-
Gideoni Alishinda WamidianiMambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
-
-
SOMO LA 34
Gideoni Alishinda Wamidiani
Kisha wakati fulani, Waisraeli walimuacha tena Yehova na kuanza kuabudu miungu ya uongo. Kwa miaka saba, Wamidiani waliiba wanyama wa Waisraeli na kuharibisha mimea yao. Kwa hiyo, juu ya kujilinda, Waisraeli walijificha mu mapango na milima. Walimulilia Yehova awasaidie. Kwa hiyo, Yehova akatuma malaika kwa mwanaume mwenye kuitwa Gideoni. Ule malaika akamuambia: ‘Yehova amekuchagua juu ukuwe mupiganaji-vita mwenye nguvu.’ Gideoni akamuuliza: ‘Namna gani nitaweza kuokoa Waisraeli? Mimi siko kitu.’
Nini njo ingesadikisha Gideoni kama kweli Yehova alikuwa amemuhagua? Gideoni alikamata manyoya ya kondoo na kuitia chini. Kisha, alimuambia Yehova: ‘Kama kesho asubui ninakuta umande ku manyoya lakini chini kunakauka, nitajua kama umenichagua juu niokoe Waisraeli.’ Siku yenye ilifuata, manyoya ilikuwa imeloana lakini chini kulikuwa kunakauka! Kisha, Gideoni akaomba kama, asubui ya kufuata manyoya njo ikuwe ya kukauka lakini chini kukuwe umande. Wakati ilifanyika vile, Gideoni akaamini kabisa kama Yehova alikuwa amemuchagua. Basi, akakusanya maaskari wake na kuenda kupigana na Wamidiani.
Yehova akaambia Gideoni: ‘Nitapatia Waisraeli ushindi. Lakini kwa sababu uko na maaskari wengi, unaweza kuwaza kama ni kwa nguvu yenu njo mulipata ushindi. Uambie kila mutu mwenye kuwa na woga arudie ku nyumba.’ Kwa hiyo, maaskari 22000 wakarudia ku nyumba, na kukabakia maaskari 10000. Kisha, Yehova akasema: ‘Ungali na maaskari wengi sana. Uwapeleke ku muto ya kidogo na uwaambie wakunywe maji. Ubakie tu na wale wenye watakunywa maji na wako wanaangalia kama hakuna adui pembeni.’ Ni wanaume 300 tu njo walifanya vile wakati walikuwa wanakunywa. Yehova alitoa ahadi kama wale wanaume kidogo watashinda jeshi la Midiani lenye kuwa na maaskari 135000.
Usiku, Yehova aliambia Gideoni: ‘Huu njo wakati wa kushambulia Wamidiani!’ Gideoni alipatia watu wake baragumu na mitungi kubwa na alikuwa ameficha mienge (torches) ndani ya ile mitungi. Kisha, akawaambia: ‘Muniangalie na mufanye vile ninafanya.’ Kisha, Gideoni akapiga baragumu, akavunja mutungi, akanyoosha mwenge wake, na kusema: ‘Upanga wa Yehova na wa Gideoni!’ Wanaume wake 300 wakafanya vilevile. Wamidiani wakaogopa na kukimbia ovyo-ovyo kila mutu mu njia yake. Kukakuwa muvurugo, na wakaanza kuuana. Tena, Yehova alisaidia Waisraeli washinde maadui wao.
“Ili nguvu zenye kupita zile za kawaida zikuwe za Mungu, hapana zenye kutoka kwetu.”—2 Wakorinto 4:7
-
-
Hana Anasali Apate Mutoto MwanaumeMambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
-
-
SOMO LA 35
Hana Anasali Apate Mutoto Mwanaume
Mwanaume Mwisraeli mwenye aliitwa Elkana alikuwa na bibi wawili: Hana na Penina. Lakini Elkana alipenda sana Hana. Kila wakati, Penina alimucheka Hana juu yeye alikuwa na watoto wengi, lakini Hana hakukuwa na mutoto. Kila mwaka, Elkana na familia yake walienda kuabudu ku tabenakulo kule Shilo. Siku moja, wakati walikuwa kule, alitambua kama bibi yake mupendwa Hana alikuwa na huzuni sana. Akamuambia: ‘Hana, tafazali usilie. Niko pale juu yako. Ninakupenda.’
Kisha, Hana alienda kusali. Aliendelea kumulilia Yehova amusaidie. Akamutolea hii ahadi: ‘Yehova, ukinipatia mutoto mwanaume, nitakupatia ule mutoto ili akutumikie maisha yake yote.’
Wakati kuhani Mukubwa Eli aliona Hana iko analia, aliwaza kama Hana analewa. Hana akamujibu: ‘Hapana, Bwana wangu, siko mulevi. Niko na shida kubwa yenye iko inanisumbua sana na njo yenye niko ninaelezea Yehova.’ Eli alitambua kama alikuwa amewazia Hana mubaya, kwa hiyo akamuambia: ‘Mungu akupatie jambo lenye unamuomba.’ Hana akajisikia muzuri zaidi, kisha akaenda. Mbele mwaka moja ienee, akazaa mutoto mwanaume na akamupatia jina Samweli. Wazia namna Hana alifurahi sana kupata mutoto!
Hana hakusahau ahadi yenye alimutolea Yehova. Kisha Samweli kuacha kunyonya, alimupeleka ku tabenakulo juu atumikie kule. Hana aliambia Eli: ‘Huyu njo mutoto mwenye niliombaka Yehova anipatie. Ninamutoa kwa Yehova juu amutumikie maisha yake yote.’ Kila mwaka, Elkana na Hana walikuwa wanaenda kuona Samweli na walikuwa wanamupelekea koti yenye haina mikono. Yehova alibariki Hana na akazaa watoto wengine, wanaume tatu na wanamuke wawili.
“Muendelee kuomba, na mutapewa; muendelee kutafuta, na mutapata.”—Matayo 7:7
-