Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Muti Mudogo Unawaka Moto
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
    • Musa iko karibu na muti wenye kuwaka moto

      SOMO LA 18

      Muti Mudogo Unawaka Moto

      Musa alifanya miaka 40 kule Midiani. Alioa na kuzaa watoto. Siku moja wakati alikuwa anachunga kondoo zake karibu na Mulima Sinai, aliona jambo la kushangaza. Muti ulikuwa unawaka moto bila kuungua! Wakati alienda karibu juu aone muzuri, alisikia sauti inatoka mu ule muti na kusema: ‘Musa! Usikaribie. Tosha viatu, juu mahali kwenye umesimama ni patakatifu.’ Yehova njo alikuwa anasema kupitia malaika.

      Musa aliogopa, kwa hiyo akaficha uso wake. Ile sauti ikasema: ‘Nimeona mateso ya Waisraeli. Nitawakomboa kutoka Misri na kuwapeleka mu inchi ya muzuri. Na ni wewe njo utatosha watu wangu mu inchi ya Misri.’ Hauone kama jambo hilo lilishangaza Musa?

      Musa akauliza: ‘Wakati wataniuliza kama nani njo alikutuma, nitawaambia nini?’ Mungu akamujibu: ‘Uwaambie kama Yehova, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo njo mwenye amekutuma.’ Kisha Musa akauliza: ‘Itakuwa namna gani kama wale watu hawanisikilize?’ Yehova alifanya mambo fulani ya kumuonyesha kama atamusaidia. Aliambia Musa atupe fimbo yake chini. Kisha ile fimbo ikakuwa nyoka! Wakati Musa alikamata ile nyoka ku mukia, ikageuka tena fimbo. Yehova akamuambia: ‘Wakati utafanya huu muujiza, watajua kama mimi njo nilikutuma.’

      Musa akasema: ‘Mimi sijue kusema muzuri.’ Yehova akamuambia: ‘Nitakuambia mambo yenye utasema, na nitatuma Haruni, ndugu yako akusaidie.’ Musa alijua kama Yehova iko pamoja naye. Kwa hiyo, alikamata bibi yake na watoto wake, na wakarudia Misri.

      “Musihangaike juu ya mambo yenye mutasema ao namna mutayasema, kwa sababu mutapewa mambo ya kusema saa hiyo.”​—Matayo 10:19

      Maulizo: Musa aliona nini wakati alikuwa anachunga kondoo zake? Yehova aliomba Musa afanye nini?

      Kutoka 3:1–4:20; Matendo 7:30-36

  • Mapigo Tatu ya Kwanza
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
    • Musa na Haruni wanasimama mbele ya Farao

      SOMO LA 19

      Mapigo Tatu ya Kwanza

      Waisraeli walikuwa watumwa. Wamisri waliwakaza wafanye kazi ya nguvu. Yehova alituma Musa na Haruni waambie Farao: ‘Acha watu wangu waende ili waniabudu katika jangwa.’ Kwa kiburi, Farao akasema hivi: ‘Sihangaikie ile mambo yenye Yehova anasema, na sitaacha Waisraeli waende.’ Kisha Farao akawaongezea kazi ya nguvu sana. Lakini Yehova alimufundisha Farao jambo fulani. Unajua alifanya nini? Alileta Mapigo Kumi juu ya Misri. Yehova alimuambia Musa: ‘Farao amekataa kunisikiliza. Kesho asubui atakuwa ku Muto Nile. Uende umuambie, juu amekataa kuacha watu wangu waende, maji yote ya Muto Nile itageuka damu.’ Musa alitii na akaenda kumuona Farao. Farao aliona vile Haruni alipiga maji ya Muto Nile kwa fimbo yake, na maji ikageuka damu. Samaki zikakufa, muto ukaanza kunuka, na watu hawakuweza tena kunywa maji ya Muto Nile. Lakini Farao alikataa kuacha Waisraeli waende.

      Kisha siku saba, Yehova alimutuma tena Musa kwa Farao ili amuambie: ‘Kama hauache watu wangu waende, chura watajaa katika inchi yote ya Misri.’ Haruni akakamata fimbo na kunyoosha mukono wake juu kisha chura wakaanza kujaa mu inchi. Chura walijaa fasi yote mu nyumba za watu, ku vitanda, na mu masahani yao. Chura walikuwa kila fasi! Farao alimuambia Musa amuombe Yehova amalize ile pigo. Farao akasema kama ataacha Waisraeli waende. Kisha Yehova akasimamisha ile pigo, na Wamisri wakakusanya wale chura mu mafungu makubwa-makubwa. Na inchi ikaanza kunuka. Lakini kwa mara ingine tena Farao hakuacha Waisraeli waende.

      Kisha pale, Yehova akamuambia Musa: ‘Uambie Haruni apige fimbo yake ku udongo, kisha mavumbi itageuka imbu.’ Palepale, imbu wakajaa kila fasi. Watu fulani wa Farao walimuambia: ‘Hii pigo inatoka kwa Mungu.’ Lakini Farao hakuacha Waisraeli waende.

      Mapigo Tatu kati ya mapigo 10 mu Misri: damu kwenye Muto Nile, chura, na imbu

      “Nitawafanya wajue nguvu zangu na uwezo wangu, na watajua kwamba jina langu ni Yehova.” ​—Yeremia 16:21

      Maulizo: Taja mapigo tatu ya kwanza. Juu ya nini Yehova alileta ile mapigo?

      Kutoka 5:1-18; 7:8–8:19; Nehemia 9:9, 10

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine