-
Walishindwa Kutimiza Ahadi YaoMambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
-
-
SOMO LA 24
Walishindwa Kutimiza Ahadi Yao
Yehova aliambia Musa hivi: ‘Panda kwenye mulima, tukutane. Nitaandika sheria zangu juu ya mabamba ya majiwe, kisha nitakupatia.’ Musa akapanda ku mulima na kukaa kule siku 40 muchana na usiku. Wakati alikuwa kule, Yehova aliandika zile Amri Kumi juu ya mabamba mbili ya majiwe na akamupatia Musa ile mabamba.
Kisha wakati fulani, Waisraeli wakawaza kama Musa amewaacha. Wakaambia Haruni: ‘Tunataka mutu wa kutuongoza. Ututengenezee mungu!’ Haruni akasema: ‘Munipatie zahabu yenu.’ Akayeyusha ile zahabu na kutengeneza sanamu ya kitoto-dume cha ngombe. Watu wakasema: ‘Huyu njo Mungu mwenye alitutosha Misri.’ Wakaanza kuabudu ile sanamu ya zahabu na wakafanya karamu. Kufanya vile ilikuwa mubaya? Ndiyo, kwa sababu wale watu walitoaka ahadi kama watamuabudu Yehova tu. Lakini sasa walishindwa kutimiza ahadi yao.
Yehova aliona ile mambo, na akaambia Musa: ‘Shuka urudie kwenye watu wako. Hawanitii na wanaabudu mungu wa uongo.’ Musa akashuka mbio kutoka ku mulima, na alikuwa anabeba ile mabamba mbili.
Wakati Musa alikaribia kambi alisikia watu wako wanaimba. Kisha akawaona wako wanacheza na kuinamia ile sanamu ya kitoto-dume cha ngombe. Musa alikasirika sana. Alitupa ile mabamba mbili chini na ikavunjika vipande-vipande. Palepale akaharibu ile sanamu. Kisha akauliza Haruni: ‘Hawa watu walikuambia nini juu uitike kufanya hili jambo la mubaya sana?’ Haruni akasema: ‘Usikasirike. Unajua vile hawa watu wanakuwaka. Walitaka niwatengenezee mungu, kwa hiyo nikatupa zahabu yao katika moto na ile sanamu ya kitoto-dume cha ngombe ikatokea!’ Haruni hakupaswa kufanya vile. Musa akarudia ku mulima na kumubembeleza Yehova asamehe wale watu.
Yehova alisamehe wale wenye walikuwa tayari kumutii. Hauone kama ilikuwa jambo la maana Waisraeli waache Musa awaongoze?
“Kila mara wakati unaweka naziri kwa Mungu, usikawie kuitimiza, kwa maana hafurahie wajinga. Naziri yenye unaweka, uitimize.”—Muhubiri 5:4
-
-
Wanajenga TabenakuloMambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
-
-
SOMO LA 25
Wanajenga Tabenakulo
Wakati Musa alikuwa ku Mulima Sinai, Yehova alimuambia ajenge hema ya pekee yenye inaitwa tabenakulo. Pale njo Waisraeli wangekuwa wanamuabudu Mungu. Na wangekuwa wanabeba ile hema fasi yote kwenye walienda.
Yehova alisema: ‘Uambie watu watoe michango ya kujenga tabenakulo.’ Waisraeli wakatoa zahabu, feza, shaba, majiwe ya bei, na vitu vingine vya bei vya kujipamba. Tena walitoa manyoya ya kondoo, vitambaa vya rangi nyekundu, ngozi za wanyama, na vitu vingine vya mingi. Waliendelea kutoa vitu mingi sana mupaka Musa akasema: ‘Michango inaenea! Musitoe tena.’
Wanaume na wanamuke mingi wenye ufundi walisaidia kujenga tabenakulo. Yehova aliwapatia akili ya kufanya ile kazi. Wamoja walitengeneza nyuzi na vitambaa, ao kupamba vitambaa. Wengine walitayarisha majiwe, zahabu, na mbao.
Watu walijenga tabenakulo sawa vile Yehova aliwaambia. Waliweka pazia (rideau) ya muzuri juu ya kugawanya tabenakulo mu sehemu mbili: Patakatifu na Patakatifu Zaidi. Mu Patakatifu Zaidi mulikuwa sanduku la agano lenye lilitengenezwa na mbao za muti wa mugunga na zahabu. Mu Patakatifu mulikuwa kitu cha kuwekea taa ya zahabu, mulikuwa meza, na mazabahu ya kuchomea uvumba. Mu kiwanja mulikuwa beseni ya shaba na mazabahu kubwa. Sanduku la agano lilikumbusha Waisraeli ahadi yenye walifanyaka ya kusema kama watamutii Yehova. Unajua agano ni nini? Ni ahadi fulani ya pekee.
Yehova alichagua Haruni na watoto wake wakuwe makuhani ku tabenakulo. Walipaswa kuichunga muzuri na kumutolea Yehova zabihu. Ni Haruni tu njo alikuwa na ruhusa ya kuingia Patakatifu Zaidi juu yeye njo alikuwa kuhani mukubwa. Aliingia Patakatifu Zaidi mara moja kila mwaka juu atoe zabihu kwa ajili ya zambi zake, zambi za familia yake, na zambi za taifa lote la Israeli.
Waisraeli walimaliza kujenga tabenakulo mwaka moja kisha kutoka Misri. Sasa walipata fasi kwenye wangemuabudu Yehova.
Yehova alionyesha kama anakubali tabenakulo. Kwa hiyo alifanya wingu likuwe juu ya ile tabenakulo. Wakati wingu liliendelea kuwa juu ya tabenakulo, Waisraeli hawakutoka kwenye walikuwa wametia kambi. Lakini wakati wingu lilitoka juu ya tabenakulo, Waisraeli walijua kama ilikuwa wakati wa kuenda. Walibomoa tabenakulo na kufuata lile wingu.
“Halafu nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha ufalme ikisema: ‘Angalia! Hema ya Mungu iko pamoja na wanadamu, na atakaa pamoja nao, na watakuwa watu wake. Na Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.’”—Ufunuo 21:3
-