Guvernema Zinaweza Kumaliza Vita?
Batu banapiganaka juu ya sababu za mingi. Bamoya banapigana juu ya mambo ya politike, juu ya matatizo ya makuta, ao juu ya haki yabo. Bengine banapigana juu ya kuongeza mipaka ya inchi yabo na kupata utajiri yenye kuwa mu inchi ingine. Bamingi banapigana juu ni batu ya kabila tofauti ao juu biko mu madini tofauti. Ni mambo gani njo guvernema ziko nafanya juu ya kumaliza vita na kuleta amani? Bataweza kabisa kumaliza vita?
Drazen_/E+ via Getty Images
GUVERNEMA ZINAJIKAZA KULETA MABADILIKO KUHUSU MATATIZO YA KUPATA MAKUTA
Kusudi: Kusaidia batu bakuwe na maisha ya muzuri. Ile mabadiliko inaweza kufanya hali ya maisha ya batu ikuwe sawasawa, juu kama hali haiko vile, batu batapigana tu.
Mipaka: Inaomba guvernema zibadilishe namna ya kutumia makuta. Mu 2022, inasemekana kama makuta 34,1 miliare ya dolare, ilitumiwa juu ya kufanya maisha ya batu ikuwe muzuri mu maeneo ya mingi. Lakini, ile ni makuta kidogo sana kwa kuilinganisha na makuta yenye ilitumiwa mu mambo ya vita.
“Tunatumiaka makuta mingi juu ya kusaidia benye biko mu vita kuliko kuitumia juu ya kuzuia vita na kulinda amani.”—António Guterres, mwandishi mukubwa wa Umoja wa Mataifa.
Mambo yenye Biblia inasema: Guvernema na matengenezo ya mu dunia zinaweza kusaidia bamaskini, lakini haziwezi kabisa kumaliza bumaskini.–Kumbukumbu la Torati 15:11; Matayo 26:11.
GUVERNEMA ZINAJIKAZA KUFANYA MAPATANO JUU YA KUFANYA AMANI
Kusudi: Kuzuia ao kumaliza mabishano kwa amani kupitia muzungumuzo ya kufanya mapatano yenye italetea faida ngambo yote mbili.
Mipaka: Ngambo moya ao ngambo yote mbili inaweza kukatala kufanya mapatano ao kukosa kukubaliana. Na ile inaweza kufanya mapatano ya amani isikuwe.
“Mapatano ya amani haikuwake tu kila mara na matokeo ya muzuri. Mapatano yenye ngambo mbili inafanya inaweza kupitikana mubaya, na ile inaweza kuleta tena vita kule mbele.”—Raymond F. Smith, wa Mambo ya Mapatano ya Amerika.
Mambo yenye Biblia inasema: Watu wanapaswa ‘kutafuta amani.’ (Zaburi 34:14) Lakini, leo watu wengi ‘hawana ushikamanifu, . . . hawataki makubaliano yoyote, . . . na ni wasaliti.’ (2 Timoteo 3:1-4) Tabia za vile zinafanyaka viongozi wa politike washindwe kumaliza vita.
GUVERNEMA ZINAJIKAZA KUACHANA NA SILAHA AO KUIPUNGUZA
Kusudi: Kupunguza ao kuacha kutumia silaha (armes), zaidi sana silaha za nyuklia (nucléaires), za kemikali (chimiques), na za kibiolojia (biologiques).
Mipaka: Mara mingi mainchi inakatalaka kuacha kutumia silaha juu inaogopaka kama haitakuwa tena na nguvu ao uwezo wa kujitetea. Hata kama banaacha kutumikisha zile silaha zote, habawezi kumaliza sababu zenye zinafanyaka batu bapigane.
“Guvernema za mingi zenye ziliahidi kuachana na silaha ao kupunguza kuzitumia kisha mwaka wa 1991, hazikutenda kulingana na vile zilisema. Ilikuwa pia vile kuhusu, mipango yenye balikamata juu ya kupunguza mambo yenye kuhatarisha na kupunguza mikokotano yenye kuwa mu dunia yote, mambo yenye ingefanya mu dunia mukuwe amani na usalama.” —Dokima “Assurer notre avenir commun : Un programme pour le désarmement.”
Mambo yenye Biblia inasema: Batu banapaswa kuacha silaha zao na ‘kufua panga zao kuwa majembe.’ (Isaya 2:4) Lakini juu ya kumaliza vita, kuko mambo mingi yenye inaomba kufanya, juu matendo ya jeuri inaanziaka njo mu moyo ya mutu.—Matayo 15:19.
GUVERNEMA ZINAUNGANA JUU YA KUZUIA VITA
Kusudi: Guvernema zinaungana juu ya kusaidiana wakati maadui wanawashambulia. Banawaza kama maadui habataanzisha vita juu bakifanya vile, batakuwa njo napigana na zile guvernema zote zenye kuungana.
Mipaka: Hata kama inchi fulani inaweza kuogopa kupigana na mainchi yenye kuungana, ile haiwezi kuzuia vita. Mainchi ya mingi haitendake kila mara kulingana na mambo yenye ilisema ao kulingana na vile ilikubaliana juu ya namna na wakati ya kutenda saa maadui wanawashambulia.
“Hata kama Shirika ya Mataifa na Umoja wa Mataifa zimejikaza kusaidia guvernema ziungane, ile haisaidie tu kuzuia vita.”—Kitabu “Encyclopedia Britannica.”
Mambo yenye Biblia inasema: Kusema kweli, inakuwaka tu muzuri wakati batu mingi banatumika pamoya. (Muhubiri 4:12) Lakini, guvernema na matengenezo yenye kuwa mu dunia, haziwezi kabisa kuleta amani na usalama. “Msiwategemee wakuu wa dunia; hao ni binadamu tu, hawawezi kuokoa. Binadamu akitoa pumzi yake ya mwisho, anarudi mavumbini alimotoka; na hapo mipango yake yote hutoweka.”—Zaburi 146:3, 4, Biblia Habari Njema.
Hata kama guvernema mingi zimejikaza sana juu ya kuleta amani, mavita inaendelea tu.