Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Yehova Ni ‘Mufunuaji wa Siri’
    Munara wa Mulinzi—2012 | Mwezi wa 6 15
    • Yehova Ni ‘Mufunuaji wa Siri’

      ‘Kwa kweli Mungu wenu ni Mungu wa miungu na Bwana wa wafalme na Mufunuaji wa siri.’​—DAN. 2:47.

      UNAWEZA KUJIBU NAMNA GANI?

      Yehova ametufunulia mambo gani ya wakati ujao?

      Vichwa sita vya kwanza vya munyama-mwitu vinafananisha nini?

      Ni sehemu gani za munyama​-mwitu na za sanamu ya Nebukadneza ambazo zinalingana?

      1, 2. Yehova ametufunulia mambo gani, na sababu gani alitufunulia mambo hayo?

      WAKATI Ufalme wa Mungu utakuja kuvunja serikali za dunia, ni serikali gani zitakazokuwa zikitawala? Tunajua jibu. Yehova Mungu, ‘Mufunuaji wa siri,’ ametufunulia hilo. Ametusaidia kuelewa serikali hizo kupitia unabii wa Danieli na wa Yohana.

      2 Katika maono, Yehova aliwaonyesha wanyama mbalimbali waliotokea moja baada ya nyingine. Tena, Danieli aliona sanamu kubwa na Yehova alimufunulia maana ya maono ya sanamu hiyo. Yehova aliandikisha mambo hayo katika Biblia kwa faida yetu. (Rom. 15:4) Alifunua mambo hayo ili imani yetu iwe nguvu na ili tujue kama karibuni Ufalme wake utaharibu serikali zote za wanadamu.​—Dan. 2:44.

      3. Ili kuelewa vizuri unabii wa Danieli na wa Yohana, tunapaswa kujua nini kwanza, na sababu gani?

      3 Unabii wa Danieli na wa Yohana unataja wafalme wanane, ao utawala wa wanadamu, na pia unaonyesha namna wafalme hao wangefuatana. Hata hivyo, ili kuelewa vizuri unabii huo ni lazima tujue vizuri maana ya unabii wa kwanza wa Biblia. Sababu gani? Kwa sababu unabii wote ulio katika Biblia unapatana na unabii huo. Tunaweza kulinganisha unabii wa kwanza wa Biblia na kamba inayounganisha kila unabii wa Biblia.

      UZAO WA NYOKA NA MUNYAMA-MWITU

      4. Ni nani wanaounda uzao wa mwanamuke, nao uzao huo utafanya nini?

      4 Kisha tu uasi uliotokea katika Edeni, Yehova aliahidi kama ‘mwanamuke’ angetokeza “uzao.”a (Soma Mwanzo 3:15.) Mwishowe, uzao huo ungeponda kichwa cha Shetani. Kisha, Yehova alifunua kama uzao huo ungetokea kupitia familia ya Abrahamu, katika taifa la Israeli, katika kabila la Yuda, na katika kizazi cha Daudi. (Mwa. 22:15-18; 49:10; Zab. 89:3, 4; Lu. 1:30-33) Yesu Kristo ndiye sehemu ya kwanza ya uzao huo. (Gal. 3:16) Sehemu ya pili ya uzao huo inaundwa na Wakristo watiwa-mafuta wa kutaniko la Kikristo. (Gal. 3:26-29) Yesu na Wakristo hao watiwa-mafuta ndio wanaounda Ufalme wa Mungu, ni kusema, serikali ambayo Mungu atatumia ili kumuharibu Shetani.​—Lu. 12:32; Rom. 16:20.

      5, 6. (a) Danieli na Yohana walizungumuzia serikali ngapi kubwa? (b) Vichwa vya munyama-mwitu vinavyozungumuziwa katika Ufunuo, vinafananisha nini?

      5 Unabii huo wa kwanza uliotolewa katika Edeni ulionyesha pia kama Shetani angetokeza “uzao.” Na kungekuwa uadui, ao chuki kati ya uzao wa Shetani na uzao wa mwanamuke. Ni nani wanaofanyiza uzao wa nyoka? Ni wale wote wanaomuiga Shetani kwa kumuchukia Mungu ao watu wake. Katika historia ya wanadamu, Shetani amefanya uzao wake utokeze serikali za kila namna, ao falme nyingi. (Lu. 4:5, 6) Lakini, ni serikali fulani tu kati ya serikali hizo ambazo zimewatesa watu wa Mungu: taifa la Israeli ao Wakristo watiwa​-mafuta. Jambo hilo linatusaidia kuelewa nini? Jambo hilo linatusaidia kuelewa kwa nini maono ya Danieli na Yohana yanataja serikali kubwa munane tu hata ikiwa kulikuwako na serikali zingine zilizotawala ulimwenguni.

      6 Kisha miaka elfu mbili hivi, Yesu aliyefufuliwa alimuonyesha mutume Yohana maono mengi yenye kushangaza sana. (Ufu. 1:1) Katika moja ya maono hayo, Yohana aliona joka mukubwa akisimama juu ya muchanga wa bahari kubwa. Joka huyo ni Shetani. (Soma Ufunuo 13:1, 2.) Tena, Yohana aliona munyama wa kuogopesha akitoka katika bahari hiyo; Shetani alimupatia munyama huyo mamlaka makubwa. Baadaye, malaika alimuambia Yohana kama vichwa saba vya yule munyama mwenye rangi nyekendu, ambaye ni sanamu ya yule munyama anayezungumuziwa katika Ufunuo 13:1, vinafananisha “wafalme saba” ao serikali saba. (Ufu. 13:14, 15; 17:3, 9, 10) Yohana alipokuwa akiandika maono hayo, wafalme watano walikuwa wameanguka, mumoja alikuwa angali anatawala na mwingine alikuwa “hajafika bado.” Hizo ni serikali gani ao mamlaka gani makubwa ya ulimwengu? Acheni tujifunze maana ya kila kichwa cha munyama anayetajwa katika Ufunuo. Tutajifunza pia namna maelezo ya nabii Danieli yalivyotoa habari zaidi juu ya serikali hizo miaka mingi mbele zianze kutawala.

      VICHWA VIWILI VYA KWANZA —MISRI NA ASIRIA

      7. Kichwa cha kwanza kinafananisha nini, na sababu gani hicho ndicho kichwa cha kwanza?

      7 Kichwa cha kwanza cha munyama kinafananisha Ufalme wa Misri. Ufalme wa Misri ulikuwa serikali kubwa ya kwanza ulimwenguni kuwachukia watu wa Mungu. Wazao wa Abrahamu ambao wangetokeza uzao ulioahidiwa walizidi kuongezeka katika inchi ya Misri. Kisha, Ufalme huo wa Misri ukaanza kuwatesa Waisraeli. Shetani alitaka kuwaangamiza watu wa Mungu mbele ili uzao huo usitokee. Namna gani? Kwa kumuchochea Farao awaue watoto wote wanaume wa Waisraeli. Yehova hakuruhusu jambo hilo litokee na aliwakomboa Waisraeli katika utumwa wa Misri. (Kut. 1:15-20; 14:13) Kisha akawapeleka Waisraeli katika Inchi ya Ahadi.

      8. Kichwa cha pili kinafananisha nini, na kilijaribu kufanya nini?

      8 Kichwa cha pili cha munyama kinafananisha serikali ya Asiria. Ufalme huo wenye nguvu ulijaribu pia kuwaangamiza watu wa Mungu. Kwa kweli, Yehova alitumia Asiria ili kuazibu ufalme wa makabila kumi ya Israeli kwa sababu ya uasi wao na ibada ya sanamu. Lakini, baadaye Asiria ilishambulia Yerusalemu. Inaonekana kama Shetani alitafuta kuangamiza kizazi ambacho kingetokeza Mufalme, Yesu Kristo. Yehova hakutaka majeshi ya Asiria yaharibu Yerusalemu, kwa hiyo aliharibu majeshi ya Asiria na kuwakomboa watu wake.​—2 Fal. 19:32-35; Isa. 10:5, 6, 12-15.

      KICHWA CHA TATU—BABILONI

      9, 10. (a) Yehova aliwaruhusu Wababiloni wafanye nini? (b) Ni mambo gani ambayo yalipaswa kutokea ili unabii utimie?

      9 Kichwa cha tatu kinafananisha ufalme ambao muji wake mukubwa ulikuwa Babiloni. Yehova aliruhusu Wababiloni waharibu Yerusalemu na kuwapeleka watu wake wafungwa huko Babiloni. Mbele ya kutokea kwa uharibifu huo, Yehova aliwaonya Waisraeli waasi kama musiba huo ungewapata. (2 Fal. 20:16-18) Yehova aliwaambia Waisraeli kama hataruhusu tena kizazi cha wafalme wao walioketi juu ya ‘kiti chake cha ufalme’ huko Yerusalemu waendelee kufanya hivyo. (1 Nya. 29:23) Lakini, Yehova aliahidi pia kama kungekuwa muzao wa Mufalme Daudi aliye na “haki ya kisheria,” ambaye angekuja na kuketi juu ya kiti cha ufalme cha Yehova.​—Eze. 21:25-27.

      10 Unabii mwengine ulionyesha kama wakati Masiya, ao Mutiwa​-mafuta atafika, Wayahudi watakuwa wangali wanaabudu katika hekalu la Yerusalemu. (Dan. 9:24-27) Unabii mwengine ulioandikwa mbele Waisraeli wapelekwe Babiloni, ulionyesha kama Masiya angezaliwa Bethlehemu. (Mika 5:2) Ili unabii huo mbalimbali utimie, iliomba Wayahudi watoke Babiloni, warudi katika inchi yao na wajenge tena hekalu. Lakini, Wababiloni walijulikana kuwa watu wasioachilia wafungwa. Kwa hiyo, namna gani watu wa Mungu wangerudi kwao? Yehova alifunulia manabii wake jambo ambalo angefanya.​—Amo. 3:7.

      11. Utawala wa Babiloni ulifananishwa na nini? (Soma maelezo yaliyo chini kwenye ukurasa wa 10.)

      11 Nabii Danieli alikuwa kati ya wafungwa waliopelekwa Babiloni. (Dan. 1:1-6) Yehova alimuonyesha serikali kubwa za ulimwengu ambazo zingetokea kisha serikali ya Babiloni kuanguka. Yehova alitumia mifano mbalimbali ili kufunua siri hizo. Kwa mufano, alimufanya Mufalme Nebukadneza wa Babiloni aote ndoto na katika ndoto hiyo Yehova alimuonyesha sanamu kubwa yenye sehemu mbalimbali. (Soma Danieli 2:1, 19, 31-38.) Kupitia nabii wake Danieli, Yehova alifunua kama kichwa cha zahabu cha sanamu hiyo kilifananisha Utawala wa Babiloni.b Kifua na mikono ya feza vilifananisha serikali kubwa ya ulimwengu ambayo ingetokea kisha ile ya Babiloni. Hiyo ingekuwa serikali gani, na ingewatendea namna gani watu wa Mungu?

      KICHWA CHA INE​—UTAWALA WA WAMEDE NA WAPERSE

      12, 13. (a) Yehova alifunua mambo gani juu ya kuanguka kwa Utawala wa Babiloni? (b) Sababu gani tunaweza kusema kama utawala wa Wamede na Waperse unafananishwa kabisa na kichwa cha ine cha munyama-mwitu?

      12 Zaidi ya miaka mia moja mbele ya siku za Danieli, Yehova alimutolea nabii Isaya maelezo juu ya utawala wa ulimwengu ambao ungeangusha utawala wa Babiloni. Yehova alionyesha namna muji wa Babiloni ungeharibiwa na pia jina la kiongozi ambaye angeshinda Babiloni. Kiongozi huyo aliitwa Sirisi ao Koreshi, Muperse. (Isa. 44:28–45:2) Danieli aliona maono mengine mawili kuhusu Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Wamede na Waperse. Katika maono ya kwanza, ufalme huo ulifananishwa na dubu aliyeinuliwa upande mumoja. Munyama huyo aliruhusiwa ‘kula nyama nyingi.’ (Dan. 7:5) Katika maono mengine, Danieli aliona utawala huo wenye sehemu mbili ukifananishwa na kondoo-dume mwenye pembe mbili.​—Dan. 8:3, 20.

      13 Yehova alitumia utawala wa Wamede na Waperse kushinda Babiloni na kuwarudisha Waisraeli katika inchi yao kama alivyoahidi. (2 Nya. 36:22, 23) Lakini, baadaye utawala huohuo ulijaribu kuwaangamiza watu wa Mungu. Kitabu cha Esta kinaeleza makusudi mabaya ya waziri mukubwa wa Waperse aliyeitwa Hamani. Alifanya mupango wa kuwaangamiza Wayahudi wote walioishi katika utawala huo wa Waperse na aliweka tarehe ya maangamizi hayo makubwa. Yehova aliwakomboa tena watu Wake na chuki ya Shetani juu ya uzao. (Esta 1:1-3; 3:8, 9; 8:3, 9-14) Kwa hiyo, tunaweza kusema kama Utawala wa Waperse unafananishwa kabisa na kichwa cha ine cha munyama-mwitu anayetajwa katika kitabu cha Ufunuo.

      KICHWA CHA TANO—UGIRIKI

      14, 15. Ni mambo gani ambayo Yehova alifunua juu ya Utawala wa Ugiriki?

      14 Katika kitabu cha Ufunuo kichwa cha tano cha munyama-mwitu kinafananisha Ugiriki (Grèce). Alipofasiria ndoto ya Nebukadneza, Danieli alionyesha kama utawala huohuo unafananishwa na tumbo na kiuno cha sanamu. Danieli alipokea tena maono mawili yaliyokuwa na maelezo zaidi juu ya ufalme wa Ugiriki na mutawala wake mwenye nguvu zaidi.

      15 Katika moja ya maono hayo, Danieli aliona ufalme wa Ugiriki ukifananishwa na chui aliyekuwa na mabawa mane, hilo lilionyesha kama utawala huo ungeshinda kwa uharaka falme zingine. (Dan. 7:6) Katika maono mengine, Danieli alieleza namna mbuzi​-dume mwenye pembe kubwa alivyovunja​-vunja kondoo​-dume mwenye pembe mbili, maana yake, Utawala wa Wamede na Waperse. Yehova alimuambia Danieli kama mbuzi​-dume huyo alifananisha Utawala wa Ugiriki na pembe kubwa ilifananisha mumoja wa wafalme wa utawala huo. Danieli alionyeshwa pia kama pembe hiyo kubwa ingevunjika, na pembe ine ndogo zingesimama mahali pa pembe hiyo kubwa. Hata ikiwa unabii huo uliandikwa mamia ya miaka mbele ya kutokea kwa Utawala wa Ugiriki, maelezo yote ya unabii huo yalitimia kabisa. Mufalme mwenye nguvu zaidi wa Ugiriki, Alexandre le Grand, alishambulia Utawala wa Wamede na Waperse. Pembe hiyo kubwa ilivunjika wakati mufalme huyo mwenye nguvu zaidi alikufa kwa gafula akiwa tu na umri wa miaka 32. Kisha, majenerali wake wane wakagawanyana utawala huo.​—Soma Danieli 8:20-22.

      16. Mufalme Antiokisi wa 4 alifanya nini?

      16 Kisha kushinda Waperse, Ugiriki ilianza kutawala watu wa Mungu. Wakati huo Wayahudi walikuwa wamekwisha rudi katika inchi yao na kujenga tena hekalu la Yerusalemu. Waisraeli walikuwa bado wachaguliwa wa Mungu na walikuwa wangali wakimuabudu Yehova katika hekalu ambalo walijenga upya, mahali ambapo Yehova alikubali aabudiwe. Hata hivyo, katika kipindi cha kuanzia mwaka wa 101 mupaka mwaka wa 200 mbele ya Kristo, Ugiriki, ni kusema, kichwa cha tano cha munyama​-mwitu, iliwashambulia watu wa Mungu. Mufalme Antiokisi wa 4, aliyekuwa mumoja wa wale walioriti utawala uliogawanyika wa Alexandre, alijenga mazabahu ya kipagani katika uwanja wa hekalu la Yerusalemu na akasema kama mutu yeyote atakayefuata dini ya Wayahudi anapaswa kufa. Uzao wa Shetani ulichukia kabisa watu wa Mungu. Lakini, baadaye utawala mwingine ulichukua nafasi ya Utawala wa Ugiriki. Ni utawala gani ambao ungefananishwa na kichwa cha sita cha munyama-mwitu?

      KICHWA CHA SITA​—ROMA, ‘YENYE KUOGOPESHA NA YENYE KUTISHA’

      17. Kichwa cha sita kilitimiza sehemu gani ya maana ya unabii wa Mwanzo 3:15?

      17 Roma ilikuwa serikali kubwa ya ulimwengu wakati Yohana alipokea maono ya munyama​-mwitu. (Ufu. 17:10) Roma ilikuwa kichwa cha sita cha munyama​-mwitu na ilitimiza sehemu ya maana ya unabii wa Mwanzo 3:15. Shetani alitumia watawala wa Roma ili kuumiza kwa muda uzao “kwenye kisigino.” Namna gani? Walimushitaki Yesu kwa uongo kwa kusema kama aliwachochea watu waasi utawala wao na wakamutundika juu ya muti. (Mt. 27:26) Lakini, kidonda hicho kilipona bila kukawia kwa sababu Yehova alimufufua Yesu.

      18. (a) Yehova alichagua taifa gani jipya, na sababu gani? (b) Namna gani uzao wa nyoka uliendelea kuchukia uzao wa mwanamuke?

      18 Viongozi wa dini ya Wayahudi walisikilizana na watawala wa Roma ili kumuua Yesu, na Waisraeli wengi walimukataa. Kwa hiyo, Yehova alikataa taifa hilo la Israeli. (Mt. 23:38; Mdo. 2:22, 23) Kisha, akajichagulia taifa jipya, “Israeli wa Mungu.” (Gal. 3:26-29; 6:16) Taifa hilo lilikuwa kutaniko la Wakristo watiwa-mafuta, na liliundwa na Wayahudi na Watu wa Mataifa. (Efe. 2:11-18) Kisha kifo na ufufuo wa Yesu, uzao wa nyoka uliendelea kuchukia sana uzao wa mwanamuke. Mara nyingi, Roma ilijaribu kuangamiza sehemu ya pili ya uzao wa mwanamuke, yaani, kutaniko la Kikristo.c

      19. (a) Danieli anafasiria namna gani utawala wa sita wa ulimwengu? (b) Habari nyingine itajibu maulizo gani?

      19 Katika ndoto ambayo Danieli alimufasiriya Nebukadneza, Roma ilifananishwa na miguu ya chuma. (Dan. 2:33) Danieli aliona tena utawala mwengine ambao ungetokana na utawala wa Roma. (Soma Danieli 7:7, 8.) Kwa miaka mingi, Roma ilikuwa ‘yenye kuogopesha na yenye kutisha na yenye nguvu isiyo ya kawaida’ kuliko maadui wake. Hata hivyo, unabii ulionyesha kama “pembe kumi” zingetokea katika utawala huo na pembe nyingine, iliyokuwa ndogo, ingekuwa na nguvu kuliko zingine zote. Pembe hizo kumi zinafananisha nini, na pembe ndogo inafananisha nini? Ni sehemu gani ya sanamu kubwa ya Nebukadneza ambayo inalingana na pembe hiyo ndogo? Habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 14 itajibu maulizo hayo.

      [Maelezo ya chini]

      a Mwanamuke huyo anafananisha tengenezo la Yehova la malaika waaminifu. Biblia inalinganisha tengenezo hilo na muke wa Yehova.​—Isa. 54:1; Gal. 4:26; Ufu. 12:1, 2.

      b Katika kitabu cha Danieli, Utawala wa Babiloni unafananishwa na kichwa cha sanamu na pia katika kitabu cha Ufunuo utawala huo unafananishwa na kichwa cha tatu cha munyama​-mwitu. Ona kisanduku kwenye ukurasa wa 12-13.

      c Hata ikiwa Roma iliharibu Yerusalemu katika mwaka wa 70, huo haukuwa utimizo wa Mwanzo 3:15. Kwa sababu wakati huo, Israeli haikuwa tena taifa chaguliwa la Mungu.

  • Yehova Anafunua Mambo Ambayo “Lazima Yatendeke Upesi”
    Munara wa Mulinzi—2012 | Mwezi wa 6 15
    • Yehova Anafunua Mambo Ambayo “Lazima Yatendeke Upesi”

      ‘Ufunuo kupitia Yesu Kristo, ambao Mungu alimupa, kuwaonyesha watumwa wake mambo ambayo lazima yatendeke upesi.’​—UFU. 1:1.

      UNAWEZA KUJIBU NAMNA GANI?

      Ni sehemu gani za sanamu kubwa ya Danieli zinazofananisha Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika?

      Namna gani Yohana anaonyesha kama Serikali Kubwa ya Uingereza na Amerika ndio imetokeza Umoja wa Mataifa?

      Danieli na Yohana wanaeleza namna gani mwisho wa utawala wa wanadamu?

      1, 2. (a) Unabii wa Danieli na wa Yohana unatusaidia kuelewa nini? (b) Vichwa sita vya kwanza vya munyama-mwitu vinafananisha nini?

      UNABII wa Danieli na wa Yohana unapatana kwa njia inayotusaidia kuelewa mambo mengi yanayotokea katika ulimwengu leo na yale yatakayotokea wakati ujao. Maono ya Yohana ya munyama​-mwitu na maelezo ya Danieli juu ya munyama mwenye kuogopesha aliyekuwa na pembe kumi, na mafasiriyo yake ya sanamu kubwa, yanatufundisha nini? Kuelewa vizuri maneno hayo ya kiunabii kutatuchochea kufanya nini?

      2 Habari ya kwanza tuliyojifunza ilizungumuzia maono ya Yohana ya munyama​-mwitu. (Ufu., sura ya 13) Tulijifunza kama vichwa sita vya kwanza vinafananisha serikali za Misri, Asiria, Babiloni, Utawala wa Wamede na Waperse, Ugiriki na Roma. Serikali hizo zote zilichukia uzao wa mwanamuke. (Mwa. 3:15) Kichwa cha sita, ni kusema, Roma kiliendelea kuutawala ulimwengu kwa miaka mingi kisha Yohana kuandika maono yake. Hata hivyo, mwishowe utawala mwengine, maana yake, kichwa cha saba, ungechukua nafasi ya Roma. Ni utawala gani huo ambao ulichukua nafasi hiyo, na ungetendea namna gani uzao wa mwanamuke?

      NAMNA SERIKALI YA UINGEREZA NA AMERIKA ILIVYOANZA

      3. Munyama mwenye kuogopesha na aliye na pembe kumi anafananisha nini, na pembe kumi zinafananisha nini?

      3 Ili kuelewa maana ya kichwa cha saba cha munyama​-mwitu anayetajwa katika Ufunuo sura ya 13, tunapaswa kulinganisha maono ya Yohana na maono ya Danieli inayozungumuzia munyama mwenye kuogopesha aliye na pembe kumi.a (Soma Danieli 7:7, 8, 23, 24.) Munyama huyo ambaye Danieli aliona anafananisha Serikali kubwa ya Ulimwengu ya Roma. (Ona kisanduku kwenye ukurasa wa 12-13.) Katika kipindi cha miaka 500 kisha Yesu, Utawala wa Roma ulianza kugawanyika. Pembe kumi za munyama huyo mwenye kuogopesha zinafananisha falme zilizotokana na utawala huo.

      4, 5. (a) Pembe ndogo ilifanya nini? (b) Kichwa cha saba cha munyama-mwitu kinafananisha nini?

      4 Katika maono yake ya munyama mwenye pembe kumi ao falme kumi, Danieli aliona pembe ingine, “ndogo,” ikitokea na kuchukua nafasi ya pembe tatu. Hilo lilitimia wakati Uingereza, iliyokuwa sehemu ndogo iliyotokana na Utawala wa Roma, ilifikia kuwa ufalme wenye nguvu. Espagne, Hollande, na France zilikuwa pia sehemu ya Utawala wa Roma. Kufikia miaka ya 1600, inchi hizo zilikuwa na nguvu sana kuliko Uingereza. Hata hivyo, Uingereza ikazishinda inchi hizo zote na kuwa ufalme wenye nguvu na wa maana kuliko falme hizo. Katika miaka ya 1700, Uingereza ilianza kuwa serikali kubwa na yenye nguvu sana duniani. Lakini mupaka hapo ilikuwa bado haijakuwa kichwa cha saba cha munyama​-mwitu.

      5 Ijapokuwa Uingereza ilipata nguvu sana, sehemu za Amerika ya kaskazini zilizokuwa zikitawaliwa na Uingereza, ziliasi na kuunda muungano wa Amerika. Hata hivyo, Uingereza haikuzuia Amerika kuwa inchi yenye nguvu, na ililinda wanajeshi wa maji wa Amerika. Kisha, siku ya Bwana kuanza katika mwaka 1914, Uingereza ilikuwa na nguvu sana na ikajulikana sana katika historia na Amerika ikawa tajiri sana duniani.b Wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, Amerika ilifanya urafiki wa pekee na Uingereza. Basi kichwa cha saba cha munyama kikawa Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika. Namna gani kichwa hiki kilitendea uzao wa mwanamuke?

      6. Kichwa cha saba kimewatendea namna gani watu wa Mungu?

      6 Siku chache kisha siku ya Bwana kuanza, kichwa cha saba kilianza kushambulia watu wa Mungu, ni kusema, ndugu za Kristo waliokuwa wangali duniani. (Mt. 25:40) Yesu alionyesha kama wakati wa kuwapo kwake, ndugu zake, ni kusema, mabaki ya uzao, wangekuwa wenye kufanya kazi nyingi duniani. (Mt. 24:45-47; Gal. 3:26-29) Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika ilianza kushambulia watakatifu hao. (Ufu. 13:3, 7) Wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, serikali hiyo iliwatesa watu wa Mungu, ikakataza vitabu vyao, na ikawafunga wawakilishi wa mutumwa mwaminifu. Kwa kipindi fulani ilionekana kama vile kichwa hicho cha saba kiliua kazi ya kuhubiri. Yehova alikuwa amekwisha kuona matukio hayo ya ajabu na alimufunulia Yohana mambo hayo. Tena, Mungu alimuambia Yohana kama sehemu ya pili ya uzao ingepata tena nguvu ili kumutumikia Yehova zaidi. (Ufu. 11:3, 7-11) Historia ya watumishi wa Yehova wa kisasa inaonyesha kama mambo hayo yalitendeka.

      SERIKALI KUBWA YA ULIMWENGU YA UINGEREZA NA AMERIKA NA MIGUU YA CHUMA NA UDONGO

      7. Ni sehemu gani ya munyama mwenye vichwa saba anayetajwa katika unabii wa Yohana inayolingana na sanamu kubwa inayotajwa katika unabii wa Danieli?

      7 Ni sehemu gani ya munyama mwenye vichwa saba anayetajwa katika unabii wa Yohana inayolingana na sanamu kubwa inayotajwa katika unabii wa Danieli? Ni serikali ya Uingereza na Amerika iliyotokana na Utawala wa Roma. Basi, tuseme nini kuhusu miguu ya sanamu ya Danieli? Miguu hiyo, ilionekana kuwa muchanganyiko wa chuma na udongo. (Soma Danieli 2:41-43.) Muchanganyiko wa chuma na udongo ulitokea wakati kichwa cha saba, ni kusema, Uingereza na Amerika, kilianza kuwa Serikali Kubwa ya Ulimwengu. Kama vile tu chuma inapochangana na udongo inatoa chombo kilicho zaifu, ndivyo, Serikali Kubwa ya Uingereza na Amerika ni zaifu kuliko Roma. Hilo lilionekana namna gani?

      8, 9. (a) Namna gani serikali kubwa ya saba ilionekana kuwa nguvu kama chuma? (b) Udongo wa miguu ya sanamu kubwa unafananisha nini?

      8 Kisha wakati fulani, kichwa cha saba cha munyama kilitenda kama chuma. Kwa mufano, kilionyesha nguvu zake kwa kushinda Vita ya Kwanza ya Ulimwengu. Wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu, Serikali Kubwa ya Uingereza na Amerika ilikuwa nguvu kama chuma.c Kisha vita hiyo, kichwa cha saba kiliendelea kwa wakati fulani kuwa nguvu kama chuma. Lakini, kuanzia mwanzo na kuendelea, utawala huo ulio kama chuma umechanganywa na udongo.

      9 Kwa miaka mingi watumishi wa Yehova walitafuta kuelewa maana ya miguu ya sanamu kubwa inayozungumuziwa katika kitabu cha Danieli. Danieli 2:41 inaonyesha kama muchanganyiko wa chuma na udogo unafanisha “ufalme” mumoja, wala si falme nyingi. Kwa hiyo, udongo unafananisha sehemu ao mambo mengine yenye kuleta migawanyiko mahali pote ambapo Serikali Kubwa ya Uingereza na Amerika inatawala; na sehemu hizo ao mambo hayo yanafanya serikali hiyo iwe zaifu ao zinapunguza nguvu zake za kutenda kuliko serikali ya Roma ambayo inafananishwa na miguu ya chuma. Unabii wa Danieli unasema kama udongo unamaanisha “uzao wa wanadamu,” ao watu wa kawaida. (Dan. 2:43) Mahali pote Serikali Kubwa ya Uingereza na Amerika inapotawala, watu wanaregeza nguvu ya serikali hiyo kwa kuomba haki zao ziheshimiwe; wanafanya hivyo kupitia, kampanye za kutetea haki za raia, vyama vya wafanya​-kazi, na vyama vya kupigania uhuru. Watu wa kawaida wanaregeza uwezo wa Serikali Kubwa ya Ulimwengu, ni kusema, Uingereza na Amerika, na kuifanya isitende tena kama ilivyokuwa ikitenda hapo mwanzoni kama chuma. Tena, kwa sababu ni sehemu tu ya watu ndio imemuchagua kiongozi wakati wa uchaguzi na pia kwa sababu ya maoni tofauti ya kisiasa ya wenye kupinga, hata viongozi wenye kupendwa sana na wanainchi hawana uwezo wa kutimiza mipango yao ao mambo waliyoahidi. Danieli alitabiri kama ‘sehemu moja ya ufalme huo itakuwa yenye nguvu na nyingine itakuwa zaifu.’​—Dan. 2:42; 2 Tim. 3:1-3.

      10, 11. (a) “Miguu” ya sanamu itapatwa na nini? (b) Je, hesabu ya vidole ina maana yoyote ya kiunabii? Fasiria.

      10 Leo, Uingereza na Amerika zimeendelea kuwa marafiki, na mara nyingi zinatumika pamoja ili kushugulikia mambo ya ulimwengu. Unabii unaozungumuzia sanamu kubwa na munyama​-mwitu unaonyesha kama hakuna serikali nyingine kubwa ya ulimwengu itakayochukua nafasi ya Serikali Kubwa ya Uingereza na Amerika. Serikali ya Uingereza na Amerika inaweza kuwa zaifu kuliko Roma inayofananishwa na miguu ya chuma, lakini nafasi yake haitachukuliwa na serikali nyingine.

      11 Je, hesabu ya vidole vya miguu ya sanamu hiyo kubwa, ina maana fulani ya pekee? Fikiria jambo hili: Katika maono mengine, Danieli anazungumuzia hesabu fulani​—kwa mufano, hesabu ya pembe juu ya vichwa vya wanyama mbalimbali. Hesabu hizo zina maana fulani. Lakini, anapozungumuzia sanamu hiyo, Danieli hataje hesabu ya vidole kwenye miguu. Kwa hiyo, inaonekana kama hesabu hiyo haina maana yoyote kama vile hesabu ya mikono, vidole vya mikono, na miguu ya sanamu haina maana yoyote. Danieli anaonyesha tu kama vidole hivyo vya miguu vinafanyizwa kwa chuma na udongo. Kupitia mafasiriyo hayo, tunaweza kusema kama Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika ndiyo serikali itakayokuwa ikitawala wakati lile “jiwe,” maana yake, Ufalme wa Mungu, litavunja miguu ya sanamu hiyo.​—Dan. 2:45.

      UINGEREZA NA AMERIKA NA MUNYAMA​-MWITU MWENYE PEMBE MBILI

      12, 13. Munyama-mwitu mwenye pembe mbili anafananisha nini, na anafanya nini?

      12 Ijapokuwa Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika ni muchanganyiko wa chuma na udongo, mambo ambayo Yesu alimuonyesha Yohana katika Ufunuo yanaonyesha kama serikali hiyo ingeendelea kuonyesha nguvu yake katika mambo yanayotendeka katika siku za mwisho. Namna gani? Yohana aliona katika maono munyama​-mwitu mwenye pembe mbili anayesema kama joka kubwa. Munyama huyo asiye wa kawaida anafananisha nini? Munyama huyo ana pembe mbili, hiyo inamaanisha serikali mbili zenye nguvu zinazotumika pamoja. Yohana aliona tena Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika, lakini hapa inatimiza daraka fulani la kipekee.​—Soma Ufunuo 13:11-15.

      13 Munyama aliye na pembe mbili anawaambia watu wafanye sanamu ya yule munyama​-mwitu aliye na vichwa saba. Yohana aliandika kama sanamu hiyo ya munyama​-mwitu itatokea, kisha itapotea, na baadaye itatokea tena. Jambo hilo lilitokea wakati serikali ya Uingereza na Amerika ilianzisha shirika fulani ili kuunganisha mataifa ya ulimwengu na kuwakilisha serikali zingine za ulimwengu.d Shirika hilo lilitokea kisha Vita ya Kwanza ya Ulimwengu na lilitwa Shirika la Mataifa. Shirika hilo lilipotea wakati Vita ya Pili ya Ulimwengu ilianza. Wakati wa vita hiyo, watu wa Mungu walitangaza kama kulingana na unabii ulio katika Ufunuo, sanamu ya munyama-mwitu ingeinuka tena. Na ndivyo ilivyokuwa, iliinuka ikiwa na jina la Umoja wa Mataifa.​—Ufu. 17:8.

      14. Kwa sababu gani Yohana anasema kama sanamu ya munyama-mwitu ni ‘mufalme wa munane’?

      14 Yohana alisema kama sanamu ya munyama ni ‘mufalme wa munane.’ Katika maana gani? Sanamu hiyo ya munyama si kichwa cha munane cha munyama​-mwitu. Ni sanamu tu ya munyama​-mwitu huyo. Mamlaka yoyote ya sanamu hiyo inatokana na mataifa yanayofanyiza umoja huo, zaidi sana Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika. (Ufu. 17:10, 11) Lakini, Yohana anasema kama sanamu hiyo ya munyama ni ‘mufalme’ kwa sababu sanamu hiyo inapata mamlaka ya kutenda mambo fulani yatakayobadilisha historia ya ulimwengu huu.

      SANAMU YA MUNYAMA INAMURARUA KAHABA

      15, 16. Kahaba anafananisha nini, na ni jambo gani limetokea juu ya wale waliokuwa wakimutegemeza?

      15 Yohana alizungumuzia mwanamuke kahaba, ambaye anaketi juu ya munyama​-mwitu mwenye rangi nyekundu na kumuongoza. Munyama huyo ndiye sanamu ya munyama​-mwitu mwenye vichwa saba. Kahaba huyo anaitwa ‘Babiloni Mukubwa.’ (Ufu. 17:1-6) Kahaba huyo anafananisha dini zote za uongo, zaidi sana dini zinazojiita kuwa za Kikristo. Dini za uongo zimeendelea kutegemeza sanamu ya munyama-mwitu, yaani, Umoja wa Mataifa, na kujaribu kuongoza shirika hilo.

      16 Lakini, katika siku ya Bwana, maji ya Babiloni Mukubwa yangekauka kabisa; maji hayo yanamaanisha watu wanaomutegemeza. (Ufu. 16:12; 17:15) Kwa mufano, wakati sanamu ya munyama ilitokea kwa mara ya kwanza, dini zinazojiita kuwa za Kikristo, ambazo ni sehemu kubwa ya Babiloni Mukubwa, zilikuwa na nguvu katika inchi za Ulaya. Lakini leo, watu wengi hawaheshimu tena dini na viongozi wa kidini na hawaziunge tena mukono. Kwa kweli, watu wengi leo wanasema kama dini zimekuwa chanzo cha vita mbalimbali na matatizo katika ulimwengu. Wengine hata wanasema waziwazi kama inafaa kukataza dini ulimwenguni.

      17. Dini ya uongo itapatwa na nini hivi karibuni, na kwa nini?

      17 Hata hivyo, dini ya uongo haitapoteza tu nguvu yake polepole na kisha imalizike. Kahaba ataendelea kuwa na nguvu, na atajaribu kuwavuta wafalme wafanye mapenzi yake mupaka wakati Mungu atatia katika mioyo ya wafalme hao wazo fulani. (Soma Ufunuo 17:16, 17.) Hivi karibuni, Yehova atachochea watawala wa dunia hii inayotawaliwa na Shetani, wanaowakilishwa na Umoja wa Mataifa, washambulie dini ya uongo. Wataharibu mali ya kahaba huyo na hataweza tena kuwatawala wafalme wa dunia. Miaka 20 ao 30 iliyopita, jambo hilo lingeweza kuonekana kama haliwezekane. Lakini, mambo yameanza kubadilika. Leo, kahaba ni kama mwenye kuyumbayumba juu ya mugongo wa munyama mwenye rangi nyekundu. Hata hivyo, kahaba huyo hataendelea kumuikalia ao kumuongoza munyama-mwitu milele. Uharibifu wake utakuwa mukubwa na utatokea kwa gafula.​—Ufu. 18:7, 8, 15-19.

      KUHARIBIWA KWA MUNYAMA-MWITU

      18. (a) Munyama-mwitu atafanya nini, na matokeo yatakuwa nini? (b) Ni serikali gani zitakazoharibiwa na Ufalme wa Mungu kulingana na Danieli 2:44? (Soma kisanduku kilicho kwenye ukurasa wa 17.)

      18 Kisha kuharibiwa kwa dini ya uongo, munyama-mwitu, ni kusema, serikali za kidunia zinazoongozwa na Shetani, atachochewa ili ashambulie Ufalme wa Mungu. Kwa kuwa hawawezi kufika mbinguni, wafalme wa dunia watawashambulia vikali watumishi wa Mungu walio duniani, kwa sababu wao wanaunga mukono Ufalme wa Mungu. Hapo sasa vita ya mwisho ya Mungu itapiganwa. (Ufu. 16:13-16; 17:12-14) Danieli anazungumuzia jambo fulani juu ya vita hiyo ya mwisho. (Soma Danieli 2:44.) Munyama​-mwitu anayetajwa katika Ufunuo 13:1, sanamu yake, na munyama​-mwitu mwenye pembe mbili, zitaharibiwa.

      19. Tunaweza kuwa na uhakika gani, na sasa ndio wakati wa kufanya nini?

      19 Tunaishi katika siku za utawala wa kichwa cha saba. Hakuna kichwa kingine kitakachotokea kwenye munyama mwitu huyo kabla hajaharibiwa. Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika itaendelea kutawala dunia wakati dini ya uongo itaangamizwa. Kila jambo lililoelezwa katika unabii wa Danieli na wa Yohana, limetimia kwelikweli. Kwa hiyo, tunaweza kuwa hakika kama uharibifu wa dini ya uongo na pia vita ya Har-Magedoni vitatukia karibuni. Mungu ametujulisha mambo hayo mbele ya wakati. Je, tutatii maonyo hayo ya kiunabii? (2 Pet. 1:19) Sasa ndio wakati wa kujiweka upande wa Yehova na kuunga mukono Ufalme wake.​—Ufu. 14:6, 7.

      [Maelezo ya chini]

      a Katika Biblia namba kumi inatumiwa ili kuonyesha kitu kilicho kamili ao chenye kuenea. Kwa hiyo, katika unabii huu namba kumi inafananisha falme zote zilizotokana na Utawala wa Roma.

      b Uingereza na Amerika zilianza katika miaka ya 1700. Lakini, maono ya Yohana yalionyesha kama serikali kubwa hiyo ingetokea mwanzoni mwa siku ya Bwana. Maono ya kitabu cha Ufunuo yalitimia katika “siku ya Bwana.” (Ufu. 1:10) Uingereza na Amerika zilianza kutumika pamoja zikiwa serikali kubwa ya dunia wakati Vita ya Kwanza ya Ulimwengu ilianza.

      c Danieli aliona mbele ya wakati namna serikali hiyo ingetokeza uharibifu mukubwa wakati wa vita hiyo, kwa hiyo aliandika hivi: “Naye atasababisha uharibifu kwa njia [yenye kuogopesha].” (Dan. 8:24) Kwa mufano, Amerika ilitupia adui zao bombe mbili za atomike na hilo lilitokeza uharibifu mukubwa sana ambao ulikuwa bado haujafanyika.

      d Soma Ufunuo​—Upeo Wake Mutukufu U Karibu! ukurasa wa 240, 241, 253.

      [Sanduku katika ukurasa wa 17]

      “FALME HIZI ZOTE” NI FALME GANI?

      Andiko la Danieli 2:44 linasema kama Ufalme wa Mungu “utazivunja na kuzikomesha falme hizi zote.” Unabii huo unazungumuzia tu falme zote zinazofananishwa na sehemu mbalimbali za sanamu ambayo mufalme Nebukadneza alilota.

      Tuseme nini kuhusu serikali zingine zote za wanadamu? Kitabu cha Ufunuo kinazungumuzia pia wafalme na kinatoa maelezo zaidi. Kitabu hicho kinaonyesha kama “wafalme wa dunia nzima inayokaliwa” watakusanywa ili kupigana na Yehova katika ‘siku kubwa ya Mungu Mweza-Yote.’ (Ufu. 16:14; 19:19-21) Kwa hiyo, kwenye Har-Magedoni si zile serikali tu zinazofananishwa na sehemu mbalimbali za sanamu ndizo zitaharibiwa, lakini serikali zingine zote za wanadamu zitaharibiwa pia.

  • Wafalme Wanane Wanafunuliwa
    Munara wa Mulinzi—2012 | Mwezi wa 6 15
    • Wafalme Wanane Wanafunuliwa

      Vitabu vya Biblia vya Danieli na Yohana vinazungumuzia wafalme wanane ao utawala wa wanadamu na namna wafalme hao wangefuatana. Ili kulewa unabii huo, tunapaswa kujua maana ya unabii wa kwanza wa Biblia.

      Kwa miaka mingi, Shetani amefanya uzao wake utokeze serikali za kila namna ao falme nyingi. (Lu. 4:5, 6) Lakini, serikali fulani kati ya hizo zimewatesa watu wa Mungu, ni kusema, taifa la Israeli ao Wakristo watiwa-mafuta. Ndiyo maana, maono ya Danieli na Yohana yanataja tu serikali kubwa munane za ulimwengu, hata kama dunia imetawaliwa na serikali nyingi.

      [Muchoro/​Picha kwenye ukurasa wa 12, 13]

      (Ili kuona maelezo hayo, ona kitabu)

      UNABII KATIKA UNABII KATIKA

      KITABU CHA DANIELI KITABU CHA UFUNUO

      1. Misri

      2. Asiria

      3. Babiloni

      4. Utawala wa Wamede na Waperse

      5. Ugiriki

      6. Roma

      7. Uingereza na Amerikaa

      8. Ushirika wa Mataifa

      na Umoja wa Mataifab

      WATU WA MUNGU

      Mwaka wa 2000,

      Mbele ya kuzaliwa kwa Yesu

      Abrahamu

      Mwaka wa 1500

      Taifa la Israeli

      Mwaka wa 1000

      Danieli Mwaka wa 500

      Mbele ya kuzaliwa kwa Yesu/

      Kisha kuzaliwa kwa Yesu

      Yohana

      Israeli wa Mungu Mwaka wa 500

      Mwaka wa 1000

      Mwaka wa 1500

      Mwaka wa 2000,

      Kisha kuzaliwa kwa Yesu

      [Maelezo ya chini]

      a Wafalme hao wawili wangetokea katika wakati wa mwisho. Ona ukurasa wa 19.

      b Wafalme hao wawili wangetokea katika wakati wa mwisho. Ona ukurasa wa 19.

      [Picha]

      Sanamu kubwa (Dan. 2:31-45)

      Wanyama wane wanaotoka katika bahari (Dan. 7:3-8, 17, 25)

      Kondoo-dume na mbuzi-dume (Dan., sura 8)

      Munyama-mwitu mwenye vichwa saba (Ufu. 13:1-10, 16-18)

      Munyama mwenye pembe mbili anawaambia watu wafanye sanamu ya munyama-mwitu mwenye vichwa saba (Ufu. 13:11-15)

      [Picha zimetolewa na]

      Photo credits: Misri na Roma: British Museum ilituruhusu kutumia picha hii; Utawala wa Wamede na Waperse: Musée du Louvre, Paris

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine