WIMBO 4
“Yehova Ni Muchungaji Wangu”
Maandishi
1. Yah ni Muchungaji wangu;
Nitamufwata yeye.
Anaujua moyo wangu;
Na sitakosa kitu.
Ananiongoza kwenye
Nafasi zenye maji.
Ananiongoza kwa upendo
Ili nipumuzike.
Aniongoza kwa upendo
Ili nipumuzike.
2. Njia zako ni za haki,
Ni zenye kupendeza.
Naomba unisaidie
Kuwa muaminifu.
Hata nikuwe mu giza,
Sitaogopa kitu.
Ninajua unanichungaka,
Uko Rafiki yangu.
Najua unanichungaka,
Uko Rafiki yangu.
3. Uko Muchungaji wangu;
Kweli sitakuacha.
Uko nanipatia nguvu
Na unanibariki.
Ninakutumainia,
Uko Mungu wa kweli.
Kwa upendo mushikamanifu
Unanitegemeza.
Upendo mushikamanifu
Unanitegemeza.