Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwbr22 Mwezi wa 9 uku. 1-15
  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha
  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha (2022)
  • Vichwa Vidogo
  • TAREHE 5-11/9
  • TAREHE 12-18/9
  • TAREHE 19-25/9
  • TAREHE 26/9–2/10
  • TAREHE 3-9/10
  • TAREHE 10-16/10
  • TAREHE 17-23/10
  • TAREHE 31/10–6/11
Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha (2022)
mwbr22 Mwezi wa 9 uku. 1-15

Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha

TAREHE 5-11/9

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 1 WAFALME 9-10

“Umusifu Yehova juu Iko na Hekima”

w99-SW 1/7 uku. 30 fu. 6

Ziara Iliyothawabishwa Sana

Alipokutana na Solomoni, malkia akaanza kumjaribu kwa “maswali ya fumbo.” (1 Wafalme 10:1) Neno la Kiebrania lililotumiwa hapo laweza kutafsiriwa “vitendawili.” Lakini hilo halimaanishi kwamba malkia alimwingiza Solomoni katika michezo isiyo na maana. Kwa kupendeza, katika Zaburi 49:4 (BHN), neno hilohilo la Kiebrania limetumiwa kufafanua maswali mazito yanayohusu dhambi, kifo, na ukombozi. Basi, yaonekana kuwa malkia wa Sheba alikuwa akizungumza na Solomoni habari nzito zilizojaribu kina cha hekima yake. Biblia yataarifu kwamba malkia “a[li]zungumza naye mambo yote aliyokuwa nayo moyoni.” Solomoni naye “akamfumbulia maswali yake yote; wala hakukuwa na neno alilofichiwa mfalme asimwambie.”​—1 Wafalme 10:2b, 3.

w99-SW 1/11 uku. 20 fu. 6

Ukarimu Unapokuwa Mwingi

Akiwa ameshangazwa na yale aliyosikia na kuona, malkia huyo alijibu kwa unyenyekevu hivi: “Heri watumishi hawa wako, wasimamao mbele yako siku zote, wakisikia hekima yako.” (1 Wafalme 10:4-8) Hakuwatangaza watumishi wa Solomoni kuwa wenye furaha kwa sababu walizungukwa na utajiri​—ingawa ndivyo ilivyokuwa. Badala yake, watumishi wa Solomoni walibarikiwa kwa sababu wangeweza kusikiliza daima hekima ambayo Solomoni alipewa na Mungu. Malkia wa Sheba ni kielelezo kizuri kama nini kwa watu wa Yehova leo, ambao wanapata kwa wingi hekima ya Muumba mwenywe na ya Mwana wake, Yesu Kristo!

w99-SW 1/7 uku. 30-31

Ziara Iliyothawabishwa Sana

Malkia wa Sheba alivutiwa sana na hekima ya Solomoni na ufanisi wa ufalme wake hivi kwamba “roho yake ilizimia.” (1 Wafalme 10:4, 5) Wengine husema kuwa fungu hilo lamaanisha malkia “alihemahema.” Msomi mmoja hata adokeza kwamba alizimia! Hata iweje, malkia alishangazwa na yale aliyoona na kusikia. Aliwatangaza watumishi wa Solomoni kuwa wenye furaha kwa kusikiliza hekima ya mfalme huyo, naye akamtukuza Yehova kwa kumweka Solomoni kwenye kiti cha ufalme. Kisha akampa mfalme zawadi zenye thamani kubwa, dhahabu pekee ilifikia, kwa bei ya sasa, dola 40000000 hivi. Naye Solomoni akamtunukia zawadi, akampa malkia “haja yake yote, kila alilotaka.”​—1 Wafalme 10:6-13.

Mali ya Kiroho

w08-SW 1/11 uku. 22 fu. 4-6

Je, Wajua?

Mfalme Sulemani alikuwa na dhahabu nyingi kadiri gani?

Maandiko yanasema kwamba Hiramu mfalme wa Tiro, alimpa Sulemani tani nne za dhahabu, na malkia wa Sheba akampa kiasi kama hicho, na meli za Sulemani zilileta zaidi ya tani 15 za dhahabu kutoka Ofiri. Simulizi hilo linasema: “Uzito wa dhahabu iliyoletwa kwa Sulemani katika mwaka mmoja ulijumlika kuwa talanta 666 za dhahabu,” au zaidi ya tani 25. (1 Wafalme 9:14, 28; 10:10, 14) Je, hilo ni kweli? Siku hizo, hazina za dhahabu za wafalme zilikuwa kubwa kadiri gani?

Bamba la kale lenye maandishi ambalo wasomi wanaliona kuwa la kweli, linasema kwamba Farao Thutmose wa Tatu wa Misri (aliyeishi miaka 3500 hivi iliyopita) alitoa tani 13.5 za dhahabu kwa ajili ya hekalu la Amun-Ra huko Karnaki. Katika karne ya nane K.W.K., Mfalme wa Ashuru, Tiglath-pilesa wa Tatu alipokea zaidi ya tani 4 za dhahabu kama kodi kutoka Tiro, na Mfalme Sargoni wa Pili akatoa kiasi kama hicho cha dhahabu kuwa zawadi kwa miungu ya Babiloni. Inaripotiwa kwamba kila mwaka Mfalme Filipo wa Pili wa Makedonia (359-336 K.W.K.) alichimbua zaidi ya tani 28 za dhahabu kutoka kwa migodi ya Pangaeum huko Thrake.

Inasemekana kwamba mwana wa Filipo, Aleksanda Mkuu (336-323 K.W.K.) alipoteka jiji la Uajemi la Susa, alichukua tani 1180 hivi za dhahabu kutoka huko na karibu tani 7000 kutoka kwa eneo lote la Uajemi. Kwa hiyo, kwa kulinganisha na ripoti hizo, ufafanuzi wa Biblia kuhusu kiasi cha dhahabu ya Mfalme Sulemani haujatiliwa chumvi.

TAREHE 12-18/9

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 1 WAFALME 11-12

“Chagua kwa Hekima Mutu wa Kuoana Naye”

w18.07 uku. 18 fu. 7

“Ni Nani Iko Upande wa Yehova?”

7 Wakati Sulemani alikuwa kijana, alikuwa na urafiki muzuri pamoja na Yehova. Mungu alimupatia Sulemani hekima nyingi sana na mugao wa maana wa kujenga hekalu la muzuri sana katika Yerusalemu. Lakini Sulemani alipoteza urafiki wake pamoja na Yehova. (1 Fa. 3:12; 11:1, 2) Sheria ya Mungu ilisema kama mufalme hakupaswa kuoa “bibi wengi, ili moyo wake usipotoke.” (Kum. 17:17) Sulemani hakutii sheria hiyo. Kisha, akafikia kuwa na bibi 700 na masuria 300! (1 Fa. 11:3) Wengi kati ya wanamuke hao hawakukuwa Waisraeli na walikuwa wanaabudu miungu ya uongo. Kwa hiyo, Sulemani hakutii pia sheria ya Mungu yenye ilikataza kuoa wanamuke wenye hawakukuwa Waisraeli.​​—Kum. 7:3, 4.

w19.01 uku. 15 fu. 6

Unaweza Kufanya Nini ili Kulinda Moyo Wako?

6 Shetani anapenda tukuwe kama yeye, ni kusema, mupinzani mwenye kukataa kanuni za Yehova na mwenye kuchochewa na roho ya kujipenda mwenyewe. Shetani hawezi kutukaza tuwaze na kutenda kama yeye. Kwa hiyo, anajaribu kufikia muradi wake kwa kutumia njia zingine. Kwa mufano, anafanya tuzungukwe na watu wenye amekwisha kupotosha. (1 Yo. 5:19) Anatumaini kama tutachagua kupitisha wakati pamoja nao, hata kama tunajua kuwa mashirika ya mubaya ‘yataharibisha’ ao kupotosha namna yetu ya kufikiri na kutenda. (1 Ko. 15:33) Alitumia ile njia ili kumudanganya Mufalme Sulemani na alipata matokeo ya muzuri. Sulemani alioa wanamuke wengi wapagani, na mwishowe “walikuwa na uvutano mukubwa juu yake” na ‘pole kwa pole waligeuza moyo wake’ mbali na Yehova.​—1 Fa. 11:3; maelezo ya chini.

w18.07 uku. 19 fu. 9

“Ni Nani Iko Upande wa Yehova?”

9 Lakini Yehova hawezi kuachilia zambi hata kidogo. Biblia inasema hivi: “Yehova akamukasirikia sana Sulemani, kwa sababu moyo wake ulikuwa umegeuka na kuacha Yehova.” Mungu alikuwa amejaribu kumusaidia Sulemani. “Alikuwa amemutokea mara mbili na alikuwa amemuonya juu ya jambo lilelile, kwamba hapaswe kufuata miungu mingine. Lakini hakutii mambo yenye Yehova alikuwa ameamuru.” Kwa hiyo, Yehova hakumukubali tena na hakumutegemeza tena. Yehova hakuruhusu wazao wa Sulemani watawale juu ya taifa lote la Israeli, na kwa mamia ya miaka walikuwa na magumu ya nguvu sana.​—1 Fa. 11:9-13.

Mali ya Kiroho

w18.06 uku. 14-15 fu. 5-8

Angekubaliwa Na Mungu

Kisha, Rehoboamu alikusanya jeshi lake ili kupigana na makabila yenye yaliasi. Lakini, Yehova alituma nabii Shemaya ili awaambia hivi: ‘Musipande kuenda kupigana na ndugu zenu wana wa Israeli. Murudi kila mumoja nyumbani kwake, kwa maana jambo hili limetokea kwa muongozo wangu.’​​—1 Fal. 12:21-24.

Ilikuwa mwepesi kwa Rehoboamu kumusikiliza Yehova? Watu wangefikiri nini juu ya mufalme wao mupya? Alikuwa amesema kama angewatia adabu “kwa mijeledi,” lakini sasa hangefanya kitu juu ya uasi huo mubaya sana! (Linganisha na 2 Mambo ya Nyakati 13:7.) Lakini, hata kama watu walifikiri mambo gani juu yake, mufalme na jeshi lake ‘walitii neno la Yehova, wakarudi nyumbani kulingana na neno la Yehova.’

Hilo linatufundisha nini? Sikuzote ni jambo la hekima kumutii Mungu hata kama watu wanatucheka kwa sababu ya kufanya hivyo. Mungu atatubariki sikuzote ikiwa tunamutii.​—Kum. 28:2

Rehoboamu alibarikiwa kwa sababu alitii? Ndiyo. Rehoboamu aliendelea kutawala makabila ya Yuda na Benyamini, na aliamua kujenga miji ya mupya katika maeneo hayo. Alifanya pia miji fulani ikuwe yenye nguvu “kwa kiwango kikubwa sana.” (2 Nya. 11:5-12) Na jambo la maana zaidi ni kwamba kwa wakati fulani alitii sheria za Yehova. Kwa sababu katika Ufalme wa makabila kumi watu walianza kuabudu sanamu, watu wengi walifanya safari ya kuenda Yerusalemu ili kuunga mukono Rehoboamu na ibada ya kweli. (2 Nya. 11:16, 17) Kwa hiyo, kwa sababu Rehoboamu alimutii Yehova, ufalme wake ulifikia kuwa wenye nguvu zaidi.

TAREHE 19-25/9

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 1 WAFALME 13-14

“Juu ya Nini Ni Jambo ya Lazima Kutosheka na Kuwa Mwenye Kiasi?”

w08-SW 15/8 uku. 8 fu. 4

Dumisha Ushikamanifu Ukiwa na Moyo Kamili

4 Kisha Yeroboamu anamwambia hivi huyo mtu wa Mungu wa kweli: “Njoo pamoja nami twende nyumbani ule chakula, nami nikupe zawadi.” (1 Fal. 13:7) Sasa nabii huyo atafanya nini? Je, akubali ukarimu wa mfalme baada ya kumtangazia ujumbe wa hukumu? (Zab. 119:113) Au akatae mwaliko wa mfalme, hata ingawa mfalme anaonekana ametubu? Bila shaka, Yeroboamu ni tajiri na anaweza kuwapa marafiki wake zawadi za bei ghali. Ikiwa nabii huyo wa Mungu ana tamaa yoyote moyoni mwake kuelekea vitu vya kimwili, inaelekea mwaliko huo wa mfalme utakuwa kishawishi kikubwa kwake. Hata hivyo, Yehova amemwamuru nabii huyo hivi: “Usile mkate wala usinywe maji, nawe usirudi kwa njia ile uliyoiendea.” Kwa hiyo, nabii huyo anajibu hivi kwa uthabiti: “Hata ukinipa nusu ya nyumba yako, siwezi kwenda pamoja nawe na kula mkate au kunywa maji mahali hapa.” Kisha nabii huyo anatoka Betheli kupitia njia nyingine. (1 Fal. 13:8-10) Uamuzi wa nabii huyo unatufundisha somo gani kuhusu ushikamanifu unaotoka moyoni?​—Rom. 15:4.

w08-SW 15/8 uku. 11 fu. 15

Dumisha Ushikamanifu Ukiwa na Moyo Kamili

15 Tunaweza kujifunza jambo gani lingine kutokana na kosa lililofanywa na yule nabii kutoka Yuda? Andiko la Methali 3:5 linasema hivi: “Mtegemee Yehova kwa moyo wako wote wala usitegemee uelewaji wako mwenyewe.” Badala ya kuendelea kumtegemea Yehova kama alivyofanya wakati uliopita, mara hii nabii huyo kutoka Yuda alitegemea akili zake mwenyewe. Kwa sababu ya kosa hilo, alipoteza uhai wake na uhusiano wake mzuri pamoja na Mungu. Mambo yaliyompata yanakazia vizuri sana umuhimu wa kuwa wenye kiasi na washikamanifu tunapomtumikia Yehova!

w08-SW 15/8 uku. 9 fu. 10

Dumisha Ushikamanifu Ukiwa na Moyo Kamili

10 Nabii huyo kutoka Yuda alipaswa kutambua ujanja wa nabii huyo mzee. Alipaswa kujiuliza, ‘Kwa nini Yehova anamtuma malaika kwa mtu mwingine akiwa na maagizo tofauti kwa ajili yangu?’ Nabii huyo angemwomba Yehova afafanue mwongozo huo waziwazi, lakini Maandiko hayaonyeshi kwamba alifanya hivyo. Badala yake, ‘alirudi pamoja na yule mwanamume mzee ili ale mkate nyumbani kwake na kunywa maji.’ Yehova hakufurahi. Mwishowe, nabii aliyedanganywa alipokuwa njiani akirudi Yuda, alikutana na simba na simba huyo akamuua. Huo ulikuwa mwisho wenye kusikitisha kama nini kwa kazi yake akiwa nabii!​—1 Fal. 13:19-25.

Mali ya Kiroho

w10-SW 1/7 uku. 29 fu. 5

Mkaribie Mungu Yeye Hutafuta Mema Ndani Yetu

Jambo muhimu hata zaidi ni kwamba maneno ya 1 Wafalme 14:13 yanatuambia jambo lenye kupendeza kumhusu Yehova na kile ambacho yeye hutafuta ndani yetu. Kumbuka kwamba jambo fulani jema ‘lilionekana ndani ya’ Abiya. Inaonekana kwamba Yehova aliuchunguza moyo wa Abiya mpaka akapata kiasi fulani cha wema. Kama msomi mmoja alivyosema, akilinganishwa na familia yao, Abiya alikuwa kama lulu pekee “katika rundo la mawe.” Yehova alithamini sana wema wake na kumthawabisha kwa kumwonyesha rehema mtu huyo aliyetoka katika familia ya watu waovu.

TAREHE 26/9–2/10

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 1 WAFALME 15-16

“Asa Alitenda kwa Uhodari​—Na Weye Utafanya Vile?”

w12 15/8 uku. 8 fu. 4

‘Kuna Sawabu kwa Ajili ya Kazi Yenu’

Katika miaka 20 iliyofuata kugawanywa kwa Israeli kuwa falme mbili, Yuda ilikuwa imeharibika sana kwa sababu ya matendo ya kipagani. Asa alipokuwa mufalme katika mwaka wa 977 mbele ya Kristo, watu waliabudu miungu ya uzazi hata kwenye makao ya mufalme. Lakini, habari iliyoongozwa na roho ya Mungu kuhusu utawala wa Asa inasema kama ‘alifanya yaliyokuwa mema na sawa machoni pa Yehova Mungu wake.’ Asa ‘aliondoa mazabahu za kigeni na mahali pa juu, akazivunja nguzo takatifu.’ (2 Nya. 14:2, 3) Asa aliondoa pia katika ufalme wa Yuda “wanaume makahaba wa hekaluni,” waliokuwa wakifanya ngono chafu na kuamini kama matendo yao yanakubaliwa na dini. Asa hakuishia pale. Pia, aliwatia watu moyo ‘wamutafute Yehova Mungu wa mababu zao’ na kushika “sheria na amri” ya Mungu.​​—1 Fal. 15:12, 13; 2 Nya. 14:4.

w17.03 uku. 19 fu. 7

Umutumikie Yehova kwa Moyo Mukamilifu!

7 Namna gani tunaweza kujua ikiwa tumejitoa kwa Yehova kwa moyo wetu wote? Tunaweza kujiuliza hivi: ‘Nitamutii Yehova hata wakati ni vigumu kufanya hivyo? Nimeazimia kabisa kufanya kutaniko lake liendelee kuwa safi?’ Asa alipaswa kuwa na ujasiri mwingi sana ili kutosha tate yake mwanamuke katika cheo chake cha malkia! Wakati fulani, unaweza kuwa na lazima ya kuwa na ujasiri kama Asa. Kwa mufano, utafanya nini ikiwa mutu fulani wa familia yako ao rafiki yako wa sana anafanya zambi, lakini hatubu, na anapaswa kutengwa na kutaniko? Utaazimia kukata urafiki na mutu huyo? Moyo wako utakuchochea kufanya nini?

it-1-F uku. 195

Asa

Kwa kweli, Asa alikosa hekima na utambuzi wa kiroho wakati fulani. Hata vile, alikuwa na sifa za muzuri na hakukuwa muasi-imani. Ile njo ilikuwa mambo ya lazima zaidi hata kama alifanya makosa fulani. Na anaonwa kuwa kati ya wafalme waaminifu wa Yuda. (2Ny 15:17) Mu kipindi ya miaka 41 ya utawala wa Asa, Israeli ilitawaliwa na wafalme munane: Yeroboamu, Nadabu, Baasha, Ela, Zimri, Omri, Tibni (mwenye alitawala sehemu fulani ya Israeli kwa kumupinga Omri), na Ahabu. (1Fa 15:9, 25, 33; 16:8, 15, 16, 21, 23, 29) Kisha Asa kufa, mwana wake Yehoshafati akakuwa mufalme.​—1Fa 15:24.

Mali ya Kiroho

w98-SW 15/9 uku. 21-22

Je, Mungu Ni Halisi Kwako?

Kwa mfano, soma unabii kuhusu adhabu ya kujenga upya Yeriko kisha uchunguze kutimizwa kwake. Andiko la Yoshua 6:26 lasema: “Yoshua akawaapisha kiapo wakati ule, akasema, Na alaaniwe mbele za BWANA mtu yule atakayeinuka na kuujenga tena mji huu wa Yeriko; ataweka msingi wake kwa kufiliwa na mzaliwa wa kwanza wake, tena atayasimamisha malango yake kwa kufiliwa na mtoto wake mwanamume aliye mdogo.” Unabii huo ulitimizwa yapata miaka 500 baadaye, kwa vile twasoma hivi kwenye 1 Wafalme 16:34: “Katika [siku za Mfalme Ahabu], Hieli Mbetheli akajenga Yeriko; akatia misingi yake kwa kufiwa na Abiramu mzaliwa wake wa kwanza, na kuyaweka malango yake kwa kufiwa na mwana wake mdogo Segubu; sawasawa na neno la BWANA alilolinena kwa Yoshua mwana wa Nuni.” Mungu aliye halisi tu ndiye angeweza kupulizia unabii mbalimbali kama huo na kushughulikia kutimizwa kwake.

TAREHE 3-9/10

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 1 WAFALME 17-18

“Mutaendelea Kuyumba-yumba Kati Ya Mawazo Mbili Tofauti Mupaka Wakati Gani?”

w17.03 uku. 14 fu. 6

Onyesha Imani kwa Kukamata Maamuzi Yenye Hekima!

6 Wakati Waisraeli walikuwa wanaishi katika Inchi ya Ahadi, walipaswa kuchagua ikiwa wangemuabudu Yehova ao kutumikia miungu mingine. (Soma Yoshua 24:15.) Pengine huo ungeonekana kuwa uamuzi mwepesi. Lakini, uamuzi wao ungewaletea uzima ao kifo. Wakati wa Waamuzi, Waisraeli waliendelea kukamata maamuzi ya mubaya. Waliacha kumuabudu Yehova na wakaanza kuabudu miungu ya uongo. (Waamuzi 2:3, 11-23) Kisha, wakati wa nabii Eliya, watu wa Mungu walipaswa kuamua ikiwa wangetumikia Yehova ao kutumikia Baali, mungu wa uongo. (1 Wafalme 18:21) Pengine hilo lingeonekana kuwa uamuzi mwepesi kwa sababu kuamua kumutumikia Yehova ni jambo la muzuri zaidi sikuzote. Mutu mwenye kuwa na hekima hangependa kutumikia mungu mwenye hana uzima. Lakini, watu hao walishindwa kukamata uamuzi. Biblia inasema kuwa Waisraeli walikuwa ‘wanayumba-yumba juu ya maoni mawili tofauti.’ Eliya alitia watu moyo kwa hekima waamue kuabudu Mungu wa kweli, Yehova.

ia uku. 88 fu. 15

Alitetea Ibada Safi

15 Kwa hiyo, manabii wa Baali wanaanza kujiendesha kama watu wa wazimu. ‘Wanaanza kuita kwa sauti yao yote, wanajikata-kata na visu na mikuki kulingana na desturi yao, mupaka damu inawatiririka.’ Hakuna chochote, bure tu! ‘Hakuna sauti yoyote, wala hakuna yeyote anayejibu.’ (1 Fal. 18:28, 29) Sababu gani? Kwa sababu hakuna Baali. Ni kitu tu Shetani aliunda katika akili zao ili wasimuabudu Yehova. Ukweli ni huu: kumuacha Yehova ili kutumikia mabwana wengine kunaongoza tu kwenye kuvunjika moyo na kupata haya.​​—Soma Zaburi 25:3; 115:4-8.

ia uku. 90 fu. 18

Alitetea Ibada Safi

18 Mbele ya Eliya kutoa sala yake, labda watu wanaokusanyika hapo wanajiuliza ikiwa Yehova hatakuwa tu wa bure kama Baali. Lakini, kisha sala hawakuwa na wakati wa kujiuliza-uliza tena. Biblia inasema hivi: ‘Ndipo moto wa Yehova ukashuka, ukakula lile toleo la kuteketezwa na zile kuni na mawe na mavumbi, nao ukaramba maji yaliyokuwa katika mutaro.’ (1 Fal. 18:38) Yehova anajibu kwa njia ya ajabu kabisa! Na sasa watu wanafanya nini wanapoona hilo?

Mali ya Kiroho

w08-SW 1/4 uku. 19, kisanduku

Alikaa Macho, na Alingoja

Ukame wa Siku za Eliya Ulikuwa wa Muda Gani?

Eliya, nabii wa Yehova alimtangazia Mfalme Ahabu kwamba ukame huo wa muda mrefu ungekwisha karibuni. Hapana shaka hilo lilitukia “katika mwaka wa tatu,” tukihesabu kuanzia siku ya kwanza ambayo Eliya alitangaza kwamba kutakuwa na ukame. (1 Wafalme 18:1) Yehova alifanya mvua inyeshe baada tu ya Eliya kusema kwamba Angefanya hivyo. Kwa hiyo, huenda watu fulani wakakata kauli kwamba ukame ulikoma kabla ya mwaka wa tatu kwisha na hivyo haukuwa wa miaka mitatu kamili. Hata hivyo, Yesu na Yakobo wanatuambia kwamba ukame uliendelea “kwa miaka mitatu na miezi sita.” (Luka 4:25; Yakobo 5:17) Je, Biblia inajipinga?

Haijipingi. Waona, majira ya kiangazi katika Israeli la kale yalikuwa marefu sana, nayo yangeendelea hata kwa miezi sita. Bila shaka, Eliya alienda kumtangazia Ahabu kuhusu ukame majira ya kiangazi yakiwa tayari marefu na makali zaidi kuliko kawaida. Kwa kweli, ukame ulikuwa umeanza miezi sita hivi mapema. Hivyo, Eliya alipotangaza mwisho wa ukame “katika mwaka wa tatu” tangu tangazo lake la mapema, tayari ukame ulikuwa umeendelea kwa miaka mitatu na nusu hivi. “Miaka mitatu na miezi sita” kamili ilikuwa imepita wakati watu wote walipokusanyika ili kushuhudia lile jaribu kubwa kwenye Mlima Karmeli.

Basi, unapofikiria ukame ambao tayari ulikuwa umeikumba nchi, wazia jinsi Ahabu alivyohisi alipotembelewa na Eliya mara ya kwanza. Watu waliamini kwamba Baali alikuwa “mwendeshaji wa mawingu,” mungu ambaye angeleta mvua na kumaliza majira ya kiangazi. Inaelekea kwamba majira ya kiangazi yalipokuwa marefu kuliko kawaida, watu walijiuliza: ‘Baali yuko wapi? Ataleta mvua wakati gani?’ Hapana shaka kwamba tangazo la Eliya kuhusu kutokuwa na mvua wala umande isipokuwa kwa agizo lake liliwafadhaisha sana waabudu hao wa Baali.​—1 Wafalme 17:1.

Hotuba: Mambo Yenye Imani ya Mujane Inaweza Kutufundisha

w14 15/2 uku. 14-15

Mujane wa Sarefathi Alibarikiwa kwa Sababu ya Imani Yake

Mwanamuke huyo alimujibu hivi: ‘Kama anavyoishi Yehova Mungu wako, mimi sina mukate, isipokuwa mukono mumoja tu wa unga katika mutungi mukubwa na mafuta kidogo katika mutungi mudogo; na tazama, ninakusanya kuni chache, nami nitaenda kutayarisha kitu kwa ajili yangu na mwanangu, nasi tutakula chakula hicho na kufa.’ (1 Fal. 17:12) Maneno hayo yanafunua nini?

Mujane huyo alitambua kwamba Eliya alikuwa Mwisraeli mwenye kumuogopa Mungu. Ndio sababu alisema “kama anavyoishi Yehova Mungu wako.” Inaonekana kwamba hata ikiwa alikuwa anajua mambo fulani kuhusu Mungu wa Israeli, hakutumia maneno “Mungu wangu” alipozungumuza kuhusu Yehova. Aliishi katika Sarefathi, muji ambao pengine ulitegemea Sidoni, muji wa Wafoinike. Inaonekana kabisa kwamba, waabudu wa Baali waliishi katika muji huo wa Sarefathi. Lakini, Yehova alikuwa ameona jambo fulani la pekee katika moyo wa mujane huyo.

Ijapokuwa mujane huyo maskini aliishi kati ya waabudu-sanamu, alionyesha imani katika Yehova. Yehova alimutuma nabii Eliya ili aweze kumusaidia mwanamuke huyo na ili mwanamuke huyo aweze naye kumusaidia Eliya. Kufikia hapa, tunaweza kujifunza jambo moja la maana.

Hata ikiwa Baali aliabudiwa katika muji wa Sarefathi, wakaaji wote wa muji huo hawakuwa wabaya kabisa. Kwa kumutuma Eliya kwa mujane huyo, Yehova alionyesha kwamba anajua watu walio na nia nzuri ambao hawajaanza bado kumutumikia. Kwa kweli, ‘katika kila taifa mutu anayemuogopa [Mungu] na kutenda uadilifu [ao haki] anakubalika kwake.’​—Mdo. 10:35.

Watu wengi wanaoishi katika eneo lako wanafanana na mujane wa Sarefathi. Ijapokuwa wanaishi kati ya watu wanaoamini sana dini ya uongo, watu hao wana hamu ya kujua kweli. Pengine wanajua mambo machache juu ya Yehova ao hawajue kitu, kwa hiyo wanahitaji kusaidiwa ili wamuabudu Mungu kwa njia inayofaa. Je, unajikaza kutafuta na kusaidia watu kama hao?

‘UNITAYARISHIE KWANZA KIPANDE KIDOGO CHA MUKATE’

Fikiria kwa uangalifu yale ambayo Eliya alimuomba mujane huyo afanye. Mujane alikuwa amemuambia kwamba angetayarisha chakula kidogo walichokuwa nacho na kukitumia pamoja na mwana wake, na baadaye wangekufa. Lakini, Eliya alisema nini? “Usiogope. Nenda, fanya kulingana na neno lako. Ila tu unitayarishie kwanza kipande kidogo cha muviringo cha mukate kutokana na kile kilichopo, nawe uniletee hiyo, na unaweza kutayarisha kitu kwa ajili yako na mwana wako baadaye. Kwa maana Yehova Mungu wa Israeli, amesema hivi: ‘Ule mutungi mukubwa wa unga hautamalizika, na ule mutungi mudogo wa mafuta hautapungua mupaka siku Yehova atakapoleta mvua juu ya uso wa inchi.’”​—1 Fal. 17:11-14.

Ikiwa ungeambiwa hivyo, pengine ungejibu hivi: ‘Unasema nini? Nikupatie chakula chetu? Hatuna kingine.’ Lakini mujane huyo hakusema hivyo. Hata ikiwa hakujua mambo mengi kumuhusu Yehova, aliamini maneno ya Eliya na alifanya namna alivyoombwa. Imani yake ilijaribiwa kabisa, lakini alitenda kwa hekima!

Mungu hakumusahau mujane huyo maskini. Kama vile Eliya alivyosema, Yehova alizidisha chakula kidogo alichobaki nacho ili kiweze kusaidia Eliya, mujane huyo, na mwana wake mupaka wakati mvua ilinyesha. Kwa kweli, ‘ule mutungi mukubwa wa unga haukumalizika, wala ule mutungi mudogo wa mafuta haukupungua, kulingana na neno la Yehova alilokuwa amesema kupitia Eliya.’ (1 Fal. 17:16; 18:1) Ikiwa mwanamuke huyo hangefanya hivyo, kipande cha mukate ambacho alitengeneza kwa unga na mafuta kidogo aliyokuwa nayo, hicho kingekuwa chakula chake cha mwisho. Lakini, alitenda kwa imani, alimutumaini Yehova, na alimukulisha Eliya kwanza.

Hilo linatufundisha kwamba Mungu anawabariki wale walio na imani. Ikiwa unaonyesha imani unapojaribiwa, Yehova atakusaidia. Atakutimizia mahitaji yako, atakulinda, atakuwa Rafiki yako ili akusaidie kupambana na jaribu.​—Kut. 3:13-15.

Katika mwaka wa 1898, gazeti Le Phare de la Tour de Sion (linaloitwa sasa Munara wa Mulinzi) lilizungumuzia somo hili ambalo tunaweza kujifunza kutokana na hadisi hiyo ya mujane: “Kwa kuwa mwanamuke huyo alikuwa na imani iliyomuwezesha kutii, basi alistahili kubarikiwa na Bwana kupitia Nabii huyo; ikiwa hangeonyesha imani, kungepatikana mujane mwingine ambaye angeonyesha imani. Hali hiyo inatufikia sisi pia. Bwana anaruhusu hali mbalimbali zitupate katika maisha ili kujaribu imani yetu. Tutabarikiwa ikiwa tunaonyesha imani; ikiwa hatutende hivyo, tutapoteza baraka zake.”

Tunapopambana na majaribu fulani, tunapaswa kutafuta uongozi wa Mungu katika Maandiko na katika vichapo vyetu vinavyotegemea Biblia. Kisha, tunapaswa kutenda kulingana na uongozi wa Yehova hata ikiwa inaweza kuwa vigumu kufanya hivyo. Bila shaka, tutabarikiwa ikiwa tunatenda kulingana na maneno haya yenye hekima: ‘Mutegemee Yehova kwa moyo wako wote wala usitegemee uelewaji wako mwenyewe. Mutambue yeye katika njia zako zote, naye atanyoosha mapito yako.’​—Met. 3:5, 6.

‘UMEKUJA HAPA ILI KUMUUA MWANA WANGU?’

Imani ya mujane huyo ilikuwa karibu kujaribiwa kwa njia nyingine. Biblia inasema hivi: ‘Baada ya mambo hayo mwana wa yule mwanamuke, mwenye nyumba hiyo, akawa mugonjwa, na ugonjwa wake ukawa mukali sana hivi kwamba akaacha kupumua.’ Alipotaka kujua sababu gani anapatwa na musiba huo, mwanamuke huyo aliyefiwa, alimuambia Eliya hivi: ‘Nina nini nawe [ao nimekufanya nini], E e mutu wa Mungu? Umekuja hapa ili kurudisha kumbukumbu la [ao kunikumbusha] kosa langu na kumuua mwana wangu?’ (1 Fal. 17:17, 18) Maneno hayo ya huzuni yanaonyesha nini?

Je, mwanamuke huyo alikuwa akifikiria kosa fulani alilofanya ambalo lilisumbua zamiri yake? Je, alifikiria kwamba kifo cha mwana wake kilikuwa malipizi ya Mungu juu ya kosa hilo na kwamba Eliya alikuwa mujumbe wa Mungu aliyeleta kifo? Biblia haiseme hivyo, lakini tunajua kwamba: Mujane huyo hakusema kwamba Mungu amemutendea isivyo haki kwa njia yoyote.

Eliya alihuzunika sana sababu ya kifo cha mwana wa mujane na kwa sababu mujane huyo alifikiri kwamba Eliya ndiye aliyemuletea musiba huo. Kisha kupeleka mwili wa mwana wa mujane katika chumba cha juu, Eliya alisali hivi: ‘Ee Yehova Mungu wangu, je, tena unaleta mabaya juu ya mujane ninayekaa naye kwa kumuua mwana wake?’ Nabii huyo alifikiri kwamba jina la Mungu lingelaumiwa ikiwa angeruhusu mwanamuke huyo mwema na mukaribishaji-wageni ateseke zaidi. Kwa hiyo Eliya alimulilia Yehova hivi: ‘Ee Yehova, Mungu wangu, tafazali, rudisha nafsi [ao uzima] ya mwana huyu ndani yake.’​—1 Fal. 17:20, 21.

“TAZAMA, MWANA WAKO YUKO HAI”

Yehova alikuwa anasikiliza. Mujane huyo alikuwa amemupatia nabii chakula na alikuwa ameonyesha imani. Inaonekana kwamba, Mungu aliruhusu ugonjwa wa mwana huyo umuue, kwa sababu alijua kwamba ufufuo wake​—ambao ndio wa kwanza katika Maandiko​—ungetokea na ungetolea vizazi vya wakati ujao tumaini. Eliya alimulilia Yehova afufue mwana huyo, naye alifanya hivyo. Wazia furaha ya mujane huyo wakati Eliya alimuambia hivi: “Tazama, mwana wako yuko hai [muzima]”! Kisha mujane huyo alimuambia Eliya hivi: ‘Kwa kweli sasa najua kwamba wewe ni mutu wa Mungu na kwamba neno la Yehova kinywani mwako ni la kweli.’​—1 Fal. 17:22-24.

Habari inayopatikana katika 1 Wafalme sura ya 17 haiseme mambo mengine tena kuhusu mwanamuke huyo. Kwa kuwa Yesu alimusifu mwanamuke huyo, inawezekana aliendelea kuwa mwaminifu kwa Yehova mupaka mwisho wa maisha yake. (Lu. 4:25, 26) Hadisi yake inatufundisha kwamba Mungu anawabariki wale wanaotendea mema watumishi wake. (Mt. 25:34-40) Inaonyesha kwamba Mungu anawatimizia watumishi wake waaminifu mahitaji yao, hata katika hali ngumu. (Mt. 6:25-34) Habari hii inaonyesha pia kwamba Yehova anatamani na ana uwezo wa kufufua wafu. (Mdo. 24:15) Tuna sababu nzuri kabisa za kuendelea kukumbuka mujane wa Sarefathi.

TAREHE 10-16/10

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 1 WAFALME 19-20

“Umuombe Yehova Akufariji”

w19.06 uku. 15 fu. 5

Umutegemee Yehova Wakati Uko na Mahangaiko

5 Soma 1 Wafalme 19:1-4. Lakini, Eliya aliogopa wakati Malkia Yezebeli alisema kama atamuua. Kwa hiyo, alikimbilia katika eneo la Beer-sheba. Alivunjika moyo sana mupaka “akaomba akufe.” Ni nini ilifanya Eliya ajisikie vile? Alikuwa mutu mwenye hakamilike, “mutu mwenye hisia kama zetu.” (Yak. 5:17) Pengine alikuwa na mahangaiko mingi na alijisikia kuwa mwenye kuchoka sana. Pengine Eliya aliwaza kama bidii yenye alikuwa amefanya ili kuendelesha ibada safi ilikuwa ya bure, aliwaza kama mambo iliendelea kuharibika katika Israeli, na kama yeye tu njo mutumishi wa Yehova mwenye alikuwa amebakia. (1 Fa. 18:3, 4, 13; 19:10, 14) Namna nabii huyo muaminifu alitenda inaweza kutushangaza. Lakini Yehova alielewa namna Eliya alikuwa anajisikia.

ia uku. 103 fu. 13

Mungu Wake Alimufariji

13 Unafikiri Yehova anajisikia namna gani anapotazama kutoka mbinguni na kuona namna nabii wake mupendwa anavyolala chini ya muti katika jangwa na anaomba kufa? Jibu haliko mbali. Eliya anapolala usingizi muzito, Yehova anamutumia malaika. Malaika anamulamusha Eliya kwa upole, anamugusa na kumuambia: ‘Amuka, kula.’ Eliya anafanya hivyo, kwa kuwa malaika alikuwa amemuwekea tayari chakula chepesi: mukate wenye joto na pia maji. Je, Eliya alimushukuru malaika huyo? Habari inasema tu kwamba nabii alikula na kunywa na kisha akaendelea kulala. Je, Eliya ni mwenye kuvunjika moyo sana hivi kwamba hawezi kuzungumuza? Hata ikiwa ni hivyo ao hapana, malaika anamulamusha kwa mara ya pili, labda wakati usiku unataka kucha. Anamuambia tena, ‘Amuka, kula,’ kisha anamutia moyo hivi, ‘kwa maana safari ni ndefu sana kwako.’​​—1 Fa. 19:5-7.

ia uku. 106 fu. 21

Mungu Wake Alimufariji

21 Kuhusu kila tukio, habari inasema kwamba Yehova hakuwa katika maonyesho hayo yenye kuogopesha sana ya nguvu za asili. Eliya anajua vizuri kwamba Yehova si kitu fulani cha kuwazia kama vile Baali ambaye ni mungu wa kuwazia tu, ambaye anatukuzwa na waabudu wake wanaodanganywa kuwa yeye ni “muendeshaji wa mawingu,” ao ni yeye anayeleta mvua. Yehova ndiye Chanzo kabisa cha nguvu zote zenye kuogopesha zinazopatikana katika vitu alivyoumba, lakini yeye pia ni mukubwa sana kuliko kila kitu alichoumba. Hawezi kuenea hata katika mbingu zenyewe! (1 Fal. 8:27) Mambo hayo yote yanamusaidia Eliya namna gani? Usisahau kwamba yeye anaogopa. Lakini, Yehova Mungu iko upande wake, Mungu aliye na nguvu za ajabu sana kama hizo; kwa hiyo, Eliya hapaswe kumuogopa Ahabu wala Yezebeli!​​—Soma Zaburi 118:6.

ia uku. 106 fu. 22

Mungu Wake Alimufariji

22 Kisha moto kupita, kunakuwa na kimya na kisha Eliya anasikia “sauti tulivu, ya chini.” Inamuomba aeleze namna anavyojisikia, naye anafanya hivyo, anaeleza mahangaiko yake kwa mara ya pili. Labda hilo linamutuliza. Lakini anatulizwa tena zaidi na maneno ambayo ile “sauti tulivu, ya chini” inamuambia. Yehova anamuhakikishia Eliya kuwa yeye [Eliya] si mutu wa bure. Namna gani? Mungu anamufunulia mambo mengi kuhusu kusudi lake la wakati ujao la kupiganisha ibada ya Baali katika Israeli. Kwa hiyo, kazi ya Eliya haikuwa ya bure, kwa sababu bado kusudi la Mungu linaendelea kutimizwa. Tena, Eliya ana daraka katika kutimizwa kwa kusudi hilo, kwa sababu Yehova anamutuma tena kufanya kazi na anamupatia maagizo kamili.​​—1 Fal. 19:12-17.

Mali ya Kiroho

w97-SW 1/11 uku. 31 fu. 2

Kielelezo cha Kujidhabihu na cha Uaminifu-Mshikamanifu

Wengi wa watumishi wa Mungu leo huonyesha roho hiyohiyo ya kujidhabihu. Baadhi yao wameacha “mashamba” yao, riziki zao, ili kuhubiri habari njema katika maeneo ya mbali au kutumikia wakiwa washiriki wa familia ya Betheli. Wengine wamesafiri hadi nchi za kigeni ili kufanya kazi kwenye miradi ya ujenzi ya Sosaiti. Wengi wamekubali zile ambazo huenda zikaitwa kazi za hali ya chini. Lakini, hakuna yeyote amtumikiaye Yehova kama mtumwa ambaye anafanya utumishi duni. Yehova huthamini wote ambao humtumikia kwa kupenda, naye atabariki roho yao ya kujidhabihu.​—Marko 10:29, 30.

TAREHE 17-23/10

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 1 WAFALME 21-22

“Iga Namna ya Yehova ya Kutumia Mamlaka”

it-1-F uku. 1266

Yehova wa Majeshi

Wakati Yoshua aliona malaika mwenye alikuya kuwatembelea karibu na Yeriko na kumuuliza ikiwa iko upande wa Israeli ao adui wa Israeli, ule malaika alimujibia hivi: “Hapana, mimi ni mukubwa wa jeshi la Yehova, na nimefika sasa.” (Yos 5:13-15) Nabii Mikaya aliambia Mufalme Ahabu na Yehoshafati hivi: “Nilimuona Yehova akiwa amekaa kwenye kiti chake cha ufalme na jeshi lote la mbinguni likiwa limesimama pembeni yake, upande wake wa kuume na upande wake wa kushoto,” Bila shaka alikuwa nazungumuzia wana wa roho wa Yehova. (1Fa 22:19-21) Maneno Yehova wa Majeshi inafaa kabisa itumiwe vile mu uwingi, juu kulingana na Biblia, malaika hawagawanywe tu mu vikundi vya makerubi, maserafi, na malaika (Isa 6:2, 3; Mwa 3:24; Ufu 5:11) lakini wanafanyiza pia vikundi vyenye kupangwa muzuri. Njo maana Yesu alisema kama iko na “malejioni zaidi ya kumi na mbili (12) ya malaika” wenye wanaweza kuya kumusaidia. (Mt 26:53) Wakati Hezekia alikuwa naomba Yehova amusaidie, alimuita “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, mwenye kukaa ukiwa mufalme juu ya makerubi,” bila shaka alikuwa nazungumuzia sanduku ya agano na alama za makerubi wenye walikuwa ku mufuniko ya ile sanduku; na ile iliwakilisha kiti ya ufalme ya Yehova yenye kuwa mbinguni. (Isa 37:16; linganisha na 1Sa 4:4; 2Sa 6:2.) Maono ya kimuujiza yenye mutumumishi wa Elisha mwenye kuwa na woga aliona, ilimufanya asikuwe tena na woga. Mu ile maono aliona milima pembeni ya muji wenye kuzungukwa na maaskari kwenye nabii Eliya alikuwa anaishi, ‘imejaa farasi na magari ya vita ya moto,’ walikuwa sehemu ya malaika wa Yehova.​—2Fa 6:15-17.

w21.02 uku. 4 fu. 9

“Kichwa cha Kila Mwanaume Ni Kristo”

9 Unyenyekevu. Yehova iko na hekima kuliko mutu mwingine yeyote. Lakini, anasikilizaka mawazo ya watumishi wake. (Mwa. 18:23, 24, 32) Alipatia wale wenye kuwa chini ya mamlaka yake nafasi ya kutoa mapendekezo yao. (1 Fa. 22:19-22) Yehova ni mukamilifu, lakini kwa sasa, hatazamie tufanye mambo kwa ukamilifu. Tofauti na ile, anasaidiaka wanadamu wenye hawakamilike wenye wanamutumikia. (Zb. 113:6, 7) Biblia hata inamuita Yehova kuwa “musaidizi.” (Zb. 27:9; Ebr. 13:6) Mufalme Daudi alitambua kama ni unyenyekevu wa Yehova tu njo ulimuwezesha kutimiza mambo yote yenye alifanya.​​—2 Sa. 22:36.

it-2-F uku. 255

Uongo

Yehova anaachaka watu wenye hawapende kweli “wapotoshwe ili wafikie kuamini uongo” kuliko kuamini habari njema juu ya Yesu Kristo. (2Te 2:9-12) Ile inaonekana wazi zamani mu mambo yenye ilifikiaka Ahabu, mufalme wa Israeli. Manabii waongo walimuhakikishia kama angepata ushindi juu ya Ramoti-Gileadi; lakini Mikaya, nabii wa Yehova, alitabiri kama Ahabu hangepata ushindi. Sawa vile inaonyeshwa mu maono yenye Yehova alifunulia Mikaya, Yehova aliruhusu kiumbe wa roho akuwe “roho ya udanganyifu” mu kinywa ya manabii wa Ahabu. Ni kusema, ule kiumbe wa roho alitumia nguvu yake juu yao ili waseme, hapana ukweli, lakini mambo yenye wao wenyewe walipenda kusema na yenye Ahabu alipenda kusikia. Hata kama Ahabu alikuwa ameonywa, alipendelea kudanganywa na maneno yao ya uongo, na ile ilimupeleka ku kifo.​—1Fa 22:1-38; 2Nya 18.

Mali ya Kiroho

w21.10 uku. 3 fu. 4-6

Kutubu Kikweli Maana Yake Nini?

4 Ku mwisho ya yote, wakati wa kutenda wa Yehova ukafika. Alimutuma Eliya ili atangaze hukumu juu ya Ahabu na Yezebeli. Familia yao yote ingeuawa. Maneno ya Eliya ilimuhuzunisha sana Ahabu! Lakini jambo ya kushangaza, Ahabu mwenye alikuwa na kiburi sana ‘akajinyenyekeza.’​​—1 Fa. 21:19-29.

5 Hata kama Ahabu alijinyenyekeza mu ile wakati, mwenendo wenye alionyesha kisha pale, ulionyesha kama hakutubu kikweli. Hakutosha ibada ya Baali mu Ufalme wake. Na hakuchochea watu wamuabudu Yehova. Na mambo ingine yenye Ahabu alifanya inahakikisha kama hakutubu kikweli.

6 Kisha, Ahabu alimuambia Yehoshafati Mufalme wa Yuda, waende pamoja ili kupigana na Wasiria. Yehoshafati alikuwa Mufalme muzuri mwenye alimutumainia Yehova. Na alimuambia Ahabu, wamuulize kwanza nabii wa Yehova mambo yenye walipaswa kufanya mbele waende ku vita. Mara moja, Ahabu hakuitika ile wazo. Akasema: “Kungali mutu mumoja mwenye kupitia yeye tunaweza kumuuliza Yehova; lakini ninamuchukia, kwa maana hatabiri hata kidogo mambo ya muzuri juu yangu, ya mubaya tu.” Hata vile, walienda kumuona nabii Mikaya. Ahabu alisema kweli, nabii wa Mungu alitabiri mambo ya mubaya kumuhusu! Kuliko kutubu na kutafuta musamaha wa Yehova, muovu Ahabu alimutupa nabii wa Yehova mu gereza. (1 Fa. 22:7-9, 23, 27) Hata kama Ahabu alimutia Mikaya mu gereza, ile haikufanya unabii usitimie. Ku vita yenye ilifuata, Ahabu aliuawa.​—1 Fa. 22:34-38.

Hotuba: Uaminifu-mushikamanifu wa Naboti Unatufundisha Nini?

w15 15/3 uku. 9-11 fu. 10-12

“Ndiyo Njia Iliyokubaliwa Nawe”

10 Kwa muda wa miaka mingi, Yehova amemusaidia ‘mutumwa mwaminifu na mwenye busara’ akuwe mwenye busara zaidi. Busara imemusaidia akuwe mwangalifu zaidi wakati anafasiria kwamba habari fulani zenye kuzungumuziwa katika Biblia, ni kivuli cha mambo makubwa yenye ingefanyika wakati unaokuja. Anafanya hivyo tu ikiwa kuna andiko fulani lenye kuonyesha wazi sababu za kufanya hivyo. Zaidi ya hilo, ilikuwa vigumu kwa watu wengi kuelewa mafasirio hayo ya zamani yenye kuhusu vifananishi na vifananishwa. Mafasirio hayo ya kutafuta kujua ni nani anafananisha nani na sababu gani, inaweza kuwa vigumu kuielewa, kuimbuka, na kuitumia katika maisha. Tena, wakati vifananishi vinakaziwa sana katika habari fulani zenye kuzungumuziwa katika Biblia, jambo hilo linaweza kupoteza mambo ya lazima yenye watu wanaweza kujifunza katika habari hizo. Kwa hiyo, leo wakati vichapo vyetu vinafasiria habari zenye kuzungumuziwa katika Biblia, vinafanya hivyo kwa njia mwepesi, vinakazia mambo yenye tunajifunza juu ya imani ya watu fulani, uvumilivu wao, namna walishikamana na Mungu, na vinakazia sifa zingine zenye walionyesha.

11 Namna gani tunaelewa leo habari juu ya Nabothi? Habari hiyo inaelezwa katika maneno mepesi sana na yenye kuwa wazi zaidi. Mutu huyo mwenye haki alikufa kwa sababu ya uaminifu wake, lakini si kwa sababu alifananisha Yesu ao Wakristo watiwa-mafuta. Alishikamana na Sheria ya Yehova wakati Ahabu na bibi yake walitumia mamlaka yao vibaya. (Hes. 36:7; 1 Fal. 21:3) Mufano wake unafundisha kila mumoja wetu kwamba anaweza kuteseka kwa sababu ya ushikamanifu wake kwa Yehova kama vile Nabothi. (Soma 2 Timotheo 3:12.) Watu wa namna zote wanaweza sasa kuelewa, kukumbuka, na kutumia katika maisha yao mambo yenye wamejifunza katika habari hiyo yenye kutia nguvu imani yetu.

12 Tunaweza kusema kwamba habari zenye kuzungumuziwa katika Biblia zinaonyesha tu mambo yenye tunajifunza katika habari hizo? Hapana. Leo, vichapo vyetu vinaonyesha zaidi kwamba habari moja ya Biblia inaweza kutukumbusha habari ingine, ao inaweza kuwa mufano wa habari ingine. Vichapo vyetu havizoee tena kufasiria kwamba habari fulani zenye kuzungumuziwa katika Biblia ni vifananishi ao vifananishwa. Kwa mufano, tunaweza kusema kwamba uaminifu wa Nabothi wakati aliteswa na kuuawa, unatukumbusha uaminifu wa Kristo, na wa watiwa-mafuta wake. Lakini pia, unatukumbusha ushikamanifu wa “kondoo wengine” wa Bwana. Mafasirio hayo yenye kuwa mwepesi sana na yenye kuwa wazi, ni njia yenye Yehova anatumia ili kutufundisha leo.

TAREH 24-30/10

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 WAFALME 1-2

“Mufano Muzuri wa Kuzoeza Wengine”

w15 15/4 uku. 13 fu. 15

Namna Wazee Wanazoeza Wengine ili Wafikie Madaraka

15 Habari ya Elisha, mwenye alichukua nafasi ya nabii Eliya, inaonyesha pia namna leo ndugu wanaweza kuonyesha kwamba wanawaheshimu wazee wenye uzoefu. Kisha nabii Eliya na Elisha kutembelea kikundi fulani cha manabii katika muji wa Yeriko, wanaume hao wawili walienda pamoja kuelekea Muto Yordani. Kwenye muto huo, ‘Eliya alichukua vazi lake rasmi, akalifunga, akapiga maji, nayo mwishowe yakagawanyika huku na huku.’ Kisha kuvuka muto kupitia udongo wenye kukauka, wanaume hao wakaendelea ‘kuzungumuza huku wakitembea.’ Ni wazi kwamba, Elisha hakufikiri hata kidogo kwamba wakati huo alikuwa amejua mambo yote. Elisha aliweka katika moyo wake kila neno mwalimu wake alimuambia mupaka wakati waliachana na nabii Eliya. Kisha Eliya akapanda katika zoruba ya upepo. Baadaye, wakati Elisha alifika kwenye Muto Yordani, akapiga maji kwa kutumia vazi la nabii Eliya, na kuita: ‘Iko wapi Yehova Mungu wa Eliya?’ Mara ingine tena, maji ikagawanyika.​—2 Fa. 2:8-14.

w15 15/4 uku. 13 fu. 16

Namna Wazee Wanazoeza Wengine ili Wafikie Madaraka

16 Je, umetambua kwamba muujiza wa kwanza wa Elisha ulifanana kabisa na ule wa nabii Eliya? Sababu gani jambo hilo ni lenye kupendeza? Inaonekana kwamba, Elisha hakufikiri kama kwa sababu alikuwa amepewa mamlaka, alipaswa kufanya mambo vile anapenda. Kwa kufuata mufano wa nabii Eliya, Elisha alionyesha kwamba alimuheshimu mwalimu wake, na jambo hilo lilifanya manabii wenzake wamutumainie. (2 Fal. 2:15) Hata hivyo, katika miaka 60 yenye Elisha alifanya katika kazi ya kutoa unabii, Yehova alimupatia uwezo wa kufanya miujiza mingi zaidi kuliko nabii Eliya. Jambo hilo linaweza kufundisha mwanafunzi nini leo?

Mali ya Kiroho

w05-SW 1/8 uku. 9 fu. 1

Mambo Makuu Katika Kitabu cha Pili cha Wafalme

2:11​—‘Eliya alipopanda katika ile dhoruba ya upepo’ alielekea ‘mbingu’ zipi? Mbingu hizo si sehemu za mbali za ulimwengu unaoonekana wala si makao ya kiroho ya Mungu pamoja na wana wake ambao ni malaika. (Kumbukumbu la Torati 4:19; Zaburi 11:4; Mathayo 6:9; 18:10) ‘Mbingu’ ambazo Eliya alipanda kuzielekea ni angahewa. (Zaburi 78:26; Mathayo 6:26) Inaonekana kwamba gari la vita lenye moto lilisonga kasi katika angahewa la dunia na kumhamisha Eliya kwenye sehemu nyingine ya dunia, ambako aliendelea kuishi kwa kipindi fulani. Kwa hakika, baada ya miaka kupita, Eliya alimwandikia barua Yehoramu mfalme wa Yuda.​—2 Mambo ya Nyakati 21:1, 12-15.

TAREHE 31/10–6/11

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 WAFALME 3-4

“Kamata Mutoto Wako”

w17.12 uku. 4 fu. 7

“Ninajua Atafufuka”

7 Ufufuo wa pili wenye kuzungumuziwa katika Maandiko ulifanywa na nabii Elisha mwenye alichukua nafasi ya nabii Eliya. Mwanamuke mumoja Mwisraeli katika Shunemu mwenye kujulikana sana na mwenye hakukuwa anazaa, alionyesha Elisha ukaribishaji-wageni kwa njia ya pekee. Kupitia nabii Elisha, Mungu alimubariki mwanamuke huyo pamoja na bwana yake mwenye kuzeeka kwa kuwawezesha kuzaa mutoto mwanaume. Kisha kupita miaka fulani, mutoto huyo akakufa. Wazia huzuni nyingi yenye mama huyo alikuwa nayo. Bwana yake alimuruhusu kufanya safari ya kilometre 30 hivi ili kumuona Elisha kwenye Mulima Karmeli. Nabii Elisha alimutuma Gehazi mutumishi wake awatangulie Shunemu. Gehazi hakuweza kufufua mutoto huyo. Kisha mama huyo mwenye alikuwa na huzuni alifika pamoja na Elisha.​​—2 Fal. 4:8-31.

w17.12 uku. 5 fu. 8

“Ninajua Atafufuka”

8 Wakati alifika katika Shunemu, Elisha alisali karibu na mwili wa mutoto huyo. Kwa muujiza, mutoto huyo akafufuka na mama yake akafurahi sana! (Soma 2 Wafalme 4:32-37.) Pengine alikumbuka maneno yenye Hana mwenye zamani hakukuwa na uwezo wa kuzaa alisema katika sala wakati alileta Samweli ili atumike katika tabenakulo, alisema hivi: ‘Yehova . . . anashusha mupaka katika Kaburi, na Yeye anainua.’ (1 Sam. 2:6) Kwa kweli, kwa kufufua kabisa mutoto huyo katika Shunemu, Mungu alionyesha uwezo wake wa kufufua watu.

Mali ya Kiroho

it-2-F uku. 672 fu. 6

Nabii

“Wana wa manabii.” Sawa vile kitabu Gesenius’ Hebrew Grammar inaonyesha (Oxford, 1952, uku. 418), neno ya Kiebrania ben (mwana wa) ao benehʹ (wana wa) inaweza kumaanisha “watu wenye kutumika pamoya mu kikundi fulani (ao mu kabila fulani).” (Linganisha na Ne 3:8, kwenye “mumoja wa watu wenye kuchanganya mafuta” moja kwa moja ni “mwana wa watu wenye kuchanganya mafuta.”) Kwa hiyo, maneno “wana wa manabii” inaweza kumaanisha masomo ya kufundisha wale wenye wamechaguliwa kwa ajili ya ile kazi ao inamaanisha tu kikundi yenye kutumika pamoya ya manabii. Biblia inaonyesha kama vile vikundi vya manabii viilikuwa Beteli, Yeriko, na Gilgali. (2Fa 2:3, 5; 4:38; linganisha na 1Sa 10:5, 10.) Samweli alikuwa nasimamia kikundi fulani kule Rama (1Sa 19:19, 20), na inaonekana Elisha alikuwa pia nasimamia kikundi fulani mu wakati yake. (2Fa 4:38; 6:1-3; Linganisha na 1Fa 18:13.) Kulingana na ile habari walijijengea fasi ya kuishi na walitumia chombo yenye waliomba. Ile inaonyesha kama inawezekana waliishi maisha ya mwepesi. Hata kama mara mingi walikuwa naishi fasi moya na kula pamoya, kila mutu alikuwa napewa mugao wake wa kuenda kutimiza kazi ya kiunabii.​—1Fa 20:35-42; 2Fa 4:1, 2, 39; 6:1-7; 9:1, 2.

Hotuba: Unaweza Kufanya Nini juu ya Kuiga Unyenyekevu wa Elisha mu Kazi ya Yehova?

w13 15/8 uku. 28-29

Elisha Aliona Magari ya Vita Yenye Moto​—Je, Wewe Pia Unayaona?

Mufalme wa Siria alikuwa akimuwinda nabii wa Mungu Elisha na alimupata kwenye muji wa Dothani, muji wenye kuzungukwa na kuta unaopatikana juu ya mulima. Usiku, mutawala wa Siria alituma farasi, magari ya vita, na vikundi vya askari huko Dothani. Ilipokuwa asubuhi, majeshi yake yalikuwa yameuzunguka muji huo.​​—2 Fal. 6:13, 14.

Mutumishi wa Elisha alipoamuka na kwenda inje, aliona watu hao waliokuja kumukamata nabii. Kwa hiyo, alilia hivi: “Ole, bwana wangu! Tutafanya nini?” Lakini, Elisha alimuambia hivi: “Usiogope, kwa maana wale walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao.” Kisha nabii huyo alisali hivi: ‘Ee Yehova, tafazali fungua macho yake, ili aone.’ Masimulizi hayo yanaendelea hivi: ‘Mara moja Yehova akafungua macho ya yule mutumishi, hivi kwamba akaona; na, tazama! lile eneo lenye milima lilikuwa limejaa farasi na magari ya vita yenye moto kumuzunguka Elisha pande zote.’ (2 Fal. 6:15-17) Jambo hili na mambo mengine yaliyotokea katika maisha ya Elisha yanatufundisha nini?

Elisha alibaki mutulivu hata ikiwa jeshi la Siria lilikuwa limeuzunguka muji kwa sababu alimutumainia Yehova na aliona namna Mungu alivyotumia nguvu zake ili kumulinda. Hatutazamie miujiza leo, lakini tunajua kwamba Yehova anawalinda watumishi wake kwa ujumla. Sisi pia tumezungukwa na farasi na magari ya vita yenye moto katika maana fulani. Ikiwa ‘tunaona’ magari hayo kwa macho yetu ya imani na ikiwa siku zote tunamutegemea Mungu, ‘tutakaa kwa usalama’ na tutapokea baraka za Yehova. (Zab. 4:8) Acheni tuone namna tunavyoweza kufaidika na mambo mengine yaliyotokea katika maisha ya Elisha.

ELISHA ANAANZA KUMUTUMIKIA ELIYA

Wakati mumoja, Elisha alipokuwa analima shamba, nabii Eliya alimukaribia na kumutupia vazi lake. Elisha alijua maana ya jambo hilo. Kwa hiyo, alifanya karamu, aliwaaga baba na mama yake, na aliondoka nyumbani kwao ili aende kumutumikia Eliya. (1 Fal. 19:16, 19-21) Kwa kuwa Elisha alikuwa tayari kuacha shuguli zake ili awe na wakati mwingi wa kumutumikia Mungu, Yehova alimutumia na baadaye alikuwa nabii pa nafasi ya Eliya.

Labda Elisha alimutumikia Eliya kwa miaka sita. Kwa miaka yote hiyo, ni Elisha aliyekuwa ‘akimimina maji juu ya mikono ya Eliya.’ (2 Fal. 3:11) Katika siku hizo, kwa kawaida watu hawakutumia kanya, vijiko, visu ao vitu vingine vinavyotumiwa ili kula chakula. Kisha kumaliza kula, mutumishi alinawisha bwana wake mikono. Kwa hiyo, kazi fulani ambazo Elisha alifanya zilikuwa za hali ya chini. Hata hivyo, aliona kumutumikia Eliya kuwa pendeleo.

Leo, Wakristo wengi wako katika namna mbalimbali za utumishi wa wakati wote. Wanafanya hivyo kwa sababu wanachochewa na imani na wanatamani kutumia nguvu zao kadiri wanavyoweza ili kumutumikia Yehova. Migawo ya wengine inawaomba waache familia zao, kwa hiyo wanaenda kufanya kazi ambazo wengi wanaona kuwa za hali ya chini, kama vile kutumika kwenye Beteli, katika ujenzi wa majengo ya ibada na mambo mengine. Kwa kuwa Yehova anaona kazi hizo kuwa za maana sana, Mukristo yeyote hawapaswi kuziona kuwa za hali ya chini ao zenye kuzaraulisha.​—Ebr. 6:10.

ELISHA ALISHIKAMANA NA MUGAWO WAKE

Mbele ya ‘kumuchukua Eliya kwenda juu kuelekea mbinguni katika zoruba ya upepo,’ Yehova alimwambia aondoke Gilgali mupaka Beteli. Eliya alimuambia Elisha, mutumishi wake, asimufuate, lakini yeye alimujibu hivi: “Mimi sitakuacha.” Walipoendelea na safari, Eliya alimuambia tena mara mbili abaki, lakini Elisha hakukubali. (2 Fal. 2:1-6) Elisha alishikamana na Eliya kama vile Ruthu alivyoshikamana na Naomi. (Rut. 1:8, 16, 17) Sababu gani? Ni wazi kwamba ilikuwa sababu Elisha alifurahia sana pendeleo ambalo Mungu alimutolea la kuwa mutumishi wa Eliya.

Elisha alituachia mufano muzuri. Ikiwa tunapewa pendeleo fulani la utumishi katika tengenezo la Mungu, tutaliona kuwa la maana sana ikiwa tunaamini katika moyo wetu kwamba ni Yehova ndiye tunayetumikia. Hakuna pendeleo nzuri zaidi kuliko kumutumikia Mungu.​—Zab. 65:4; 84:10.

“OMBA LILE NINALOPASWA KUKUTENDEA”

Kadiri wanaume hao wawili walivyoendelea na safari yao, Eliya alimuambia Elisha hivi: “Omba lile ninalopaswa kukutendea kabla sijachukuliwa kutoka kwako.” Ombi la Elisha lilifanana na lile ambalo Sulemani alifanya miaka fulani hapo zamani kwa sababu lilihusu mambo ya kiroho. Elisha aliomba ‘sehemu mbili za roho ya Eliya zije juu yake.’ (1 Fal. 3:5, 9; 2 Fal. 2:9) Katika Israeli, muzaliwa wa kwanza alipaswa kupokea sehemu mbili za uriti. (Kum. 21:15-17) Kwa hiyo basi, Elisha alitaka atambuliwe kuwa muriti wa kiroho wa Eliya. Zaidi ya hilo, inaonekana kwamba Elisha alitaka kuwa na roho ya ujasiri kama ile ya Eliya, aliyekuwa “na wivu kwelikweli kwa ajili ya Yehova.”​—1 Fal. 19:13, 14.

Eliya alitenda namna gani kuhusiana na ombi la mutumishi wake? Nabii huyo alimuambia Elisha hivi: “Umeomba jambo gumu. Ukiniona wakati nitakapochukuliwa kutoka kwako, itakuwa hivyo kwako; lakini kama sivyo, haitakuwa hivyo.” (2 Fal. 2:10) Inaonekana kwamba jibu la Eliya lilikuwa na maana mbili. Kwanza, ni Mungu tu ndiye angeamua ikiwa Elisha atapewa jambo aliloomba. Pili, ikiwa Elisha angependa kupewa jambo aliloomba, alipaswa kuazimia kubaki na Eliya hata kutokee nini.

MAMBO AMBAYO ELISHA ALIONA

Mungu alijibu namna gani ombi la Elisha la kutaka apewe sehemu mbili za roho ya Eliya? Masimulizi hayo yanaendelea hivi: ‘Na ikawa kwamba walipokuwa wanatembea, wakizungumuza huku wakitembea, tazama! gari la vita lenye moto na farasi wenye moto, nao wakawatenganisha hao wawili; na Eliya akaanza kupanda katika ile zoruba ya upepo kuelekea mbinguni. Wakati huo wote Elisha alikuwa akiona jambo hilo.’* Hivyo ndivyo Yehova alivyojibu ombi la Elisha. Elisha alimuona Eliya akichukuliwa kutoka kwake, alipokea sehemu mbili ya roho ya Eliya, na alifikia kuwa muriti wa kiroho wa nabii huyo.​—2 Fal. 2:11-14.

Elisha aliokota vazi ambalo lilikuwa limeanguka kutoka kwa Eliya na kulivaa. Vazi hilo lilimutambulisha kuwa nabii wa Mungu. Jambo lingine lililoonyesha kwamba Elisha alikuwa amechaguliwa kuwa nabii lilionekana baadaye alipofanya muujiza wa kugawanya maji ya Muto Yordani.

Bila shaka, Elisha alishangazwa sana na mambo aliyoona wakati Eliya alichukuliwa katika zoruba ya upepo. Sababu gani? Sababu si jambo la kawaida kuona gari la vita lenye moto na farasi zenye moto! Mambo hayo yalihakikisha kwamba Yehova alijibu ombi la Elisha. Bila shaka, Mungu anapojibu sala zetu, sisi hatuone katika maono magari ya vita yenye moto ao farasi zenye moto. Lakini tunaweza kutambua kwamba Mungu anatumia nguvu zake kubwa ili mapenzi yake yafanyike. Na tunapoona namna Yehova anavyobariki sehemu inayoonekana ya tengenezo lake hapa duniani, ni kama vile ‘tunaona’ gari lake la mbinguni likisonga mbele.​—Eze. 10:9-13.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine