SOMO YA 20
Namna Kutaniko Inapangwa
Yehova ni Mungu wa utaratibu. (1 Wakorinto 14:33) Njo maana, watu wake wanapaswa kupangwa muzuri. Kutaniko ya Kikristo inapangwa namna gani? Na weye unaweza kufanya nini juu mu kutaniko muendelee kuwa utaratibu?
1. Nani njo kichwa cha kutaniko?
“Kristo ni kichwa cha kutaniko.” (Waefeso 5:23) Yesu iko mbinguni, lakini yeye njo iko naongoza kazi za watu wa Yehova mu dunia yote. Yesu ameweka “mutumwa muaminifu na mwenye busara,” ni kusema, kikundi kidogo ya wazee wenye wamemutumikia Yehova kwa miaka mingi. Wale wazee wanaitwa pia Baraza Yenye Kuongoza. (Soma Matayo 24:45-47.) Zamani, mitume na wazee mu Yerusalemu njo walikuwa wanapatia makutaniko maagizo. Vilevile leo, Baraza Yenye Kuongoza njo inapatiaka makutaniko mu dunia yote maagizo. (Matendo 15:2) Lakini, wazee wa Baraza Yenye Kuongoza hawako viongozi wetu. Wanasomaka Biblia juu ya kujua mambo yenye Yehova anapenda wafanye na wako tayari kufuata muongozo wa Yesu.
2. Wazee ni nani na wako na kazi gani?
Wazee ni wanaume wenye wamemutumikia Yehova kwa uaminifu kwa miaka mingi. Wako pale juu ya kufundisha watu wa Yehova mambo yenye iko mu Biblia, kuwasaidia, na kuwatia moyo. Hawalipiwake. Wanatumikaka “kwa kupenda mbele ya Mungu; hapana kwa kupenda faida yenye haiko ya haki, lakini kwa hamu.” (1 Petro 5:1, 2) Watumishi wa huduma ni wanaume mu kutaniko wenye wanasaidiaka wazee. Kisha wakati fulani, wao pia wanaweza kutimiza mambo yenye inaombwa juu wakuwe wazee.
Baraza Yenye Kuongoza inawekaka wazee fulani kuwa waangalizi wa muzunguko. Kazi yao ni kutembelea makutaniko juu wapatie ndugu na dada maagizo na kuwatia moyo. Wanawekaka wazee na watumishi wa huduma wenye wanatimiza mambo yenye Biblia inaomba.—1 Timoteo 3:1-10, 12; Tito 1:5-9.
3. Kila Shahidi anapaswa kufanya nini?
Ndugu na dada wote mu kutaniko ‘wanasifu jina la Yehova’ kwa kutoa majibu, kwa kupitisha vipindi, hotuba, maonyesho, na kwa kuimba wakati wa mikutano ya kutaniko. Tena, wanafanya vile kwa kuhubiri kadiri wanaweza.—Soma Zaburi 148:12, 13.
TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI
Tuone Yesu ni kiongozi wa namna gani, namna wazee wanajikaza kufuata mufano wake, na namna tunaweza kutii Yesu na kutii wazee.
4. Yesu ni kiongozi muzuri
Yesu anatupatia mualiko wenye kufurahisha. Musome Matayo 11:28-30, na kisha muzungumuzie hii maulizo:
Yesu ni kiongozi wa namna gani? Na anapenda tujisikie namna gani wakati iko natuongoza?
Namna gani wazee wanafuata mufano wa Yesu? Muangalie VIDEO.
Biblia inaonyesha namna wazee wanapaswa kufanya kazi yao.
Musome Isaya 32:2 na 1 Petro 5:1-3, na kisha muzungumuzie hii maulizo:
Kama Yesu, wazee wanajikaza juu ya kusaidia wengine wajisikie muzuri. Kujua vile kunafanya ujisikie namna gani?
Wazee wanafuata mufano wa Yesu mu njia gani zingine?
5. Wazee wanafundisha kupitia mufano wao
Yesu anapenda wazee waone kazi yao namna gani? Muangalie VIDEO.
Yesu anawekea wazee mufano. Musome Matayo 23:8-12, na kisha muzungumuzie hii maulizo:
Biblia inapatia wazee mashauri gani? Unawaza viongozi wa dini wanafuataka ile mashauri?
Wazee wanajikazaka kuendelea kuwa na urafiki muzuri na Yehova, na wanasaidiaka watu wa familia yao wafanye vile pia
Wazee wanahangaikiaka kila mutu mu kutaniko
Wazee wanahubiriaka kila juma
Wazee wanafundishaka mu kutaniko. Tena, wanasaidiaka ku kazi ya usafi na kazi zingine
6. Ni muzuri tutii wazee
Biblia inaonyesha juu ya nini ni muzuri kabisa tutii wazee. Musome Waebrania 13:17, na kisha muzungumuzie hii maulizo:
Juu ya nini Biblia inasema kama tunapaswa kuwa tayari kutii wale wenye wanaongoza? Unaona ile mawazo namna gani?
Musome Luka 16:10, na kisha muzungumuzie hii ulizo:
Juu ya nini tutii wazee hata mu mambo yenye tunaweza kuona kama haiko ya maana sana?
WATU FULANI WANASEMAKA: “Haiko lazima ukuwe mu dini fulani.”
Juu ya nini unawaza kama ni muzuri kumuabudu Mungu mu kutaniko fulani?
KWA KIFUPI
Yesu njo kichwa ao kiongozi wa kutaniko. Tuko tayari kutii wazee wenye ameweka juu wanatutiaka moyo na kutufundisha kupitia mufano wao.
Maulizo ya kujikumbusha
Nani njo kichwa cha kutaniko?
Wazee wanasaidiaka kutaniko namna gani?
Kila Shahidi wa Yehova anapaswa kufanya nini?
HABARI ZINGINE
Ona mambo yenye kuonyesha kama Baraza Yenye Kuongoza na wazee wengine wanahangaikiaka sana Wakristo wote.
Kutia Nguvu Ndugu na Dada Wakati Kazi Yetu Inakatazwa (4:22)
Ujifunze juu ya kazi yenye waangalizi wa muzunguko wanafanyaka.
Maisha ya Mwangalizi wa Muzunguko mu Maeneo ya Mashamba (4:51)
Ona mambo ya maana yenye wanamuke wanafanyaka mu kutaniko.
“Je, Mashahidi wa Yehova Wanawaacha Wanawake Wafundishe?” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 9, 2012)
Ona namna wazee wanafanyaka yao yote juu watie moyo Wakristo wenzao.