Familia
Yehova njo alianzishaka familia
Wazazi
Ona “Wazazi”
Baba
Ona “Baba”
Mama
Ona “Mama”
Bwana, Bibi
Ona “Ndoa”
Watoto
Watoto wako na daraka gani mu familia?
Juu ya nini watoto wanapaswa kutii wazazi wao?
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Zb 78:1-8—Waisraeli wanaelezea watoto wao matendo ya mababu zao juu watoto wamutumainie Yehova na wasimuasi
Lu 2:51, 52—Hata kama Yesu ni mukamilifu, wakati iko kijana anaendelea kutii wazazi wake wenye hawakamilike
Juu ya nini pengine inakuwaka nguvu kwa watoto kuheshimia wazazi wao?
Mungu anaonaka namna gani watoto wenye kuasi?
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Kum 21:18-21—Sheria ya Musa inaamuru kuua mutoto mwenye anakuwa kichwa-nguvu, muasi, na mulevi, lakini mwenye anakatala kurekebishwa
2Fa 2:23, 24—Wakati kikundi ya vijana wanamukosea heshima nabii Elisha, mwenye alimuwakilisha Mungu, wengi wanauawa na dubu wawili
Namna gani wazazi wanapaswa kuona pendeleo ya kukomalisha watoto?
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Law 26:9—Kwa waisraeli, kuzala watoto ni baraka ya Yehova
Yob 42:12, 13—Juu Yobu alionyesha uaminifu-mushikamanifu, Yehova anamubariki yeye na bibi yake kwa kuwapatia watoto wengine kumi
Namna gani watoto mu familia wanapaswa kutendeana mu njia yenye itamufurahisha Yehova?
Habari ya Biblia yenye inaweza kusaidia:
Mwa 27:41; 33:1-11—Yakobo anafanya yote yenye anaweza juu ya kumuonyesha Esau heshima na juu ya kufanya amani; Esau naye anamutendea kwa upendo
Watoto wenye walishakomala, wako na daraka gani kuelekea wazazi wao na watate (ao wakambo) wao?
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Mwa 11:31, 32—Wakati anatoka Uru, Abrahamu anaenda na baba yake, Tera, na anamuhangaikia mupaka wakati ule baba yake anakufa
Mt 15:3-6—Kupitia Sheria ya Musa Yesu anaonyesha kama watoto wenye kukomala wanapaswa kusaidia wazazi wenye wako mu uhitaji
Wakwe
Ona “Wakwe”
Watate
Ona “Watate”