Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Rahabu Alificha Wapelelezi
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
    • Rahabu analinda wapelelezi kwa kutuma maaskari mu njia ingine

      SOMO LA 30

      Rahabu Alificha Wapelelezi

      Wakati wapelelezi Waisraeli walienda Yeriko, waliingia mu nyumba ya mwanamuke mwenye kuitwa Rahabu. Wakati mufalme wa Yeriko alijua, alituma maaskari ku nyumba ya Rahabu. Lakini Rahabu alificha wale wapelelezi wawili ku sehemu ya juu ya nyumba yake na akatuma wale maaskari mu njia ingine. Kisha Rahabu akaambia wale wapelelezi: ‘Nitawasaidia juu ninajua kama Yehova iko pamoja na ninyi na mutakamata hii inchi. Tafazali, munitolee ahadi kama mutaokoa familia yangu.’

      Wapelelezi wakaambia Rahabu: ‘Tunakutolea ahadi kama hakuna mutu ndani ya nyumba yako mwenye ataumia. Funga kamba nyekundu kwenye dirisha, na watu wa familia yako wataokolewa.’

      Nyumba ya Rahabu, yenye iko na kamba nyekundu ku dirisha, haianguke wakati kuta za Yeriko zinaanguka

      Rahabu akashusha wale wapelelezi kupitia dirisha kwa kutumia kamba. Wakaenda kujificha ku milima siku tatu mbele ya kurudia kwa Yoshua. Kisha Waisraeli wakavuka Muto Yordani na kujitayarisha kukamata inchi. Yeriko ilikuwa muji wa kwanza wenye walikamata. Yehova aliwaambia wazunguke muji mara moja kila siku kwa siku sita. Siku ya saba, walizunguka muji mara saba. Kisha makuhani wakapiga tarumbeta, na maaskari wakalalamika kwa nguvu yao yote. Kuta za ule muji zikaanguka! Lakini nyumba ya Rahabu, yenye ilikuwa ku ukuta haikuanguka. Rahabu na familia yake waliokolewa kwa sababu alimutegemea Yehova.

      “Vilevile, je, Rahabu . . . hakutangazwa pia kuwa mwenye haki kupitia matendo, kisha kukaribisha muzuri wale wajumbe na kuwatosha inje kupitia njia ingine?”​—Yakobo 2:25

      Maulizo: Juu ya nini Rahabu alisaidia wapelelezi? Waisraeli walifanyaka nini juu wakamate muji wa Yeriko? Ni nini ilipata Rahabu na familia yake?

      Yoshua 2:1-24; 6:1-27; Waebrania 11:30, 31; Yakobo 2:24-26

  • Yoshua na Wagibeoni
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
    • Wagibeoni wenye kuvala manguo ya kupasuka-pasuka wanaenda kuonana na Yoshua na maaskari wake

      SOMO LA 31

      Yoshua na Wagibeoni

      Habari juu ya kuanguka kwa Yeriko ilienea sana mu mataifa ingine ya Kanaani. Wafalme wa ile mataifa wakasikilizana juu wapigane na Waisraeli. Lakini Wagibeoni wakachagua kufanya jambo lingine. Wakavaa manguo ya kupasuka-pasuka na wakaenda kuonana na Yoshua, wakamuambia: ‘Tumetoka katika inchi ya mbali sana. Tumesikia habari juu ya Yehova na mambo yote yenye aliwafanyia wakati mulikuwa Misri na Moabu. Kama munatutolea ahadi kuwa hamutapigana na sisi, tutakuwa watumishi wenu.’

      Yoshua aliamini mambo yenye walisema na akawaambia kama hatapigana nao. Kisha siku tatu, akavumbua kama hawakutoka mu inchi ya mbali, walitoka Kanaani. Yoshua akauliza Wagibeoni: ‘Juu ya nini mulitudanganya?’ Wakamujibu: ‘Tuliogopa! Tunajua kama Yehova Mungu wenu iko anawapigania. Tafazali, musituue.’ Yoshua akatimiza mambo yenye aliwaambia, akawaacha waendelee kuishi.

      Kisha wakati kidogo, wafalme tano Wakanaani na maaskari wao wakatuma habari za kuogopesha za kusema kama watapigana na Wagibeoni. Yoshua na maaskari wake walitembea usiku muzima juu waende kuokoa Wagibeoni. Vita ikaanza asubui sana siku ya kufuata. Wakanaani walianza kukimbia ngambo zote. Kila fasi kwenye walikimbilia Yehova aliangusha majiwe ya mukubwa-mukubwa sana juu yao. Kisha Yoshua akamuomba Yehova afanye jua isimame. Mbele ya pale, hakuna siku yenye jua ilisimamaka. Sasa, juu ya nini Yoshua aliomba Yehova afanye jua isimame? Ni juu Yoshua alikuwa anamutumainia kabisa Yehova. Jua ikasimama siku muzima mupaka wakati Waisraeli walipata ushindi juu ya wafalme Wakanaani na maaskari wao.

      Yoshua anaangalia mbinguni na kumuomba Yehova afanye jua isimame

      “Neno lenu ‘Ndiyo’ limaanishe ndiyo, na ‘Hapana’ yenu imaanishe hapana, kwa maana lenye kupita hayo linatoka kwa ule muovu.”​—Matayo 5:37

      Maulizo: Wagibeoni walifanya nini juu Waisraeli wasipigane nao? Namna gani Yehova alisaidia Waisraeli?

      Yoshua 9:1–10:15

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine