-
“Mufalme wa Kaskazini” Katika Wakati wa MwishoMunara wa Mulinzi (Gazeti la Funzo)—2020 | Mwezi wa 5
-
-
HABARI YA KUJIFUNZA YA 19
“Mufalme wa Kaskazini” Katika Wakati wa Mwisho
“Katika wakati wa mwisho mufalme wa kusini atasukumana naye [mufalme wa kaskazini].”—DA. 11:40.
WIMBO 150 Mtafute Mungu Upate Ukombozi
KIFUPI CHA HABARIa
1. Unabii wa Biblia unatusaidia kujua nini?
NI NINI itapata watu wa Yehova hivi karibuni? Hatuna lazima ya kuwazia-wazia mambo. Unabii wa Biblia unatusaidia kujua mambo ya maana yenye itatupata sisi wote. Kuko unabii fulani wenye unatusaidia kujua mambo yenye serikali fulani za nguvu zaidi ku dunia zitafanya. Unabii huo unapatikana katika Danieli sura ya 11. Unazungumuzia historia ya wafalme wawili wenye kushindana, ni kusema, mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini. Sehemu kubwa ya unabii huo imekwisha kutimia, kwa hiyo, tunaweza kuwa hakika kama sehemu yenye kubakia itatimia pia.
2. Kulingana na Mwanzo 3:15 na Ufunuo 11:7 na 12:17, ni mambo gani ya maana yenye tunapaswa kukumbuka wakati tunajifunza unabii wa Danieli?
2 Ili tuelewe unabii wenye unapatikana katika Danieli sura ya 11, tunapaswa kujua kama unabii huo unazungumuzia tu watawala na serikali zenye zimetawala inchi kwenye watu wa Mungu waliishi, ao zenye zimeshambulia watu wa Mungu. Na hata kama watumishi wa Mungu wako kidogo sana ku dunia, mara mingi serikali za ulimwengu zinawatesa. Juu ya nini? Juu kusudi kubwa la Shetani na ulimwengu wake wote ni kuharibu wale wenye wanamutumikia Yehova na Yesu. (Soma Mwanzo 3:15 na Ufunuo 11:7; 12:17.) Tena, unabii wa Danieli unapaswa kupatana na unabii mwingine wa Biblia. Na tunapaswa kulinganisha unabii wa Danieli na sehemu zingine za Biblia ili tuelewe muzuri unabii huo.
3. Tutazungumuzia nini mu habari hii na mu habari yenye kufuata?
3 Kwa hiyo, tutazungumuzia sasa Danieli 11:25-39. Tutaona mufalme wa kaskazini alikuwa nani na mufalme wa kusini alikuwa nani kuanzia mwaka wa 1870 mupaka mwaka wa 1991, na tutaona juu ya nini ni muzuri tubadilishe namna tulikuwa tunaelewa sehemu moja ya unabii huo. Mu habari yenye kufuata, tutazungumuzia Danieli 11:40–12:1, na tutapata mafasirio ya mupya juu ya mambo yenye sehemu hiyo ya unabii inaonyesha kuhusu kipindi cha wakati kuanzia mwaka wa 1991 mupaka ku vita ya Armagedoni. Wakati unajifunza zile habari mbili, itakuwa muzuri uchunguze pia muchoro “Wafalme Wenye Kushindana Katika Wakati wa Mwisho.” Lakini, inafaa tujue kwanza wafalme hao wawili ni nani.
NAMNA YA KUTAMBUA MUFALME WA KASKAZINI NA MUFALME WA KUSINI
4. Ni mambo gani tatu yenye inatusaidia kutambua mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini?
4 Zamani, jina “mufalme wa kaskazini” lilizungumuzia mufalme mwenye alikuwa anatawala maeneo yenye ilikuwa kaskazini mwa Israeli na jina “mufalme wa kusini” lilizungumuzia mufalme mwenye alikuwa anatawala maeneo yenye ilikuwa kusini mwa Israeli. Juu ya nini tunasema vile? Juu malaika alimuambia Danieli hivi: “Nimekuja ili kukufanya uelewe mambo yenye yatapata watu wako [watu wa Mungu] katika kipindi cha mwisho cha zile siku.” (Da. 10:14) Kufikia Pentekoste ya 33 K.K.Y., taifa la Israeli la kimwili njo lilikuwa watu wa Mungu. Lakini, kuanzia wakati huo na kuendelea, Yehova alionyesha waziwazi kama wanafunzi waaminifu wa Yesu njo walikuwa sasa watu wake. Kwa hiyo, sehemu kubwa ya unabii wa Danieli sura ya 11 inahusu wanafunzi wa Kristo, hapana taifa la kimwili la Israeli. (Mdo. 2:1-4; Ro. 9:6-8; Gal. 6:15, 16) Na mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini wamebadilika-badilika kwa miaka mingi yenye imepita. Lakini, kuko mambo fulani yenye haikubadilika. Jambo la kwanza, wafalme hao walitawala inchi kwenye watu wa Mungu waliishi ao walishambulia watu wa Mungu. Jambo la pili, namna wametendea watu wa Mungu ilionyesha kama walimuchukia Mungu wa kweli, Yehova. Na jambo la tatu, wafalme hao wawili wamepigania mamlaka.
5. Je, kulikuwa mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini kati ya mwaka wa 100 na mwaka wa 1870? Fasiria.
5 Wakati fulani kisha mwaka wa 100, Wakristo wengi sana wa uongo walianza kuingia mu kutaniko la kweli la Kikristo; walifundisha mafundisho ya wapagani na kufanya kweli za Neno la Mungu zisikuwe wazi. Kuanzia wakati huo mupaka mwaka wa 1870, hapakukuwa kikundi cha watu wa Mungu wenye kupangwa muzuri ku dunia. Magugu, ni kusema, Wakristo wa uongo, waliongezeka sana na kufunika Wakristo wa kweli. (Mt. 13:36-43) Juu ya nini ni muzuri kujua jambo hilo? Juu jambo hilo linaonyesha kama mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini hawangekuwa watawala ao serikali zenye zilitawala kati ya mwaka wa 100 na mwaka wa 1870. Wakati huo hapakukuwa watu wa Mungu wenye kupangwa muzuri wenye wafalme hao wangeweza kushambulia.b Lakini, mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini wangetokea tena wakati kidogo kisha mwaka wa 1870. Juu ya nini tunasema vile?
6. Ni wakati gani watu wa Mungu walianza tena kuwa kikundi chenye kupangwa muzuri? Fasiria.
6 Kuanzia mwaka wa 1870, watu wa Mungu walianza tena kuwa kikundi chenye kupangwa muzuri. Ni katika mwaka huo njo Charles Taze Russell na wenzake walianzisha kikundi cha kujifunza Biblia. Ndugu Russell na wenzake walitimiza daraka la ule mujumbe mwenye alitabiriwa mwenye ‘alifungua njia’ mbele Ufalme wa Kimasiya usimamishwe. (Mal. 3:1) Yehova alikuwa tena sasa na kikundi cha watu wenye kupangwa muzuri! Je, kulikuwa serikali zenye zingeshambulia watumishi wa Mungu wakati huo? Acha tuone.
MUFALME WA KUSINI NI NANI?
7. Ni nani alikuwa mufalme wa kusini wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu?
7 Kufikia mwaka wa 1870, Uingereza ilikuwa imekuwa serikali kubwa zaidi mu dunia, na ilikuwa na jeshi la nguvu zaidi mu dunia yote. Serikali hiyo ilifananishwa na pembe ya kidogo yenye ilishinda pembe zingine tatu, ni kusema, Ufaransa, Uhispania, na Uholanzi (Pays-Bas). (Da. 7:7, 8) Na serikali ya Uingereza ilikuwa mufalme wa kusini wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu. Wakati uleule, Inchi ya Amerika ilikuwa imekuwa inchi tajiri zaidi mu dunia na ilianza kushirikiana sana na Uingereza.
8. Ni nani amekuwa mufalme wa kusini mu kipindi chote cha siku za mwisho?
8 Wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, serikali ya Amerika na Uingereza ilifanya mapatano ya kijeshi na jeshi lao lilikuwa na nguvu sana. Wakati huo, Uingereza na Amerika ikakuwa marafiki sana na ikakuwa Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika. Kama vile Danieli alitabiri, mufalme huyo alijifanyia “jeshi kubwa sana na lenye nguvu.” (Da. 11:25) Mu siku za mwisho, serikali ya muungano ya Uingereza na Amerika imekuwa mufalme wa kusini.c Lakini sasa, ni nani amekuwa mufalme wa kaskazini?
MUFALME WA KASKAZINI ANATOKEA TENA
9. Ni wakati gani mufalme wa kaskazini alitokea tena, na namna gani Danieli 11:25 ilitimia?
9 Mu mwaka wa 1871, mwaka moja kisha Russell na wenzake kuanzisha kikundi chao cha kujifunza Biblia, mufalme wa kaskazini alitokea tena. Mwaka huo, Otto von Bismarck aliunganisha maeneo mingi na kuanzisha Utawala wa Ujerumani. Wilhelm wa Kwanza, mufalme wa eneo la Prussia, alikuwa mutawala wa kwanza wa utawala wa Ujerumani, na alimuweka Bismarck kuwa kiongozi wa serikali ya Ujerumani.d Mu miaka mingi yenye ilifuata, Ujerumani ilitawala inchi fulani katika Afrika na maeneo ya Bahari ya Pasifiki, na ilianza kushindana na Uingereza. (Soma Danieli 11:25.) Utawala wa Ujerumani ulifanya jeshi la nguvu na ulifikia kuwa na jeshi la pili mu dunia la maaskari wenye kupigana kwenye maji. Wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, Ujerumani ilitumia jeshi lake ili kupigana na maadui wake.
10. Namna gani Danieli 11:25b, 26 ilitimia?
10 Danieli alitabiri pia mambo yenye ingepata Utawala wa Ujerumani na jeshi lake. Unabii unasema kama mufalme wa kaskazini “hatasimama.” Sababu gani? “Kwa sababu watafanya mipango mibaya juu yake. Na wale wenye wanakula vyakula vyake vitamu watatokeza kuanguka kwake.” (Da. 11:25b, 26a) Wakati wa Danieli, wale wenye wanakula “vyakula vitamu vya mufalme” walitia ndani maofisa wakubwa wa mufalme wenye walikuwa ‘wanamutumikia mufalme.’ (Da. 1:5) Unabii huo unazungumuzia nani hapa? Unazungumuzia maofisa wa cheo cha juu katika Utawala wa Ujerumani, kutia ndani majenerali wa mutawala wa Ujerumani na washauri wa kijeshi, wenye walifikia kuangusha utawala huo.e Unabii haukusema tu kama utawala huo ungeanguka lakini ulionyesha pia matokeo ya vita yenye utawala huo ungepigana na mufalme wa kusini. Kuhusu mufalme wa kaskazini, unabii unasema hivi: “Lakini jeshi lake, litaharibiwa, na wengi watauawa.” (Da. 11:26b) Mu Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, sawa vile tu unabii ulisema, jeshi la Ujerumani ‘liliharibiwa’ ao kushindwa, na watu wengi ‘waliuawa.’ Watu wengi walikufa katika ile vita kuliko vita ingine yoyote ya mbele ya pale.
11. Mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini walifanya nini?
11 Andiko la Danieli 11:27, 28 linazungumuzia mambo yenye ingetokea mbele ya Vita ya Kwanza ya Ulimwengu. Linasema kama mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini ‘wangekaa kwenye meza moja wakiambiana uongo.’ Linasema pia kama mufalme wa kaskazini angejikusanyia “mali nyingi.” Ni vile mambo ilikuwa kabisa. Ujerumani na Uingereza waliambiana kama walitaka amani, lakini maneno yao ilionekana kuwa uongo wakati vita ilitokea mu mwaka 1914. Na mu miaka ya mbele ya mwaka wa 1914, Ujerumani ilifikia kuwa inchi ya pili yenye kuwa tajiri zaidi mu dunia. Kisha, ili kutimiza Danieli 11:29 na sehemu ya kwanza ya mustari wa 30, Ujerumani ilipigana na mufalme wa kusini lakini ilishindwa.
WAFALME HAO WANASHAMBULIA WATU WA MUNGU
12. Wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini walifanya nini?
12 Kuanzia mwaka wa 1914, wafalme hao wawili wameendelea kupigana kati yao na kushambulia watu wa Mungu tena na tena. Kwa mufano, wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, serikali ya Ujerumani na serikali ya Uingereza zilitesa watumishi wa Mungu, wenye walikataa kupigana vita. Na serikali ya Amerika ilitia ndani ya gereza ndugu wenye walikuwa wanaongoza kazi ya kuhubiri. Ile mateso ilitimiza unabii wa Ufunuo 11:7-10.
13. Mu miaka ya 1930 na wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu, mufalme wa kaskazini alifanya nini?
13 Kisha, mu miaka ya 1930 na zaidi sana wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu, mufalme wa kaskazini alishambulia watu wa Mungu bila huruma. Wakati chama cha Nazi kilianza kutawala Ujerumani, Hitler na wenzake walikataza kazi ya watu wa Mungu. Mufalme wa kaskazini aliua watumishi wengi wa Yehova na alituma maelfu mu kambi za mateso. Ile yote ilitabiriwa na Danieli. Mufalme wa kaskazini aliweza “kuchafua patakatifu” na “kuondoa zabihu ya kuendelea” kwa kuzuia kwa ukali watu wa Mungu wasisifu jina la Yehova waziwazi. (Da. 11:30b, 31a) Hitler, kiongozi wa chama cha Nazi alifikia hata kusema kama atamaliza watumishi wote wa Mungu katika Ujerumani.
MUFALME MUPYA WA KASKAZINI ANATOKEA
14. Ni nani alikuwa mufalme wa kaskazini kisha Vita ya Pili ya Ulimwengu? Fasiria.
14 Kisha Vita ya Pili ya Ulimwengu, serikali ya Kikomunisti ya Muungano wa Sovieti ilianza kutawala maeneo makubwa yenye ilikuwa imenyanganya Ujerumani, na ikakuwa mufalme wa kaskazini. Kama vile serikali ya kidikteta ya Nazi ilifanya, Muungano wa Sovieti ulitesa kila mutu mwenye alimutii Mungu wa kweli kuliko kutii serikali.
15. Mufalme wa kaskazini alifanya nini kisha Vita ya Pili ya Ulimwengu kumalizika?
15 Kisha tu Vita ya Pili ya Ulimwengu kumalizika, mufalme mupya wa kaskazini, ni kusema, Muungano wa Sovieti na inchi zenye kumuunga mukono, alishambulia watu wa Mungu. Kupatana na unabii wa Ufunuo 12:15-17, mufalme huyo alikataza kazi yetu ya kuhubiri na kupeleka maelfu ya watumishi wa Yehova mu uhamisho katika Siberia. Kwa kweli, katika kipindi chote cha siku za mwisho, mufalme wa kaskazini amemwanga “muto” wa mateso juu ya watu wa Mungu ili kujaribu kusimamisha kazi yao, lakini ameshindwa.f
16. Namna gani Muungano wa Sovieti ulitimiza unabii wa Danieli 11:37-39?
16 Soma Danieli 11:37-39. Ili kutimiza unabii huo, mufalme wa kaskazini ‘hakumuheshimia Mungu wa baba zake’ hata kidogo. Namna gani? Muungano wa Sovieti ulikuwa na kusudi la kuondoa dini zote, kwa hiyo, ulijaribu kuvunja mamlaka ya dini hizo. Tangu mwaka wa 1918, serikali ya Sovieti ilikuwa imetoa amri yenye ilifikia kufanya masomo ianze kufundisha wanafunzi kama hakuna Mungu. Namna gani mufalme huyo wa kaskazini ‘alimutukuza mungu wa ngome’? Muungano wa Sovieti ulitumia feza mingi ili kufanya jeshi lake likuwe nguvu na kutengeneza silaha mingi za nyuklia ili kutia nguvu mamlaka yake. Wote wawili, mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini, walifikia kujikusanyia silaha za nguvu zenye zinaweza kuua mamilioni ya watu!
MAADUI WAWILI WANATUMIKA PAMOJA
17. “Chukizo lenye linaleta uharibifu” ni nini?
17 Mufalme wa kaskazini ametumika pamoja na mufalme wa kusini katika jambo moja la maana. Walitumika pamoja ili ‘kusimamisha lile chukizo lenye linaleta uharibifu.’ (Da. 11:31) “Chukizo” hilo ni Umoja wa Mataifa.
18. Sababu gani Umoja wa Mataifa unaitwa “chukizo”?
18 Umoja wa Mataifa unaitwa “chukizo” kwa sababu unasema kama unaweza kufanya jambo fulani lenye Ufalme wa Mungu tu njo unaweza kufanya, ni kusema, kuleta amani mu dunia. Na unabii unasema kama chukizo hilo “linaleta uharibifu” kwa sababu Umoja wa Mataifa utashambulia na kuharibu dini zote za uongo.—Ona muchoro “Wafalme Wenye Kushindana Katika Wakati wa Mwisho.”
JUU YA NINI NI LAZIMA TUJUE HISTORIA HII?
19-20. (a) Juu ya nini ni lazima tujue historia hii? (b) Habari yenye kufuata itajibu ulizo gani?
19 Ni lazima tujue historia hii kwa sababu inaonyesha kama kuanzia mwaka wa 1870 mupaka mwaka wa 1991, unabii wa Danieli kuhusu mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini ulitimia. Njo maana tunaweza kuwa hakika kama sehemu yenye inabakia ya unabii huo itatimia pia.
20 Mu mwaka wa 1991, Muungano wa Sovieti ulianguka. Sasa, nani njo mufalme wa kaskazini leo? Habari yenye kufuata itajibu ulizo hilo.
WIMBO 128 Kuvumilia Mpaka Mwisho
a Tuko tunajionea mambo yenye kuhakikisha kama unabii wa Danieli juu ya “mufalme wa kaskazini” na “mufalme wa kusini” unaendelea kutimia. Juu ya nini tuko hakika na jambo hilo? Na juu ya nini tuko na lazima ya kuelewa mambo yenye unabii huo unazungumuzia?
b Juu ya sababu yenye kuonyeshwa hapa, haifae tena kusema kama Mutawala wa Roma Aurélien (270-275 K.K.Y.) alikuwa “mufalme wa kaskazini” ao kama Malkia wa Siria Zenobia (267-272 K.K.Y.) alikuwa “mufalme wa kusini.” Hii mafasirio inabadilisha mambo yenye ilichapishwa mu sura ya 13 na 14 ya kitabu Sikiliza Unabii wa Danieli!
d Mu mwaka wa 1890, Mufalme Wilhelm wa Pili alimuondoa Bismarck kwenye madaraka.
e Walifanya mambo mingi yenye ilifanya utawala huo uanguke haraka. Kwa mufano, waliacha kumutegemeza mufalme, walifunua habari za siri kuhusu vita, na walilazimisha mufalme aache madaraka.
f Kama vile Danieli 11:34 inaonyesha, kwa muda kidogo, mufalme wa kaskazini aliacha kutesa Wakristo wa kweli. Kwa mufano, ilikuwa vile wakati Muungano wa Sovieti ulianguka mu mwaka wa 1991.
-
-
Ni Nani “Mufalme wa Kaskazini” Leo?Munara wa Mulinzi (Gazeti la Funzo)—2020 | Mwezi wa 5
-
-
HABARI YA KUJIFUNZA YA 20
Ni Nani “Mufalme wa Kaskazini” Leo?
“Atakuja mupaka kwenye mwisho wake, na hakutakuwa mwenye atamusaidia.”—DA. 11:45.
WIMBO 95 Nuru Inazidi Kuongezeka
KIFUPI CHA HABARIa
1-2. Tutazungumuzia nini katika habari hii?
KULIKO zamani, leo tuko na mambo mingi yenye kuhakikisha kama tunaishi ku mwisho wa siku za mwisho za mupangilio huu wa mambo. Karibuni, Yehova na Yesu Kristo wataharibu serikali zote zenye zinapinga Ufalme wa Mungu. Mbele jambo hilo litokee, mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini wataendelea kupigana kati yao na kushambulia watu wa Mungu.
2 Katika habari hii, tutazungumuzia unabii wenye kupatikana mu Danieli 11:40–12:1. Tutajua mufalme wa kaskazini ni nani leo na tutaona juu ya nini hatupaswe kuogopa magumu yenye iko mbele.
MUFALME MUPYA WA KASKAZINI ANATOKEA
3-4. Ni nani mufalme wa kaskazini leo? Fasiria.
3 Kisha Muungano wa Sovieti kuanguka mu mwaka wa 1991, watu wa Mungu wenye walikuwa wanaishi katika eneo hilo kubwa walipata “musaada kidogo,” ni kusema, walipata uhuru kwa wakati fulani. (Da. 11:34) Kwa hiyo, waliweza kuhubiri kwa uhuru, na kisha wakati kidogo hesabu ya wahubiri iliongezeka sana mu inchi zenye zilikuwa sehemu ya Muungano wa Sovieti. Lakini, kisha miaka fulani, serikali ya Urusi na inchi zenye kuiunga mukono zilifikia kuwa mufalme wa kaskazini. Kama vile tulijifunza mu habari yenye kutangulia, kusudi serikali fulani ikuwe mufalme wa kaskazini ao mufalme wa kusini, inapaswa kufanya mambo tatu: (1) kutawala inchi kwenye watu wa Mungu wanaishi ao kuwashambulia, (2) kuonyesha kupitia matendo yake ao inamuchukia Yehova na watu wake, na (3) vkupigana na mufalme mwingine mushindani.
4 Ona sababu zenye zinatufanya tuseme kama serikali ya Urusi na inchi zenye kuiunga mukono njo mufalme wa kaskazini leo. (1) Zimeshambulia watu wa Mungu kwa kukataza kazi yao ya kuhubiri na kutesa mamia ya maelfu ya ndugu na dada wenye kuishi mu maeneo yenye wanaongoza. (2) Ile matendo yao inaonyesha kama wanamuchukia Yehova na watu wake. (3) Wameendelea kupigana na mufalme wa kusini, ni kusema, Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika. Tuone basi namna serikali ya Urusi na inchi zenye kuiunga mukono zimetimiza daraka la mufalme wa kaskazini.
MUFALME WA KASKAZINI NA MUFALME WA KUSINI WANAENDELEA KUSUKUMANA
5. Danieli 11:40-43 inazungumuzia kipindi gani cha wakati, na ni mambo gani inafanyika wakati huo?
5 Soma Danieli 11:40-43. Sehemu hii ya unabii inazungumuzia wakati wa mwisho. Inaonyesha namna mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini wanaendelea kushindana. Danieli alitabiri kama, katika wakati wa mwisho, mufalme wa kusini “atasukumana” na mufalme wa kaskazini, ao “atapigana mapembe naye.”—Da. 11:40; maelezo ya chini.
6. Ni nini inaonyesha kama wafalme wawili wameendelea kusukumana?
6 Mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini wanaendelea kushindana kwa sababu kila mumoja wao anapenda yeye njo atawale ulimwengu. Kwa mufano, fikiria mambo yenye ilitokea kisha Vita ya Pili ya Ulimwengu wakati Muungano wa Sovieti na inchi zenye kuunga mukono muungano huo zilianza kutawala sehemu kubwa ya Ulaya. Mufalme wa kusini alifanya mapatano na inchi zingine ili zitie pamoja majeshi yao juu ya kuanzisha shirika la kijeshi la kupiganisha mufalme wa kaskazini. Shirika hilo linaitwa Shirika la Makubaliano ya Atlantiki ya Kaskazini (OTAN). Mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini wanaendelea kushindana kwa kutumia feza mingi ili kutengeneza silaha za nguvu sana. Kila mumoja wao amepigana na mwingine kwa kutegemeza maadui wa mwenzake katika vita mu Afrika, Asia, na Amerika Latini. Mu miaka ya hivi karibuni, serikali ya Urusi na inchi zenye kuiunga mukono zimeeneza mamlaka yao mu dunia yote. Mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini wamepigana pia kwa kutumia ordinatere. Kila mumoja ameendelea kushitaki mwenzake kama iko anatumia programu za mubaya za ordinatere ili kufanya mwenzake apoteze feza na ili kuharibu serikali yake. Na kama vile Danieli alitabiri, mufalme wa kaskazini anaendelea kushambulia watu wa Mungu.—Da. 11:41.
MUFALME WA KASKAZINI ANAINGIA KATIKA “INCHI YA LILE PAMBO”
7. “Inchi ya lile Pambo” ni nini?
7 Danieli 11:41 inasema kama mufalme wa kaskazini ataingia katika “inchi ya lile Pambo.” Ni inchi gani? Zamani, ilikuwa inchi ya Israeli; inchi ya Israeli ilionwa kuwa “ya muzuri sana kuliko inchi zote.” (Eze. 20:6) Lakini ile inchi ilikuwa ya maana sana, zaidi sana kwa sababu ni pale watu walikuwa wanamuabudia Yehova. Kuanzia Pentekoste ya mwaka wa 33 K.K.Y., ile “inchi” haiko inchi fulani yenye kupatikana mahali fulani ku dunia, na haiwezi kuwa vile, kwa sababu watu wa Yehova wanapatikana mu dunia yote. Lakini, leo “inchi ya lile Pambo” ni eneo la mufano kwenye watu wa Yehova wanafanyia mambo ya kiroho sawa vile kumuabudu Yehova kupitia mikutano na kazi ya kuhubiri.
8. Namna gani mufalme wa kaskazini ameingia katika “inchi ya lile Pambo”?
8 Katika siku za mwisho, mufalme wa kaskazini ameingia mara mingi katika “inchi ya lile Pambo.” Kwa mufano, wakati serikali ya Ujerumani yenye ilikuwa inaongozwa na chama cha Nazi ilikuwa mufalme wa kaskazini, zaidi sana wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu, mufalme huyo aliingia katika “inchi ya lile Pambo” kwa kutesa na kuua watu wa Mungu. Kisha Vita ya Pili ya Ulimwengu, wakati Muungano wa Sovieti ulikuwa mufalme wa kaskazini, mufalme huyo aliingia katika “inchi ya lile Pambo” kwa kutesa watu wa Mungu na kuwapeleka mbali na makao yao.
9. Mu miaka ya hivi karibuni, namna gani serikali ya Urusi na inchi zenye kuiunga mukono zimeingia katika “inchi ya lile Pambo”?
9 Mu miaka ya hivi karibuni, serikali ya Urusi na inchi zenye kuiunga mukono zimeingia pia katika “inchi ya lile Pambo.” Namna gani? Mu mwaka wa 2017, mufalme huyu wa kaskazini amekataza kazi ya watu wa Yehova na kutia wamoja kati ya ndugu na dada zetu mu gereza. Pia, amekataza vichapo vyetu, na hata Tafsiri ya Ulimwengu Mupya. Tena, amenyanganya majengo ya biro yetu ya tawi katika Urusi na amenyanganya pia Majumba ya Ufalme na Majumba ya Mikusanyiko. Njo maana, mu mwaka wa 2018, Baraza Lenye Kuongoza limesema kama serikali ya Urusi na inchi zenye kuiunga mukono njo mufalme wa kaskazini. Lakini, hata wakati watu wa Yehova wanateswa kwa ukali, wanakataa kuunga mukono matendo yoyote ya kupinga serikali fulani ao kutafuta kuibadilisha. Kuliko kufanya vile, wanatii shauri la Biblia la kusali kwa ajili ya “wale wote wenye kuwa katika vyeo vya juu,” zaidi sana wakati watu hao wanakamata maamuzi yenye inahusu uhuru wa ibada.—1 Ti. 2:1, 2.
JE, MUFALME WA KASKAZINI ATASHINDA MUFALME WA KUSINI?
10. Je, mufalme wa kaskazini atashinda mufalme wa kusini? Fasiria.
10 Unabii wenye kupatikana katika Danieli 11:40-45 unazungumuzia zaidi sana mambo yenye mufalme wa kaskazini atafanya. Maana yake atashinda mufalme wa kusini? Hapana. Mufalme wa kusini atakuwa angali ‘muzima’ wakati Yehova na Yesu wataharibu serikali zote ku vita ya Armagedoni. (Ufu. 19:20) Juu ya nini tuko hakika na jambo hilo? Fikiria mambo yenye unabii wa kitabu cha Danieli na Ufunuo unaonyesha.
Wakati wa Armagedoni, Ufalme wa Mungu, wenye kufananishwa na jiwe, utamaliza utawala wa wanadamu, wenye kufananishwa na sanamu kubwa (Ona fungu la 11)
11. Unabii wa Danieli 2:43-45 unaonyesha nini? (Ona picha ku jalada la gazeti hili.)
11 Soma Danieli 2:43-45. Nabii Danieli anazungumuzia serikali mbalimbali zenye zilishambulia watu wa Mungu. Zinafananishwa na sehemu mbalimbali za sanamu kubwa ya metali. Serikali ya mwisho kati ya serikali hizo inafananishwa na vikanyangio vya sanamu vyenye kutengenezwa na chuma chenye kuchanganywa na udongo. Vile vikanyangio vinafananisha Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika. Unabii huo unaonyesha kama Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika itakuwa ingali inatawala wakati Ufalme wa Mungu utapiga na kuharibu serikali za wanadamu.
12. Kichwa cha saba cha munyama wa pori kinafananisha nini, na juu ya nini ni jambo la maana kujua vile?
12 Mutume Yohana anazungumuzia pia serikali kubwa za ulimwengu zenye zilitawala watu wa Yehova. Katika unabii wa Yohana, serikali hizo zinafananishwa na munyama wa pori mwenye kuwa na vichwa saba. Kichwa cha saba cha ule munyama kinafananisha Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika. Ni jambo la maana kujua vile kwa sababu hakuna vichwa vingine vyenye vinatokea kisha kichwa cha saba. Kichwa cha saba cha munyama huyu kitakuwa kingali kinatawala wakati Kristo na majeshi yake ya mbinguni watakiharibu pamoja na sehemu yenye kubakia ya ule munyama.b—Ufu. 13:1, 2; 17:13, 14.
MUFALME WA KASKAZINI ATAFANYA NINI HIVI KARIBUNI?
13-14. “Gogu wa inchi ya Magogu” ni nani, na pengine ni nini itamuchochea ashambulie watu wa Mungu?
13 Unabii fulani wenye uliandikwa na Ezekieli, unatuambia mambo yenye inaweza kutokea katika siku za mwisho za mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini. Kama unabii wenye kupatikana katika Ezekieli 38:10-23; Danieli 2:43-45; 11:44–12:1; na Ufunuo 16:13-16, 21 unazungumuzia wakati na matukio ileile, basi tunaweza kutazamia mambo hii itokee.
14 Wakati fulani kisha taabu kubwa kuanza, “wafalme wa dunia yote yenye kuikaliwa na watu” watajiunga pamoja ili kufanya muungano wa mataifa. (Ufu. 16:13, 14; 19:19) Biblia inaita muungano huo “Gogu wa inchi ya Magogu.” (Eze. 38:2) Muungano huo wa mataifa utashambulia watu wote wa Mungu kwa mara ya mwisho na utajaribu kuwaharibu kabisa. Ni nini itachochea muungano huo ushambulie watu wa Mungu? Katika unabii fulani kuhusu wakati huo, mutume Yohana alisema kama mvua kubwa ya majiwe yenye haiko ya kawaida itapiga maadui wa Mungu. Mvua hiyo ya majiwe ya mufano inaweza kufananisha ujumbe mukali wa hukumu wenye watu wa Yehova watatangaza. Inawezekana ni ujumbe huo njo utachochea Gogu wa Magogu ashambulie watu wa Mungu ili awaharibu kabisa.—Ufu. 16:21.
15-16. (a) Pengine Danieli 11:44, 45 inazungumuzia matukio gani? (b) Ni nini itapata mufalme wa kaskazini na serikali zingine zenye kufanyiza Gogu wa Magogu?
15 Pengine ujumbe huo mukali na shambulizi hilo la mwisho lenye litafanywa na maadui wa Mungu njo matukio yenye inazungumuziwa mu Danieli 11:44, 45. (Soma.) Katika andiko hilo, Danieli anasema kama “habari kutoka mashariki na kutoka kaskazini” zinasumbua mufalme wa kaskazini, na kwa hiyo, atatoka na iko na “kasirani kali.” Nia ya mufalme wa kaskazini ni “kuangamiza watu wengi.” Inaonekana kama “watu wengi” wenye andiko hilo linataja ni watu wa Yehova.c Pengine katika andiko hilo, Danieli iko anazungumuzia shambulizi la mwisho kabisa juu ya watu wa Mungu.
16 Shambulizi hilo lenye mufalme wa kaskazini atafanya pamoja na serikali zingine za dunia, linamufanya Mweza-Yote akasirike sana na kuleta vita ya Armagedoni. (Ufu. 16:14, 16) Wakati huo, mufalme wa kaskazini ataharibiwa pamoja na mataifa ingine yenye kufanyiza Gogu wa Magogu, na hakuna “mwenye atamusaidia.”—Da. 11:45.
Ku vita ya Armagedoni, Yesu Kristo na majeshi yake ya mbinguni wataharibu ulimwengu muovu wa Shetani na kuokoa watu wa Mungu(Ona fungu la 17)
17. Mikaeli “ule mukubwa” mwenye Danieli 12:1 inazungumuzia ni nani, na anafanya nini?
17 Andiko lenye kufuata katika unabii wa Danieli linatupatia habari zaidi juu ya namna mufalme wa kaskazini na inchi zingine zenye kumuunga mukono zitaharibiwa na namna tutaokolewa. (Soma Danieli 12:1.) Andiko hili maana yake nini? Mikaeli ni jina lingine la Mufalme wetu mwenye kutawala, Kristo Yesu. ‘Amesimama kwa ajili’ ya watu wa Mungu tangu mwaka wa 1914 wakati Ufalme wake ulisimamishwa mbinguni. Hivi karibuni, ‘atasimama,’ ao ataharibu maadui wake, ku vita ya Armagedoni. Ile vita itakuwa tukio la mwisho mu kipindi chenye Danieli anaita “wakati wa taabu” kubwa kabisa katika historia. Unabii wa Yohana katika kitabu cha Ufunuo unaita wakati wenye utatangulia ile vita kuwa “taabu kubwa.”—Ufu. 6:2; 7:14.
JINA LAKO ‘LITAANDIKWA KATIKA KILE KITABU’?
18. Sababu gani tunaweza kupambana bila woga na matukio ya wakati wenye kuja?
18 Tunaweza kupambana bila woga na matukio ya wakati wenye kuja kwa sababu Danieli na Yohana, wote wawili, wanaonyesha kama wale wenye kumutumikia Yehova na Yesu wataokoka kipindi hicho cha taabu kubwa yenye haijatokeaka. Danieli anasema kama majina ya wale wenye wataokoka itakuwa ‘imeandikwa katika kile kitabu.’ (Da. 12:1) Tunaweza kufanya nini ili majina yetu iandikwe katika kile kitabu? Tunapaswa kuonyesha waziwazi kama tuko na imani katika Yesu, Mwana-kondoo wa Mungu. (Yoh. 1:29) Tunapaswa kujitoa kwa Mungu na kubatizwa. (1 Pe. 3:21) Na tunapaswa kutegemeza Ufalme wa Mungu kwa kufanya yote yenye tunaweza ili kusaidia wengine wajifunze juu ya Yehova.
19. Tunapaswa kufanya nini sasa, na juu ya nini?
19 Sasa njo wakati wa kumutegemea Yehova zaidi na tengenezo lake lenye kufanyizwa na watumishi wake waaminifu. Sasa njo wakati wa kutegemeza Ufalme wa Mungu. Kama tunafanya vile, tutaokolewa wakati Ufalme wa Mungu utaharibu mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini.
WIMBO 149 Wimbo wa Ushindi
a Ni nani “mufalme wa kaskazini” leo, na namna gani atafikia mwisho wake ao kuharibiwa? Kujua majibu ya ile maulizo kunaweza kutia nguvu imani yetu na kutusaidia tukuwe tayari kupambana na majaribu yenye itatupata hivi karibuni.
b Ili kupata habari zaidi kuhusu Danieli 2:36-45 na Ufunuo 13:1, 2, ona Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 6, 2012, ukurasa wa 7-19.
c Ili kupata habari zaidi, ona Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 5, 2015, ukurasa wa 29-30.
-
-
Wafalme Wenye Kushindana Katika Wakati wa MwishoMunara wa Mulinzi (Gazeti la Funzo)—2020 | Mwezi wa 5
-
-
Wafalme Wenye Kushindana Katika Wakati wa Mwisho
Unabii fulani wenye kuonyeshwa katika muchoro huu unazungumuzia matukio yenye ilitokea wakati uleule. Unabii huo wote unaonyesha kama tunaishi “wakati wa mwisho.”—Da. 12:4.
Maandiko Ufu. 11:7; 12:13, 17; 13:1-8, 12
Unabii “Munyama wa pori” ametawala dunia kwa maelfu ya miaka. Katika wakati wa mwisho, kichwa chake cha saba kinaumizwa. Kisha, kichwa chake kinapona na “dunia yote” inafuata ule munyama. Shetani anatumia ule munyama ili “kupigana vita na wale wenye kubakia.”
Utimizo Kisha Garika, serikali zenye kumupinga Yehova zinatokea. Kisha miaka mingi, wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, serikali ya Uingereza inakuwa zaifu sana. Inapata nguvu tena wakati inajiunga na Inchi ya Amerika. Zaidi sana wakati wa mwisho, Shetani anatumia serikali zote za dunia ili kutesa watu wa Mungu.
Maandiko Da. 11:25-45
Unabii Mufalme wa kaskazini na mufalme na kusini wanapigania mamlaka wakati wa mwisho.
Utimizo Ujerumani inapigana na Uingereza na Amerika. Mu mwaka wa 1945, Muungano wa Sovieti na inchi zenye kuunga mukono muungano huo zinakuwa mufalme wa kaskazini. Mu mwaka wa 1991, Muungano wa Sovieti unaanguka, na kisha, serikali ya Urusi na inchi zenye kuiunga mukono zinakuwa mufalme wa kaskazini.
Maandiko Isa. 61:1; Mal. 3:1; Lu. 4:18
Unabii Yehova anatuma “mujumbe” wake ili ‘afungue njia’ mbele Ufalme wa Kimasiya usimamishwe. Ule “mujumbe” anaanza ‘kutangazia wapole habari njema.’
Utimizo Kuanzia mwaka wa 1870, Russell na wenzake wanatumika kwa bidii ili kufasiria watu kweli za Biblia. Katika miaka ya 1880, wanaanza kukazia kama watumishi wa Mungu wanapaswa kuhubiri. Wanachapisha habari kama vile “Wahubiri 1 000 Wanahitajiwa” na “Mumetiwa Mafuta ili Kuhubiri.”
Maandiko Mt. 13:24-30, 36-43
Unabii Mutu fulani anapanda ngano mu shamba. Kisha, adui fulani anapanda magugu mu shamba hilo. Magugu inakomaa na kufunika ngano. Wakati wa mavuno, magugu inatenganishwa na ngano.
Utimizo Kuanzia mwaka wa 1870, tofauti kati ya Wakristo wa kweli na Wakristo wa uongo inaanza kuonekana wazi zaidi na zaidi. Katika wakati wa mwisho, Wakristo wa kweli wanakusanywa na kutenganishwa na Wakristo wa uongo.
Maandiko Da. 2:31-33, 41-43
Unabii Vikanyangio vya chuma na udongo vya sanamu ya munyama yenye kutengenezwa na metali mbalimbali.
Utimizo Udongo unafananisha watu wa kawaida, wenye Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika inatawala, wenye wanapinga serikali hiyo. Watu hao wanafanya serikali hiyo ikuwe zaifu na ishindwe kutawala kwa mamlaka yenye kuwa nguvu kama chuma.
Maandiko Mt. 13:30; 24:14, 45; 28:19, 20
Unabii “Ngano” inakusanywa mu “depo” na “mutumwa muaminifu na mwenye busara” anawekwa juu ya “watumishi wa nyumbani.” Kazi ya kuhubiri “habari njema ya Ufalme” inaanza kufanywa katika “dunia yote yenye kuikaliwa na watu.”
Utimizo Mu mwaka wa 1919, mutumwa muaminifu anawekwa ili asimamie watu wa Mungu. Kuanzia wakati huo, Wanafunzi wa Biblia wanahubiri kwa bidii sana. Leo, Mashahidi wa Yehova wanahubiri mu inchi zaidi ya 200 na wanachapisha vichapo vyenye kutegemea Biblia mu luga zaidi ya 1 000.
Maandiko Da. 12:11; Ufu. 13:11, 14, 15
Unabii Munyama wa pori mwenye pembe mbili anaambia watu wafanye “sanamu ya munyama wa pori,” na anapatia “pumuzi ile sanamu.”
Utimizo Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika inaanzisha Ushirika wa Mataifa. Mataifa ingine inaunga mukono ushirika huo. Kisha, mufalme wa kaskazini anajiunga pia na Ushirika wa Mataifa, lakini ni kuanzia tu mwaka wa 1926 mupaka mwaka wa 1933. Watu waliamini kama Ushirika wa Mataifa njo utaleta amani mu dunia, jambo lenye Ufalme wa Mungu tu njo unaweza kufanya. Na wanaamini vile pia kuhusu Umoja wa Mataifa wenye ulianzishwa kisha.
Maandiko Da. 8:23, 24
Unabii Mufalme mwenye kuonekana kuwa mukali analeta “uharibifu kwa njia ya ajabu.”
Utimizo Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika imeua watu wengi na kuleta uharibifu mukubwa. Kwa mufano, wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu, Inchi ya Amerika ilileta uharibifu mukubwa sana kuliko uharibifu wowote wenye ulikuwa umekwisha kutokea wakati iliangusha bombe mbili za atomu juu ya taifa lenye lilikuwa adui wa Uingereza na Amerika.
Maandiko Da. 11:31; Ufu. 17:3, 7-11
Unabii Munyama “mwenye rangi nyekundu yenye kungaa” mwenye kuwa na pembe kumi anatoka mu abiso na yeye njo mufalme wa munane. Kitabu cha Danieli kinaita ule mufalme kuwa “chukizo lenye linaleta uharibifu.”
Utimizo Ushirika wa Mataifa unaacha kufanya kazi wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu. Kisha vita hiyo, Umoja wa Mataifa ‘unasimamishwa’ ao unaundwa. Watu waliamini kama Umoja wa Mataifa njo utaleta amani mu dunia, jambo lenye Ufalme wa Mungu njo unaweza kufanya. Ni vile pia waliamini kuhusu Ushirika wa Mataifa wenye ulikuwa mbele yake. Umoja wa Mataifa utashambulia dini.
Maandiko 1 Te. 5:3; Ufu. 17:16
Unabii Mataifa inatangaza “amani na usalama,” na “zile pembe kumi” na “ule munyama wa pori” wanashambulia “ule kahaba” na kumuharibu. Kisha, mataifa yote inaharibiwa.
Utimizo Mataifa itasema kama imeleta amani na usalama mu dunia. Kisha, mataifa yenye kuunga mukono Umoja wa Mataifa itaharibu matengenezo ya dini za uongo. Tukio hilo litakuwa mwanzo wa taabu kubwa. Ile taabu itamalizika wakati Yesu ataharibu ulimwengu wote wa Shetani ku Armagedoni.
Maandiko Eze. 38:11, 14-17; Mt. 24:31
Unabii Gogu anashambulia inchi ya watu wa Mungu. Kisha, malaika wanakusanya wale “wenye kuchaguliwa.”
Utimizo Mufalme wa kaskazini na serikali zingine za dunia, wanashambulia watu wa Mungu. Wakati fulani kisha shambulizi hilo kuanza, mabaki ya watiwa-mafuta wanapelekwa mbinguni.
Maandiko Eze. 38:18-23; Da. 2:34, 35, 44, 45; Ufu. 6:2; 16:14, 16; 17:14; 19:20
Unabii “Ule mwenye kukaa” juu ya “farasi mweupe” anakamilisha “ushindi wake” kwa kuharibu Gogu na jeshi lake. “Ule munyama wa pori” ‘anatupwa ndani ya ziwa la moto,’ na ile sanamu kubwa inapondwa-pondwa.
Utimizo Yesu, Mufalme mwenye kutawala Ufalme wa Mungu, anakuja kuokoa watu wa Mungu. Yeye na watawala wenzake 144 000 na majeshi yake ya malaika, wanaharibu muungano wa mataifa. Huo utakuwa mwisho wa ulimwengu wa Shetani.
-