Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • jy sura 64 uku. 152-uku. 153 fu. 2
  • Ni Jambo la Lazima Kusamehe

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ni Jambo la Lazima Kusamehe
  • Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Ni Nani kwa Kweli Mutumwa Mwaminifu na Mwenye Busara?’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Tuwe Tayari Kusameheana
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Mutumwa Muaminifu na Mwenye Busara Ni Nani?
    Ni Nani Wanafanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Musikwaze “Hawa Wadogo”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
jy sura 64 uku. 152-uku. 153 fu. 2
Mutumwa anamukamata mutumwa mwenzake na kumubana shingo

SURA YA 64

Ni Jambo La Lazima Kusamehe

MATAYO 18:21-35

  • INAOMBA KUSAMEHE MARA SABA?

  • MUFANO WA MUTUMWA MWENYE HANA HURUMA

Petro amesikia mashauri ya Yesu kuhusu namna ya kumaliza magumu kati ya ndugu; ndugu wawili wanapaswa kujikaza kumaliza magumu yao wao wawili tu. Hata hivyo, inaonekana Petro anapenda kujua ni mara ngapi mutu anapaswa kujikaza kusamehe.

Petro anauliza hivi: “Bwana, kama ndugu yangu ananitendea zambi, ninapaswa kumusamehe mara ngapi? Mupaka mara saba (7)?” Viongozi fulani wa dini wanafundisha kama mutu anaweza kusamehe mupaka mara tatu. Kwa hiyo, inawezekana Petro anaona kuwa mutu atakuwa amesamehe sana ikiwa amesamehe ndugu yake “mupaka mara saba (7).”—Matayo 18:21.

Lakini, wazo la kuhesabia makosa yenye mutu fulani amekufanyia halipatane na jambo lenye Yesu anafundisha. Kwa hiyo anamurekebisha Petro kwa kusema hivi: “Ninakuambia, hapana mupaka mara saba (7), lakini mupaka mara makumi saba na saba (77).” (Matayo 18:22) Kwa maneno mengine, hilo linamaanisha kusamehe bila mipaka. Petro hapaswe kujiwekea mipaka juu ya mara yenye anaweza kusamehe ndugu yake.

Mufalme anasamehe deni la mutumwa

Kisha Yesu anatoa mufano ili kusaidia Petro na wengine waelewe muzuri kuwa wanapswa kusamehe. Ni mufano wa mutumwa fulani mwenye anashindwa kuiga bwana wake mwenye huruma. Mufalme huyo anataka watumwa wake wamulipe madeni yao. Wanamuletea mutumwa mumoja mwenye kuwa na deni kubwa ya talanta 10 000 [dinari 60 000 000]. Hana namna ya kulipa deni hiyo. Kwa hiyo mufalme anaamuru kuwa mutumwa huyo, bibi yake, na watoto wake wauzishwe ili kulipa deni hiyo. Wakati mutumwa huyo anasikia hivyo, anapiga magoti na kuinama chini kwenye miguu ya bwana wake, na kumuomba hivi: “Univumilie, nitakulipa kila kitu.”—Matayo 18:26.

Mutumwa anafungisha mutumwa mwenzake katika gereza

Mufalme huyo anamusikilia huruma, na kwa huruma anafuta deni hiyo kubwa yenye mutumwa alikuwa nayo. Kisha tu mufalme kufanya hivyo, mutumwa huyo anaenda na kukuta mutumwa mwenzake mwenye iko na deni lake la dinari 100. Anamukamata mutumwa mwenzake, anamubana shingo na kusema hivi: “Lipa deni lako lote.” Lakini mutumwa huyo mwenzake anapiga magoti mbele yake na kumuomba hivi: “Univumilie, nitakulipa.” (Matayo 18:28, 29) Hata hivyo, mutumwa huyo mwenye alisamehewa deni na mufalme anakosa kufuata mufano wa bwana wake. Anafungisha katika gereza mutumwa mwenzake mwenye kuwa na deni kidogo sana, mupaka amulipe deni lenye iko nalo.

Mufalme anafungisha mutumwa mwenye hana huruma katika gereza

Kisha Yesu anasema kuwa watumwa wengine wenye wanaona tendo hilo lenye kukosa huruma wanamuelezea bwana wao, na bwana huyo anakasirika, anamuita mutumwa huyo na kumuambia hivi: “Mutumwa muovu, nilifuta lile deni lako lote wakati uliniomba. Je, wewe pia haungemusikilia mutumwa mwenzako huruma kama vile nilikusikilia huruma?” Mufalme huyo mwenye kukasirika anafungisha mutumwa huyo katika gereza mupaka alipe deni lake lote. Yesu anamalizia hivi: “Ni vile pia Baba yangu wa mbinguni atawatendea ninyi kama kila mumoja wenu hamusamehe ndugu yake kutoka moyoni.”—Matayo 18:32-35.

Kwa kweli, hilo ni jambo lenye tunapaswa kujifunza kuhusu kusamehe! Mungu ametusamehe deni kubwa ya zambi. Hata kama ndugu Mukristo anatutendea kosa gani, ni la kidogo sana wakati linalinganishwa na deni hiyo ya zambi. Na Yehova anatusamehe, hapana mara moja tu, lakini mara maelfu. Je, hamuone kama tunapaswa kusamehe ndugu zetu mara nyingi, hata kama tuko na sababu ya kulalamika? Kama vile Yesu alifundisha katika Mahubiri ya Mulimani, Mungu ‘atatusamehe madeni yetu, kama vile sisi pia tumesamehe wenye kuwa na madeni yetu.’—Matayo 6:12.

  • Ni nini inamuchochea Petro aulize juu ya kusamehe ndugu yake, na sababu gani anaweza kuona kuwa mutu atakuwa amesamehe sana ikiwa anasamehe mupaka mara saba?

  • Kuko tofauti gani kati ya namna mufalme anatenda wakati mutumwa wake anamuomba huruma na namna mutumwa huyo anatendea mutumwa mwenzake?

  • Mufano wa Yesu unatufundisha nini?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine