-
Kiongozi Mupya na Wanamuke Mbili Wenye UhodariMambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
-
-
SOMO LA 32
Kiongozi Mupya na Wanamuke Wawili Wenye Uhodari
Kisha kuongoza watu wa Yehova kwa miaka mingi, Yoshua alikufa na miaka 110. Wakati Yoshua alikuwa muzima, Waisraeli walimuabudu Yehova. Lakini kisha Yoshua kufa, walianza kuabudu sanamu, sawa vile Wakanaani. Kwa sababu Waisraeli hawakuendelea kumutii, Yehova aliacha mufalme Yabini wa Kanaani awatese. Watu walimulilia Yehova awasaidie. Kwa hiyo, Yehova akachagua kiongozi mupya mwenye kuitwa Baraka. Ule kiongozi angewasaidia watu wamurudilie Yehova.
Debora, nabii mwanamuke, alimuita Baraka. Wakati alifika, akamuambia kama Yehova anasema hivi: ‘Ukamate wanaume 10000, na uende kupigana na maaskari wa Yabini mu bonde la muto Kishoni. Kule utashinda Sisera, mukubwa wa maaskari wa Yabini.’ Baraka akaambia Debora: ‘Nitaenda kama tu utaenda pamoja na mimi.’ Debora akamujibu: ‘Nitaenda na wewe. Lakini ujue kama, haiko wewe njo utaua Sisera. Yehova amesema kama mwanamuke njo atamuua.’
Debora alienda pamoja na Baraka na maaskari wake ku Mulima Tabori juu wajitayarishe kupigana vita. Wakati tu Sisera alisikia vile, akakusanya magari ya vita na maaskari wake mu bonde. Debora akaambia Baraka: ‘Leo ni siku yenye Yehova atakupatia ushindi.’ Baraka na wanaume wake 10000 walitoka ku mulima na kushuka ili wapigane na maaskari wa Sisera wenye nguvu sana.
Kisha, Yehova akafanya maji ijae mu bonde la Kishoni. Magari ya vita ya Sisera ikakwama mu matope. Sisera akatoka mu gari lake na kuanza kukimbia. Baraka na maaskari wake walishinda maaskari wa Sisera, lakini Sisera alikimbia! Akaenda kujificha mu hema ya mwanamuke mwenye kuitwa Yaeli. Ule mwanamuke akamupatia maziwa akunywe, kisha akamufunika blanketi. Ule mwanaume mwenye nguvu akalala usingizi; alikuwa amechoka. Kisha, Yaeli akaingia kwenye alikuwa analala na kumupigilia musumari ya hema mu kichwa na akakufa.
Baraka alikuja kutafuta Sisera. Yaeli akatoka inje ya hema na kumuambia: ‘Ingia nikuonyeshe mwanaume mwenye uko unatafuta.’ Baraka akaingia na kukuta Sisera amekufa. Baraka na Debora wakaimbia Yehova wimbo wa kumusifu kwa sababu alikuwa amepatia Waisraeli ushindi juu ya maadui wao. Mu miaka 40 yenye ilifuata, Waisraeli waliishi mu amani.
“Wanamuke wenye kutangaza habari njema ni jeshi kubwa.”—Zaburi 68:11
-
-
Rutu na NaomiMambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
-
-
SOMO LA 33
Rutu na Naomi
Wakati kulikuwa njaa mu inchi ya Israeli, mwanamuke Mwisraeli mwenye kuitwa Naomi alihamia Moabu na bwana yake na watoto wake wanaume wawili. Kisha, bwana ya Naomi akakufa. Mutoto wake mumoja alioa Rutu, na mwingine alioa Orpa, wanamuke Wamoabu. Lakini, kisha wakati fulani watoto wa Naomi walikufa.
Wakati Naomi alipata habari kama njaa ilikuwa imeisha mu inchi ya Israeli, aliamua kurudia. Rutu na Orpa walienda pamoja naye, lakini, wakati walikuwa mu njia, Naomi aliwaambia hivi: ‘Mulikuwa bibi wazuri kwa watoto wangu na mulikuwa wakwe wazuri kwangu. Ninapenda muolewe tena. Murudie Moabu.’ Wakamuambia: ‘Tunakupenda sana! Hatupendi kukuacha.’ Naomi akaendelea kuwabembeleza warudie. Kisha, Orpa akarudia, lakini Rutu akabakia. Naomi akamuambia: ‘Orpa anarudia kwa watu wake na kwa miungu yake. Rudia naye, na uende ku nyumba ya mama yako.’ Lakini, Rutu akamuambia: ‘Sitakuacha. Watu wako watakuwa watu wangu, na Mungu wako Mungu wangu.’ Unawaza Naomi alijisikia namna gani wakati Rutu alimuambia vile?
Rutu na Naomi walifika Israeli mwanzo wa mavuno ya mbegu ya shayiri (orge). Siku moja, Rutu alienda kuokota mbegu ya shayiri mu shamba la mwanaume mwenye kuitwa Boazi, mwenye alikuwa mutoto wa Rahabu. Boazi alipata habari kama Rutu alikuwa Mumoabu mwenye alikataa kabisa kuachana na Naomi. Aliambia wafanyakazi wake waache mbegu fulani mu shamba juu Rutu aziokote.
Mangaribi, Naomi aliuliza Rutu: ‘Leo ulifanya kazi mu shamba la nani?’ Rutu akamujibia: ‘Mu shambala Boazi.’ Naomi akamuambia: ‘Boazi ni mutu wa jamaa ya bwana yangu. Uendelee kufanya kazi mu shamba lake pamoja na wanamuke wengine. Pale hakuna mutu mwenye atakusumbua.’
Rutu aliendelea kufanya kazi mu shamba la Boazi mupaka wakati kazi ya kuvuna iliisha. Boazi alitambua kama Rutu ni mwanamuke muzuri na mwenye bidii. Ile wakati, kama mwanaume anakufa bila kuzaa watoto, mutu wa jamaa yake alipaswa kuoa bibi yake. Basi, Boazi alioa Rutu. Wakazaa mutoto mwenye aliitwa Obedi, mwenye alifikia kuwa tate (nkambo) wa Mufalme Daudi. Marafiki wa Naomi walifurahi sana. Walimuambia: ‘Kwanza, Yehova alikupatia Rutu mwenye anakupenda sana, na sasa uko na mujukuu. Yehova asifiwe.’
“Kuko rafiki mwenye anashikamana sana na mutu kuliko ndugu.”—Mezali 18:24
-