelea kumpiga “kofi.” (2 Wakorintho 12:7) Iwe alikuwa na matatizo ya afya, kama vile matatizo ya macho au tatizo lingine, Paulo alijua kwamba Shetani angetumia matatizo hayo na matokeo yake ili kumnyang’anya shangwe na utimilifu wake. (Methali 24:10) Leo, huenda Shetani akawachochea watu wa familia, wanashule, au hata serikali za kimabavu kuwatesa watumishi wa Mungu kwa njia fulani.
Hotuba: Ujifunze Kutokana na Wale Wenye Kuwa na Uzoefu mu Kazi ya Kuhubiri
Uwe Muhubiri Mwenye Kufanya Maendeleo
1 Wakristo wanapaswa kufanya maendeleo katika mahubiri. Ndio sababu Yesu alipatia wanafunzi wake mazoezi ambayo yaliwasaidia wakomalishe ufundi wao wa kuhubiri. (Lu. 9:1-5; 10:1-11) Sababu hiyo ilifanya pia Akila na Prisila wamuchukue Apolo na ‘kumufafanulia [kumufasiria] kwa usahihi zaidi njia ya Mungu.’ (Mdo. 18:24-26) Sababu hiyo hiyo ilimuchochea Paulo amutie moyo Timotheo aendelee kukomalisha ufundi wake wa kufundisha, ili maendeleo yake “yawe wazi kwa watu wote.” (1 Tim. 4:13-15) Hata kama tumekuwa wahubiri wa habari njema kwa muda murefu, tuna lazima ya kuendelea kukomalisha ufundi wetu wa kuhubiri.
2 Iga Wengine: Njia moja ya kutusaidia tukomalishe ufundi wetu wa kuhubiri ni kuiga wengine. (Met. 27:17) Kwa hiyo, wakati muhubiri mwenzako anaanzisha mazungumuzo, fuata kwa uangalifu. Omba wahubiri wenye uzoefu mashauri, na usikilize mapendekezo yao kwa uangalifu. (Met. 1:5) Utafanya nini ikiwa uko na matatizo ya kurudilia watu, kuanzisha funzo la Biblia, ao kufanya sehemu ingine ya mahubiri? Omba mwangalizi wa kikundi chenu cha mahubiri ao ndugu mwengine mwenye uzoefu akuzoeze. Pia kumbuka kwamba roho takatifu ya Yehova inaweza kuongeza uwezo wetu, kwa hiyo, muombe Yehova roho yake mara kwa mara.—Luka 11:13.
3 Ndugu ao dada akikupatia pendekezo fulani la kukusaidia ukomalishe ufundi wako, usikasirike hata kama haukumuomba musaada wowote. (Mhu. 7:9) Kama Apolo, ukubali pendekezo hilo kwa unyenyekevu na umushukuru. Kufanya hivyo kunaonyesha kama uko na hekima.—Met. 12:15.
Hotuba: Wahubiri Wakristo Wanapaswa Kusali
Wahubiri Wakristo Wanahitaji Kusali
1 Hatuwezi kutimiza kazi ya kuhubiri kwa nguvu yetu wenyewe. Yehova anatupa nguvu ya kufanya kazi hiyo. (Flp. 4:13) Anatumia malaika zake ili kutusaidia kupata watu walio mfano wa kondoo. (Ufu. 14:6, 7) Ni Yehova anayekomalisha mbegu za kweli tunazopanda na kutilia maji. (1 Kor. 3:6, 9) Ni jambo la lazima sana wahubiri Wakristo wamtegemee Baba yetu wa mbinguni katika sala!
2 Kwa Ajili yao Wenyewe: Tunapaswa kusali kila mara tunapohubiri. (Efe. 6:18) Tunaweza kusali kwa ajili ya mambo fulani gani? Tunaweza kumwomba Mungu atusaidie tuwe na maoni mazuri kuhusu eneo letu na kutupa ujasiri. (Mdo. 4:29) Tunaweza kumwomba Yehova atuongoze kwenye watu wenye mioyo ya haki ambao tunaweza kujifunza nao Biblia. Ikiwa msikilizaji anatuuliza ulizo, tunaweza kufanya sala fupi ya moyoni ili kumwomba Yehova atusaidie kutoa jibu linalofaa. (Ne. 2:4) Tunaweza pia kumwomba atupe hekima ili tutie kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza maishani mwetu. (Yak. 1:5) Pia, Yehova anafurahi tunapotia katika sala zetu maneno ya shukrani kwa ajili ya pendeleo la kuwa watumishi wake.—Kol. 3:15.
3 Kwa Ajili ya Wengine: Tunapaswa pia “kusali kwa ajili ya mutu na mwenzake,” na hata kutaja majina ya wahubiri wenzetu katika sala inapofaa. (Yak. 5:16; Mdo. 12:5) Je, afya mbaya inakuzuia kufanya mengi katika kazi ya kuhubiri? Kwa hiyo, sali kwa ajili ya wahubiri wenzako walio na afya nzuri. Usiwazie kwamba sala zako haziwezi kuwasaidia wengine! Ni vizuri pia kusali kwa ajili ya wenye mamlaka ili wawe na mwelekeo unaofaa kuhusu kazi ya kuhubiri, ili ndugu zetu ‘waendelee kuishi maisha shwari na matulivu.’—1 Tim. 2:1, 2.
4 Kutangaza habari njema katika dunia yote inayokaliwa ni mgawo ambao hatuwezi kutimiza kwa nguvu yetu wenyewe. Ikiwa ‘tunadumu katika sala’ Yehova atatusaidia kutimiza kazi hiyo.—Rom. 12:12.