-
Rahabu Alificha WapeleleziMambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
-
-
SOMO LA 30
Rahabu Alificha Wapelelezi
Wakati wapelelezi Waisraeli walienda Yeriko, waliingia mu nyumba ya mwanamuke mwenye kuitwa Rahabu. Wakati mufalme wa Yeriko alijua, alituma maaskari ku nyumba ya Rahabu. Lakini Rahabu alificha wale wapelelezi wawili ku sehemu ya juu ya nyumba yake na akatuma wale maaskari mu njia ingine. Kisha Rahabu akaambia wale wapelelezi: ‘Nitawasaidia juu ninajua kama Yehova iko pamoja na ninyi na mutakamata hii inchi. Tafazali, munitolee ahadi kama mutaokoa familia yangu.’
Wapelelezi wakaambia Rahabu: ‘Tunakutolea ahadi kama hakuna mutu ndani ya nyumba yako mwenye ataumia. Funga kamba nyekundu kwenye dirisha, na watu wa familia yako wataokolewa.’
Rahabu akashusha wale wapelelezi kupitia dirisha kwa kutumia kamba. Wakaenda kujificha ku milima siku tatu mbele ya kurudia kwa Yoshua. Kisha Waisraeli wakavuka Muto Yordani na kujitayarisha kukamata inchi. Yeriko ilikuwa muji wa kwanza wenye walikamata. Yehova aliwaambia wazunguke muji mara moja kila siku kwa siku sita. Siku ya saba, walizunguka muji mara saba. Kisha makuhani wakapiga tarumbeta, na maaskari wakalalamika kwa nguvu yao yote. Kuta za ule muji zikaanguka! Lakini nyumba ya Rahabu, yenye ilikuwa ku ukuta haikuanguka. Rahabu na familia yake waliokolewa kwa sababu alimutegemea Yehova.
“Vilevile, je, Rahabu . . . hakutangazwa pia kuwa mwenye haki kupitia matendo, kisha kukaribisha muzuri wale wajumbe na kuwatosha inje kupitia njia ingine?”—Yakobo 2:25
-
-
Yoshua na WagibeoniMambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
-
-
SOMO LA 31
Yoshua na Wagibeoni
Habari juu ya kuanguka kwa Yeriko ilienea sana mu mataifa ingine ya Kanaani. Wafalme wa ile mataifa wakasikilizana juu wapigane na Waisraeli. Lakini Wagibeoni wakachagua kufanya jambo lingine. Wakavaa manguo ya kupasuka-pasuka na wakaenda kuonana na Yoshua, wakamuambia: ‘Tumetoka katika inchi ya mbali sana. Tumesikia habari juu ya Yehova na mambo yote yenye aliwafanyia wakati mulikuwa Misri na Moabu. Kama munatutolea ahadi kuwa hamutapigana na sisi, tutakuwa watumishi wenu.’
Yoshua aliamini mambo yenye walisema na akawaambia kama hatapigana nao. Kisha siku tatu, akavumbua kama hawakutoka mu inchi ya mbali, walitoka Kanaani. Yoshua akauliza Wagibeoni: ‘Juu ya nini mulitudanganya?’ Wakamujibu: ‘Tuliogopa! Tunajua kama Yehova Mungu wenu iko anawapigania. Tafazali, musituue.’ Yoshua akatimiza mambo yenye aliwaambia, akawaacha waendelee kuishi.
Kisha wakati kidogo, wafalme tano Wakanaani na maaskari wao wakatuma habari za kuogopesha za kusema kama watapigana na Wagibeoni. Yoshua na maaskari wake walitembea usiku muzima juu waende kuokoa Wagibeoni. Vita ikaanza asubui sana siku ya kufuata. Wakanaani walianza kukimbia ngambo zote. Kila fasi kwenye walikimbilia Yehova aliangusha majiwe ya mukubwa-mukubwa sana juu yao. Kisha Yoshua akamuomba Yehova afanye jua isimame. Mbele ya pale, hakuna siku yenye jua ilisimamaka. Sasa, juu ya nini Yoshua aliomba Yehova afanye jua isimame? Ni juu Yoshua alikuwa anamutumainia kabisa Yehova. Jua ikasimama siku muzima mupaka wakati Waisraeli walipata ushindi juu ya wafalme Wakanaani na maaskari wao.
“Neno lenu ‘Ndiyo’ limaanishe ndiyo, na ‘Hapana’ yenu imaanishe hapana, kwa maana lenye kupita hayo linatoka kwa ule muovu.”—Matayo 5:37
-