Wazazi
Ni sababu gani zenye zilifanyaka Yehova aanzishe ndoa?
Namna gani wazazi wanapaswa kuona watoto wao?
Ona pia “Watoto; Vijana”
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Mwa 33:4, 5—Yakobo anaona kama watoto wake ni baraka kutoka kwa Yehova
Kut 1:15, 16, 22; 2:1-4; 6:20—Amramu na Yokebedi wanazala Musa na wanatia uzima wao mu hatari juu ya kumulinda
Wazazi wanapaswa kufanyia nini watoto wao?
Kum 6:6, 7; 11:18, 19; Mez 22:6; 2Ko 12:14; 1Ti 5:8
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
1Sa 1:1-4—Elkana anapeleka familia yake Shilo kwa ajili ya sikukuu, na anakamata mipango juu kila mutoto aweze kutoa zabihu
Lu 2:39, 41—Kama kawaida, Yosefu na Maria wanasafiri na watoto wao kutoka Nazareti kuenda Yerusalemu kwa ajili ya sikukuu ya Pasaka
Kuzoeza watoto mu njia za Yehova kunaletaka faida gani?
Ona pia 2Ti 3:14, 15
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
1Sa 2:18-21, 26; 3:19—Wazazi wa Samweli wanatoa mutoto wao juu atumike ku tabenakulo, lakini wanamutembelea kila mara na wanamusaidia kutimiza mahitaji yake; wakati Samweli anakomala anakuwa mutu wa kiroho na anamutumikia Yehova kwa uaminifu
Lu 2:51, 52—Yesu anaendelea kutii wazazi wake hata kama hawakamilike
Wazazi wanaweza kupata wapi muongozo juu ya kukomalisha watoto wao?
Kum 6:4-9; Efe 6:4; 2Ti 3:14-17
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Amu 13:2-8—Kisha kuambiwa kama bibi yake atazala mutoto, Manoa anaomba maagizo juu ya namna ya kukomalisha ule mutoto
Zb 78:3-8—Yehova anapenda wazazi wafundishe watoto wao mambo yenye wamejifunza mu Biblia
Hata kama mutoto anakomalia mu familia yenye kumupenda Mungu, nini njo inaweza kufanya afikie kumuacha Yehova?
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Mwa 6:1-5; Yud 6—Hata kama walipitisha miaka mingi sana pamoya na Yehova mbinguni, malaika wengi waliamua kumuasi
1Sa 8:1-3—Hata kama Samweli ni nabii muaminifu na mwenye haki, watoto wake wanafikia kuwa wadanganyifu na wenye kupotoka
Wazazi wanapaswa kuanza kufundisha watoto wao njia za Mungu wakati gani?
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Kum 29:10-12, 29; 31:12; Ezr 10:1—Wakati watu wanakutana ili kujifunza juu ya Yehova, watoto pia wako pale
Lu 2:41-52—Kama kawaida, Yosefu na Maria wanapeleka watoto wao, kutia ndani Yesu, ku karamu ya Pasaka ku hekalu ya Yerusalemu
Ni mifano gani inaweza kusaidia wazazi walinde watoto wao juu wengine wasiwatendee mubaya?
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Kut 19:4; Kum 32:11, 12—Yehova anajilinganisha na tai, mwenye anabebaka, kulinda, na kuhangaikia vitoto vyake
Isa 49:15—Yehova anaahidi kama atahangaikia na kulinda watumishi wake kwa huruma, kupita hata vile mama anahangaikiaka mutoto wake
Mt 2:1-16—Shetani anajaribu kumuua mutoto Yesu kwa kuongoza watu wenye elimu ya nyota waende kwa mufalme muovu Herode, lakini Yehova anamulinda mwana wake kwa kumuongoza Yosefu na familia yake waende Misri
Mt 23:37—Yesu anafananisha nia yake ya kusaidia watu wake na namna kuku anakusanyaka vitoto vyake chini ya mabawa
Juu ya nini wazazi wanapaswa kufundisha watoto wao kuhusu mambo ya ngono?
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Law 15:2, 3, 16, 18, 19; Kum 31:10-13—Sheria ya Musa inasema mambo waziwazi juu ya ngono, na Yehova anaomba watoto wakuwe pale wakati ile sheria inasomwa
Zb 139:13-16—Daudi, muandikaji wa zaburi, anamusifu Yehova juu ya namna aliumbaka mwili wa mwanadamu na namna alipatiaka wanadamu uwezo wa kuzala watoto
Mez 2:10-15—Ujuzi na hekima kutoka kwa Yehova vinaweza kutulinda juu watu wenye kupotoka wasitutendee mubaya
Juu ya nini wazazi wanapaswa kutolea watoto wao nizamu kwa upendo?
Mez 13:24; 29:17; Yer 30:11; Efe 6:4
Ona pia Zb 25:8; 145:9; Kol 3:21
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Zb 32:1-5—Hata kama Daudi anaona kuwa nizamu ya Yehova inamulemea, kujua kama Yehova anakuwaka anasamehe wenye wanatubu kikweli kunamutuliza
Yon 4:1-11—Nabii Yona iko naongea na Yehova kwa kasirani na bila heshima; hata vile, Yehova anamufundisha rehema kwa uvumilivu
Juu ya nini tunaweza kusema kama kupatia mutoto nizamu ni kumupenda?
Ona pia Mez 15:32; Ufu 3:19