-
Mapigo Ingine SitaMambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
-
-
SOMO LA 20
Mapigo Ingine Sita
Musa na Haruni walienda kuambia Farao: ‘Mungu anasema, kama hauache watu wangu waende, nitatuma mainzi juu ya inchi yako.’ Mainzi ya mingi ikaanza kuingia mu nyumba za Wamisri wote, matajiri na maskini. Inchi yote ikajaa mainzi. Lakini mu eneo la Gosheni, kwenye Waisraeli walikuwa wanaishi, hakukukuwa mainzi. Hii pigo ya ine na zile za kufuata zilipata Wamisri tu. Farao akamubembeleza Musa hivi: ‘Muombe Yehova atoshe hii mainzi, njo mutaenda.’ Lakini, Wakati Yehova alitosha mainzi, Farao akabadilisha mawazo. Unawaza Farao angefikia kutii?
Yehova alisema: ‘Farao akiendelea kukataa kuacha watu wangu waende, wanyama wa Wamisri watagonjwa na kufa.’ Siku yenye ilifuata, wanyama wakaanza kufa. Wanyama wa Waisraeli hawakukufa. Lakini Farao aliendelea kuwa na kichwa-nguvu na hakupenda Waisraeli waende.
Kisha Yehova akaambia Musa aende tena kwa Farao na atupe majivu mu hewa. Ile majivu ikakuwa mavumbi, ikajaa mu hewa na ikaenea mu inchi yote ya Wamisri. Ile mavumbi ikaleta majipu kwenye mwili wa Wamisri na wanyama wao wote. Lakini, Farao alikataa kuacha Waisraeli waende.
Yehova akamutuma tena Musa kwa Farao amuambie hivi: ‘Ungali unakataa kuacha watu wangu waende? Kesho mvua ya majiwe itanyesha juu ya inchi.’ Siku yenye kufuata, Yehova akafanya mvua ya majiwe inyeshe, na kukakuwa mingurumo, na moto. Wamisri walikuwa hawajaonaka mvua kubwa kama ile. Miti yote na mimea yote iliharibika, miti na mimea ya Gosheni njo tu ilibakia. Farao akasema: ‘Mumubembeleze Yehova ili mvua iache kunyesha! Kisha nitawaacha muende.’ Lakini, wakati tu mvua iliacha kunyesha, Farao akabadilisha tena mawazo yake.
Kisha Musa akasema: ‘Sasa nzige zitakula mimea yote yenye ilibakia kisha mvua ya majiwe kunyesha.’ Makundi ya nzige ikakula kila kitu chenye kilibakia mu mashamba na ku miti. Farao akamubembeleza Musa hivi: ‘Umuombe Yehova atoshe hizi nzige.’ Lakini hata kisha Yehova kutosha zile nzige, Farao aliendelea kuwa na kichwa-nguvu.
Yehova aliambia Musa: ‘Nyoosha mukono wako juu.’ Palepale fasi yote kukakuwa giza. Mu siku tatu, Wamisri hawakuweza kuona kitu ao mutu. Waisraeli tu njo walikuwa na mwangaza mu nyumba zao.
Farao akaambia Musa: ‘Wewe na watu wako munaweza kuenda. Lakini muache wanyama wenu hapa.’ Musa akasema: ‘Tunapaswa kuenda na wanyama wetu ili tumutolee Mungu wetu zabihu.’ Farao alikasirika sana. Akaambia hivi Musa kwa kasirani: ‘Toka hapa! Nikikuona tena, nitakuua!’
“Na mutaona tena tofauti kati ya mutu mwenye haki na mutu muovu, kati ya mutu mwenye kumutumikia Mungu na mwenye hamutumikie.”—Malaki 3:18
-
-
Pigo ya KumiMambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
-
-
SOMO LA 21
Pigo la Kumi
Musa aliambia Farao kama hangeonana naye tena. Lakini mbele atoke kwa Farao alimuambia: ‘Katikati ya usiku, kila mutoto wa kwanza katika inchi ya Misri, kuanzia mutoto wa kwanza wa Farao mupaka mutoto wa kwanza wa watumwa, atakufa.’
Yehova aliambia Waisraeli watayarishe chakula cha pekee. Alisema: ‘Muchinje kondoo dume ao mbuzi wa mwaka moja, kisha mupakae damu yake ku miimo (encadrement) ya milango ya nyumba zenu. Muchome ile nyama na kuikula na mukate yenye haina chachu. Muvae nguo na viatu na mukuwe tayari kuenda. Usiku wa leo nitawakomboa.’ Hauone kama Waisraeli walipaswa kufurahi kabisa?
Katikati ya usiku, malaika wa Yehova alipita ku kila nyumba mu inchi ya Misri. Mutoto wa kwanza wa kila nyumba yenye haikupakaliwa damu ku miimo ya mulango, alikufa. Lakini ule malaika aliacha nyumba zenye zilikuwa zimepakaliwa damu. Kila mutoto wa kwanza alikufa mu kila familia ya Wamisri, za matajiri na maskini. Lakini hakuna mutoto Mwisraeli mwenye alikufa.
Hata mutoto wa Farao alikufa. Farao hakuweza kuvumilia tena. Palepale akaambia Musa na Haruni: ‘Musimame. Mutoke hapa. Muende muabudu Mungu wenu. Mukamate wanyama wenu na muende!’
Ule usiku wenye Waisraeli walitoka Misri, mwezi ilikuwa yote muviringo. Walikuwa wamepangwa kulingana na familia na makabila yao. Kulikuwa wanaume Waisraeli 600000, na wanamuke na watoto wengi. Na watu wengine wengi walienda pamoja nao ili wamuabudu Yehova. Sasa Waisraeli walikuwa huru kabisa!
Ili kukumbuka vile Yehova aliwakomboa, kila mwaka walikuwa wanatayarisha ile chakula ya pekee, yenye inaitwa Pasaka.
“Kwa sababu hii nimekuacha ubakie: ili nionyeshe nguvu zangu kuhusiana na wewe na ili jina langu litangazwe katika dunia yote.”—Waroma 9:17
-