Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Anatumia Muti wa Tini ili Kufundisha Somo Fulani Kuhusu Imani
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
    • Yesu na wanafunzi wake wanaona kwamba muti wa tini wenye hauzae matunda umekauka

      SURA YA 105

      Anatumia Muti Wa Tini Ili Kufundisha Somo Fulani Kuhusu Imani

      MATAYO 21:19-27 MARKO 11:19-33 LUKA 20:1-8

      • MUTI WA TINI WENYE ULIKAUKA—SOMO KUHUSU IMANI

      • MAMLAKA YA YESU YANAPINGWA

      Siku ya Kwanza kisha midi, Yesu anatoka Yerusalemu na anarudia Betania, upande wa mashariki wa Mulima wa Mizeituni. Bila shaka analala kwa rafiki zake Lazaro, Maria, na Marta.

      Sasa ni asubui ya tarehe 11 Mwezi wa Nisani. Yesu na wanafunzi wake wako njiani tena, wakirudi Yerusalemu. Huko atakuwa kwenye hekalu mara ya mwisho. Na ni siku ya mwisho ya utumishi wake mbele ya watu wengi mbele asherehekee Pasaka, aanzishe Ukumbusho wa kifo chake, na kisha apatwe na majaribu na kifo.

      Wakati walikuwa wanatoka Betania upande wa Mulima wa Mizeituni kuelekea Yerusalemu, Petro anaona ule muti wenye Yesu alilaani asubui yenye ilipita. Anashangaa na kusema hivi: “Rabi, ona! ule muti wa tini wenye ulilaani umekauka.”—Marko 11:21.

      Lakini, sababu gani Yesu alifanya ule muti ukauke? Anafunua sababu katika jibu lake: “Kwa kweli ninawaambia ninyi, kama muko na imani na hamuna mashaka, hamutafanya tu jambo lenye nilifanyia muti wa tini, lakini hata mukiambia mulima huu, ‘Ondoka na utupwe katika bahari,’ jambo hilo litatendeka. Na mambo yote yenye munaomba katika sala, kama muko na imani, mutayapokea.” (Matayo 21:21, 22) Kwa hiyo anarudilia jambo lenye alikuwa amesema kuhusu uwezo wa imani wa kuhamisha mulima.—Matayo 17:20.

      Kwa hiyo kwa kufanya muti ukauke, Yesu anaonyesha kuwa ni jambo la maana kumuamini Mungu. Anasema hivi: “Mambo yote yenye munaomba katika sala, mukuwe na imani kwamba mumekwisha kuyapokea, na mutayapata.” (Marko 11:24) Ni somo la maana kabisa kwa wanafunzi wote wa Yesu! Jambo hilo linafaa kabisa kwa mitume kwa sababu ya majaribu makali yenye watapata hivi karibuni. Kuko uhusiano mwengine kati ya muti wa tini kukauka na sifa ya imani.

      Kama muti huo wa tini, taifa la Israeli liko na sura yenye kudanganya. Watu wa taifa hili wako katika agano pamoja na Mungu, na kwa inje wanaonekana kuwa wenye kushika Sheria yake. Lakini, wanashindwa kuzaa matunda mazuri na wanamukataa hata Mwana wa Mungu! Kwa hiyo, kwa kufanya muti wa tini ukauke, Yesu anaonyesha namna mwisho utakuwa kwa taifa hilo lenye kushindwa kuzaa matunda na lenye kukosa imani.

      Kisha wakati kidogo, Yesu na wanafunzi wake wanaingia katika Yerusalemu. Na kulingana na desturi yake, Yesu anaenda kwenye hekalu na anaanza kufundisha. Bila shaka wakubwa wa makuhani na wazee wa watu wangali wanakumbuka mambo yenye Yesu alifanyia wabadilisha-feza siku yenye ilipita. Wanamuuliza: “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Ao ni nani alikupatia mamlaka hii ya kufanya mambo haya?”—Marko 11:28.

      Yesu anawajibu: “Nitawauliza ulizo moja. Munijibu, na mimi nitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani. Ubatizo wa Yohana ulitoka mbinguni ao kwa wanadamu? Munijibu.” Sasa wale wenye kumupinga ndio wanajikuta mbele ya tatizo. Makuhani na wazee wanaanza kuambiana: “Kama tunasema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atasema, ‘Basi, sababu gani hamukumuamini?’ Lakini je, tupime kusema, ‘Ulitoka kwa wanadamu’?” Walifikiri kwa njia hiyo kwa sababu waliogopa watu, “kwa maana wote waliona kwamba kwa kweli Yohana alikuwa nabii.”—Marko 11:29-32.

      Wale wenye wanamupinga Yesu wanashindwa kupata jibu la muzuri. Basi wanajibu: “Hatujue.” Yesu anawaambia: “Na mimi sitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.”—Marko 11:33.

      • Nini inafanya tarehe 11 Mwezi wa Nisani ikuwe ya maana sana?

      • Yesu anafundisha mambo gani kupitia muti wa tini wenye alifanya ukauke?

      • Namna gani Yesu anajibu watu wenye wanamuuliza kama ni kwa mamlaka gani anafanya mambo yote hayo?

  • Anatoa Mifano Mbili Kuhusu Mashamba ya Mizabibu
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
    • Cultivators killing the vineyard owner’s son

      SURA YA 106

      Anatoa Mifano Mbili Kuhusu Mashamba Ya Mizabibu

      MATAYO 21:28-46 MARKO 12:1-12 LUKA 20:9-19

      • MUFANO KUHUSU WATOTO WAWILI

      • MUFANO KUHUSU WALIMAJI WA SHAMBA LA MIZABIBU

      Kwenye hekalu, Yesu anatoka tu kuwavuruga wakubwa wa makuhani na wazee wa watu, wenye walimutega kwa kumuuliza ni kwa mamlaka ya nani anafanya mambo. Jibu la Yesu linawanyamazisha. Kisha anatoa mufano wenye kuonyesha namna wako kabisa.

      Yesu anaeleza: “Mutu fulani alikuwa na watoto wawili. Akamuendea wa kwanza, akamuambia, ‘Mutoto wangu, leo uende kufanya kazi katika shamba la mizabibu.’ Huyu akamujibu na kusema, ‘Sitaenda,’ lakini kisha, akasikitika na akaenda. Akamukaribia wa pili na kumuambia jambo lilelile. Huyo akajibu, ‘Nitaenda, Bwana,’ lakini hakuenda. Kati ya hao wawili, ni nani alifanya mapenzi ya baba yake?” (Matayo 21:28-31) Jibu liko wazi: ni mutoto wa kwanza mwenye mwishowe alifanya mapenzi ya baba yake.

      Basi Yesu anaambia wale wenye kumupinga: “Kwa kweli ninawaambia ninyi kwamba wakusanya-kodi na makahaba wanawatangulia ninyi kuingia katika Ufalme wa Mungu.” Mbele, wakusanya-kodi na makahaba hawakumutumikia Mungu. Lakini, kama ule mutoto wa kwanza, walifikia kutubu na sasa wanamutumikia. Tofauti na wao, viongozi wa dini wako kama ule mutoto wa pili, wanasema kuwa wao ni watu wenye kumutumikia Mungu, lakini wanashindwa kufanya hivyo kabisa. Yesu anawaambia: “Yohana alikuja kwenu na kuwaonyesha mambo yenye kuwa sawa, lakini hamukumuamini. Hata hivyo, wakusanya-kodi na makahaba walimuamini, na hata kisha ninyi kuona jambo hilo, hamukusikitika ili mumuamini.”—Matayo 21:31, 32.

      Yesu analeta mufano mwengine tena. Mara hii, Yesu anaonyesha kwamba viongozi wa dini hawashindwe tu kumutumikia Mungu, lakini wao ni waovu. Yesu anaeleza: “Mutu fulani alipanda shamba la mizabibu na kulizungushia ukuta, akachimba shimo kwa ajili ya kikamulio cha divai na akasimamisha munara; kisha akalipangisha kwa walimaji na akasafiri kuenda katika inchi ingine. Wakati kipindi chake kilifika akatuma mutumwa kwa walimaji ili akusanye kutoka kwao sehemu fulani ya matunda ya shamba la mizabibu. Lakini wakamukamata, wakamupiga, na wakamufukuza mikono wazi. Tena akatuma mutumwa mwingine kwao, na huyo wakamupiga kwenye kichwa na kumukosea heshima. Na akatuma mwingine, na huyo wakamuua, na wengine wengi, wamoja wao wakawapiga na wengine wakawaua.”—Marko 12:1-5.

      Je, watu wenye wanasikiliza Yesu wataelewa mufano huo? Pengine wanakumbuka maneno haya ya Isaya: “Shamba la mizabibu la Yehova wa majeshi ni nyumba ya Israeli; watu wa Yuda ndilo shamba lenye alikuwa anapenda sana. Aliendelea kutumaini haki, lakini angalia! kulikuwa ukosefu wa haki.” (Isaya 5:7) Ni kama tu mufano wa Yesu. Mwenye shamba ni Yehova, na shamba la mizabibu ni taifa la Israeli, lenye kukingwa na kulindwa na Sheria ya Mungu. Yehova alituma manabii ili kufundisha watu wake na kuwasaidia wazae matunda ya muzuri.

      Lakini, “walimaji” walitesa na kuua “watumwa” wenye walitumwa kwao. Yesu anasema: “Mutu mumoja [mwenye shamba la mizabibu] mwenye alibakia naye alikuwa mwana wake mupendwa. Akamutuma wa mwisho, akisema: ‘Watamuheshimia mwana wangu.’ Lakini wale walimaji wakaambiana, ‘Huyu ndiye muriti. Mukuje, tumuue, na uriti utakuwa wetu. Basi wakamukamata na kumuua.”—Marko 12:6-8.

      Sasa Yesu anauliza: “Mwenye shamba la mizabibu atafanya nini?” (Marko 12:9) Viongozi wa dini wanajibu: “Kwa sababu ni waovu, ataleta uharibifu mubaya juu yao na kupangisha shamba hilo la mizabibu kwa walimaji wengine, wenye watamupatia matunda kwa wakati wake.”—Matayo 21:41.

      Kwa hiyo, bila kujua wanatangaza hukumu juu yao wenyewe, kwa sababu wako kati ya “walimaji” wa “shamba la mizabibu” la Yehova, ni kusema, taifa la Israeli. Matunda yenye Yehova anatazamia kwa wale walimaji inatia ndani imani katika Mwana wake, Masiya. Yesu anawaangalia viongozi hao wa dini na kuwaambia: “Je, hamujasoma hata siku moja andiko hili: ‘Jiwe lenye wajenzi walikataa ndilo limekuwa jiwe kubwa la pembe. Hili limetoka kwa Yehova, na ni la ajabu katika macho yetu’?” (Marko 12:10, 11) Kisha Yesu anawaambia waziwazi hivi: “Ndiyo sababu ninawaambia ninyi, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu na kupewa taifa lenye kuzaa matunda yake.”—Matayo 21:43.

      Waandishi na wakubwa wa makuhani wanatambua kama Yesu “alisema mufano huo juu yao.” (Luka 20:19) Sasa kuliko wakati mwengine wowote, wanataka kumuua mwenye kuwa na haki ya kuwa “muriti.” Lakini wanaogopa watu, wenye wanamuona Yesu kuwa nabii, kwa hiyo hawajaribu kumuua wakati huo.

      • Watoto wawili katika mufano wa Yesu wanafananisha nani?

      • Katika mufano wa pili, ni nani anafananishwa na “mwenye shamba,” “shamba la mizabibu,” “walimaji,” “watumwa,” na “muriti”?

      • Ni nini inangojea “walimaji”?

  • Mufalme Anaita Wenye Walialikwa Kwenye Karamu ya Ndoa
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
    • Mufalme anaambia watumwa wafukuze inje mutu mwenye havae nguo ya karamu ya ndoa

      SURA YA 107

      Mufalme Anaita Wenye Walialikwa Kwenye Karamu Ya Ndoa

      MATAYO 22:1-14

      • MUFANO WA KARAMU YA NDOA

      Utumishi wa Yesu unakuwa karibu na kufika mwisho. Anaendelea kutumia mifano ili kuonyesha waziwazi tabia za waandishi na wakubwa wa makuhani. Kwa hiyo, wanataka kumuua. (Luka 20:19) Lakini Yesu anaendelea kufunua tabia zao. Anatoa mufano mwengine:

      “Ufalme wa mbinguni unaweza kufananishwa na mufalme mwenye alifanyia mwana wake karamu ya ndoa. Na akatuma watumwa wake waite wale wenye walialikwa kwenye karamu ya ndoa, lakini hawakutaka kuja.” (Matayo 22:2, 3) Yesu anaanza mufano wake kwa kutaja “Ufalme wa mbinguni.” Bila shaka, “mufalme” anapaswa kuwa Yehova Mungu. Mwana wa mufalme na wale wenye kualikwa kwenye karamu ya ndoa ni nani? Hapo pia, haiko nguvu kutambua kwamba mwana wa mufalme ni Yesu, na wale wenye walialikwa ni wale wenye watakuwa pamoja na Mwana katika Ufalme wa mbinguni.

      Ni nani wenye wanaalikwa wa kwanza? Yesu na mitume wamekuwa wakihubiria nani juu ya Ufalme? Wayahudi. (Matayo 10:6, 7; 15:24) Walikubali agano la Sheria katika mwaka wa 1513 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, na wakakuwa wa kwanza kupata nafasi ya kufanyiza “ufalme wa makuhani.” (Kutoka 19:5-8) Lakini, ni wakati gani wangeitwa kwenye “karamu ya ndoa”? Kwa kweli, mualiko huo ulianza katika mwaka wa 29 wakati wetu, wakati Yesu alianza kuhubiri juu ya Ufalme wa mbinguni.

      Waisraeli wengi waliitikia mualiko huo namna gani? Kama vile Yesu alisema, “hawakutaka kuja.” Viongozi wengi wa dini na watu hawakukubali kama yeye ni Masiya na Mufalme mwenye aliwekwa na Mungu.

      Kwa hiyo, Yesu alionyesha kwamba Wayahudi walipewa nafasi ingine: “Tena [mufalme] akatuma watumwa wengine, na kusema, ‘Muambie wale wenye walialikwa: “Muangalie! Nimetayarisha chakula changu cha muchana, ngombe-dume wangu na wanyama wenye kunona wamechinjwa, na kila kitu kiko tayari. Mukuje kwenye karamu ya ndoa.”’ Lakini kwa sababu hawakuhangaika, wakaenda, mumoja kwenye shamba lake mwenyewe, na mwingine kwenye biashara yake; lakini wengine wakakamata watumwa wake, wakawatendea kwa zarau na kuwaua.” (Matayo 22:4-6) Hilo linapatana na mambo yenye yangefanyika kisha tu kuanzishwa kwa kutaniko la Kikristo. Wakati huo, Wayahudi walikuwa wangali na nafasi ya kuwa katika Ufalme, lakini wengi walikataa mualiko huo, na hata kuwatendea mubaya ‘watumwa wa mufalme.’—Matendo 4:13-18; 7:54, 58.

      Taifa hilo lilipatwa na nini? Yesu anaeleza: “Mufalme akakasirika sana, akatuma majeshi yake na kuua wale wauaji na kuchoma muji wao.” (Matayo 22:7) Wayahudi walipata matokeo hayo mabaya katika mwaka wa 70 kisha kuzaliwa kwa Yesu, wakati Waroma waliharibu “muji wao,” Yerusalemu.

      Ni kusema kama hakuna mwengine mwenye angealikwa kwa sababu wao walikataa mualiko wa mufalme? Hapana, kulingana na mufano wa Yesu. Anaendelea kusema: “Kisha akaambia watumwa wake, ‘Karamu ya ndoa iko tayari, lakini wale wenye walialikwa hawakustahili. Kwa hiyo, muende kwenye barabara zenye kupeleka inje ya muji, na mualike kwenye karamu ya ndoa mutu yeyote mwenye mutapata.’ Basi watumwa hao wakaenda kwenye barabara na kukusanya wote wenye walipata, watu waovu na watu wazuri; na chumba cha karamu za ndoa kikajaa watu wenye kula chakula.”—Matayo 22:8-10.

      Maneno hayo yalitimia wakati mutume Petro alisaidia watu wa mataifa, ni kusema, watu wenye hawakuwa Wayahudi kwa kuzaliwa ao kwa kugeuzwa imani, ili wakuwe Wakristo wa kweli. Katika mwaka wa 36 kisha kuzaliwa kwa Yesu, mukubwa wa jeshi Muroma Kornelio na familia yake walipokea roho ya Mungu, na kupata tumaini la kuwa sehemu ya ufalme wa mbinguni wenye Yesu alizungumuzia.—Matendo 10:1, 34-48.

      Yesu anaonyesha kama haiko wote wenye kuja kwenye karamu ndio mwishowe watakubaliwa na “mufalme.” Anasema: “Wakati mufalme aliingia ili kuchunguza wageni, akaona mutu mwenye hakukuwa anavaa nguo ya ndoa. Basi akamuuliza, ‘Mwenzangu, uliingia humu namna gani bila nguo ya ndoa?’ Akakosa la kusema. Halafu mufalme akaambia watumishi wake, ‘Mumufunge mikono na miguu, kisha mumutupe inje katika giza. Ni kule atalia na kusaga meno yake.’ Kwa maana wenye walialikwa ni wengi, lakini wenye walichaguliwa ni wachache.”—Matayo 22:11-14.

      Pengine viongozi wa dini hawaelewe maana ao mambo yote yenye iko anazungumuzia. Lakini, wanachukizwa na wanaazimia hata zaidi kuondolea mbali mutu mwenye kuwapatisha haya hivyo.

      • Katika mufano wa Yesu, “mufalme” ni nani, “mwana wake” ni nani, na wale wenye walialikwa kwanza kwenye karamu ni nani?

      • Ni wakati gani Wayahudi walitolewa tena nafasi ingine ya kukubali mwaliko, na ni nani walialikwa kisha?

      • Wenye walialikwa ni wengi lakini wenye kuchaguliwa ni wadogo, hilo linaonyesha nini?

  • Wanashindwa Kumunasa Yesu Katika Mitego Yao
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
    • Yesu anaonyesha sarafu ya kodi na anajibu maulizo yenye ujanja ya Wafarisayo

      SURA YA 108

      Wanashindwa Kumunasa Yesu Katika Mitego yao

      MATAYO 22:15-40 MARKO 12:13-34 LUKA 20:20-40

      • VITU VYA KAISARI KWA KAISARI

      • WENYE WATAFUFULIWA WATAFUNGA NDOA?

      • AMRI ZENYE KUWA KUBWA ZAIDI

      Maadui wa Yesu wanakasirika. Ametoka tu kuzungumuzia mifano yenye kufunua uovu wao. Sasa Wafarisayo wanataka kumutega. Wanapenda aseme jambo fulani lenye litafanya wamutoe kwa gavana Muroma, na wanalipa wanafunzi wao fulani ili wamunase katika mitego.—Luka 6:7.

      Wanamuambia hivi: “Mwalimu, tunajua wewe unasema na kufundisha bila kukosea na hauna ubaguzi, lakini unafundisha njia ya Mungu kupatana na kweli: Je, tunaruhusiwa kulipa Kaisari kodi ya kichwa ao hapana?” (Luka 20:21, 22) Yesu hadanganywe na maneno yao yenye kuonekana kuwa ya muzuri, kwa sababu yanaficha ujanja na unafiki wao. Kama anasema, ‘Hapana, hamupaswe kulipa kodi hiyo,’ atashitakiwa kuwa mutu mwenye anataka kupindua utawala wa Roma. Lakini kama anasema, ‘Ndiyo, mulipe kodi,’ watu wenye hawapendi kutawaliwa na Waroma watakasirika na kumugeukia. Basi, anajibu namna gani?

      Yesu anajibu hivi: “Sababu gani munanijaribu, ninyi wanafiki? Munionyeshe feza moja ya kichele ya kodi.” Wakamuletea dinari. Akawaambia: “Sura hii na muandiko huu ni ya nani?” Wakasema: “Ni ya Kaisari.” Kisha Yesu akawatolea muongozo wa muzuri sana: “Basi, mulipe Kaisari vitu vya Kaisari, lakini Mungu vitu vya Mungu.”—Matayo 22:18-21.

      Watu hao wanashangazwa na maneno ya Yesu. Kisha kunyamazishwa na jibu lake lenye hekima, wanaenda zao. Lakini siku ingali inaendelea, na mitego ya kumunasa haijamalizika. Kisha Wafarisayo kushindwa kumunasa, viongozi wa kikundi kingine cha dini wanamukaribia Yesu.

      Wasadukayo, wenye wanasema kama hakuna ufufuo, wakamuuliza ulizo kuhusu ufufuo na ndoa kati ya mutu na bibi ya ndugu yake. Wanauliza: “Mwalimu, Musa alisema: ‘Kama mutu yeyote anakufa bila kupata watoto, ndugu yake anapaswa kumuoa bibi yake na kumuinulia ndugu yake uzao.’ Sasa kulikuwa ndugu saba (7) katikati yetu. Wa kwanza akaoa na akakufa, na kwa sababu hakukuwa na uzao wowote, akamuachia ndugu yake bibi yake. Ikakuwa vilevile kwa ule wa pili na wa tatu (3), mupaka wote saba (7). Mwishowe, ule mwanamuke naye akakufa. Basi, wakati wa ufufuo, ule mwanamuke atakuwa bibi ya nani kati ya hao saba (7)? Kwa maana alikuwa bibi yao wote.”—Matayo 22:24-28.

      Yesu anatumia maandishi ya Musa yenye kukubaliwa na Wasadukayo, kwa kusema hivi: “Munakosea, kwa sababu hamujue Maandiko wala nguvu za Mungu. Kwa maana wakati wanafufuliwa kutoka kwa wafu, wanaume hawaoe na wanamuke hawaolewe, lakini wao ni kama malaika wa mbinguni. Hata hivyo, kuhusu kufufuliwa kwa wafu, je, hamukusoma katika kitabu cha Musa, katika habari kuhusu ule muti mudogo wa miiba, kwamba Mungu alimuambia: ‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu na Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo’? Yeye haiko Mungu wa wafu, lakini ni Mungu wa wazima. Mumekosea sana.” (Marko 12:24-27; Kutoka 3:1-6) Watu wakashangazwa na jibu lake.

      Yesu amewanyamazisha Wafarisayo na Wasadukayo, kwa hiyo, viongozi hawa wapinzani wanajiunga pamoja ili kuja kumujaribu tena. Mwandishi mumoja anamuuliza: “Mwalimu, ni amri gani ndiyo kubwa zaidi katika Sheria?”—Matayo 22:36.

      Yesu anajibu: “Ya kwanza ni hii, ‘Sikia, Ee Israeli, Yehova Mungu wetu ni Yehova mumoja, na unapaswa kumupenda Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote na kwa nguvu zako zote.’ Ya pili ni hii, ‘Unapaswa kumupenda jirani yako kama wewe mwenyewe.’ Hakuna amri nyingine yenye kuwa kubwa zaidi kuliko hizi.”—Marko 12:29-31.

      Wakati ule mwandishi alisikia jibu hilo, akajibu hivi: “Mwalimu, umesema muzuri kupatana na kweli, ‘Yeye ni Mumoja, na hakuna mwingine isipokuwa yeye’; na mutu kumupenda kwa moyo wake wote, na kwa uelewaji wake wote, na kwa nguvu zake zote, na pia kumupenda jirani yake kama yeye mwenyewe ni muzuri sana kuliko matoleo yote mazima ya kuteketezwa na zabihu.” Halafu Yesu, wakati alitambua kwamba amejibu kwa hekima, akamuambia: “Wewe hauko mbali na Ufalme wa Mungu.”—Marko 12:32-34.

      Kwa muda wa siku tatu (Nisani 9, 10, na 11) Yesu amekuwa akifundisha katika hekalu. Watu fulani, kama vile ule mwandishi, wamefurahia kumusikiliza. Lakini hapana viongozi wa dini, wenye sasa ‘hawawezi tena kumuuliza ulizo.’

      • Namna gani Wafarisayo wanajaribu kutega Yesu, na hilo lilikuwa na matokeo gani?

      • Wakati Wasadukayo wanajaribu kumutega Yesu, namna gani anaepuka mutego wao?

      • Yesu anakazia mambo gani ya lazima sana wakati anajibu ulizo la mwandishi?

  • Anakemea Waziwazi Viongozi Wa Dini Wenye Kumupinga
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
    • Yesu anafunua unafiki wa viongozi wa dini

      SURA YA 109

      Anakemea Waziwazi Viongozi Wa Dini Wenye Kumupinga

      MATAYO 22:41–23:24 MARKO 12:35-40 LUKA 20:41-47

      • KRISTO NI MWANA WA NANI?

      • YESU ANAFUNUA UNAFIKI WA WATU WENYE KUMUPINGA

      Viongozi wa dini wenye kumupinga Yesu wanashindwa kumuharibishia Yesu sifa ao kumunasa katika mutego ili wamutoe kwa Waroma. (Luka 20:20) Sasa, wakati angali kwenye hekalu tarehe 11 Mwezi wa Nisani, Yesu anawageukia na kuwaonyesha yeye ni nani. Yeye ndiye anaanzisha mazungumuzo. Anawauliza hivi: “Munawaza nini juu ya Kristo? Yeye ni mwana wa nani?” (Matayo 22:42) Inajulikana muzuri kwamba Kristo, ao Masiya, anapaswa kuwa katika kizazi cha Daudi. Na ni hivyo wanamujibu.—Matayo 9:27; 12:23; Yohana 7:42.

      Yesu anauliza: “Basi, sababu gani Daudi kwa kuongozwa na roho anamuita Kristo Bwana, wakati anasema, ‘Yehova alimuambia Bwana wangu: “Kaa kwenye mukono wangu wa kuume mupaka niweke maadui wako chini ya miguu yako”’? Basi, kama Daudi anamuita Bwana, yeye ni mwana wake namna gani?”—Matayo 22:43-45.

      Wafarisayo wanabakia kimya, kwa sababu wanatumainia kupata mutu wa kizazi cha Daudi ili awakomboe kutoka katika mikono ya Waroma. Lakini akitumia maneno ya Daudi yenye kupatikana katika Zaburi 110:1, 2, Yesu anaonyesha kwamba Masiya hapaswe kuwa tu mutawala mwanadamu. Yeye ni Bwana wa Daudi, na kisha kukaa kwenye mukono wa kuume wa Mungu, ataanza kutawala. Jibu la Yesu linanyamazisha waandishi na Wafarisayo.

      Wanafunzi na wengine wengi wamekuwa wakisikiliza. Sasa Yesu anaanza kuzungumuza nao na kuwaambia wafanye angalisho na waandishi na Wafarisayo. Wao “wamejiikalisha katika kiti cha Musa” ili kufundisha Sheria ya Mungu. Yesu anaelezea hivi wasikilizaji wake: “Mambo yote yenye wanawaambia, muyafanye na kuyashika, lakini musitende kulingana na matendo yao, kwa maana wao wanasema lakini hawatende mambo yenye wanasema.”—Matayo 23:2, 3.

      Kisha Yesu anawapatia mifano ya unafiki wao, na kusema: “Kwa maana wanapanua visanduku vyenye kuwa na maandiko ndani vyenye wanavaa kama ulinzi.” Wayahudi fulani walivaa kwenye paji la uso ao kwenye mukono visanduku vidogo kama hivyo vyenye vilikuwa na maneno ya Sheria. Wafarisayo wananenepesha visanduku vyao ili kuonyesha watu kama wako na bidii kuhusu Sheria. Tena, “wanarefusha sehemu za chini za nguo zao.” Waisraeli walipaswa kutia uzi kwenye sehemu ya chini ya nguo zao, lakini Wafarisayo walirefusha sehemu hizo za chini kwenye nguo zao. (Hesabu 15:38-40) Wanafanya yote hayo “ili waonekane na watu.”—Matayo 23:5.

      Hata wanafunzi wa Yesu wangeambukizwa na tamaa hiyo ya kutaka makubwa, kwa hiyo anawashauria hivi: “Lakini ninyi, musiitwe Rabi, kwa maana Mwalimu wenu ni mumoja, na ninyi wote ni ndugu. Zaidi ya hayo, musiite mutu yeyote baba yenu duniani, kwa maana Baba yenu ni mumoja, Ule wa mbinguni. Wala musiitwe viongozi, kwa maana Kiongozi wenu ni mumoja, Kristo.” Kwa hiyo basi, wanafunzi wanapaswa kuwa na mawazo gani juu yao na wanapaswa kutenda namna gani? Yesu anawaambia: “Lakini mwenye kuwa mukubwa zaidi kati yenu anapaswa kuwa mutumishi wenu. Kila mutu mwenye kujiinua atanyenyekezwa, na kila mutu mwenye kujinyenyekeza atainuliwa.”—Matayo 23:8-12.

      Tena, Yesu anatangazia waandishi na Wafarisayo wanafiki ole mbalimbali zenye kufuatana. Anasema hivi: “Ole kwenu, waandishi na Wafarisayo, wanafiki! kwa sababu munafungia watu Ufalme wa mbinguni; kwa maana ninyi wenyewe hamuingie, na wale wenye wanataka kuingia munawazuia.”—Matayo 23:13.

      Yesu anakemea Wafarisayo sababu hawajue mambo ya maana kulingana na mawazo ya Yehova. Kwa mufano, wanasema: “Kama mutu yeyote anaapa kwa hekalu, hakuna ubaya; lakini kama mutu yeyote anaapa kwa zahabu ya hekalu, anapaswa kutimiza kiapo chake.” Kwa kukazia sana akili yao juu ya zahabu yenye kuwa kwenye hekalu kuliko kukazia ibada yenye inapaswa kutolewa kwenye hekalu, wanaonyesha kwamba wao ni vipofu. Na ‘wamepuuza mambo mazito zaidi ya Sheria, ni kusema, haki, rehema, na uaminifu.’—Matayo 23:16, 23; Luka 11:42.

      Yesu anaita Wafarisayo hawa ‘viongozi vipofu, wenye kuchuya imbu lakini wanameza ngamia!’ (Matayo 23:24) Wanatosha imbu katika divai yao wakati wa karamu kwa sababu kidudu hicho hakiko safi. Lakini kupuuza mambo mazito ya Sheria ni kama vile kumeza ngamia mwenye pia wakati wa karamu ni munyama muchafu, tena mukubwa sana.—Mambo ya Walawi 11:4, 21-24.

      • Sababu gani Wafarisayo wanabakia kimya wakati Yesu anawauliza kuhusu maneno yenye Daudi alisema katika Zaburi 110?

      • Sababu gani Wafarisayo wananenepesha visanduku vyao vyenye kuwa na maandiko na wanarefusha uzi kwenye nguo zao?

      • Yesu anatolea wanafunzi wake shauri gani?

  • Siku ya Mwisho ya Yesu Kwenye Hekalu
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
    • Yesu anamuangalia mujane mumoja masikini akitumbukiza feza mbili za vichele zenye samani kidogo sana katika kisanduku cha hazina

      SURA YA 110

      Siku Ya Mwisho Ya Yesu Kwenye Hekalu

      MATAYO 23:25–24:2 MARKO 12:41–13:2 LUKA 21:1-6

      • YESU ANAENDELEA KUHUKUMU VIONGOZI WA DINI

      • HEKALU LITAHARIBIWA

      • MUJANE MASKINI ANATOA MUCHANGO WA FEZA MBILI ZA VICHELE ZENYE SAMANI KIDOGO SANA

      Wakati wa mwisho wa Yesu kuonekana kwenye hekalu, anaendelea kufunua unafiki wa waandishi na Wafarisayo, kwa kuwaita waziwazi wanafiki. Anatumia maneno ya mufano, kwa kusema: “Munasafisha upande wa inje wa kikombe na wa sahani, lakini ndani vimejaa pupa na kukosa kujizuia. Mufarisayo kipofu, safisha kwanza ndani ya kikombe na sahani, ili upande wake wa inje ukuwe safi pia.” (Matayo 23:25, 26) Hata kama Wafarisayo wanatilia sana mukazo mambo yenye kuhusu usafi wakati wa karamu na usafi wa mwili, wanapuuza hali ya kiroho na wanashindwa kusafisha moyo wao wa mufano.

      Unafiki wao unaonekana pia katika utayari wao wa kujenga na kupamba makaburi kwa ajili ya manabii. Lakini Yesu anaonyesha kama wao ni “wana wa wale wenye waliua manabii.” (Matayo 23:31) Maneno hayo ni ya kweli kwa sababu wanafanya nguvu yao yote ili wamuue Yesu.—Yohana 5:18; 7:1, 25.

      Yesu anaonyesha jambo lenye linangojea viongozi hawa wa dini kama hawatubu: “Ninyi nyoka, uzao wa nyoka-vipiri, mutakimbia namna gani hukumu ya Gehena?” (Matayo 23:33) Gehena, ni kusema, Bonde la Hinomu, lenye kuwa karibu linatumiwa ili kuchoma uchafu ao takataka, na ni mahali pa mufano penye kufananisha uharibifu wa milele wenye kuwangojea waandishi na Wafarisayo waovu.

      Wanafunzi wa Yesu watamuwakilisha wakiwa “manabii na watu wenye hekima na wafundishaji wa watu wote.” Watawatendea namna gani? Yesu anaambia viongozi hao wa dini hivi: “Wamoja kati yao [wanafunzi wangu] mutawaua na kuwapigilia misumari kwenye miti, na wamoja kati yao mutawapiga mijeledi katika masinagogi yenu na kuwatesa katika muji baada ya muji, ili damu yote yenye haina kosa yenye ilimwangwa katika dunia ikuje juu yenu, kuanzia damu ya Abeli mwenye alikuwa bila kosa mupaka damu ya Zekaria . . . mwenye muliua.” Anawaambia hivi: “Kwa kweli ninawaambia ninyi, mambo yote haya yatafikia kizazi hiki.” (Matayo 23:34-36) Maneno hayo yanatimia katika mwaka wa 70 kisha kuzaliwa kwa Yesu, wakati majeshi ya Waroma yanaharibu Yerusalemu na kuua maelfu ya Wayahudi.

      Yesu anahuzunika wakati anakumbuka hali hii yenye kuogopesha. Anasema hivi kwa huzuni: “Yerusalemu, Yerusalemu, muuaji wa manabii na mwenye kupiga majiwe wale wenye walitumwa kwake—ni mara ngapi nilitaka kukusanya watoto wako, kama vile kuku anakusanya vitoto vyake chini ya mabawa yake! Lakini hamukutaka. Angalia! Mungu ameacha nyumba yenu.” (Matayo 23:37, 38) Wale wenye wanasikia maneno haya wanapaswa kujiuliza ni “nyumba” gani anazungumuzia. Je, alikuwa anazungumuzia hekalu hilo lenye utukufu la Yerusalemu, lenye linaonekana kuwa ni lenye kulindwa na Mungu?

      Kisha Yesu anaongeza hivi: “Ninawaambia ninyi, tangu sasa hamutaniona tena mupaka wakati mutasema, ‘Amebarikiwa ule mwenye anakuja katika jina la Yehova!’” (Matayo 23:39) Anataja maneno ya unabii yenye kuwa katika Zaburi 118:26: “Amebarikiwa ule mwenye anakuja katika jina la Yehova; tunakubariki tukiwa katika nyumba ya Yehova.” Ni wazi kwamba, hakuna mutu mwenye angesema maneno hayo katika hekalu kwa sababu lingeharibiwa.

      Yesu anaenda sasa sehemu ya hekalu kwenye kunapatikana visanduku vya hazina. Watu wanaweza kutia michango yao katika tundu ndogo kwenye sehemu ya juu ya kisanduku. Yesu anaona Wayahudi wengi wakifanya hivyo; matajiri “walikuwa wanatumbukiza ndani feza nyingi za vichele” kama zawadi. Kisha Yesu anamuangalia mujane maskini mwenye anatumbukiza ndani “feza mbili za vichele zenye samani kidogo sana.” (Marko 12:41, 42) Bila shaka, Yesu anajua kwamba Mungu anapendezwa sana na zawadi yake.

      Anaita wanafunzi wake na kusema: “Kwa kweli ninawaambia ninyi, mujane huyu maskini ametoa zaidi ya wote wenye walitia feza ndani ya masanduku ya hazina.” Namna gani? Anaeleza: “Wote walitoa kutokana na wingi wa feza zao, lakini yeye, hata kama ni maskini, alitoa kila kitu chenye alikuwa nacho, kila kitu chenye alikuwa nacho lazima ili kuishi.” (Marko 12:43, 44) Mujane huyo iko tofauti kabisa na viongozi wa dini!

      Nisani 11 inaendelea, Yesu anaondoka kwenye hekalu, na hii ndio mara yake ya mwisho. Mumoja kati ya wanafunzi wake anashangaa: “Mwalimu, ona namna majiwe na majengo haya ni ya ajabu!” (Marko 13:1) Kwa kweli, majiwe fulani ya ukuta wa hekalu ni makubwa sana, na yanafanya hekalu likuwe nguvu sana. Kwa hiyo maneno ya Yesu yanaonekana kuwa yenye kushitusha wakati anasema: “Unaona majengo haya makubwa? Hakuna jiwe lenye litaachwa hapa juu ya jiwe bila kuangushwa chini.”—Marko 13:2.

      Kisha kusema maneno hayo, Yesu pamoja na wanafunzi wake wanatambuka Bonde la Kidroni na wanapanda kwenye Mulima wa Mizeituni. Wakati huu iko pamoja na wanafunzi wake ine: Petro, Andrea, Yakobo, na Yohana. Wakati wako huko, wanaweza kuona vizuri hekalu lenye kupendeza.

      • Yesu anafanya nini wakati anatembelea hekalu kwa mara ya mwisho?

      • Yesu anatabiri nini kuhusu hekalu?

      • Sababu gani Yesu anasema kwamba mujane alitoa muchango mukubwa kuliko matajiri?

  • Mitume Wanaomba Alama
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
    • Yesu anajibia maulizo ya mitume wake ine

      SURA YA 111

      Mitume Wanaomba Alama

      MATAYO 24:3-51 MARKO 13:3-37 LUKA 21:7-38

      • WANAFUNZI INE WANAOMBA ALAMA

      • KUTIMIZWA KWA ALAMA KATIKA SIKU ZA MITUME NA KUENDELEA

      • TUNAPASWA KUENDELEA KUWA MACHO

      Ni Siku ya Pili kisha muchana, na siku ya Nisani 11 inaanza kumalizika. Tena utumishi mukubwa wa Yesu duniani unakaribia kufika mwisho. Muchana amekuwa akifundisha katika hekalu, na usiku amekuwa akienda kulala inje ya muji. Watu wamependezwa sana na mafundisho yake. Walikuwa “wanakuja asubui sana katika hekalu ili wamusikilize.” (Luka 21:37, 38) Yesu amekaa sasa kwenye Mulima wa Mizeituni pamoja na mitume wake ine: Petro, Andrea, Yakobo, na Yohana.

      Mitume hao ine wamekuja kwake kwa siri. Wanaogopa kwa ajili ya hekalu kwa sababu Yesu ametoka tu kutabiri kwamba hakuna jiwe lenye litaachwa juu ya jiwe. Kuko mambo mengi yenye yangali yanawahangaisha. Hapo mbele Yesu aliwaambia hivi: “Muendelee kuwa tayari, kwa sababu Mwana wa binadamu atakuja katika saa yenye hamutazamie.” (Luka 12:40) Alizungumuzia pia “siku yenye Mwana wa binadamu atafunuliwa.” (Luka 17:30) Je, maelezo hayo yanapatana kwa njia fulani na mambo yenye alitoka tu kuzungumuzia kuhusu hekalu? Mitume wanapenda kujua zaidi. Wanamuuliza: “Tuambie mambo haya yatakuwa wakati gani, na ni nini itakuwa alama ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mupangilio wa mambo?”—Matayo 24:3.

      Pengine wanawaza kwamba hawataona tena hekalu sababu litaharibiwa. Tena, wanauliza kuhusu kuwapo kwa Mwana wa binadamu. Pengine wanakumbuka kwamba Yesu alitoa mufano kuhusu “mutu fulani wa familia ya kifalme” mwenye “alisafiri kuenda inchi ya mbali ili afanywe kuwa mufalme na kisha arudie.” (Luka 19:11, 12) Na mwishowe, wanajiuliza ni nini itatokea wakati wa “umalizio wa mupangilio wa mambo.”

      Katika jibu lake lenye mambo mengi, Yesu anatoa alama yenye kuonyesha ni wakati gani mupangilio wa mambo wa Wayahudi na hekalu lake vitafikia mwisho. Lakini anatoa maelezo mengi zaidi. Wakati wenye kuja, alama hii itasaidia Wakristo watambue kwamba wanaishi katika kipindi cha “kuwapo” kwake na kwamba wanakaribia mwisho wa mupangilio wote wa mambo wa dunia.

      Kadiri miaka inaendelea, mitume wanaona utimizo wa unabii wa Yesu. Wanaanza kujionea mambo mengi yenye alitabiri. Kwa hiyo, Wakristo wenye kuwa macho wenye wanaishi miaka 37 kisha, katika mwaka wa 70 kisha kuzaliwa kwa Yesu, wako tayari kwa ajili ya uharibifu wenye kukaribia wa mupangilio wa Wayahudi na hekalu lao. Lakini, haiko mambo yote yenye Yesu anatabiri ndiyo yanatimia katika kipindi chenye kuongoza kwenye mwaka wa 70 kisha kuzaliwa kwa Yesu. Kwa hiyo, ni alama gani itaonyesha kama Yesu amekuwa Mufalme? Yesu anafunulia mitume wake jibu.

      Yesu anatabiri kama kutakuwa “vita na habari za vita” na kama “taifa litasimama kupigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme.” (Matayo 24:6, 7) Anasema tena kama “kutakuwa matetemeko makubwa ya inchi na mahali pamoja kisha pengine kutakuwa upungufu wa chakula na magonjwa hatari.” (Luka 21:11) Yesu anaonya wanafunzi wake hivi: “Watu watawakamata ninyi na kuwatesa.” (Luka 21:12) Manabii wa uongo watatokea na kupoteza watu wengi. Uvunjaji wa sheria utaongezeka, na upendo wa watu wengi utapoa. Tena, anasema kama “habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote yenye kukaliwa na watu ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote, na kisha ule mwisho utakuja.”—Matayo 24:14.

      Hata kama unabii wa Yesu unatimizwa kwa kiasi fulani kupitia matukio fulani yenye yanatokea mbele na wakati Waroma wanaharibu Yerusalemu, ingewezekana unabii huo ufikie kutimia kwa njia kubwa zaidi? Unaona ushuhuda wenye kuonyesha kwamba unabii huo wa maana unaendelea kutimia kwa njia kubwa katika wakati wetu?

      Jambo moja lenye Yesu alitia katika alama ya kuwapo kwake ni kutokea kwa “lile chukizo lenye linaleta uharibifu.” (Matayo 24:15) Katika mwaka wa 66 kisha kuzaliwa kwa Yesu, chukizo hilo lilikuwa “majeshi yenye kupiga kambi” ya Waroma, pamoja na bendera zao za ibada. Waroma wanazunguka Yerusalemu na kuharibu kuta zake fulani. (Luka 21:20) Hivyo, “lile chukizo” linasimama kwenye halingepaswa kusimama, nafasi kwenye Wayahudi waliona kuwa “mahali patakatifu.”

      Yesu anatabiri tena hivi: “Kutakuwa taabu kubwa yenye haijatokea tangu mwanzo wa ulimwengu mupaka sasa, hapana, na haitatokea tena.” Katika mwaka wa 70 kisha kuzaliwa kwa Yesu, Waroma wanaharibu Yerusalemu. Shambulio hilo la “muji mutakatifu” wa Wayahudi, kutia ndani hekalu lake, linaonekana kuwa taabu kubwa, na maelfu ya watu wanaharibiwa. (Matayo 4:5; 24:21) Huo ulikuwa uharibifu mukubwa wa muji wenye Wayahudi walikuwa hawajapata kuona, na ulimaliza namna ya ibada yenye Wayahudi walikuwa wemefuata kwa mamia ya miaka. Vilevile, hivi karibuni utimizo mukubwa wa maneno ya Yesu, bila shaka utakuwa wenye kuogopesha.

      KUWA NA UHAKIKA KATIKA SIKU ZA MWISHO

      Mazungumuzo ya Yesu pamoja na mitume wake kuhusu alama ya kuwapo kwake katika Ufalme na mwisho wa umalizio wa mupangilio wa mambo yangali yanaendelea. Sasa anawaonya kuhusu hatari ya kufuata “Makristo wa uongo na manabii wa uongo.” Anawaambia kama Makristo hao watajaribu “kupotosha, ikiwezekana, hata wale wenye kuchaguliwa.” (Matayo 24:24) Lakini wachaguliwa hawa hawatadanganywa. Makristo wa uongo wangeonekana tu kwa inje. Lakini kuwapo kwa Yesu hakutaonekana.

      Wakati anazungumuzia taabu kubwa yenye itatokea mwisho wa umalizio wa mupangilio huu wa mambo, Yesu anasema hivi: “Jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa mwangaza wake, na nyota zitaanguka kutoka mbinguni, na nguvu za mbingu zitatikiswa.” (Matayo 24:29) Wakati mitume wanasikia maelezo hayo hawajue kabisa jambo lenye litatokea, lakini bila shaka, litaogopesha sana.

      Mambo hayo yenye kuogopesha yatakuwa na matokeo gani juu ya wanadamu? Yesu anasema: “Watu watazimia kwa woga na kwa sababu ya kungojea mambo yenye yatakuja juu ya dunia yenye kukaliwa, kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.” (Luka 21:26) Kwa kweli, Yesu anaeleza kwamba kipindi hicho kitakuwa kibaya zaidi katika historia ya mwanadamu.

      Yesu anahakikishia mitume wake waziwazi kwamba haiko wote ndio wataomboleza wakati ‘Mwana wa binadamu anakuja na nguvu na utukufu mwingi.’ (Matayo 24:30) Amekwisha kuonyesha kama Mungu atatenda “kwa sababu ya wale wenye kuchaguliwa.” (Matayo 24:22) Kwa hiyo, wanafunzi waaminifu wa Yesu wanapaswa kutenda namna gani wakati mambo hayo ya kuogopesha yenye Yesu alizungumuzia yatatokea? Yesu anatia wanafunzi wake moyo hivi: “Lakini wakati mambo haya yataanza kutokea, musimame wima na kuinua vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu unakaribia.”—Luka 21:28.

      Namna gani wanafunzi wa Yesu wenye kuishi wakati huo watajua kama mwisho unakuwa karibu? Yesu anatoa mufano kuhusu muti wa tini: “Wakati tu matawi yake machanga yanakuwa teketeke na kutoa majani, munajua kwamba kipindi cha joto kinakaribia. Vilevile ninyi pia, wakati mutaona mambo yote hayo, mujue kama iko karibu kwenye milango. Kwa kweli ninawaambia ninyi kwamba kizazi hiki hakitapita hata kidogo mupaka mambo haya yote yatokee.”—Matayo 24:32-34.

      Kwa hiyo, wakati wanafunzi wake wenye kuishi katika kipindi hicho wataona mambo mbalimbali ya alama yakitimizwa, wataelewa kama mwisho unakuwa karibu. Kwa wale wanafunzi wake wenye watakuwa wazima wakati wa kipindi hicho cha maana, Yesu anawatolea onyo hili:

      “Kuhusu siku ile na saa ile, hakuna mutu mwenye anajua, ikuwe malaika wa mbinguni ao Mwana, lakini Baba tu. Kwa maana kama vile siku za Noa zilikuwa, ni vile kuwapo kwa Mwana wa binadamu kutakuwa. Kwa maana kama vile walikuwa katika siku hizo mbele ya Garika, walikuwa wanakula na kunywa, wanaume walikuwa wanaoa na wanamuke walikuwa wanaolewa, mupaka siku Noa aliingia ndani ya safina, na hawakuhangaika mupaka Garika ikakuja na kuwaharibu wote, ni vile kuwapo kwa Mwana wa binadamu kutakuwa.” (Matayo 24:36-39) Yesu analinganisha tukio hilo na Garika ya siku ya Noa. Jambo hilo lilitokea katika dunia yote.

      Mitume wenye wanasikiliza Yesu kwenye Mulima wa Mizeituni wanaelewa bila shaka kama wanapaswa kuendelea kuwa macho. Yesu anasema: “Mujiangalie ninyi wenyewe ili mioyo yenu isilemewe hata kidogo na kula kupita kiasi na kunywa sana na mahangaiko ya maisha, na kwa kushitukia siku ile ikuje juu yenu mara moja kama mutego. Kwa maana itakuja juu ya wale wote wenye kuishi katika dunia yote. Basi, muendelee kukesha, mukimulilia Mungu kila wakati ili muweze kuponyoka mambo haya yote yenye yanapaswa kutokea na kusimama mbele ya Mwana wa binadamu.”—Luka 21:34-36.

      Hapa, Yesu anaonyesha tena kama mambo yenye anatabiri yatakuwa katika dunia yote. Matukio yenye anatabiri hayatagusa Yerusalemu tu na taifa la Wayahudi kwa miaka 30 ao 40 tu. Lakini yatakuja “juu ya wale wote wenye kuishi katika dunia yote.”

      Anasema kama wanafunzi wake wanapaswa kuendelea kuwa macho, wenye kukesha, na kuwa tayari. Anakazia wazo hilo kupitia mufano huu mwengine: “Mujue jambo hili: Kama mwenye nyumba angejua ni wakati gani usiku mwizi atakuja, angekaa macho na hangeruhusu nyumba yake ivunjwe. Kwa hiyo ninyi pia mukuwe tayari, kwa sababu Mwana wa binadamu atakuja katika saa yenye hamuwazie.”—Matayo 24:43, 44.

      Yesu anatolea wanafunzi wake sababu ingine ya kutazamia mambo ya muzuri. Anawahakikishia kwamba wakati unabii wake unaendelea kutimia, kutakuwa “mutumwa” mwenye kuwa macho na mwenye kutenda. Yesu anazungumuzia hali fulani yenye mitume wanaweza kuwazia haraka: “Ni nani kwa kweli mutumwa mwaminifu na mwenye busara mwenye bwana wake ameweka juu ya watumishi wake wa nyumbani, ili kuwapatia chakula chao kwa wakati wenye kufaa? Mwenye furaha ni mutumwa huyo Kama bwana wake wakati atakuja atamukuta akifanya vile! Kwa kweli ninawaambia ninyi, atamuweka juu ya mali zake zote.” Lakini kama ule “mutumwa” anakuwa na nia mbaya na kutesa “wenzake,” bwana “atamupatia azabu kwa ukali mukubwa zaidi.”—Matayo 24:45-51; linganisha na Luka 12:45, 46.

      Lakini, Yesu haseme kama kikundi cha wafuasi wake watakuwa na nia ya mubaya. Kwa hiyo, ni somo gani lenye Yesu anapenda kufundisha wanafunzi wake? Anapenda wakae macho na wenye kutenda, kama vile atafasiria hilo waziwazi katika mufano mwengine.

      • Ni nini inasukuma mitume kuuliza Yesu kuhusu matukio ya wakati wenye kuja, lakini inaonekana kama wako na mawazo gani katika akili?

      • Ni wakati gani unabii wa Yesu unaanza kutimia, na namna gani?

      • Ni mambo gani yataonyesha kuwapo kwa Kristo?

      • Namna gani “chukizo” linatokea, na ni matukio gani yanafuata kutokea kwake?

      • Watu watatenda namna gani wakati watajionea utimizo wa unabii wa Yesu?

      • Ni mufano gani wenye Yesu anatoa ili kusaidia wanafunzi wake watambue kama mwisho unakuwa karibu?

      • Ni nini inaonyesha kama unabii wa Yesu utatimia katika dunia yote?

      • Ni onyo gani Yesu anatolea wanafunzi wake wenye wanaishi karibu na mwisho wa mupangilio wa mambo?

  • Mufano wa Mabikira Kumi—Somo Kuhusu Kukesha
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
    • Mabikira watano wenye busara wakiwa na taa zao zenye kuwaka

      SURA YA 112

      Mufano Wa Mabikira Kumi—somo Kuhusu Kukesha

      MATAYO 25:1-13

      • YESU ANATOA MUFANO WA MABIKIRA KUMI

      Yesu anaendelea kujibu ulizo la mitume wake kuhusu alama ya kuwapo kwake na ya umalizio wa mupangilio wa mambo. Sasa, anawatolea shauri lenye hekima kupitia mufano mwengine. Wale wenye kuishi wakati wa kuwapo kwake wataona kutimizwa kwa mufano huo.

      Anaanza mufano wake, kwa kusema: “Ufalme wa mbinguni unaweza kufananishwa na mabikira kumi (10) wenye walikamata taa zao na kuenda kumupokea bwana-arusi. Watano (5) kati yao walikuwa wapumbavu, na watano (5) walikuwa wenye busara.”—Matayo 25:1, 2.

      Yesu hatake kusema kama nusu ya wanafunzi wake wenye wanariti Ufalme wa mbinguni ni wapumbavu na kama wengine nusu ni wenye busara. Lakini anapenda kuonyesha kwamba kuhusu Ufalme, kila mwanafunzi wake anaweza kuchagua kukesha ao kukengeushwa. Yesu iko hakika kwamba kila mwanafunzi wake anaweza kubaki muaminifu na kupokea baraka kutoka kwa Baba yake.

      Katika mufano, mabikira wote kumi wanaenda kumupokea bwana-arusi na wanaenda kujiunga na kikundi cha kusindikiza bwana-arusi na bibi-arusi. Wakati anafika, mabikira wataangazia njia kwa taa zao, wakionyesha heshima kwa bwana-arusi wakati analeta bibi-arusi wake katika nyumba yenye ilitayarishwa kwa ajili yake. Lakini sasa mambo yanatendeka namna gani?

      Yesu anaeleza hivi: “Wale wapumbavu walibeba taa zao lakini hawakubeba mafuta ya kuongeza, lakini wale wenye busara walibeba taa zao pamoja na mafuta katika chupa zao. Wakati bwana-arusi alikawia kuja, wote walisinzia na kuanza kulala.” (Matayo 25:3-5) Bwana-arusi hafike haraka kama vile alitazamiwa. Inaonekana anachelewa sana, kwa hiyo mabikira wanalala. Pengine mitume wanakumbuka yale yenye Yesu alieleza kuhusu mutu fulani wa familia ya kifalme mwenye alisafiri na ‘mwishowe alirudia kisha kupokea ufalme.’—Luka 19:11-15.

      Katika mufano wa mabikira kumi, Yesu anaeleza jambo lenye linatokea wakati mwishowe bwana-arusi anafika: “Katikati ya usiku kukatokea sauti kubwa: ‘Bwana-arusi anafika! Muende mumupokee.’” (Matayo 25:6) Je, mabikira wako tayari na wenye kukesha?

      Yesu anaendelea hivi: “Kisha wale mabikira wote wakasimama na kutayarisha taa zao. Wale wapumbavu wakaambia wenye busara, ‘Mutupatie sehemu kidogo ya mafuta yenu, kwa sababu taa zetu zinakaribia kuzimika.’ Wale wenye busara wakawajibu, na kusema: ‘Pengine hakutakuwa ya kutuenea sisi na ninyi. Lakini muende kwa wenye kuyauzisha, na mujinunulie yenu.’”—Matayo 25:7-9.

      Kwa hiyo mabikira watano wapumbavu hawakeshe na hawako tayari kwa ajili ya kufika kwa bwana-arusi. Wanakosa mafuta yenye kuenea kwa ajili ya taa zao na wanajaribu kutafuta mafuta. Yesu anaeleza: “Wakati walikuwa wanaenda kununua mafuta, bwana-arusi akafika. Wale mabikira wenye walikuwa tayari wakaingia pamoja naye kwenye karamu ya ndoa, na mulango ukafungwa. Kisha, wale mabikira wengine pia wakakuja, na kusema, ‘Bwana, Bwana, tufungulie!’ Akawajibu, ‘Ninawaambia kweli, siwajue ninyi.’” (Matayo 25:10-12) Matokeo yenye kuhuzunisha kabisa kwa sababu hawakuendelea kuwa tayari na hawakukesha.

      Mitume wanaweza kutambua kwamba bwana-arusi mwenye Yesu anazungumuzia ni yeye mwenyewe. Hapo mbele alijifananisha na bwana-arusi. (Luka 5:34, 35) Sasa mabikira wenye busara ni nani? Wakati alizungumuzia “kundi ndogo,” wenye wangepewa Ufalme, Yesu alitumia maneno haya: “Muvae nguo na mukuwe tayari na taa zenu zikuwe zenye kuwaka.” (Luka 12:32, 35) Kwa hiyo katika mufano huu kuhusu mabikira, mitume wanaweza kuelewa kwamba Yesu anazungumuzia juu yao wenyewe. Kwa hiyo, ni ujumbe gani Yesu anapenda kutoa kupitia mufano huo?

      Yesu anapenda kuhakikisha kwamba wanaelewa. Kwa hiyo anamalizia mufano huo kwa kuwaambia hivi: “Muendelee kukesha, kwa sababu hamujue siku wala saa.”—Matayo 25:13.

      Ni wazi kwamba Yesu anaonya wafuasi wake waaminifu kwamba wakati wa kuwapo kwake, wanapaswa, ‘kuendelea kukesha.’ Atakuja, na wanapaswa kuwa tayari na kukesha, kama wale mabikira tano ili wasipoteze tumaini lao la maana sana na kukosa baraka.

      • Namna gani mabikira waaminifu watano wako tofauti na mabikira wapumbavu watano katika kukesha na kuwa tayari?

      • Bwana-arusi anafananisha nani, na mabikira wanafananisha nani?

      • Ni ujumbe gani Yesu anapenda kutoa kuhusiana na mufano wa mabikira kumi?

  • Mufano wa Talanta—Somo Kuhusu Bidii
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
    • Mutumwa anazika mufuko wa feza katika udongo

      SURA YA 113

      Mufano Wa Talanta—somo Kuhusu Bidii

      MATAYO 25:14-30

      • YESU ANATOA MUFANO WA TALANTA

      Wakati angali na mitume wake ine kwenye Mulima wa Mizeituni, Yesu anawatolea mufano mwengine. Siku kidogo mbele ya hapo, wakati alikuwa Yeriko alitoa mufano wa mina ili kuonyesha kwamba Ufalme haungekuja wakati huo. Mufano wenye anatoa sasa uko na mambo yenye kufanana na mufano wenye alikuwa ametoa wakati huo. Mufano huu ni sehemu ya jibu lake kwa ulizo lenye kuhusu kuwapo kwake na kuhusu umalizio wa mupangilio wa mambo. Unaonyesha kwamba wanafunzi wake wanapaswa kufanya kwa bidii mambo yenye anawaomba.

      Yesu anaanza kwa kusema hivi: “Ni kama mutu mwenye alikuwa karibu kusafiri kuenda katika inchi ingine, mwenye aliita watumwa wake na kuwapatia mali zake.” (Matayo 25:14) Kwa kuwa Yesu alikuwa tayari amejifananisha na mutu mwenye kusafiri katika inchi ingine “ili afanywe kuwa mufalme,” mitume wangeelewa haraka kwamba Yesu ndiye ule “mutu” mwenye kuzungumuziwa sasa.—Luka 19:12.

      Mbele mutu huyo asafiri na kuenda katika inchi ingine, anaachia watumwa wake mali. Wakati wa utumishi wake wa miaka tatu na nusu, Yesu alikazia kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu, na alizoeza wanafunzi wake kufanya kazi hiyo. Sasa anaenda zake, akiwa hakika kwamba wataendelea kufanya mambo kulingana na mazoezi yenye aliwatolea.—Matayo 10:7; Luka 10:1, 8, 9; linganisha na Yohana 4:38; 14:12.

      Katika mufano huo, namna gani mutu huyo anagawanya mali zake? Yesu anaeleza: “Akapatia mumoja talanta tano (5), mwingine mbili, na mwingine moja, kila mumoja kulingana na uwezo wake mwenyewe, kisha akaenda katika inchi ingine.” (Matayo 25:15) Namna gani watumwa hao watatumikisha mali zenye walipewa? Watazitumia kwa bidii ili kuletea bwana wao faida nyingi? Yesu anaambia mitume hivi:

      “Mara moja ule mwenye alipokea talanta tano (5) akaenda na kufanya nazo biashara, akapata faida ya talanta zingine tano (5). Vilevile, ule mwenye alipokea talanta mbili, akapata faida ya talanta zingine mbili. Lakini mutumwa mwenye alipokea talanta moja tu akaenda akachimba katika udongo na kuficha zile feza za bwana wake.” (Matayo 25:16-18) Mambo yanakuwa namna gani wakati bwana wao anarudi?

      Yesu anaendelea: “Kisha wakati murefu, bwana wa watumwa hao akarudia na kufanya hesabu nao.” (Matayo 25:19) Wale watumwa wawili wa kwanza walifanya yao yote, “kila mumoja kulingana na uwezo wake mwenyewe.” Kila mutumwa alikuwa na bidii, alitumika sana, na alipata faida wakati alitumikisha mali yenye walimupatia. Ule mwenye alipokea talanta tano alipata ingine tano, na ule mwenye alipokea talanta mbili alipata ingine mbili. (Wakati huo, mufanyakazi alipaswa kutumika sana kwa miaka karibu 19 ili kupata mushahara wenye kulingana na talanta moja.) Bwana wao alisifu kila mumoja wao kwa maneno haya: “Umefanya muzuri, mutumwa mwema na mwaminifu! Ulikuwa mwaminifu katika mambo kidogo. Nitakuweka usimamie mambo mengi. Ingia katika furaha ya bwana wako.”—Matayo 25:21.

      1. Mutumwa anazika mufuko wa feza katika udongo; 2. Mutumwa huyo anatupwa inje katika giza

      Mambo yako tofauti na mutumwa mwenye alipokea talanta moja. Anasema hivi: “Bwana nilijua wewe ni mutu mugumu, unavuna mahali kwenye haukupanda na unakusanya mahali kwenye haukupepulia. Kwa hiyo, niliogopa na nikaenda kuficha talanta yako katika udongo. Angalia, mali yako ndiyo hii.” (Matayo 25:24, 25) Hakuweza hata kutia feza hizo katika benki ili bwana wake azichukue pamoja na faida. Kwa kweli, ametenda tofauti na vile bwana wake alimuomba.

      Ndiyo sababu, bwana wake anamuita “mutumwa muovu na muvivu.” Talanta yenye alikuwa nayo inapewa mutumwa mwingine mwenye iko tayari kutumika kwa bidii. Bwana anajulisha kanuni yake: “Kila mutu mwenye kuwa na kitu, ataongezewa, na atakuwa na vingi. Lakini ule mwenye hana, atanyanganywa hata kile chenye iko nacho.”—Matayo 25:26, 29.

      Wanafunzi wa Yesu wanahubiri

      Mufano huu unapaswa kufanya wanafunzi wafikiri sana. Wanapaswa kuelewa kwamba, pendeleo la kufanya wanafunzi, lenye Yesu amewatolea ni la maana sana. Na anatazamia kwamba watatumika kwa bidii. Yesu hawaze kama wote wanapaswa kutimiza kwa namna ileile kazi ya kuhubiri yenye amewatolea. Kama vile inaonyeshwa katika mufano huo, kila mumoja wao angefanya yote yenye anaweza “kulingana na uwezo wake mwenyewe.” Inamaanisha kama Yesu hatapendezwa hata kidogo ikiwa mumoja kati yao anakuwa “muvivu” na anashindwa kufanya yake yote ili kuongeza mali za Bwana.

      Mitume wanapaswa kufurahi kabisa, wakati wanasikia maneno haya: “Kila mutu mwenye kuwa na kitu, ataongezewa”!

      • Katika mufano wa talanta, bwana ni nani, na watumwa ni nani?

      • Yesu anafundisha wanafunzi wake somo gani?

  • Mufalme Yesu Kristo Anahukumu Kondoo na Mbuzi
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
    • Watu wa mataifa yote wanaangalia juu mbinguni wakingojea hukumu ya Yesu

      SURA YA 114

      Mufalme Yesu Kristo Anahukumu Kondoo Na Mbuzi

      MATAYO 25:31-46

      • YESU ANATOA MUFANO WA KONDOO NA MBUZI

      Kwenye Mulima wa Mizeituni, Yesu anatoka tu kuzungumuzia mifano ya talanta na ya mabikira kumi. Namna gani anamalizia jibu lake kwa ulizo la mitume lenye kuhusu alama ya kuwapo kwake na ya umalizio wa mupangilio wa mambo? Anafanya hivyo kwa kutoa mufano wake wa mwisho, ule wa kondoo na mbuzi.

      Anaanza kwa kufasiria maneno yenye kupatana na mufano wake. Anawaambia hivi: “Wakati Mwana wa binadamu atakuja katika utukufu wake, na malaika wote pamoja naye, basi atakaa kwenye kiti chake cha ufalme chenye utukufu.” (Matayo 25:31) Bila shaka, mutu wa maana katika mufano huu haiko mwengine, ni Yesu. Mara nyingi alijiita mwenyewe “Mwana wa binadamu.”—Matayo 8:20; 9:6; 20:18, 28.

      Yesu anakaa katika kiti chake chenye utukufu na anahukumu watu waaminifu kuwa kondoo

      Mufano huu utatimia wakati gani? Ni wakati Yesu “atakuja katika utukufu wake” pamoja na malaika zake na kukaa kwenye “kiti chake chenye utukufu.” Amekwisha kuzungumuzia kuhusu “Mwana wa binadamu akikuja juu ya mawingu ya mbinguni akiwa na nguvu na utukufu mwingi” pamoja na malaika zake. Hilo litatokea wakati gani? “Kisha tu taabu ya siku hizo.” (Matayo 24:29-31; Marko 13:26, 27; Luka 21:27) Kwa hiyo, mufano huu unapaswa kutimia wakati Yesu atakuja katika utukufu wake. Kisha, atafanya nini?

      Yesu anaeleza hivi: “Wakati Mwana wa binadamu atakuja . . . , mataifa yote yatakusanywa mbele yake, na atatenganisha watu mumoja na mwingine, kama vile muchungaji anatenganisha kondoo na mbuzi. Na ataweka kondoo kwenye mukono wake wa kuume, lakini mbuzi kwenye mukono wake wa kushoto.”—Matayo 25:31-33.

      Kuhusu kondoo, Yesu anasema: “Kisha Mufalme ataambia wale wenye kuwa kwenye mukono wake wa kuume: ‘Mukuje, ninyi wenye mumebarikiwa na Baba yangu, muriti Ufalme wenye ulitayarishwa kwa ajili yenu tangu kuwekwa musingi wa ulimwengu.’” (Matayo 25:34) Sababu gani kondoo wanakubaliwa na Mufalme?

      Mufalme anaeleza hivi: “Kwa maana nilikuwa na njaa, mukanipatia chakula; nilikuwa na kiu, mukanipatia kitu cha kunywa. Nilikuwa mugeni, mukanikaribisha muzuri; nilikuwa uchi, mukanivalisha. Nilikuwa mugonjwa mukanihangaikia. Nilikuwa katika gereza mukanitembelea.” Wakati kondoo hao, ni kusema, “wale wenye kufanya mambo yenye kuwa sawa,” wanauliza, namna gani walitenda mambo mazuri, Yesu anawajibu hivi: “Kwa kadiri mulitendea vile mumoja wa wadogo zaidi kati ya hawa ndugu zangu, mulinitendea mimi.” (Matayo 25:35, 36, 40, 46) Hawafanye mambo haya ya muzuri mbinguni, kwa sababu huko hakuna wagonjwa na wenye njaa. Mambo hayo ya muzuri yanapaswa kuwa matendo yenye walifanyia ndugu za Kristo hapa duniani.

      Kikundi cha watu wenye hawako waaminifu wanahukumiwa kuwa mbuzi

      Mambo yako namna gani kuhusu mbuzi wenye kuwa kwenye mukono wa kushoto? Yesu anasema: “Kisha [Mufalme] ataambia wale wenye kuwa kwenye mukono wake wa kushoto: ‘Mutoke muende mbali na mimi, ninyi wenye mumelaaniwa, muende katika moto wa milele wenye ulitayarishwa kwa ajili ya Ibilisi na malaika zake. Kwa maana nilikuwa na njaa, lakini hamukunipatia chakula; nilikuwa na kiu, lakini hamukunipatia kitu cha kunywa. Nilikuwa mugeni, lakini hamukunikaribisha; nilikuwa uchi, lakini hamukunivalisha; nilikuwa mugonjwa na nilikuwa katika gereza, lakini hamukunihangaikia.’” (Matayo 25:41-43) Mbuzi wanastahili kabisa hukumu hiyo kwa sababu walishindwa kutendea muzuri ndugu za Kristo wenye kuwa duniani namna inapaswa.

      Mitume wanajifunza kwamba maamuzi yenye yatafanywa wakati huo wa hukumu yatakuwa na matokeo ya milele. Yesu anawaambia hivi: “Halafu [Mufalme] atawajibu na kusema: ‘Kwa kweli ninawaambia ninyi, kwa kadiri hamukutendea vile mumoja wa hawa wadogo zaidi, hamukunitendea mimi.’ Hawa wataangamizwa milele, lakini wale wenye kufanya mambo yenye kuwa sawa wataingia katika uzima wa milele.”—Matayo 25:45, 46.

      Jibu la Yesu kwa ulizo la mitume linatolea wafuasi wake mambo mengi ya kufikiria, linawasaidia kuchunguza matendo na mambo yenye kuwa katika mioyo yao.

      • Katika mufano wa Yesu kuhusu kondoo na mbuzi, “Mufalme” ni nani, na mufano huo utatimia wakati gani?

      • Sababu gani kondoo watahukumiwa kuwa wenye kustahili kukubaliwa na Yesu?

      • Watu fulani watahukumiwa kuwa mbuzi kwa musingi gani, na ni mambo gani yanangojea kondoo na mbuzi?

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine