Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Yobu Alikuwa Nani?
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
    • Wanaume 3 wanakuja kumuona Yobu mwenye iko na majipu ku mwili wake wote

      SOMO LA 16

      Yobu Alikuwa Nani?

      Mu inchi ya Usi, mulikuwa mutu mwenye alimuabudu Yehova. Aliitwa Yobu. Alikuwa na vitu mingi sana na alikuwa na familia kubwa. Alikuwa mutu muzuri, alisaidia maskini, alisaidia bibi wenye bwana zao walikuwa wamekufa, na watoto wenye hawakukuwa na wazazi. Lakini, ni kusema kama hangepataka magumu juu alikuwaka anafanya mambo ya muzuri?

      Shetani Ibilisi

      Yobu hakujua kama Shetani Ibilisi alikuwa anamuangalia. Yehova alimuuliza Shetani hivi: ‘Umeona mutumishi wangu Yobu? Hakuna mutu mwenye iko sawa yeye mu dunia. Ananisikilizaka na anafanyaka mambo ya muzuri.’ Shetani akamujibu: ‘Ni kweli Yobu anakutii. Unamulinda na kumubariki. Umemupatia vitu mingi na wanyama. Umunyanganye vile vitu vyote, na ataacha kukuabudu.’ Yehova akamuambia: ‘Unaweza kujaribu Yobu. Lakini usimuue.’ Juu ya nini Yehova aliacha Shetani ajaribu Yobu? Alikuwa hakika kama Yobu angeendelea kuwa muaminifu.

      Shetani alianza kuletea Yobu majaribu mbalimbali. Kwanza, alituma watu fulani wenye kuitwa Wasabea ili waibe ngombe na punda za Yobu. Kisha, moto ukaua kondoo zote za Yobu. Watu wengine wenye kuitwa Wakaldayo, waliiba ngamia zake. Wakaua watumishi wenye walikuwa wanachunga wale wanyama. Kisha jaribu ya mubaya sana mu zote ikatokea. Watoto wote wa Yobu walikuwa wanajifurahisha mu nyumba. Kisha ile nyumba ikawaangukia, na wakakufa. Yobu alihuzunika sana, lakini hakuacha kumuabudu Yehova.

      Shetani alitaka Yobu ateseke tena sana, kwa hiyo, akamuletea Yobu majipu ku mwili wote. Yobu alisikia maumivu sana. Hakujua juu ya nini ile mambo yote ilikuwa inamupata. Lakini, Yobu aliendelea kumuabudu Yehova. Mungu aliona ile mambo yote, na akamupenda Yobu sana.

      Kisha Shetani akatuma watu tatu waende kumujaribu Yobu. Walimuambia: ‘Ulifanya zambi lakini unapenda kuificha. Njo maana Mungu anakupatia malipizi.’ Yobu alisema: ‘Sijafanya kosa hata moja.’ Lakini akaanza kuwaza kama Yehova njo alimuletea ile majaribu, na akasema kama Mungu hakumutendea kwa haki.

      Kijana mumoja mwenye aliitwa Elihu alikuwa anasikiliza ile mazungumuzo bila kusema kitu. Kisha akasema: ‘Mambo yote yenye mumesema haiko ya kweli. Yehova ni mukubwa sana kupita vile tunaweza kuelewa. Hawezi kufanya mambo ya mubaya hata kidogo. Anaonaka mambo yote na anasaidiaka watu wakati wa majaribu.’

      Yobu na bibi yake na mutoto mudogo

      Kisha Yehova akamuuliza Yobu: ‘Ulikuwa wapi wakati niliumba mbingu na dunia? Juu ya nini unasema kama sikutendee kwa haki? Uko unasema tu, lakini haujue juu ya nini mambo ilitokea vile.’ Yobu aliitika makosa yake na kusema: ‘Nilijidanganya. Nilisikia habari zako, lakini sasa nimekujua. Unaweza kufanya mambo yote. Unihurumie juu ya maneno yote yenye nilisema.’

      Wakati majaribu yake iliisha, Yehova alimuponyesha Yobu na kumupatia vitu mingi kuliko vyenye alikuwaka navyo. Yobu aliishi maisha ya murefu na ya furaha. Yehova alibariki Yobu kwa sababu alimutii hata wakati ilikuwa nguvu kufanya vile. Utafuata mufano wa Yobu kwa kuendelea kumuabudu Yehova hata kutokee nini?

      “Mumesikia juu ya uvumilivu wa Yobu na mumeona matokeo yenye Yehova alileta.”​—Yakobo 5:11

      Maulizo: Shetani alimuletea Yobu majaribu gani? Namna gani Yehova alibariki Yobu?

      Yobu 1:1–3:26; 4:7; 32:1-5; 34:5, 21; 35:2; 36:15, 26; 38:1-7; 40:8; 42:1-17

  • Musa Alichagua Kumuabudu Yehova
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
    • Miriamu iko karibu na iko anaangalia wakati binti ya Farao anamupata Musa

      SOMO LA 17

      Musa Alichagua Kumuabudu Yehova

      Mu inchi ya Misri, watu wa familia ya Yakobo walikuwa wanaitwa Waisraeli. Kisha Yakobo na Yosefu kufa, Farao mwingine alianza kutawala. Aliogopa juu aliwaza kama Waisraeli wataongezeka na watakuwa na nguvu kupita Wamisri. Kwa hiyo, ule Farao alifanya Waisraeli kuwa watumwa. Aliwakaza kutengeneza matofali (briques) na kufanya kazi ya nguvu mu mashamba. Lakini hata kama Wamisri waliwakaza kufanya kazi ya nguvu, Waisraeli waliendelea kuongezeka. Kwa sababu Farao hakufurahia jambo hilo, alisema waue watoto wanaume wote Waisraeli wakati wanazaliwa. Waisraeli waliogopa sana, haiko vile?

      Mwanamuke mumoja Mwisraeli mwenye aliitwa Yokebedi, alizaa mutoto mwanaume wa sura ya muzuri. Juu wasimuue, alimuweka mu kitunga, na akamuficha mu matete pembeni ya Muto Nile. Miriamu, dada ya ule mutoto, alibakia karibu na pale juu aone jambo lenye litatokea.

      Binti ya Farao alienda kunawa ku muto na akaona kile kitunga. Mu kile kitunga, aliona mutoto iko analia, na akamusikilia huruma. Miriamu akamuuliza: ‘Nikutafutie mwanamuke mwenye atakunyonyeshea huyu mutoto?’ Wakati binti ya Farao aliitika, Miriamu akaleta Yokebedi, mama yake. Binti ya Farao akamuambia: ‘Kamata huyu mutoto, uanze kumunyonyesha, nitakulipa.’

      Musa anakimbia

      Wakati ule mutoto alikomaa, Yokebedi akamuleta kwa binti ya Farao, naye akamupanga jina Musa na akamuchunga sawa vile mutoto wake. Walimukomalisha sawa vile mutoto wa mufalme na walimupatia kila kitu chenye alipenda. Lakini Musa hakusahau Yehova. Alijua kama yeye alikuwa Mwisraeli, hapana Mumisri. Na alichagua kumutumikia Yehova.

      Wakati alikuwa na miaka 40, Musa alipenda kusaidia Waisraeli wenzake. Wakati aliona Mumisri iko anapiga mutumwa Mwisraeli, Musa alipiga sana ule Mumisri na kumuua. Kisha akamuficha mu muchanga. Wakati Farao alijua jambo hilo, alitafuta kumuua Musa. Lakini Musa akakimbilia mu inchi ya Midiani. Yehova alimuchunga wakati alikuwa kule.

      “Kwa imani Musa, . . . alikataa kuitwa mwana wa binti ya Farao, akachagua kutendewa mubaya pamoja na watu wa Mungu.”​—Waebrania 11:24, 25

      Maulizo: Wamisri walitendea Waisraeli namna gani? Juu ya nini Musa alikimbia kutoka Misri?

      Mwanzo 49:33; Kutoka 1:1-14, 22; 2:1-15; Matendo 7:17-29; Waebrania 11:23-27

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine