Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w13 1/10 uku. 5
  • Mungu Anafanya Mipango ili Kukomboa Wanadamu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mungu Anafanya Mipango ili Kukomboa Wanadamu
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Walimngoja Masihi
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 1/10 uku. 5
[Picha katika ukurasa wa 5]

KICHWA | BIBLIA INAZUNGUMUZIA HABARI GANI?

Mungu Anafanya Mipango ili Kukomboa Wanadamu

Mungu alimuahidi Abrahamu, mwanaume mwaminifu, kwamba “uzao” ulioahidiwa angekuwa mumoja kati ya wazao wake. Kupitia mutu huyo, watu wa “mataifa yote” wangepata baraka. (Mwanzo 22:18) Kisha Yakobo, mujukuu wa Abrahamu, alihamia Misri, ambako familia yake iliongezeka sana na kuwa taifa la zamani la Israeli.

[Picha katika ukurasa wa 5]

Baadaye, huko Misri, Farao mukali sana aliwafanya Waisraeli kuwa watumwa mupaka Mungu alipotokeza nabii Musa, ambaye aliongoza taifa hilo inje ya inchi ya Misri kwa kugawanya kimuujiza maji ya Bahari Nyekundu. Kisha hapo, Mungu aliwapatia Waisraeli sheria, kutia ndani Amri Kumi, ili kuwaongoza na kuwalinda. Sheria hizo zilionyesha umaana wa kutoa matoleo ili kupata musamaha wa zambi. Akiongozwa na roho ya Mungu, Musa aliwaambia Waisraeli kwamba Mungu angewatumia nabii mwengine. Nabii huyo angekuwa ndio “uzao” ulioahidiwa.

Zaidi ya miaka 400 baadaye, Mungu alimuahidi Mufalme Daudi kwamba yule anayekuja, “uzao” uliotabiriwa katika Edeni, angekuwa mutawala wa ufalme ambao ungedumu milele. Mutu huyo angekuwa ndiye Masiya, Mukombozi aliyewekwa na Mungu ili kuokoa wanadamu na kurudisha Paradiso duniani.

Kupitia Daudi na manabii wengine, Mungu alifunua polepole habari nyingi kuhusu Masiya huyo. Daudi na manabii hao walitabiri kwamba Masiya angekuwa munyenyekevu na mwema na kwamba chini ya utawala wake mambo kama vile njaa, ukosefu wa haki, na vita, yangeisha. Wanadamu wote wangekuwa na amani kati yao na hata pamoja na wanyama. Mambo kama vile magonjwa, kuteseka, na kifo, ambayo hayakuwa katika kusudi la Mungu la mwanzoni, yangeisha, na watu waliokufa watafufuliwa na kuishi tena duniani.

Kupitia nabii Mika, Mungu alitabiri kwamba Masiya angezaliwa huko Bethlehemu na pia kupitia nabii Danieli, Mungu alitabiri kwamba Masiya angeuawa baadaye. Lakini Mungu angemufufua Masiya kutoka kwa wafu na kumufanya kuwa Mufalme huko mbinguni. Pia Danieli aliona mbele ya wakati kwamba mwishowe Ufalme wa Masiya ungechukua milele nafasi ya serikali zingine zote. Je, kweli Masiya alikuja kama ilivyotabiriwa?

​—Habari hii inategemea Mwanzo sura ya 22-50, na pia Kutoka, Kumbukumbu la Torati, 2 Samweli, Zaburi, Isaya, Danieli, Mika, Zekaria 9:9.

JINA TAKATIFU LA MUNGU

Katika Biblia jina Yehova linaonekana kwa mara ya kwanza katika andiko la Mwanzo 2:4. Jina hilo la pekee linapatikana mara 7 000 hivi katika maandishi ya luga ya kwanza ya Maandiko Matakatifu. Maana ya jina hilo, “Yeye Anafanya Kuwa,” inatuhakikishia kwamba Mungu anaweza kabisa kutimiza mambo yote anayokusudia na anayoahidi.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine