-
Yakobo Alipata UritiMambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
-
-
SOMO LA 12
Yakobo Alipata Uriti
Isaka alikuwa na miaka 40 wakati alimuoa Rebeka. Alimupenda sana. Kisha wakati fulani, wakazaa watoto wawili, mapasa wanaume.
Jina la mukubwa lilikuwa Esau, na jina la mudogo lilikuwa Yakobo. Esau alipenda kutembea-tembea, na alijua sana kuwinda wanyama. Lakini, Yakobo alipenda kubakia ku nyumba.
Ile wakati, watu walizoea kupatia mutoto wa kwanza mashamba mingi na feza mingi kisha baba yake kufa. Ile njo waliita uriti. Mu familia ya Isaka, uriti haikukuwa tu mashamba na feza. Mwenye angepewa uriti njo mwenye Yehova angetumia ili kutimiza ahadi zenye alikuwa amefanyia Abrahamu. Esau hakuona zile ahadi kuwa za maana, lakini Yakobo alijua kama zilikuwa za maana sana.
Siku moja, Esau alitoka kuwinda, na alikuwa amechoka sana. Esau alisikia harufu ya chakula tamu yenye Yakobo alikuwa anapika, kisha akamuambia: ‘Ninasikia njaa sana! Unipatie kwa ile chakula ya mwekundu!’ Yakobo akamuambia: ‘Nitakupatia, lakini uitike kwanza kama utanipatia uriti wako!’ Esau akamuambia: ‘Sina lazima ya ule uriti! Ninakupatia. Nipatie tu chakula nikule.’ Unawaza kama Esau alifanya muzuri? Hapana. Esau alipatia Yakobo kitu cha maana sana juu tu ya chakula.
Wakati Isaka alikuwa muzee sana, alipenda kumubariki mutoto wake mukubwa. Lakini, Rebeka alisaidia mutoto wao mudogo Yakobo, ili apate ile baraka. Wakati Esau alijua vile, alikasirika sana na akapanga kuua ndugu yake Yakobo. Isaka na Rebeka walitaka kulinda Yakobo, basi wakamuambia: ‘Uende uishi na Labani, mujomba wako, mupaka kasirani ya Esau itulie.’ Yakobo alisikiliza shauri la wazazi wake, na akakimbia ili Esau asimuue.
“Mutu atapata faida gani kama anapata ulimwengu muzima lakini anapoteza uzima wake? Kwa kweli, mutu anaweza kutoa nini ili apate uzima wake?”—Marko 8:36, 37
-
-
Yakobo na Esau WanasikilizanaMambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
-
-
SOMO LA 13
Yakobo na Esau Wanasikilizana
Yehova aliambia Yakobo kama atamulinda sawa vile alilindaka Abrahamu na Isaka. Yakobo alienda kuishi Harani. Alioa wakati alikuwa kule, akakuwa na familia kubwa, na vitu mingi.
Kisha, Yehova aliambia Yakobo hivi: ‘Rudia katika inchi yenu.’ Basi, Yakobo na familia yake wakaanza safari ya murefu ya kurudia. Wakati walikuwa mu njia, watu fulani walikuja kumuambia Yakobo hivi: ‘Ndugu yako Esau iko anakuja, na iko na wanaume 400!’ Yakobo aliogopa, aliwaza kama Esau atamutendea mubaya yeye na familia yake. Alisali hivi kwa Yehova: ‘Tafazali uniokoe ili ndugu yangu asinitendee mubaya.’ Siku yenye ilifuata, Yakobo alitumia Esau zawadi mingi. Alimutumia kondoo, mbuzi, ngombe, ngamia, na punda za mingi.
Ule usiku, wakati Yakobo alikuwa peke yake, aliona malaika! Malaika alianza kupigana naye. Walipigana mupaka asubui. Hata kama Yakobo aliumia, hakuacha kupigana. Kisha malaika akamuambia: ‘Niache niende.’ Lakini Yakobo akamujibu: ‘Sitakuacha kama haujanibariki.’
Ku mwisho malaika akamubariki Yakobo. Na Yakobo akajua kama Yehova atamulinda juu Esau asimutendee mubaya.
Asubui, Yakobo aliona kwa mbali Esau iko anakuja na wanaume 400. Yakobo aliacha familia yake nyuma, akapita mbele na kuinama mupaka chini mara saba mbele ya ndugu yake Esau. Esau alienda mbio na kumukumbatia. Wote wawili wakaanza kulia na kisha wakasikilizana. Unawaza Yehova alijisikia namna gani wakati aliona namna Yakobo alijikaza kusikilizana na ndugu yake?
Kisha, Esau alirudia kwake, na Yakobo akaendelea na safari yake. Yakobo alikuwa na watoto wanaume 12. Majina yao ni Rubeni, Simeoni, Lawi, Yuda, Dani, Naftali, Gadi, Asheri, Isakari, Zabuloni, Yosefu, na Benyamini. Mungu alitumia mumoja kati ya wale watoto, ni kusema, Yosefu, juu akomboe watu wake. Unajua alifanya vile namna gani? Acha tuone.
“Muendelee kupenda maadui wenu na kusali kwa ajili ya wale wenye kuwatesa ninyi, ili muonyeshe kuwa ninyi ni wana wa Baba yenu mwenye kuwa mbinguni.”—Matayo 5:44, 45
-