Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lv sura 1 uku. 4-13
  • ‘Kumupenda Mungu Kunamaanisha Hivi’

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • ‘Kumupenda Mungu Kunamaanisha Hivi’
  • Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘KUMUPENDA MUNGU KUNAMAANISHA HIVI’
  • ‘KUZISHIKA AMRI ZAKE’
  • ‘AMRI ZAKE SI MUZIGO MUZITO’
  • Upendo wa Mungu Hauna Mwisho
    Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu
  • Baki Katika Upendo wa Mungu
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Saidia Wengine Wawe Wenye ‘Kutii Kutoka Moyoni’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Barua Kutoka kwa Baraza Lenye Kuongoza
    Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu
Ona Habari Zaidi
Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
lv sura 1 uku. 4-13
Jua linatua kwa njia yenye kupendeza sana katika kisiwa na katika habari

Sura ya 1

‘Kumupenda Mungu Kunamaanisha Hivi’

‘Kumupenda Mungu kunamaanisha hivi, kwamba tuzishike amri zake; na bado amri zake si muzigo muzito.’—1 YOHANA 5:3.

1, 2. Ni kitu gani kinakusukuma wewe umupende Yehova Mungu?

WEWE unamupenda Mungu? Ikiwa umekwisha kujitoa kwa Yehova Mungu, utajibu bila kusita, ndiyo! Na una haki ya kujibu hivyo! Inafaa kabisa sisi tumupende Yehova. Kwa sababu anatupenda, hilo linatusukuma kabisa tumupende. Biblia inasema hivi: “Kwa habari yetu, sisi tunaonyesha upendo, kwa sababu [Yehova] alitupenda sisi kwanza.”—1 Yohana 4:19.

2 Yehova ndiye aliyeanza kuonyesha kama anatupenda. Ametupatia dunia ambayo ni mahali pazuri pa kuishi. Anatutimizia mahitaji yetu ya kimwili. (Mathayo 5:43-48) Na zaidi sana, anatutimizia mahitaji yetu ya kiroho. Ametupatia Neno lake, Biblia. Tena, anatuomba tumukaribie katika sala; anatuhakikishia kama atatusikiliza na kutupatia roho yake takatifu ili itusaidie. (Zaburi 65:2; Luka 11:13) Jambo kubwa zaidi ni hili: alimutuma Mwana wake mupendwa sana ili awe zabihu, na kwa hiyo, atukomboe katika zambi na kifo. Hauone kama Yehova ametuonyesha kabisa upendo mukubwa?​—Yohana 3:16; Waroma 5:8.

3. (a) Ni lazima tufanye nini ili kubaki katika upendo wa Mungu? (b) Ni ulizo gani la maana ambalo tunapaswa kujiuliza, na jibu linapatikana wapi?

3 Yehova anataka tuendelee kufaidika na upendo wake milele. Lakini kila mumoja wetu anapaswa kuchagua ikiwa atapenda kuendelea kufaidika na upendo wa Mungu ao hapana. Neno la Mungu linatushauri hivi: Mubaki ‘katika upendo wa Mungu, mukitazamia uzima wa milele.’ (Yuda 21) Andiko hilo linatuonyesha kwamba ni lazima tufanye mambo yanayoonyesha wazi kama tunamupenda Mungu. Kwa hiyo, tunapaswa kujiuliza ulizo hili la maana, “Ninaweza kufanya nini ili nionyeshe kama ninamupenda Mungu?” Jibu la ulizo hilo linapatikana katika maneno ambayo mutume Yohana aliandika kwa uongozi wa roho takatifu: ‘Kumupenda Mungu kunamaanisha hivi, kwamba tuzishike amri zake; na bado amri zake si muzigo muzito.’ (1 Yohana 5:3) Ni lazima tuchunguze vizuri maana ya maneno hayo, kwa sababu tunataka tumuonyeshe Mungu wetu kama tunamupenda sana.

‘KUMUPENDA MUNGU KUNAMAANISHA HIVI’

4, 5. Eleza namna ulivyoanza kumupenda Yehova katika moyo wako.

4 ‘Kumupenda Mungu.’ Mutume Yohana alitaka kusema nini wakati aliandika maneno hayo? Alikuwa akizungumuzia namna kila mumoja wetu anavyojisikia kumuelekea Mungu. Je, unakumbuka wakati ulianza kumupenda Yehova katika moyo wako?

Mwanaume anasali
Mwanaume anaonyesha kama amejitoa kwa Mungu kwa kubatizwa katika maji

Kujitoa kwa Mungu na kubatizwa kunaonyesha mwanzo wa maisha ya kumutii Yehova kwa upendo

5 Kumbuka namna ulivyojisikia ulipojua kwa mara ya kwanza kweli juu ya Yehova na makusudi yake, na namna ulivyoanza kuwa na imani. Ulielewa kama wewe ulizaliwa katika zambi, na kwa hiyo, ulikuwa mbali na Mungu. Lakini, Yehova alikufungulia njia kupitia Kristo ili ufikie ukamilifu ambao Adamu alipoteza na uweze kupata uzima wa milele. (Mathayo 20:28; Waroma 5:12, 18) Polepole ulianza kuelewa kama Yehova alijinyima sana kwa kutuma Mwana wake mupendwa sana ili akufe kwa ajili yako. Ulipoelewa mambo hayo, moyo wako ulifurahi na ukaanza kujisikia kama unamupenda Mungu ambaye amekuonyesha upendo mukubwa kama huo.​—1 Yohana 4:9, 10.

6. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunamupenda kwelikweli mutu fulani, na upendo wako kwa Mungu ulikusukuma kufanya nini?

6 Lakini, namna ulivyojisikia ilikuwa tu ni mwanzo wa upendo wako wa kweli kwa Yehova. Haitoshe kujisikia tu moyoni kama unamupenda Mungu, wala si kwa maneno tu. Mutu anayemupenda Mungu kwelikweli hatasema tu “ninamupenda Yehova.” Imani ya kweli inaonekana kwa matendo, vilevile upendo wa kweli unaonekana kwa matendo. (Yakobo 2:26) Kwa hiyo, tunaonyesha kama tunamupenda mutu fulani kwa kufanya mambo yanayomupendeza. Ndio sababu, wakati ulianza kumupenda Yehova katika moyo wako, ulijisikia kuwa unapenda kuishi kama vile Baba yako wa mbinguni anavyotaka. Wewe ni mwenye kubatizwa? Ikiwa ni hivyo, hilo linaonyesha kama upendo wako mukubwa na uaminifu wako ndio ulikusukuma ufanye uamuzi huo muzuri zaidi katika maisha yako. Ulijitoa kwa Yehova katika sala ili kufanya mapenzi yake, na ulikubali kubatizwa ili kuonyesha kwamba ulijitoa kwake. (Waroma 14:7, 8) Ili uonyeshe kama unatimiza naziri yako kwa Yehova, kuna jambo lingine ambalo mutume Yohana alizungumuzia, ambalo unapaswa kufanya.

‘KUZISHIKA AMRI ZAKE’

7. Taja amri fulani za Mungu, na kushika amri za Mungu kunamaanisha nini?

7 Yohana anaeleza kama kumupenda Mungu ni ‘kuzishika amri zake.’ Unaweza kutaja amri fulani za Mungu? Kupitia Neno lake Biblia, Yehova anatupatia amri fulani zilizo wazi. Kwa mufano, anakataza mambo kama vile kulewa, uasherati, kuabudu sanamu, kuiba na kusema uongo. (1 Wakorintho 5:11; 6:18; 10:14; Waefeso 4:28; Wakolosai 3:9) Kushika amri za Mungu kunamaanisha kuishi kulingana na sheria za mwenendo safi zinazoonyeshwa wazi katika Biblia.

8, 9. Namna gani tunaweza kujua yale yanayomupendeza Yehova hata katika hali ambazo sheria ya Biblia haitajwe waziwazi? Toa mufano.

8 Lakini, ili kumupendeza Yehova haitoshe tu kutii amri zake zinazotajwa waziwazi. Yehova hatuwekee sheria nyingi ili kuongoza kila jambo tunalofanya katika maisha yetu ya kila siku. Ndio sababu, tunaweza kukutana na hali zingine ambazo Biblia haiseme waziwazi kile tunapaswa kufanya. Tukikutana na hali kama hizo, namna gani tunaweza kujua jambo la kufanya ili kumupendeza Yehova? Biblia inaonyesha waziwazi mawazo ya Mungu. Wakati tunajifunza Biblia, tunajua yale ambayo Mungu anataka na yale ambayo anachukia. (Zaburi 97:10; Methali 6:16-19) Tunafikia kutambua mawazo na matendo anayofurahia. Tukiendelea kujifunza sifa za Yehova na namna zake za kutenda, tutaanza pia kuacha mawazo yake yaongoze maamuzi na matendo yetu. Kwa hiyo, hata tukikutana na hali fulani ambayo hakuna sheria ya Biblia inayotajwa waziwazi, mara nyingi tunaweza kujua “yale yaliyo mapenzi ya Yehova.”—Waefeso 5:17.

9 Kwa mufano, hakuna amri ya waziwazi katika Biblia inayokataza kutazama filme ao programe ya televizyo inayoonyesha watu wenye kuuana ao kufanya uasherati. Lakini, je, tuna lazima kabisa ya sheria inayokataza waziwazi kutazama mambo hayo? Tunajua namna Yehova anavyoona mambo hayo. Neno lake linatuambia waziwazi hivi: ‘Mutu yeyote anayependa jeuri nafsi ya Yehova hakika inamuchukia.’ (Zaburi 11:5) Biblia inasema tena hivi: “Mungu atawahukumu waasherati na wazinzi.” (Waebrania 13:4) Tukifikiria sana maneno hayo ya Biblia, tunaweza kujua waziwazi ni jambo gani linamupendeza Yehova. Kwa hiyo, tutakataa kujifurahisha kwa kutazama picha ao mambo yanayoonyesha mazoea ambayo Mungu wetu anachukia. Tunajua vizuri kwamba ili kumufurahisha Yehova tunapaswa kukataa mambo machafu ya kujifurahisha ambayo dunia hii inajaribu kufanya yaonekane kuwa yasiyo na ubaya wowote.a

10, 11. Sababu gani tunafurahia sana kumutii Yehova katika maisha yetu, na utii wetu unapaswa kuwa namna gani?

10 Ni sababu gani ya kwanza kabisa inayotusukuma kushika amri za Mungu? Sababu gani tunataka kuishi kila siku kulingana na mawazo ya Mungu? Hatuchague kufanya hivyo kwa sababu tu ya kuogopa azabu ao malipizi, ao kwa kuepuka tu matokeo mabaya yanayowapata wale wanaopuuza sheria za Mungu. (Wagalatia 6:7) Lakini, ikiwa tunamutii Yehova ni kwa sababu hiyo ndio njia nzuri kabisa ya kumuonyesha kama tunamupenda. Kama vile mutoto anavyotaka baba yake amufurahie na amukubali, sisi pia tunataka Yehova atufurahie na atukubali. (Zaburi 5:12) Yeye ni Baba yetu, na tunamupenda. Jambo linalotufurahisha sana ao kututosheleza zaidi kuliko mambo yote ni kujua kama maisha yetu yanaweza kufanya tukubaliwe na Yehova.—Methali 12:2.

11 Kwa hiyo, hatumutii Mungu kwa kulazimishwa; hatutii tu mambo ambayo yanatupendeza, wala hatumutilie Mungu masharti ili kumutii.b Ni kusema, hatuchague ni amri gani tutatii na ni amri gani tutapuuza, hatutii tu wakati kufanya hivyo ni kwa faida yetu ao wakati si vigumu kufanya hivyo. Lakini ‘tunatii kutoka moyoni.’ (Waroma 6:17) Mawazo yetu ni kama yale ya mutunga-zaburi, aliyeandika hivi: “Nitapendezwa na amri zako ambazo nimezipenda.” (Zaburi 119:47) Ndiyo, tunapenda kabisa kumutii Yehova. Tunatambua kama anastahili jambo hilo na anaomba tumutii kikamili na bila kumutilia masharti. (Kumbukumbu la Torati 12:32) Tunataka Yehova aseme juu yetu yale ambayo Neno lake linasema juu ya Noa. Muzee huyo mwaminifu alionyesha kama anamupenda Mungu kwa kumutii miaka mingi. Kwa hiyo, Biblia inasema hivi: ‘Noa akafanya kulingana na yote ambayo Mungu alikuwa amemuamuru. Alifanya vivyo hivyo.’—Mwanzo 6:22.

12. Ni wakati gani utii wetu unaweza kufurahisha moyo wa Yehova?

12 Yehova anajisikia nanma gani wakati tunamutii kwa kupenda? Neno lake linasema kama wakati tunafanya hivyo, ‘moyo wake unafurahi.’ (Methali 27:11) Je, ni kweli kama wakati tunatii tunafurahisha kabisa moyo wa Bwana, Mutawala wa ulimwengu wote? Ndiyo, na kuna sababu inayomufanya afurahi! Yehova alituumba tukiwa na uhuru wa kuchagua. Ni kusema, tunaweza kuchagua kumutii Mungu ao hapana. (Kumbukumbu la Torati 30:15, 16, 19, 20) Tunapochagua kumutii Yehova bila kulazimishwa na tunapofanya hivyo kwa sababu tunasukumwa na moyo wenye kujaa upendo kwake, utii kama huo unamufanya Baba yetu wa mbinguni awe na furaha nyingi sana na shangwe. (Methali 11:20) Tena, tunapofanya hivyo, tunachagua namna nzuri zaidi ya kuishi.

‘AMRI ZAKE SI MUZIGO MUZITO’

13, 14. Sababu gani tunaweza kusema kama amri za Mungu ‘si muzigo muzito?’ Toa mufano ili kufasiria jambo hilo.

13 Mutume Yohana anatuambia jambo moja lenye kutia moyo kuhusu amri za Yehova. Anasema hivi: ‘Amri zake si muzigo muzito.’c Tafsiri nyingine ya Biblia inasema hivi: “Amri zake si ngumu.” (Habari Njema kwa Watu Wote) Mambo ambayo Yehova anataka tufanye si magumu wala si yenye kutugandamiza. Wanadamu wasio wakamilifu wanaweza kutii sheria zake.

14 Ili kuelewa jambo hilo vizuri, acha tuchukue mufano. Tuseme rafiki yako wa sana anakuomba umusaidie kuhama. Ana mizigo mingi ya kuhamisha. Mizigo mingine haina uzito sana, inaweza kubebwa na mutu mumoja bila magumu, lakini mizigo mingi ni mizito na inaomba kunyanguliwa na kubebwa na watu wawili. Rafiki yako ndiye anayekuchagulia mizigo ambayo utabeba. Unawaza anaweza kukuomba ubebe mizigo ambayo ni mizito sana na anajua kama hautaiweza? Hapana. Hawezi kupenda uteseke kwa kubeba mizigo hiyo mizito peke yako. Vilevile, Mungu wetu mwenye upendo na mwema hatuombe tutii amri zilizo ngumu sana. (Kumbukumbu la Torati 30:11-14) Yeye hawezi hata kidogo kutuomba tubebe muzigo muzito kama huo. Yehova anajua mipaka yetu, kwa sababu “yeye mwenyewe analijua vema umbo letu, akikumbuka kwamba sisi ni mavumbi.”—Zaburi 103:14.

15. Sababu gani tunaweza kuwa hakika kama ikiwa Yehova ametupatia amri zake ni kwa faida yetu?

15 Kwa kweli amri za Yehova si muzigo muzito hata kidogo; ikiwa ametupatia amri hizo ni kwa faida yetu. (Isaya 48:17) Ndio sababu Musa aliwaambia Waisraeli wa zamani hivi: ‘Yehova akatuamuru tushike masharti yote haya, tumuogope Yehova Mungu wetu kwa ajili ya hali njema yetu sikuzote, ili tupate kuendelea kuwa hai kama ilivyo leo hii.’ (Kumbukumbu la Torati 6:24) Sisi pia tunaweza kuwa hakika kama wakati Yehova anatupatia sheria zake, ni kwa faida yetu; anataka tuwe na maisha mazuri milele. Ni hivyo, kwa sababu Yehova ni Mungu mwenye hekima isiyo na mipaka. (Waroma 11:33) Kwa hiyo, anajua mambo ambayo yanatufaa zaidi. Tena, Yehova ni mufano muzuri zaidi wa upendo. (1 Yohana 4:8) Upendo ndio sifa yake kubwa zaidi, na kila jambo analosema ao kufanya ni sababu ya upendo. Amri zote ambazo anapatia watumishi wake zinategemea upendo.

16. Sababu gani inawezekana kubaki watiifu kwa Mungu hata ikiwa ulimwengu huu uliopotoka una uvutano mubaya na pia mwili wetu usiokamilika?

16 Lakini hilo halimaanishe kama ni vyepesi kumutii Mungu. Tunapaswa kupiganisha uvutano wa ulimwengu huu uliopotoka ambao ‘unakaa katika nguvu za yule muovu.’ (1 Yohana 5:19) Tena tunapaswa kupiganisha mwili wetu usiokamilika, ambao unatusukuma kila mara kuvunja sheria za Mungu. (Waroma 7:21-25) Lakini, kwa kuwa tunamupenda Mungu, tunaweza kushinda mambo hayo. Yehova anawabariki wale wanaomutii kwa sababu wanamupenda. Anawapa roho yake takatifu ‘wale wanaomutii yeye akiwa mutawala.’ (Matendo 5:32) Roho hiyo inazaa tunda nzuri sana ndani yetu, ni kusema, sifa nzuri sana zinazoweza kutusaidia tubaki watiifu kwa Mungu.—Wagalatia 5:22, 23.

17, 18. (a) Tutachunguza nini katika kitabu hiki, na tunapofanya hivyo, lazima tukumbuke nini? (b) Sura inayofuata itazungumuzia nini?

17 Katika kitabu hiki, tutachunguza kanuni za Yehova na sheria zake kuhusu mwenendo safi na mambo mengine mengi yanayoonyesha mapenzi yake. Tunapochunguza kanuni hizo, ni lazima tukumbuke mambo haya: Yehova hatulazimishe kutii amri na kanuni zake; anataka tutii kwa moyo wote wenye kuchochewa na upendo. Tusisahau kama Yehova anatuomba tuishi kwa njia ambayo itatuletea faida sana leo na ambayo itatuongoza kwenye uzima wa milele. Basi, acheni tujue kama kutii kwetu kutoka moyoni ni njia nzuri sana ya kumuonyesha Yehova kama tunamupenda kabisa.

18 Kwa upendo Yehova ametupatia zamiri ili itusaidie kutofautisha yaliyo mema na yaliyo mabaya. Lakini, zamiri yetu inapaswa kufundishwa ili ituongoze vizuri. Sura inayofuata itazungumuzia jambo hilo.

a Soma Sura ya 6 ili kujua namna ya kujifurahisha inayofaa.

b Hata mashetani wanaweza kutii kwa kulazimishwa. Wakati Yesu aliwaamuru mashetani wawatoke watu fulani, mashetani hao walilazimika kutambua mamlaka ya Yesu na kumutii hata kama hawakutaka kufanya hivyo.—Marko 1:27; 5:7-13.

c Neno la Kigiriki linalotafsiriwa ‘muzigo muzito’ kwenye 1 Yohana 5:3 linatafsiriwa ‘-enye kugandamiza’ kwenye Matendo 20:29, 30 na linazungumuzia waasi-imani wenye kugandamiza ambao ‘wangesema mambo yaliyopotoka’ ili kuwadanganya watu.

UNAWAZA NAMNA GANI?

  • Yehova anataka watumishi wake wamutii kwa sababu gani, na kwa nini kufanya hivyo ni kwa faida yetu?—Kumbukumbu la Torati 5:28-33.

  • Je, Yehova anaona utii wetu kuwa wa lazima?—1 Samweli 15:22, 23.

  • Yesu aliona namna gani jambo la kumutii Mungu, na mufano wake unaweza kutufundisha nini?—Yohana 8:29.

  • Sababu gani Yehova anastahili utii wetu?—Ufunuo 4:11.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine