Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha
© 2023 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
TAREHE 1-7/5
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 MAMBO YA NYAKATI 17-19
“Ona Wengine Vile Yehova Anawaona”
Utatia Moyo Wako Katika Mambo Yenye Kuandikwa?
7 Tuzungumuzie sasa mufano wa Yehoshafati, mutoto mwanaume wa Asa. Alikuwa na sifa nyingi za muzuri zenye zilimupendeza Yehova. Na wakati alimutegemea Yehova, alifanya mambo mengi ya muzuri. Lakini yeye pia alikamata maamuzi fulani ya mubaya. Kwa mufano, alifanya mipango ili mutoto wake mwanaume aoe mutoto mwanamuke mumoja wa Ahabu, mufalme mubaya. Kisha, Yehoshafati alijiunga na Ahabu ili kupigana vita na Wasiria, hata kama nabii Mikaya alimuonya asifanye hivyo. Katika vita hivyo, Wasiria walimushambulia Yehoshafati na kujaribu kumuua. (2 Mambo ya Nyakati 18:1-32) Wakati alirudia Yerusalemu, nabii Yehu alimuuliza hivi: ‘Je, waovu wanapaswa kupewa musaada, na je, unapaswa kuwapenda wale wanaomuchukia Yehova?’—Soma 2 Mambo ya Nyakati 19:1-3.
Ufikiri Sana Juu ya Upendo wa Yehova Wenye Hauna Mwisho
8 Yehova anapenda tujue kwamba anatupenda na kwamba hakazie sana makosa yetu kwa sababu anatafuta mambo mazuri yenye kuwa ndani yetu. (2 Mambo ya Nyakati 16:9) Acha sasa tuchunguze namna Yehova aliona mambo mazuri yenye ilikuwa ndani ya Mufalme Yehoshafati wa Yuda. Yehoshafati alifanya uamuzi mubaya kwa kujiunga na Mufalme Ahabu wa Israeli ili kupiganisha Wasiria huko Ramothi-gileadi. Hata kama manabii wa uongo 400 walimuambia Mufalme muovu Ahabu kwamba atapata ushindi, Mikaya, nabii wa kweli wa Yehova, aliambia Yehoshafati na Ahabu kwamba ikiwa wanapigana vita hiyo, watashindwa. Na maneno ya nabii Mikaya ilitimia kabisa. Ahabu alikufa kwenye vita, na Yehoshafati aliponea kwa bahati. Kisha vita hiyo, Yehova alitumia Yehu ili kumushauria Yehoshafati kwa sababu ya kosa lenye alifanya. Lakini, Yehu alimuambia pia hivi: “Kuna mambo mema ambayo yameonekana kwako.”— 2 Mambo ya Nyakati 18:4, 5, 18-22, 33, 34; 19:1-3.
9 Miaka mingi mbele ya hapo, Yehoshafati alikuwa ameambia wakubwa, Walawi, na makuhani kwamba wazunguke katika miji yote ya Yuda ili kufundisha watu Sheria ya Yehova. Walipata matokeo mazuri sana, kwa sababu hata watu wa mataifa mengine walifikia kumujua Yehova. (2 Mambo ya Nyakati 17:3-10) Kwa hiyo, hata kama Yehoshafati alichukua uamuzi mubaya kisha, Yehova hakusahau mambo mazuri yenye alikuwa amefanya katika maisha yake hapo zamani. Mufano huo unatutia moyo sana kwa sababu wakati fulani sisi pia tunafanya makosa. Hata hivyo, ikiwa tunafanya nguvu yetu yote ili kumutumikia Yehova, ataendelea kutupenda na hatasahau mambo mazuri yenye tumefanya.
Mali ya Kiroho
Umutumikie Yehova kwa Moyo Mukamilifu!
10 Yehoshafati, mutoto mwanaume wa Asa, “akaendelea kutembea katika njia ya Asa baba yake.” (2 Mambo ya Nyakati 20:31, 32) Namna gani? Kama baba yake, Yehoshafati alitia watu moyo waendelee kumuabudu Yehova. Alituma wanaume katika miji mbalimbali ya Yuda ili wafundishe watu mambo yenye kuwa katika “kitabu cha Sheria ya Yehova.” (2 Mambo ya Nyakati 17:7-10) Alienda hata kwa watu wenye walikuwa katika eneo lenye milima la Efraimu katika eneo la ufalme wa kaskazini wa Israeli, “ili kuwarudisha kwa Yehova.” (2 Mambo ya Nyakati 19:4) Yehoshafati alikuwa mufalme mwenye ‘alimutafuta Yehova kwa moyo wake wote.’—2 Mambo ya Nyakati 22:9.
11 Leo, Yehova anapenda watu katika dunia yote wafundishwe juu yake, na sisi wote tunaweza kusaidia katika kazi hiyo. Umejiwekea muradi wa kufanya kazi hiyo kila mwezi? Unapenda kufundisha wengine Biblia ili wao pia waanze kumuabudu Yehova? Unasali kwa ajili ya jambo hilo? Ikiwa unajikaza, Yehova anaweza kukusaidia kuanzisha funzo la Biblia. Utakuwa tayari kujifunza na mutu fulani hata kama hilo linaweza kukuomba utumie wakati wako wa mapumuziko? Na kama vile tu Yehoshafati alijikaza kusaidia wengine waanze tena kumutumikia Yehova, tunaweza kujikaza kusaidia wale wenye wameacha kuhubiri na kukusanyika. Pia, wazee wa kutaniko wanapanga kutembelea na kusaidia watengwa wenye kuwa katika eneo la kutaniko wenye pengine wameacha mwenendo wao wa zambi wa zamani.
Hotuba: Endelea Kuwa na Mawazo ya Muzuri Hata Kama Watu Hawapendezwe
Endelea Kuwa na Mawazo ya Muzuri juu ya Mahubiri
11 Watu fulani hawapendezwe na ujumbe wetu. Wanaona kama hawana lazima ya Mungu wala Biblia. Hawamuamini Mungu juu wako wanaona mateso mingi mu dunia. Wanakatala Biblia juu wanaona kama viongozi wengi wa dini ni wanafiki, hawaishi kupatana na mambo yenye iko mu Biblia. Wengine wanahangaikia zaidi kazi zao, familia, mambo yao ya kipekee, na hawaone namna gani Biblia inaweza kusaidia. Namna gani tunaweza kuchunga furaha yetu wakati tunahubiria watu wenye hawapendezwe kabisa na Biblia?
12 Uonyeshe kama unahangaikia wengine. Watu wengi wenye ku mwanzo hawakukuwa wanapendezwa na habari njema walifikia kuipenda kisha, juu muhubiri fulani aliwaonyesha kabisa kama anawahangaikia. (Soma Wafilipi 2:4.) Kwa mufano, David, mwenye tulishataja, anasema hivi: “Kama mutu fulani anasema kama hawapendezwe, tunatia kwanza pembeni mambo ya Biblia na mambo ya vichapo na kisha tunamuambia: ‘Nilipenda kujua juu ya nini unawaza vile.’” Watu wanaonaka kama tunawahangaikia. Wanaweza kusahau mambo yenye tuliwaambia, lakini pengine hawawezi kusahau namna tulifanya wajisikie. Pengine mwenye-nyumba hawezi kutuachia wakati tuseme, lakini tunaweza kuonyesha kama tunamuhangaikia kupitia namna yetu ya kutenda na pia kupitia ishara za uso.
13 Tunaonyesha kama tunahangaikia watu wakati tunabadilisha namna yetu ya kusema ili ujumbe wetu upatane na hali ya mwenye-nyumba na ili aufurahie. Kwa mufano, kuko alama fulani zenye zinakuonyesha kama mu hii nyumba muko watoto? Wazazi wanaweza kufurahia sana mashauri ya Biblia kuhusu namna ya kukomalisha watoto na namna ya kuwa na maisha ya familia yenye furaha. Unaona kufuli za mingi ku mulango? Unaweza kuamua kuzungumuza juu ya jeuri na namna ile inafanya watu waogope sana leo. Pengine mwenye-nyumba anaweza kufurahia kujua kama kuko siku ile hali itaisha. Ikuwe ni hali gani, usaidie kabisa wale wenye wanapenda kujua namna mashauri ya Biblia inaweza kuwasaidia. Katarína, mwenye tulishataja, anasema hivi: “Siwezi kusahau namna Biblia imenisaidia mu maisha yangu.” Matokeo inakuwa gani? Katarína anaamini kabisa mambo yenye iko anasema, na watu wenye iko anazungumuza nao wanaona vile.
14 Ukubali musaada wa wengine. Paulo alimufundisha Timoteo ufundi wake wa kuhubiri na kufundisha na alimutia moyo afundishe wengine pia namnna ya kufanya vile. (1 Ko. 4:17) Sawa vile Timoteo, na siye pia tunaweza kujifunza mambo fulani kupitia uzoefu wa ndugu na dada mu kutaniko. (Soma Mezali 27:17.) Fikiria mufano wa ndugu mwenye kuitwa Shawn. Wakati fulani alifanya kazi ya upainia katika eneo lenye watu wengi walifurahia kuwa mu dini yao. Namna gani aliendelea kuchunga furaha yake? Anasema hivi: “Wakati wowote wenye iliwezekana, nilihubiri pamoja na ndugu ao dada fulani. Wakati tulitoka ku mulango moja ili kuenda ku mulango ingine, tulitumia ile wakati ili kusaidiana kukomalisha ufundi wetu wa kufundisha. Kwa mufano, tulizungumuzia mambo yenye mwenye-nyumba alisema na namna tulimujibia. Kisha tulizungumuzia namna tunaweza kufanya wakati ingine ikiwa mwenye-nyumba anasema mambo ya kufanana na ile.”
15 Usali kwa Yehova ili akusaidie. Umuombe Yehova akusaidie kila wakati unahubiri, juu bila musaada wa roho yake takatifu hakuna mwenye anaweza kutimiza jambo lolote. (Zb. 127:1; Lu. 11:13) Wakati unamuomba Yehova akusaidie, umuambie mambo waziwazi. Kwa mufano, umuombe Yehova akuongoze kwa kila mutu mwenye anapenda kujifunza juu yake na mwenye iko tayari kusikiliza. Kisha utende kulingana na sala yako kwa kuhubiria kila mutu mwenye unakutana naye.
TAREHE 8-14/5
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 MAMBO YA NYAKATI 20-21
“Umutumainie Yehova Mungu Wako”
Namna ya Kupambana na Mwisho wa Ulimwengu huu kwa Umoja
8 Katika siku za Mufalme Yehoshafati, watu wa Mungu walipambana na ‘umati mukubwa’ wa maadui wenye kuogopesha kutoka katika maeneo yenye ilikuwa inawazunguka. (2 Nya. 20:1, 2) Jambo la kufurahisha ni kwamba, watu wa Mungu hawakujaribu kupiganisha maadui wao kwa nguvu zao wenyewe. Lakini, walimutegemea Yehova. (Soma 2 Mambo ya Nyakati 20:3, 4.) Na Waisraeli hawakufanya hivyo wakiwa mumoja-mumoja, lakini walitenda kwa umoja. Biblia inasema kwamba “watu wote wa Yuda walikuwa wamesimama mbele za Yehova, hata watoto wao, wake zao na wana wao.” (2 Nya. 20:13) Wote pamoja, iwe ni vijana ao hapana, walijikaza kufuata muongozo wa Yehova, na Yehova aliwalinda. (2 Nya. 20:20-27) Mufano huo muzuri unaonyesha namna watu wa Mungu wanapaswa kupambana na magumu kwa umoja.
Nyie Wenye Mumetoka tu Kuoana—Mutie Kazi ya Yehova pa Nafasi ya Kwanza
7 Yehova alisema na Yehoshafati kupitia Mulawi mwenye kuitwa Yahazieli. Yehova alisema hivi: “Musimame mahali penu, musimame bila kutikisika, na muone wokovu wa Yehova kwa ajili yenu.” (2 Ny. 20:13-17) Kwa kawaida, haiko vile njo watu wanapiganaka vita! Lakini, ile maagizo haikutolewa na mwanadamu; ni Yehova njo aliitoa. Juu Yehoshafati alimutegemea sana Mungu, alitii ile maagizo. Wakati walienda ili kukutana na maadui, Yehoshafati aliweka mbele waimbaji wenye hawakukuwa na silaha, hapana maaskari wenye walikuwa na uzoefu sana. Yehova hakuachilia Yehoshafati. Alimusaidia kwa kupiga maadui wake.—2 Ny. 20:18-23.
Mali ya Kiroho
it-2-F uku. 1190 fu. 5, 6
Yehoramu
Yehoramu hakufuata njia ya muzuri ya baba yake Yehoshafati. Uvutano mubaya wa bibi yake Atalia ulichangia mwenendo wake mubaya. (2Fa 8:18) Zaidi ya kuua ndugu zake sita na wakubwa fulani wa Yuda, alichochea watu wamuache Yehova na wafuate miungu ya uongo. (2Ny 21:1-6, 11-14) Wakati wote wenye alikuwa mufalme, mu utawala wake mulikuwa muvurugo na pia inje ya utawala wake. Kwanza, Waedomu waliasi; kisha Walibna pia waliasi Yuda. (2Fa 8:20-22) Mu barua yenye nabii Eliya alimuandikia Yehoramu, alimuonya hivi: “Yehova analeta pigo kubwa kwa watu wako, kwa wana wako, kwa bibi zako, na kwa mali zako zote.” Zaidi ya ile, weye Mufalme Yehoramu, “utateseka kwa magonjwa mengi, kutia ndani ugonjwa wa matumbotumbo yako, mupaka matumbotumbo yako yatatoka inje kwa sababu ya ugonjwa huo, siku kwa siku.”—2Ny 21:12-15.
Ni vile njo mambo ilifanyika. Yehova aliruhusu Waarabu na Wafilisti washambulie Yuda na kukamata bibi za Yehoramu na watoto wake. Mungu aliruhusu tu Yehoahazi (mwenye kuitwa pia Ahazia), mutoto wa mwisho ya Yehoramu aponyoke. Alifanya vile juu tu ya agano yenye alifanyaka pamoya na Daudi. “Na kisha mambo hayo yote, Yehova akamupiga [Yehoramu] kwa ugonjwa wenye hauwezi kupona katika matumbotumbo yake.” Kisha miaka mbili, “matumbotumbo yake yalitoka inje” na pole kwa pole alifikia kufa. Ni vile maisha ya ule mutu mubaya ilifikia mwisho. “Hakuna mutu yeyote mwenye alihuzunika wakati alikufa.” Basi wakamuzika katika muji wa Daudi, “lakini hapana katika makaburi ya wafalme.” Mwana wake Ahazia akakuwa mufalme pa nafasi yake.—2Ny 21:7, 16-20; 22:1; 1Ny 3:10, 11.
TAREHE 15-21/5
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 MAMBO YA NYAKATI 22-24
“Yehova Anabariki Matendo ya Uhodari”
w09 1/4 uku. 24 fu. 1-2
Yehoashi Alimwacha Yehova kwa Sababu ya Marafiki Wabaya
HALI zilikuwa zenye kutisha sana katika jiji la Yerusalemu palipokuwa hekalu la Mungu. Mfalme Ahazia alikuwa ameuawa. Wazia yale ambayo mama ya Ahazia anayeitwa Athalia, alifanya muda mfupi tu baada ya Mfalme Ahazia kuuawa! Aliamuru wana wa Ahazia wauawe, yaani, alitaka wajukuu wake mwenyewe wauawe! Unajua kwa nini?— Ni kwa sababu alitaka kuwa mtawala badala ya yeyote kati yao.
Hata hivyo, mjukuu mmoja wa Athalia, mtoto mchanga Yehoashi hakuuawa, lakini nyanya yake hakujua. Ungependa kujua jinsi alivyoepuka kuuawa?— Shangazi wa Yehoashi anayeitwa Yehosheba alimficha yule mtoto mchanga katika hekalu la Mungu. Aliweza kufanya hivyo kwa sababu Kuhani Mkuu Yehoyada alikuwa mume wake. Yehosheba na Yehoyada walihakikisha kwamba Yehoashi alikuwa salama salimini.
w09 1/4 uku. 24 fu. 3-5
Yehoashi Alimwacha Yehova kwa Sababu ya Marafiki Wabaya
Yehoashi alifichwa hekaluni kwa miaka sita. Akiwa humo alifundishwa kumhusu Yehova Mungu na sheria zake. Hatimaye, Yehoashi alipokuwa na miaka saba, Yehoyada alichukua hatua ya kumfanya kuwa mfalme. Ungependa kujua jinsi Yehoyada alivyofanya jambo hili na yaliyompata nyanya ya Yehoashi, yule Malkia mwovu Athalia?—
Yehoyada aliwakusanya kisiri walinzi waliokuwa wakiwalinda wafalme huko Yerusalemu siku hizo. Aliwaeleza jinsi yeye na mkewe walivyokuwa wamemficha mtoto mchanga wa Mfalme Ahazia ili asiuawe. Halafu Yehoyada akamleta Yehoashi mbele ya walinzi hao ambao walitambua kwamba yeye ndiye anayepaswa kuwa mtawala. Kisha wakapanga yale ambayo wangefanya.
Yehoyada akamleta Yehoashi nje na kumtawaza, yaani, alimfanya kuwa mfalme. Alipofanya hivyo, watu “wakaanza kupiga makofi na kusema: ‘Mfalme na aishi!’” Wale walinzi wakamzunguka Yehoashi ili kumlinda. Athalia aliposikia kelele ya shangwe, alikimbia nje na kujaribu kuzuia jambo hilo. Lakini Yehoyada aliwaamuru wale walinzi wamuue Athalia.—2 Wafalme 11:1-16.
it-1-F uku. 776 fu. 8
Kuzika, na Mahali pa Kuzikia
Kuhani Mukubwa Yehoyada mwenye alikuwa kuhani muzuri alipewa heshima wakati alizikwa “katika Muji wa Daudi pamoja na wafalme,” ni yeye tu njo mutu mwenye hakukuwa mu kizazi ya kifalme mwenye anatajwa mu maandiko kuwa alipewa ile pendeleo.—2Ny 24:15, 16.
Mali ya Kiroho
it-2-F uku. 1231 fu. 10
Zekaria
12. Mwana wa Kuhani Mukubwa Yehoyada. Kisha kifo ya Yehoyada, Mufalme Yehoashi aliacha ibada ya kweli, na alisikiliza washauri wabaya kuliko kusikiliza manabii wa Yehova. Zekaria, mwenye alikuwa mutoto wa shangazi yake (2Ny 22:11), alitolea watu onyo kali juu ya ile jambo, lakini kuliko kutubu, watu walimupiga majiwe katika kiwanja ya hekalu. Wakati alikuwa anakufa, Zekaria alisema hivi: “Yehova aone jambo hili na akuombe utoe hesabu.” Ile ombi ya kiunabii ilijibiwa. Zaidi ya Siria kufanya uharibifu mukubwa katika Yuda, watumishi wawili wa Yehoashi walimuua “kwa sababu alikuwa amemwanga damu ya wana wa Yehoyada kuhani.” Tafsiri ya Septante ya Kigiriki na Vulgate ya Kilatini vinasema kama Yehoashi aliuawa kwa sababu alimwanga damu ya “mwana” wa Yehoyada. Lakini maandishi ya Wamasora na Peshitta ya Kisiriyaki, vinatumia neno “wana.” Inawezekana vinatumia neno ya uwingi ili kuonyesha kama Zekaria, mwana wa Yehoyada, mwenye alikuwa nabii na kuhani alikuwa mutu wa maana sana.—2Ny 24:17-22, 25.
Hotuba: Roho ya Yehova Itakusaidia Ukuwe Hodari
w10-SW 15/2 uku. 6-8 fu. 6-10
‘Sema Neno la Mungu kwa Ujasiri’
6 Njia ya moja kwa moja ya kupata roho takatifu ya Mungu ni kumwomba akupe roho hiyo. Yesu aliwaambia hivi watu waliomsikiliza: “Ikiwa ninyi, mjapokuwa waovu, mnajua jinsi ya kuwapa watoto wenu zawadi zilizo njema, je, Baba aliye mbinguni hatawapa hata zaidi roho takatifu wale wanaomwomba!” (Luka 11:13) Kwa kweli, tunapaswa kusali sikuzote ili tupate roho takatifu. Ikiwa tunaogopa kuhubiri barabarani, kwa njia isiyo rasmi, au katika maeneo ya kibiashara, tunaweza kumwomba Yehova atupatie roho yake ili itusaidie kupata ujasiri.—1 The. 5:17.
7 Hivyo ndivyo alivyofanya mwanamke Mkristo anayeitwa Rosa.a Siku moja Rosa alipokuwa kazini, mwalimu mwenzake alikuwa akisoma ripoti iliyoonyesha jinsi watoto walivyokuwa wakiteswa katika shule nyingine. Mwalimu huyo alifadhaishwa sana na mambo aliyosoma akasema hivi kwa sauti, “Ulimwengu unaelekea wapi?” Rosa hakupoteza nafasi hiyo ya kutoa ushahidi. Alifanya nini ili apate ujasiri wa kuanzisha mazungumzo? Rosa anasema hivi: “Nilisali kwa Yehova na kuomba roho yake inisaidie.” Alitoa ushahidi mzuri, kisha akapanga kumrudia mwalimu huyo. Mfikirie pia msichana mwenye umri wa miaka mitano anayeitwa Milane, ambaye anaishi New York City. Milane anasema hivi: “Kila siku kabla ya kwenda shuleni, mimi na mama yangu tunasali kwa Yehova.” Wanasali kuhusu nini? Wanasali ili Milane awe na ujasiri wa kusimama imara na kusema waziwazi kuhusu Mungu wake! Mama yake anasema: “Kufanya hivyo kumemsaidia Milane kueleza msimamo wake kuhusu sikukuu za kuzaliwa na sikukuu nyingine na pia kutoshiriki katika sherehe hizo.” Je, mifano hiyo haionyeshi kwamba sala inaweza kutusaidia kupata ujasiri?
8 Fikiria pia jambo lililomsaidia nabii Yeremia kupata ujasiri. Yehova alipomweka rasmi awe nabii kwa mataifa, Yeremia alisema hivi: “Tazama, mimi hakika sijui jinsi ya kusema, kwa sababu mimi ni mvulana tu.” (Yer. 1:4-6) Hata hivyo, baada ya muda, Yeremia alihubiri kwa bidii na kwa ujasiri sana hivi kwamba wengi walimwona kuwa mtangazaji wa msiba. (Yer. 38:4) Kwa miaka zaidi ya 65, alitangaza kwa ujasiri hukumu za Yehova. Alijulikana sana katika Israeli kwa sababu ya kuhubiri kwa ujasiri na bila woga hivi kwamba Yesu alipozungumza kwa ujasiri miaka 600 hivi baadaye, watu fulani waliamini kwamba Yesu ni Yeremia aliyefufuka. (Mt. 16:13, 14) Nabii Yeremia ambaye alisitasita mwanzoni alishinda jinsi gani woga aliokuwa nao? Anasema hivi: ‘Moyoni mwangu [neno la Mungu] likawa kama moto unaowaka ambao umefungiwa ndani ya mifupa yangu; nami nikachoka kujizuia.’ (Yer. 20:9) Ndiyo, neno la Yehova lilimtia nguvu Yeremia na kumchochea kusema.
9 Mtume Paulo aliandika hivi katika barua yake kwa Waebrania: “Neno la Mungu liko hai nalo lina nguvu na ni lenye makali zaidi kuliko upanga wowote wenye makali kuwili nalo huchoma hata kufikia kugawanya nafsi na roho, na viungo na urojorojo wake, nalo linaweza kutambua fikira na makusudio ya moyo.” (Ebr. 4:12) Ujumbe wa Mungu au neno lake linaweza kutuchochea jinsi lilivyomchochea Yeremia. Kumbuka kwamba ingawa wanadamu ndio waliotumiwa kuandika Biblia, si kitabu chenye hekima ya wanadamu, kwa kuwa kiliandikwa kwa mwongozo wa roho ya Mungu. Tunasoma hivi kwenye 2 Petro 1:21: “Unabii haukuletwa wakati wowote kwa mapenzi ya mwanadamu, bali wanadamu walisema yaliyotoka kwa Mungu kama walivyoongozwa na roho takatifu.” Tunapotenga wakati ili kujifunza Biblia kwa undani, akili zetu zinajaa ujumbe ulioongozwa na roho takatifu. (Soma 1 Wakorintho 2:10.) Ujumbe huo unaweza kuwa “kama moto unaowaka” ndani yetu, hivi kwamba hatutaweza kujizuia kuutangaza.
10 Ili tufaidike kabisa na funzo letu la Biblia, tunapaswa kujifunza na kuruhusu ujumbe wa Biblia upenye ndani kabisa ya moyo wetu na kubadili utu wetu wa ndani. Kwa mfano, nabii Ezekieli aliambiwa katika maono ale kitabu cha kukunjwa chenye ujumbe mkali ili awatangazie watu ambao hawakumsikiliza. Ezekieli alipaswa kuelewa kabisa ujumbe huo na kuishi kulingana nao. Ikiwa Ezekieli angefanya hivyo, kazi ya kutangaza ujumbe huo ingependeza na ingekuwa tamu kama asali.—Soma Ezekieli 2:8–3:4, 7-9.
TAREHE 22-28/5
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 MAMBO YA NYAKATI 25-27
“Yehova Anaweza Kukupatia Nyingi Zaidi Kuliko Hizo”
it-2-F uku. 1186 fu. 3
Yehoashi
Yehoashi alipatia mufalme wa Yuda maaskari elfu mia moja ili kupigana na Waedomu. Lakini, kisha kupata shauri ya “mutu fulani wa Mungu wa kweli” wale maaskari waliombwa warudie kwao hata kama walikuwa wamelipwa talanta 100 za feza ($660600). Walikasirika sana pengine juu hawangepata tena vitu vyenye kukamatwa ku vita vyenye waliwazia kama watapata. Kisha kurudia mu ufalme wa kaskazini, walianza kushambulia miji ya ufalme wa kusini, kutoka Samaria (pengine njo kwenye walitia kambi yao) mupaka Bet-horoni.—2Ny 25:6-10, 13.
Namna Gani Unaweza ‘Kuonja’ Wema wa Yehova?
16 Ukuwe tayari kuacha mambo fulani ili kufanya kazi ya Yehova. Hatulazimike kuacha kila kitu juu tu ya kumufurahisha Yehova. (Muh. 5:19, 20) Lakini, kama hatupende kufanya mengi zaidi mu kazi ya Yehova juu tu hatupende kuacha mambo fulani yenye tunapendaka, tunaweza kufanya kosa sawa ya mutu mwenye Yesu alizungumuzia mu mufano wake. Ule mutu alitumika sana juu apate vitu mingi vya muzuri bila kuhangaikia mambo ya Mungu. (Soma Luka 12:16-21.) Ndugu Christian, mwenye anaishi mu inchi ya Ufaransa, anasema hivi: “Sikukuwa namupatia Yehova nguvu na wakati wangu. Ilikuwa pia vile kwa familia yangu.” Yeye na bibi yake waliamua kufanya kazi ya upainia. Lakini juu wafikie ile muradi, walipaswa kuacha kazi zao. Ili kupata makuta kidogo ya kuwasaidia kuishi, walianza kufanya kazi ya kusafisha nyumba ao biro, na walijifunza namna ya kutosheka na kidogo yenye walikuwa wanapata. Kufanya vile, kuliwaletea baraka gani? Christian anasema hivi: “Sasa tunafurahia kazi ya mahubiri na kuona vile mafunzo yetu ya Biblia na pia marudio yetu wako wanajifunza juu ya Yehova.”
Mali ya Kiroho
w07-SW 15/12 uku. 10 fu. 1-2
Je, Una Mshauri wa Mambo ya Kiroho?
AKIWA na umri wa miaka 16 tu, Uzia aliwekwa kuwa mfalme wa ufalme wa kusini wa Yuda. Alitawala kwa miaka zaidi ya 50, kuanzia mwishoni mwa karne ya tisa mpaka mwanzoni mwa karne ya nane K.W.K. Tangu akiwa na umri mdogo, Uzia ‘aliendelea kufanya yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova.’ Ni nini kilichomchochea kuishi maisha ya uadilifu? Masimulizi ya historia yanasema hivi: “[Uzia] akaendelea kuwa na mwelekeo wa kumtafuta Mungu katika siku za Zekaria, aliyekuwa akiwafundisha watu kumwogopa Mungu wa kweli; na katika zile siku alizokuwa akimtafuta Yehova, Mungu wa kweli alimfanikisha.”—2 Mambo ya Nyakati 26:1, 4, 5.
Mbali na masimulizi hayo ya Biblia, hatuna habari zaidi kumhusu Zekaria, aliyekuwa mshauri wa mfalme Uzia. Hata hivyo, ingawa ‘alikuwa akiwafundisha watu kumwogopa Mungu wa kweli,’ Zekaria alikuwa na uvutano mzuri juu ya mtawala huyo kijana na alimchochea kufanya yaliyo sawa. Kitabu kimoja (The Expositor’s Bible) kinasema kwamba bila shaka Zekaria “alikuwa mtu aliyejua mafundisho ya kiroho, mwenye uzoefu mkubwa sana wa kiroho, na aliyeweza kuwapa wengine ujuzi aliokuwa nao.” Msomi mmoja wa Biblia alikata kauli hii kumhusu Zekaria: “Alijua sana unabii, naye . . . alikuwa mtu mwenye akili, mtu mwema aliyejitoa kwa Mungu; na inaonekana kwamba alimchochea sana Uzia.”
TAREHE 29/5–4/6
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 MAMBO YA NYAKATI 28-29
“Unaweza Kumutumikia Yehova Hata Kama Wazazi Wako Hawakuwekee Mufano Muzuri”
Uige Marafiki wa Sana wa Yehova
8 Namna Hezekia alikomaa ilikuwa tofauti sana na namna Ruthu alikomaa. Hezekia alikuwa katika taifa lenye kutolewa kwa Mungu. Lakini Waisraeli wote hawakuendelea kuwa waaminifu. Mufalme Ahazi, baba ya Hezekia, alikuwa mubaya. Alizarau hekalu la Mungu na kuchochea watu waabudu miungu mingine. Ahazi alifikia hata kutoa ndugu fulani za Hezekia ili wachomwe wangali wazima kwa ajili ya mungu wa uongo. Wakati Hezekia alikuwa mutoto, maisha yake ilikuwa katika hatari!—2 Wafalme 16:2-4, 10-17; 2 Mambo ya Nyakati 28:1-3
Uige Marafiki wa Sana wa Yehova
9 Mufano mubaya wa Ahazi ungeweza kumuchochea Hezekia amukasirikie Yehova. Leo, watu fulani wenye wamepata magumu madogo sana kuliko ya Hezekia, wanawaza kwamba wako na haki ya kumukasirikia Yehova ao tengenezo lake. (Methali 19:3) Wengine wanawaza kwamba hali mubaya ya familia yao inaweza kuwafanya wakuwe na maisha mabaya ao wafanye pia makosa kama wazazi wao. (Ezekieli 18:2, 3) Lakini, mawazo hayo ni ya kweli?
10 Maisha ya Hezekia yanaonyesha kwamba jibu la ulizo hilo ni hapana! Hakuna hata jambo moja lenye linaweza kutufanya tumukasirikie Yehova. Haletee watu mateso. (Ayubu 34:10) Ni kweli kwamba wazazi wanaweza kufundisha watoto wao kufanya mambo mazuri ao mabaya. (Methali 22:6; Wakolosai 3:21) Lakini hilo halimaanishe kwamba namna tulikomaa katika familia yetu itaonyesha ikiwa tutakuwa watu wa namna gani. Sababu gani? Kwa sababu Yehova ametupatia zawadi ya uhuru wa kuchagua, ni kusema, uwezo wa kuchagua kati ya mema na mabaya. (Kumbukumbu la Torati 30:19) Namna gani Hezekia alitumia zawadi hiyo ya maana sana?
11 Baba ya Hezekia alikuwa kati ya wafalme wabaya zaidi wa Yuda; lakini Hezekia alikuwa kati ya wafalme wazuri zaidi. (Soma 2 Wafalme 18:5, 6.) Alikataa kufuata mufano mubaya wa baba yake. Lakini, alichagua kusikiliza kwa uangalifu manabii wa Yehova kama vile Isaya, Mika, na Hosea. Alitii kabisa mashauri na maonyo yenye walimutolea. Hilo lilimuchochea atengeneze mambo mengi yenye baba yake aliharibisha. Alisafisha hekalu, alimuomba Mungu asamehe zambi za watu, na alivunja-vunja sanamu katika inchi yote. (2 Mambo ya Nyakati 29:1-11, 18-24; 31:1) Kisha, wakati Senakeribu, mufalme wa Asiria alitafuta kushambulia Yerusalemu, Hezekia alionyesha imani na hakuogopa hata kidogo. Alitegemea ulinzi wa Yehova na kutia nguvu watu wake. (2 Mambo ya Nyakati 32:7, 8) Wakati fulani Hezekia alikuwa na kiburi, lakini kisha Yehova kumushauria, alijinyenyekeza. (2 Mambo ya Nyakati 32:24-26) Ni wazi kwamba, Hezekia ni mufano muzuri zaidi wenye tunapaswa kuiga. Hakuacha hali ya familia yake iharibishe maisha yake. Lakini alionyesha kwamba alikuwa rafiki ya Yehova.
Mali ya Kiroho
Nathani—Alitetea Ibada Safi kwa Uaminifu
Kwa kuwa Nathani alikuwa mwabudu mwaminifu wa Yehova, alikubali kwa shauku mupango huo wa Daudi wa kujenga mara ya kwanza duniani mahali pa ibada safi penye kudumu. Kwenye pindi hiyo, inaelekea kwamba Nathani alitoa maoni yake mwenyewe kuliko kutoa maoni ya Yehova. Usiku huo, Mungu alimuagiza nabii wake amupelekee mufalme ujumbe tofauti: Daudi hangestahili kujenga hekalu la Yehova. Mutu atakayelijenga atakuwa mumoja wa wana wa Daudi. Nathani alimutangazia Daudi kwamba Mungu alikuwa akifanya agano pamoja naye, kwamba kiti chake cha ufalme kitafanywa ‘imara mupaka wakati usio na kipimo.’—2 Sam. 7:4-16.
Mawazo ya Nathani kuhusu kujenga hekalu hayakupatana na mapenzi ya Mungu. Hata hivyo, bila kunungunika, nabii huyo munyenyekevu alikubali na kuunga mukono kusudi la Yehova. Ni mufano muzuri wa kuiga kabisa ikiwa Mungu anaturekebisha katika njia fulani! Mambo ambayo nabii Nathani alifanya baadaye yanaonyesha kwamba aliendelea kukubaliwa na Mungu. Kwa kweli, inaonekana kwamba Yehova alimupatia Nathani nabii na pia Gadi mwonaji wa mufalme, roho yake, ili wamushauri Daudi kuweka wanamuziki 4 000 katika hekalu.—1 Nya. 23:1-5; 2 Nya. 29:25.
TAREHE 5-11/6
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 MAMBO YA NYAKATI 30-31
“Kukusanyika Pamoya Kunatuletea Faida”
it-1-F uku. 1132 fu. 4
Hezekia
Bidii Yake kwa Ajili ya Ibada ya Kweli. Hezekia alionyesha bidii yake kwa ajili ya ibada ya Yehova kisha tu kuwekwa kuwa mufalme wakati alikuwa na miaka 25. Jambo ya kwanza yenye alifanya ilikuwa kufungua tena hekalu na kuitengeneza. Kisha, akakusanya makuhani na walawi na akawaambia hivi: “Ni tamaa ya moyo wangu kufanya agano pamoja na Yehova Mungu wa Israeli.” Ile ilikuwa agano ya ushikamanifu kwa sababu agano ya sheria ilikuwa ingali natumika, lakini ilizarauliwa. Kwa hiyo, ni sawa vile walifanya upya agano ya sheria mu Yuda. Kwa bidii alipanga walawi mu kazi zao mbalimbali, akarudisha tena mupango wa viombo vya muziki na nyimbo za sifa. Ilikuwa Nisani, mwezi wenye Pasaka ilipaswa kusherehekewa. Lakini hekalu, makuhani, na walawi hawakukuwa safi. Kufikia siku ya 16, mwezi wa Nisani, hekalu ilikuwa imetakaswa na vyombo vyake vilikuwa vimerudishwa. Kwa hiyo, iliomba kufanya toleo ya pekee ya kufunika zambi kwa ajili ya Waisraeli wote. Kwanza, wakubwa wa muji walileta zabihu, matoleo ya zambi kwa ajili ya ufalme, kwa ajili ya patakatifu, na kwa ajili ya watu, kisha watu wakatoa maelfu ya matoleo ya kuteketezwa.—2Ny 29:1-36.
it-1-F uku. 1132 fu. 5
Hezekia
Kwa sababu watu hawakukuwa safi haikuwezekana washerehekee Pasaka wakati wenye ilikuwa inafanywa kwa ukawaida. Hezekia alitumia sheria yenye iliruhusu wale wenye hawakukuwa safi washerehekee Pasaka kisha mwezi moja. Hezekia hakualika tu watu wenye walikuwa mu eneo ya Yuda, lakini alialika pia watu wenye walikuwa mu eneo ya Israeli. Aliwaalika kupitia barua zenye alituma kupitia wakimbiaji kutoka Beer-sheba mupaka Dani. Watu wengi walichekelea wale wakimbiaji; hata vile watu fulani kutoka Asheri, Manase, na Zabuloni walijinyenyekeza na kuja, na watu fulani kutoka Efraimu na Isakari walikuja pia. Zaidi yao, kulikuwa pia watu wenye hawakukuwa Waisraeli wenye walikuwa wanaabudu Yehova. Haikukuwa mwepesi kwa waabudu wa kweli wenye walikuwa mu ufalme wa kaskazini kuja ku ile Pasaka. Wao pia, sawa vile wale wajumbe, wangepambana na upinzani na kuchekelewa kwa sababu ufalme wa makabila kumi ulikuwa mu hali ya mubaya sana, ulikuwa umezama mu ibada ya uongo, na watu walikuwa wanaishi mu woga wa kushambuliwa na Waashuru.—2Ny 30:1-20; Hes 9:10-13.
it-1-F uku. 1132 fu. 6, 7
Hezekia
Kisha Pasaka, walifanya Sikukuu ya Mikate Yenye Haina Chachu kwa siku saba. Ilifurahisha sana na wakaamua kuongeza siku zingine saba. Hata kama walikuwa mu kipindi ya nguvu, baraka ya Yehova ilikuwa mingi hivi kwamba “kulikuwa furaha kubwa katika Yerusalemu, kwa maana tangu siku za Sulemani mwana wa Daudi mufalme wa Israeli, jambo kama hilo halikukuwa limetendeka katika Yerusalemu.”—2Ny 30:21-27.
Ilikuwa kabisa kurudishwa kwa ibada ya kweli, haikukuwa tu furaha ya muda kidogo yenye watu wangekuwa nayo yenye haingeendelea; mambo yenye ilifuata ilionyesha vile. Mbele warudie kwao, watu wenye walikuwa ku ile sikukuu waliharibu nguzo takatifu, walibomoa mahali pa juu na mazabahu, na kukata miti mitakatifu katika Yuda na Benyamini na hata katika Efraimu na Manase. (2Ny 31:1) Hezekia aliwawekea mufano muzuri kwa kuponda ile nyoka ya shaba yenye Musa alikuwa ametengeneza, kwa sababu watu walikuwa wameifanya kuwa sanamu na walikuwa wanatoa zabihu za kuteketezwa juu yake. (2Fa 18:4) Kisha ile sikukuu kubwa, Hezekia alihakikisha kama ibada ya kweli itaendelea kwa kupanga vikundi vya makuhani na kufanya mipango ili kazi yenye kufanywa ku hekalu iendelee kutegemezwa. Alitia watu moyo waheshimie sheria kwa kutoa sehemu moya ya kumi na toleo ya matunda ya kwanza kwa ajili ya walawi na makuhani, na watu walikubali kwa moyo wote.—2Ny 31:2-12.
Mali ya Kiroho
“Kama Munajua Mambo Haya, Ninyi Ni Wenye Furaha Ikiwa Munayatenda”
14 Njia ingine ya kuonyesha kama tuko wanyenyekevu ni kuwa wasikilizaji wazuri. Andiko la Yakobo 1:19 linatuambia tukuwe ‘wepesi wa kusikiliza.’ Yehova ni musikilizaji muzuri zaidi. (Mwa. 18:32; Yos. 10:14) Kwa mufano, soma mazungumuzo yenye kupatikana katika Kutoka 32:11-14. (Soma.) Hata kama Yehova hakukuwa na lazima ya mawazo ya Musa, alimuruhusu Musa aeleze namna alikuwa anajisikia. Je, unaweza kumusikiliza kwa uvumilivu mutu fulani mwenye alifanya makosa zamani na kisha ufuate pendekezo lake? Lakini, Yehova anasikilizaka kwa uvumilivu wanadamu wote wenye kusali kwa imani.
15 Ujiulize hivi: ‘Kama Yehova alionyesha unyenyekevu sana mupaka akasikiliza watu kama vile alimusikiliza Abrahamu, Raheli, Musa, Yoshua, Manoa, Eliya, na Hezekia, mimi pia sipaswe kufanya vile? Ninaweza kuonyesha ndugu na dada zangu wote heshima zaidi kwa kuwasikiliza na kufuata mapendekezo yao kama inawezekana? Kuko mutu fulani mu kutaniko letu ao mu familia yetu mwenye ninapaswa kuhangaikia zaidi? Nitafanya nini juu ya jambo hilo?’—Mwa. 30:6; Amu. 13:9; 1 Fa. 17:22; 2 Ny. 30:20.
Hotuba: Umusifu Yehova kwa Kutoa Majibu ku Mikutano
Umusifu Yehova Katika Kutaniko
13 Ni mashauri gani yenye kufaa yenye inaweza kukusaidia kutoa majibu yenye kutia moyo ku mikutano? Tuzungumuzie basi mashauri fulani.
14 Utayarishe kila mukutano. Wakati unafanya mipango mbele ya wakati na kutayarisha muzuri, hautaogopa kutoa majibu. (Mez. 21:5) Kwa kweli, kila mutu iko na programu yake ya kutayarisha mikutano. Eloise, dada mujane mwenye kuwa na miaka zaidi ya 80, anaanza kutayarisha funzo la Munara wa Mulinzi ku mwanzo-mwanzo wa juma. Anasema hivi: “Ninafurahia mikutano zaidi kama ninajifunza mbele ya wakati.” Joy, dada mwenye kufanya kazi ya kimwili yenye kumukamata wakati wote, anapanga wakati Siku ya Posho ili kujifunza Munara wa Mulinzi. Anasema hivi: “Ni mwepesi kukumbuka kama ninajifunza muda mufupi mbele ya mikutano.” Ike, muzee wa kutaniko mwenye kuwa na mambo mingi ya kufanya na mwenye kuwa pia painia, anasema hivi: “Ninaona kama ni muzuri zaidi kwangu kujifunza kwa vipindi vifupi-vifupi vya wakati katika juma lote kuliko kujifunza siku moja kwa wakati murefu.”
15 Unaweza kufanya nini ili kutayarisha muzuri mikutano? Kila wakati mbele ya kuanza kujifunza, umuombe Yehova akupatie roho takatifu. (Lu. 11:13; 1 Yo. 5:14) Kisha, tumia dakika fulani ili kuchunguza habari yote: chunguza kichwa cha habari, vichwa vidogo-vidogo, picha, na visanduku. Sasa wakati uko unajifunza kila fungu, ujikaze kusoma maandiko mengi kati ya maandiko yenye kutajwa. Ufikiri sana juu ya habari yenye unajifunza, na ukazie zaidi mahali kwenye unapenda kutoa majibu. Wakati unatayarisha muzuri, utapata faida zaidi na hautaona kuwa ni nguvu kutoa majibu.—2 Ko. 9:6.
16 Kama inawezekana, tumia programu na site zetu za Enternete zenye kuwa mu luga yenye unajua. Kupitia tengenezo lake, Yehova ametupatia programu na site za Enternete ili kutusaidia kutayarisha mikutano. Programu JW Library® inatusaidia kuchukua vichapo vya kujifunza katika vyombo vyetu vya kielektroniki kama vile tablete, ao telefone. Kisha tunaweza kujifunza ao hata kusoma ao kusikiliza habari fulani kila wakati na kila mahali. Watu fulani wanatumia programu hiyo ili kujifunza wakati wa mapumuziko ku kazi ao ku masomo, ao wakati wako wanasafiri. Watchtower Library na Watchtower MAKTABA KWENYE ENTERNETE, vinafanya ikuwe mwepesi sana kutafuta mawazo makubwa mu habari yenye tunapenda kujifunza kwa uangalifu zaidi.
17 Kama inawezekana, tayarisha majibu mbalimbali kwa ajili ya kila habari ya kujifunza. Juu ya nini? Juu pengine hautatajwa kila mara wakati unatia mukono juu. Inawezekana wengine watatia mukono juu wakati huohuo, na kiongozi anaweza kuchagua mumoja kati yao. Ili mikutano imalizike kwa wakati, kiongozi anaweza kuomba watu kidogo watoe majibu juu ya wazo fulani. Kwa hiyo, usikwazike ao kuvunjika moyo kama hakutaje ku mwanzo-mwanzo wa funzo. Kama unatayarisha majibu mbalimbali, utakuwa na nafasi za mingi zaidi za kutoa majibu. Kusoma andiko ni kati ya majibu yenye unaweza kutayarisha. Lakini, kama inawezekana, ujitayarishe ili kutoa majibu mu maneno yako mwenyewe.
18 Utoe majibu ya mafupi. Mara mingi, majibu ya mufupi na ya mwepesi njo yenye inatiaka moyo zaidi. Kwa hiyo, ukuwe na muradi wa kutoa majibu ya mufupi. Ujikaze kutoa majibu kwa segonde 30 hivi. (Mez. 10:19; 15:23) Kama umetoa majibu ku mikutano kwa miaka mingi, uko na daraka la maana, ni kusema, unapaswa kuonyesha mufano muzuri kwa kutoa majibu ya mufupi. Kama unazungumuzia mambo mingi yenye kufanya dakika fulani, wengine wanaweza kuogopa, na kufikiri kama hawawezi kufikia uwezo wako wa kujibu. Tena, kutoa majibu ya mufupi kunaruhusu watu wengi zaidi watoe majibu wakati wa mikutano. Zaidi sana, kama wewe njo unapewa nafasi ya kutoa jibu la kwanza, utoe jibu la mwepesi, na lenye kujibu ulizo moja kwa moja. Usijaribu kuzungumuzia mawazo yote ya fungu. Kisha wazo kubwa la fungu kuzungumuziwa, unaweza kutoa maelezo juu ya mawazo ingine.—Ona kisanduku “Ninaweza Kutoa Majibu Juu ya Mambo Gani?”
TAREHE 12-18/6
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 MAMBO YA NYAKATI 32-33
“Utie Wengine Nguvu Wakati wa Magumu”
it-1-F uku. 212 fu. 6
Ashuru
Senakeribu. Senakeribu, mwana wa Sargoni wa Pili, alishambulia ufalme wa Yuda mu mwaka wa 14 wa utawala wa Hezekia (732 M.K.Y.). (2Fa 18:13; Isa 36:1) Hezekia aliasi Waashuru na alivunja mapatano yenye baba yake Ahazi alifanya pamoja nao. (2Fa 18:7) Kwa hiyo Senakeribu alishambulia Yuda, na inasemekana kama alikamata miji 46 (linganisha na Isa 36:1, 2), na kisha, wakati alikuwa mu kambi yake ya Lakishi, alimuomba Hezekia amulipe ushuru wa talanta 30 za zaabu (karibu $11560000) na talanta 300 za feza (karibu $1982000). (2Fa 18:14-16; 2Ny 32:1; linganisha na Isa 8:5-8.) Hata kama ile ushuru ililipwa, Senakeribu alituma musemaji wake ili kuomba wamuache akamate Yerusalemu bila kupigana. (2Fa 18:17–19:34; 2Ny 32:2-20) Ile ilifanya Yehova aharibu maaskari wa Senakeribu 185000 mu usiku moja na akamulazimisha ule Muashuru mwenye kiburi arudie Ninawi. (2Fa 19:35, 36) Kule, kisha wakati fulani wana wake wawili walimuua na mwana wake mwingine, Esar-hadoni akakuwa mufalme pa nafasi yake. (2Fa 19:37; 2Ny 32:21, 22; Isa 37:36-38) Hii matukio yote, kutosha tu habari kuhusu kuuawa kwa maaskari Waashuru, inaandikwa pia ku chombo ya udongo kwenye kunaandikwa historia ya Senakeribu na ku chombo ya udongo kwenye kunaandikwa historia ya Esar-hadoni.—PICHA, Buk. 1, uku. 957.
Ni Nani Walio Wachungaji Saba na Watawala Wadogo Wanane Leo?
12 Sikuzote Yehova iko tayari kutusaidia kutatua matatizo ambayo hatuwezi kutatua, lakini anapenda sisi pia tujikaze. Hezekia alizungumuza na “wakuu wake na wanaume wake wenye nguvu,” na wote pamoja wakaamua ‘kuziba maji ya mabubujiko yaliyokuwa inje ya jiji . . . Tena [Hezekia] akajipa moyo na kujenga ukuta wote uliovunjika na kusimamisha minara juu yake, na upande wa inje ukuta mwingine, . . . na kutengeneza silaha kwa wingi na ngao.’ (2 Nya. 32:3-5) Ili kulinda na kuchunga watu wake wakati huo, Yehova alitumia wanaume fulani wenye nguvu, kama vile, Hezekia, wakuu wake, na manabii waliokuwa nguvu kiroho.
Ni Nani Walio Wachungaji Saba na Watawala Wadogo Wanane Leo?
13 Jambo ambalo Hezekia alifanya baadaye lilikuwa la maana sana kuliko hata kuzuia maji ao kujenga vizuri kuta. Kwa kuwa alikuwa muchungaji mwenye kuhangaikia watu, Hezekia alikusanya watu na kuwatia moyo kupitia maneno haya: ‘Musiogope wala musiwe na hofu kwa sababu ya mufalme wa Ashuru . . . , kwa maana kuna wengi walio pamoja nasi kuliko wale walio pamoja naye. Yeye, mukono wa nyama uko pamoja naye, lakini sisi, Yehova Mungu wetu yuko pamoja nasi ili kutusaidia na kupigana vita vyetu.’ Hilo lilitia imani yao nguvu kabisa. Yehova alikuwa tayari kuwapigania watu wake! Wayahudi waliposikia maneno hayo ‘walianza kujitegemeza juu ya maneno ya Hezekia mufalme wa Yuda.’ Ona kwamba ni “maneno ya Hezekia” ndio yaliyotia watu moyo. Yeye na wakuu wake na wanaume wake wenye nguvu, na vilevile manabii Mika na Isaya, walikuwa wachungaji wazuri, kama vile Yehova alivyotabiri kupitia nabii wake.—2 Nya. 32:7, 8; soma Mika 5:5, 6.
Mali ya Kiroho
Kutubu Kikweli Maana Yake Nini?
11 Kisha, Yehova alijibia sala za Manase. Aliona namna ule mwanaume alibadilisha moyo wake, sawa vile sala zake zilionyesha. Njo maana Yehova alisikiliza Manase wakati alimuomba amusamehe na alimuruhusu akuwe tena Mufalme. Manase alifanya yake yote ili kuonyesha kabisa kama alitubu kikweli. Alifanya jambo yenye Ahabu hakufanyaka. Alibadilisha tabia yake. Alipinga ibada ya uongo na akachochea ibada ya kweli. (Soma 2 Mambo ya Nyakati 33:15, 16.) Manase alikuwa kabisa na lazima ya uhodari na imani ili kufanya vile, juu mbele atubu, alikuwa mufano mubaya kwa familia yake, kwa watu wake wenye vyeo, na kwa watu wengi kwa miaka mingi. Wakati Manase alikuwa muzee, alijikaza kutosha mambo fulani ya mubaya yenye alikuwa amefanya. Pengine, alikuwa mufano muzuri kwa mujukuu wake Yosia, mwenye alifikia kuwa Mufalme muzuri sana.—2 Fa. 22:1, 2.
12 Mufano wa Manase unaweza kutufundisha nini? Alijinyenyekeza, na alifanya hata zaidi. Alisali, na kumuomba Yehova amuhurumie. Na alibadilisha tabia yake. Alijikaza sana ili kurekebisha mambo yote ya mubaya yenye alikuwa amefanya. Alifanya yake yote ili kumuabudu Yehova na alisaidia wengine wafanye vile. Mufano wa Manase, unapatia hata wale wenye walifanya zambi nzito, tumaini. Mambo yenye ilimupata Manase, inaonyesha kama Yehova Mungu ni ‘mwema na iko tayari kusamehe.’ (Zb. 86:5) Yehova anasamehe wale wenye wanatubu kikweli.
TAREHE 19-25/6
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 MAMBO YA NYAKATI 34-36
“Uko Nafaidika Kabisa na Neno ya Mungu?”
it-1-F uku. 1152 fu. 6
Hulda
Wakati Yosia alisikia usomaji wa “kitabu cha sheria” chenye kuhani mukubwa alipata wakati walikuwa wanatengeneza hekalu, alituma kikundi ya watu wamuulize Yehova. Walienda kwa Hulda, na Hulda alirudilia maneno ya Yehova na kusema kama mambo yote ya mubaya yenye inaandikwa mu ile “kitabu” kwa ajili ya wale wenye hawatii itapata ile taifa ya waasi. Hulda alisema pia kama, kwa sababu Yosia alijinyenyekeza mbele ya Yehova, hatajionea ile musiba lakini atakusanywa pamoja na mababu zake na atalalishwa katika kaburi lake kwa amani.—2Fa 22:8-20; 2Ny 34:14-28.
w09-SW 15/6 uku. 10 fu. 20
Uwe na Bidii kwa Ajili ya Nyumba ya Yehova!
20 Wakati wa kazi ya kurudisha ibada safi ambayo Mfalme Yosia alianzisha, Kuhani Mkuu Hilkia ‘alikipata kile kitabu cha sheria ya Yehova kupitia mkono wa Musa.’ Hilkia alimpa Shafani, mwandishi wa mfalme kitabu hicho, naye Shafani akaanza kumsomea Yosia ujumbe wa kitabu hicho. (Soma 2 Mambo ya Nyakati 34:14-18.) Kulikuwa na matokeo gani? Papo hapo mfalme alirarua mavazi yake kwa huzuni naye akawaamuru watu wamtafute Yehova. Kupitia nabii wa kike Hulda, Mungu alitoa ujumbe ambao ulishutumu mazoea fulani ya kidini yaliyokuwa yakifanywa huko Yuda. Hata hivyo, jitihada nzuri za Yosia za kuondoa ibada ya sanamu zilionekana wazi, naye aliendelea kuwa na kibali cha Yehova ingawa ilitabiriwa kwamba misiba ingepata taifa hilo. (2 Nya. 34:19-28) Tunaweza kujifunza nini kutokana na hilo? Bila shaka, tamaa yetu ni kama ile ya Yosia. Tunataka kufuata haraka mwongozo wa Yehova na kuchukua kwa uzito onyo kuhusu hatari ya kuruhusu uasi-imani na ukosefu wa uaminifu uchafue ibada yetu. Na tunaweza kuwa na hakika kwamba Yehova ataona na kuthamini bidii yetu kwa ajili ya ibada safi, kama tu alivyofanya katika kisa cha Yosia.
Mali ya Kiroho
Utatia Moyo Wako Katika Mambo Yenye Kuandikwa?
15 Mwishowe, mufano wa Yosia unaweza kutufundisha nini? Hata kama Yosia alikuwa mufalme muzuri, alifanya kosa lenye lilimuletea kifo. (Soma 2 Mambo ya Nyakati 35:20-22.) Ni nini ilitokea? Yosia alianza kupigana vita na Neko, mufalme wa Misri, hata kama hakukuwa na sababu ya kufanya hivyo. Kwa kweli, Neko mwenyewe alimuambia Yosia kama hakupenda kupigana vita naye. Biblia inasema kama maneno ya Neko ‘yalitoka kinywani mwa Mungu.’ Lakini Yosia alienda kupigana vita na akauawa. Sasa, sababu gani alipigana vita na Neko? Biblia haiseme.
16 Yosia alipaswa kutafuta kujua ikiwa mambo yenye Neko alikuwa amesema yalitoka kabisa kwa Yehova. Namna gani? Alipaswa kumuuliza Yeremia, nabii moja kati ya manabii wa Yehova. (2 Mambo ya Nyakati 35:23, 25) Pia, Yosia alipaswa kuchunguza mambo muzuri. Neko alikuwa anaenda Karkemishi ili kupigana vita na taifa lingine, hapana Yerusalemu. Na Neko hakujaribu kumutukana Yehova ao watu wake. Yosia hakufikiria kwa uangalifu mambo hayo mbele akamate uamuzi wake. Hilo linatufundisha jambo gani? Wakati tuko na magumu na tunapaswa kukamata uamuzi fulani, tunapaswa kwanza kufikiria mambo yenye Yehova anaweza kupenda tufanye.
17 Wakati tunapaswa kukamata uamuzi fulani, ni lazima tufikirie kwanza kanuni za Biblia zenye zinaweza kutusaidia na namna tunaweza kuzitumia. Katika hali fulani, tunaweza kupenda kutafuta habari zaidi katika vichapo vyetu ao hata kuomba muzee fulani mashauri. Anaweza kutusaidia kufikiri juu ya kanuni zingine za Biblia. Fikiria hali hii: Dada mumoja anaolewa na mutu mwenye haiko Shahidi. Anapanga siku fulani ili kuenda katika mahubiri. (Matendo 4:20) Lakini, siku hiyo bwana yake hapendi aende katika mahubiri. Anamuambia kama kumepita siku fulani hawapitishe wakati mwingi pamoja na kwamba anapenda waende pamoja nafasi fulani. Kwa hiyo, dada huyo anafikiria maandiko ya Biblia yenye yanaweza kumusaidia akamate uamuzi wenye hekima. Anajua kama anapaswa kumutii Mungu na kama Yesu alituamuru kufanya wanafunzi. (Mathayo 28:19, 20; Matendo 5:29) Lakini anakumbuka pia kama bibi anapaswa kujitiisha kwa bwana yake na kama watumishi wa Mungu wanapaswa kuwa na usawaziko. (Waefeso 5:22-24; Wafilipi 4:5) Bwana yake anajaribu kumukataza kuenda katika mahubiri, ao anapenda tu apitishe wakati pamoja naye siku hiyo? Kwa sababu sisi ni watumishi wa Yehova, tunapenda kukamata maamuzi yenye kuwa na usawaziko na yenye kumupendeza.
Hotuba: Utumie Nguvu ya Neno ya Mungu mu Mahubiri
‘Neno la Mungu . . . Liko na Nguvu’
7 Ni nini inaweza kutusaidia tutumie muzuri Neno la Mungu katika kazi yetu ya kuhubiri? Hatua ya kwanza ni kulitumia mara kwa mara wakati tunahubiri na kufundisha. Ndugu mumoja alisema hivi juu ya jambo hilo: “Ikiwa ungehubiri nyumba kwa nyumba pamoja na Yehova, ungezungumuza wewe mwenyewe ao ungemuacha azungumuze?” Alipenda kusema kuwa: Wakati tunasoma moja kwa moja Neno la Mungu katika kazi ya kuhubiri, tunamuacha Yehova azungumuze na mwenye nyumba. Andiko lenye kuchaguliwa muzuri, linaweza kuwa na nguvu zaidi kuliko jambo lolote lenye tunaweza kusema. (1 Tes. 2:13) Ujiulize hivi: ‘Ninajikaza kabisa kutumia kila nafasi yenye kujitokeza ili kusomea Neno la Mungu watu wenye ninahubiria habari njema?’
8 Kwa kweli, zaidi ya kusomea tu Biblia wale wenye tunazungumuza nao, tunapaswa kufanya mambo mengine. Sababu gani? Kwa sababu wengi hawajue mambo mengi ao hawajue kitu juu ya Biblia. Ilikuwa hivyo wakati wa mitume, na ni hivyo leo pia. (Rom. 10:2) Kwa hiyo, hatupaswe kufikiri kuwa mutu ataelewa wazo kubwa la andiko kwa sababu tu tunalisoma. Tunapaswa kukazia sehemu fulani za andiko, pengine kwa kurudilia maneno yenye kukazia wazo kubwa, na kufasiria maana ya maneno hayo. Ikiwa tunafanya hivyo, hilo linaweza kufanya ujumbe wa Neno la Mungu uguse akili na mioyo ya wasikilizaji wetu.—Soma Luka 24:32.
9 Ni muzuri pia kutanguliza maandiko katika njia yenye kufanya watu waheshimie Biblia. Kwa mufano, tunaweza kusema hivi: “Tuone Muumbaji wetu anasema nini juu ya habari hii.” Wakati tunazungumuza na mutu mwenye hajue mafundisho ya Kikristo, tunaweza kusema hivi: “Ona mambo yenye Maandishi Matakatifu yanasema.” Ao ikiwa tunahubiria mutu fulani mwenye hapendezwe na mambo ya dini, tunaweza kumuuliza hivi: “Umekwisha kusikia mezali hii ya zamani?” Kwa kweli, tunapaswa kufikiria hali ya kila mutu na kupatanisha utangulizi wetu na hali yake.—1 Kor. 9:22, 23.
10 Wengi wametambua kuwa kutumia Neno la Mungu katika kazi ya kuhubiri kunaweza kugusa sana moyo watu wenye wanahubiria. Fikiria mufano huu. Ndugu mumoja alirudilia mwanaume mumoja mwenye kuzeeka mwenye alikuwa amesoma magazeti yetu kwa miaka mingi. Kuliko kumutolea tu gazeti la Munara wa Mulinzi la hivi karibuni, ndugu huyo aliamua kusoma andiko fulani lenye lilikuwa katika gazeti hilo. Alisoma 2 Wakorintho 1:3, 4, lenye kusema hivi: ‘Baba ya rehema nyororo na Mungu wa faraja yote . . . anatufariji katika ziki yetu yote.’ Maneno hayo yaligusa sana moyo wa mwenye nyumba huyo na akaambia ndugu asome tena andiko hilo mara ya pili. Mwanaume huyo alieleza namna yeye na bibi yake walikuwa na lazima ya faraja, na sasa anapendezwa na ujumbe wa Biblia. Kwa kweli, Neno la Mungu liko na nguvu katika kazi yetu ya kuhubiri.—Mdo. 19:20.
TAREHE 26/6–2/7
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | EZRA 1-3
“Acha Yehova Akutumikishe”
Unaona Mambo Yenye Zekaria Aliona?
WAYAHUDI walikuwa na furaha sana. Yehova Mungu “alichochea roho ya Mufalme Koreshi wa Uajemi” juu aachilie Waisraeli wenye walikuwa walishapitisha miaka mingi mu Babiloni mu utumwa. Mufalme alitoa tangazo juu Wayahudi warudie kwao “na kujenga upya nyumba ya Yehova Mungu wa Israeli.” (Ezr. 1:1, 3) Ile ilikuwa amri ya kufurahisha sana! Ilimaanisha kama Wayahudi wangeweza tena kuabudu Mungu wa kweli mu inchi yenye alikuwa amewapatia.
Taji na Magari ya Kukokotwa Vinawalinda
2 Zekaria alijua kuwa wanaume na wanawake wenye walirudia Yerusalemu walikuwa wenye imani. Ni wao ndio ‘Mungu wa kweli aliiamusha roho’ yao ili waache maisha yao ya muzuri na biashara yao. (Ezra 1:2, 3, 5) Waliacha inchi yenye walikuwa wanajua ili wahamie katika inchi yenye wengi kati yao walikuwa hawajaona hata kidogo. Kazi ya kujenga upya hekalu la Yehova ilikuwa jambo la maana, ndiyo sababu Wayahudi hao walifanya safari hiyo yenye magumu ya kilometre 1600 hivi kwa kupitia katika njia yenye milima na majiwe-majiwe.
Mali ya Kiroho
w06-SW 15/1 uku. 19 fu. 1
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ezra
1:3-6. Sawa na Waisraeli waliobaki Babiloni, Mashahidi wengi wa Yehova hawawezi kuwa wahudumu wa wakati wote au kutumikia mahali penye uhitaji mkubwa. Lakini wao huwaunga mkono na kuwatia moyo wale wanaoweza kufanya hivyo, nao hutoa michango ya hiari kuendeleza kazi ya kuhubiri kuhusu Ufalme na kufanya wanafunzi.