- 
	                        
            
            Mashahidi wa Yehova Ni Watu wa Namna Gani?Ni Nani Wanafanya Mapenzi ya Yehova Leo?
 - 
                            
- 
                                        
SOMO LA 1
Mashahidi wa Yehova Ni Watu wa Namna Gani?
Denmaki
Taiwan
Venezuela
India
Unajua Mashahidi wa Yehova ngapi? Pengine wamoja kati yetu ni majirani wako, wafanyakazi wenzako, ao wanafunzi wenzako. Ao pengine tumekwisha kuzungumuza na wewe juu ya Biblia. Kwa kweli, sisi ni nani, na juu ya nini tunazungumuzaka na wengine juu ya mambo yenye tunaamini?
Tuko kama watu wengine. Tunatoka mu desturi mbalimbali, na tuko na hali mbalimbali za maisha. Wamoja kati yetu walikuwa mu dini ingine zamani, na wengine hawakukuwa wanamuamini Mungu. Lakini, mbele ya kuwa Mashahidi, sisi wote tulikamata wakati wa kuchunguza muzuri mafundisho ya Biblia. (Matendo 17:11) Tuliona kama mambo yenye tulijifunza ni ya kweli, na kwa hiyo kila mumoja wetu aliamua yeye mwenyewe kumuabudu Yehova Mungu.
Kujifunza Biblia kunatuletea faida. Sisi pia tuko na magumu na uzaifu kama watu wengine. Lakini, juu tunajikaza kutumia kanuni za Biblia mu maisha yetu ya kila siku, maisha yetu imebadilika na imekuwa muzuri zaidi. (Zaburi 128:1, 2) Ile ni sababu moja kati ya sababu zenye zinatuchochea tuambie wengine juu ya mambo ya muzuri yenye tumejifunza mu Biblia.
Tunafuata kanuni za Mungu mu maisha yetu. Kanuni hizo zenye zinapatikana mu Biblia, zinatusaidia kuwa na hali ya muzuri, kuheshimia watu wengine, na kuonyesha sifa mbalimbali kama vile unyoofu ao uaminifu na wema. Kanuni hizo zinatusaidia ili tukuwe na afya ya muzuri na tukuwe wanainchi wazuri, na zinasaidia familia zetu zikuwe na umoja na mwenendo muzuri. Juu tunaamini kabisa kama “Mungu hana ubaguzi,” tunajiona kuwa familia moja ya ndugu na dada mu dunia yote, hatuna ubaguzi wa rangi ya ngozi, na hatuache mambo ya politike itugawanye. Hata kama tuko kama watu wengine, familia yetu ya ndugu na dada mu dunia yote ni ya pekee.—Matendo 4:13; 10:34, 35.
Juu ya nini Mashahidi wa Yehova wako kama watu wengine?
Mashahidi wamejifunza kanuni gani mu Biblia?
 
 - 
                                        
 
- 
	                        
            
            Juu ya Nini Tunaitwa Mashahidi wa Yehova?Ni Nani Wanafanya Mapenzi ya Yehova Leo?
 - 
                            
- 
                                        
SOMO LA 2
Juu ya Nini Tunaitwa Mashahidi wa Yehova?
Noa
Abrahamu na Sara
Musa
Yesu Kristo
Watu wengi wanawaza kama Mashahidi wa Yehova ni jina la dini ya mupya. Lakini, miaka zaidi ya 2 700 yenye imepita, Mungu wa kweli aliita watumishi wake kuwa “mashahidi” wake. (Isaya 43:10-12) Mbele ya mwaka wa 1931, tulikuwa tunaitwa Wanafunzi wa Biblia. Juu ya nini tulikamata jina Mashahidi wa Yehova?
Jina hilo linaonyesha Mungu wetu ni nani. Jina la Mungu, Yehova, linapatikana mara 7 000 hivi katika maandishi ya zamani ya Biblia. Mu tafsiri za mingi za Biblia wameondoa jina hilo, na nafasi ya jina hilo wametia majina ya cheo ao ya heshima, kama vile Bwana ao Mungu. Lakini Mungu wa kweli yeye mwenyewe njo alimuambia Musa kama jina lake ni Yehova. Alimuambia Musa hivi: “Hilo ndilo jina langu milele.” (Kutoka 3:15) Jina hilo linaonyesha kama iko tofauti na miungu yote ya uongo. Tuko wenye furaha sana juu tunaitwa kwa jina takatifu la Mungu.
Jina hilo linaonyesha kazi yetu. Watu wengi wa zamani, kuanzia Abeli mutu mwenye haki, walimuamini Yehova na walitoa ushahidi juu yake. Noa, Abrahamu, Sara, Musa, Daudi, na wengine walijiunga na “wingu [hilo] kubwa la mashahidi.” (Waebrania 11:4–12:1) Kama vile tu mutu anaweza kutoa ushahidi kwenye tribinali ili kutetea mutu fulani mwenye hana kosa, sisi pia hatutaacha kuelezea wengine kweli juu ya Mungu wetu.
Tunafuata mufano wa Yesu. Biblia inaita Yesu “shahidi muaminifu na wa kweli.” (Ufunuo 3:14) Yesu mwenyewe alisema kama ‘alijulisha jina la Mungu’ na aliendelea ‘kutoa ushahidi juu ya ile kweli’ kuhusu Mungu. (Yohana 17:26; 18:37) Kwa hiyo, wanafunzi wa kweli wa Kristo wanapaswa kuitwa kwa jina la Yehova na kujulisha watu wengine jina hilo. Mashahidi wa Yehova wanajikaza kufanya vile.
Juu ya nini Wanafunzi wa Biblia walikamata jina Mashahidi wa Yehova?
Yehova amekuwa na mashahidi hapa ku dunia kuanzia wakati gani?
Ni nani mwenye kuwa Shahidi mukubwa zaidi wa Yehova?
 
 - 
                                        
 
- 
	                        
            
            Namna Gani Kweli ya Biblia Ilipatikana Tena?Ni Nani Wanafanya Mapenzi ya Yehova Leo?
 - 
                            
- 
                                        
SOMO LA 3
Namna Gani Kweli ya Biblia Ilipatikana Tena?
Wanafunzi wa Biblia, mu miaka ya 1870
Gazeti la kwanza la Munara wa Mulinzi, mwaka wa 1879
Munara wa Mulinzi leo
Biblia ilisema mbele ya wakati kama kisha kifo cha Kristo, walimu wa uongo wangetokea kati ya Wakristo wa kwanza-kwanza na wangepotosha kweli ya Biblia. (Matendo 20:29, 30) Kisha wakati fulani, jambo hilo lilitokea kabisa. Walimu hao wa uongo walichanga mafundisho ya Yesu na mafundisho ya wapagani, na hilo likatokeza Ukristo wa uongo. (2 Timoteo 4:3, 4) Namna gani tunaweza kuwa hakika kama leo tunaelewa muzuri mambo yenye Biblia inafundisha kabisa?
Wakati ulifika ili Yehova afunue kweli. Yehova alitabiri kama katika ‘wakati wa mwisho ujuzi wa kweli ungekuwa mwingi.’ (Danieli 12:4) Mu mwaka wa 1870, kikundi kidogo cha watu wenye walikuwa wanatafuta kweli, walitambua kama mafundisho mingi ya dini haikupatana na Biblia. Kwa hiyo, walianza kujifunza Biblia ili waelewe mafundisho ya kweli ya Biblia, na Yehova aliwasaidia kuelewa maandiko.
Wanaume waaminifu walijifunza Biblia kwa uangalifu. Wanafunzi hao wa Biblia wenye bidii walikuwa wanatumia njia ya kujifunza yenye tunaendelea kutumia mupaka leo. Walikuwa wanajifunza fundisho moja la Biblia, wakati walikuwa wanamaliza fundisho hilo, walikuwa wanakamata fundisho lingine. Wakati ilikuwa nguvu kuelewa andiko fulani la Biblia, walikuwa wanatafuta maandiko ingine yenye kufasiria andiko hilo. Wakati walifikia uamuzi wenye kupatana na Maandiko ya Biblia, waliandika jambo hilo. Kwa kufanya vile, waliacha Biblia ijifasirie yenyewe. Kwa hiyo, walivumbua kweli juu ya jina la Mungu na Ufalme wake, kusudi lake juu ya wanadamu na dunia, hali ya watu wenye wamekufa, na tumaini la ufufuo. Kutafuta kweli mu Biblia kuliwasaidia waachane na mafundisho na desturi za mingi za uongo.—Yohana 8:31, 32.
Kufikia mwaka wa 1879, Wanafunzi hao wa Biblia waliona kama wakati ulikuwa umefika wa kutangazia watu mafundisho ya kweli. Kwa hiyo, mu mwaka huo, walianza kuchapisha gazeti Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova, gazeti hilo linaendelea kuchapishwa mupaka leo. Sasa tunafundisha watu mafundisho ya kweli ya Biblia mu inchi 240 na mu luga zaidi ya 900. Leo ujuzi wa kweli ni mwingi sana kuliko wakati mwingine wowote!
Kisha kifo cha Kristo, kulitokea nini juu ya mafundisho ya kweli ya Biblia?
Ni nini imetusaidia kupata tena ile kweli ya Neno la Mungu?
 
 - 
                                        
 
- 
	                        
            
            Juu ya Nini Tulikuwa na Lazima ya Biblia Tafsiri ya Ulimwengu Mupya?Ni Nani Wanafanya Mapenzi ya Yehova Leo?
 - 
                            
- 
                                        
SOMO LA 4
Juu ya Nini Tulikuwa na Lazima ya Tafsiri ya Ulimwengu Mupya?
Congo (Kinshasa)
Rwanda
Maandishi ya Symmachus (miaka 300 ao 400 hivi kisha kuzaliwa kwa Yesu) yenye kuwa na jina la Mungu katika Zaburi 69:31.
Kwa miaka mingi, Mashahidi wa Yehova walitumia tafsiri mbalimbali za Biblia, walichapisha tafsiri hizo, na walizigawia watu. Lakini tuliona kama, ili kusaidia muzuri watu wapate “ujuzi wenye hauna makosa wa ile kweli,” wenye Mungu anapenda kila mutu apate, iliomba kuwa na tafsiri ya mupya ya Biblia. (1 Timoteo 2:3, 4) Kwa hiyo, mu mwaka wa 1950 tulianza kutoa sehemu za Biblia yetu Tafsiri ya Ulimwengu Mupya yenye kutumia luga ya sasa. Biblia hiyo imetafsiriwa kwa uaminifu na bila makosa mu luga zaidi ya 170.
Tulikuwa na lazima ya tafsiri ya Biblia yenye kuwa mwepesi kuelewa ao kusikia muzuri. Luga zinabadilikaka kisha wakati fulani, na Biblia za mingi ziko na maneno yenye haiko wazi ao ya zamani yenye kuwa nguvu kuelewa. Tena, maandishi ya zamani ya Biblia yenye haina makosa na yenye kukaribia maandishi ya kwanza-kwanza imevumbuliwa. Ile maandishi imesaidia kuelewa muzuri Kiebrania, Kiaramu, na Kigiriki chenye kilitumiwa ili kuandika Biblia.
Tulikuwa na lazima ya tafsiri yenye haibadilishe neno la Mungu. Kuliko kubadilisha maandishi yenye iliongozwa na roho ya Mungu, watafsiri wa Biblia wanapaswa kufuata kwa uaminifu maandishi ya kwanza-kwanza. Lakini, tafsiri za mingi za Biblia hazitumie jina la Mungu, Yehova.
Tulikuwa na lazima ya tafsiri ya Biblia yenye inamutukuza ule mwenye aliandikisha Biblia. (2 Samweli 23:2) Kama vile mufano wenye kuwa hapa chini unaonyesha, mu Tafsiri ya Ulimwengu Mupya, jina Yehova limerudishwa nafasi kwenye lilikuwa mu maandishi ya zamani ya Biblia, ni kusema, mara 7 000 hivi. (Zaburi 83:18) Kwa sababu wale wenye walitafsiri Biblia hiyo walitafuta habari kwa bidii na kwa miaka mingi, mutu anasikiaka furaha wakati iko anaisoma juu inaonyesha waziwazi mawazo ya Mungu. Ikuwe uko na Tafsiri ya Ulimwengu Mupya mu luga yako ao hapana, tunakutia moyo kusoma Neno la Yehova kila siku.—Yoshua 1:8; Zaburi 1:2, 3.
Juu ya nini tulikuwa na lazima ya tafsiri ya mupya ya Biblia?
Kila mutu mwenye anapenda kujua mapenzi ya Mungu anapaswa kufanya nini kila siku?
 
 -