Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp25 na. 1 uku. 6-8
  • Guvernema Zinaweza Kumaliza Vita?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Guvernema Zinaweza Kumaliza Vita?
  • Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • GUVERNEMA ZINAJIKAZA KULETA MABADILIKO KUHUSU MATATIZO YA KUPATA MAKUTA
  • GUVERNEMA ZINAJIKAZA KUFANYA MAPATANO JUU YA KUFANYA AMANI
  • GUVERNEMA ZINAJIKAZA KUACHANA NA SILAHA AO KUIPUNGUZA
  • GUVERNEMA ZINAUNGANA JUU YA KUZUIA VITA
  • Juu ya Nini Wanadamu Wanashindwa Kuleta Amani?​—Biblia Inasema Nini?
    Habari Zingine
  • Vita Itaisha Wakati Gani?​—Biblia Inasema Nini?
    Habari Zingine
  • Namna Vita Itamalizika
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2025
Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2025
wp25 na. 1 uku. 6-8

Guvernema Zinaweza Kumaliza Vita?

Batu banapiganaka juu ya sababu za mingi. Bamoya banapigana juu ya mambo ya politike, juu ya matatizo ya makuta, ao juu ya haki yabo. Bengine banapigana juu ya kuongeza mipaka ya inchi yabo na kupata utajiri yenye kuwa mu inchi ingine. Bamingi banapigana juu ni batu ya kabila tofauti ao juu biko mu madini tofauti. Ni mambo gani njo guvernema ziko nafanya juu ya kumaliza vita na kuleta amani? Bataweza kabisa kumaliza vita?

Ku kipande ya picha kwenye kuko bafanyakazi benye biko najenga nyumba na biko naongelea juu ya ile kazi.

Drazen_/E+ via Getty Images

GUVERNEMA ZINAJIKAZA KULETA MABADILIKO KUHUSU MATATIZO YA KUPATA MAKUTA

Kusudi: Kusaidia batu bakuwe na maisha ya muzuri. Ile mabadiliko inaweza kufanya hali ya maisha ya batu ikuwe sawasawa, juu kama hali haiko vile, batu batapigana tu.

Mipaka: Inaomba guvernema zibadilishe namna ya kutumia makuta. Mu 2022, inasemekana kama makuta 34,1 miliare ya dolare, ilitumiwa juu ya kufanya maisha ya batu ikuwe muzuri mu maeneo ya mingi. Lakini, ile ni makuta kidogo sana kwa kuilinganisha na makuta yenye ilitumiwa mu mambo ya vita.

“Tunatumiaka makuta mingi juu ya kusaidia benye biko mu vita kuliko kuitumia juu ya kuzuia vita na kulinda amani.”—António Guterres, mwandishi mukubwa wa Umoja wa Mataifa.

Mambo yenye Biblia inasema: Guvernema na matengenezo ya mu dunia zinaweza kusaidia bamaskini, lakini haziwezi kabisa kumaliza bumaskini.–Kumbukumbu la Torati 15:11; Matayo 26:11.

Ku kipande ya picha kwenye kuko mikono mbili ya batu yenye kusalimiana kisha kufanya mapatano.

GUVERNEMA ZINAJIKAZA KUFANYA MAPATANO JUU YA KUFANYA AMANI

Kusudi: Kuzuia ao kumaliza mabishano kwa amani kupitia muzungumuzo ya kufanya mapatano yenye italetea faida ngambo yote mbili.

Mipaka: Ngambo moya ao ngambo yote mbili inaweza kukatala kufanya mapatano ao kukosa kukubaliana. Na ile inaweza kufanya mapatano ya amani isikuwe.

“Mapatano ya amani haikuwake tu kila mara na matokeo ya muzuri. Mapatano yenye ngambo mbili inafanya inaweza kupitikana mubaya, na ile inaweza kuleta tena vita kule mbele.”—Raymond F. Smith, wa Mambo ya Mapatano ya Amerika.

Mambo yenye Biblia inasema: Watu wanapaswa ‘kutafuta amani.’ (Zaburi 34:14) Lakini, leo watu wengi ‘hawana ushikamanifu, . . . hawataki makubaliano yoyote, . . . na ni wasaliti.’ (2 Timoteo 3:1-4) Tabia za vile zinafanyaka viongozi wa politike washindwe kumaliza vita.

Ku kipande ya picha kwenye kuko bipande ya bunduki yenye kuvunjika.

GUVERNEMA ZINAJIKAZA KUACHANA NA SILAHA AO KUIPUNGUZA

Kusudi: Kupunguza ao kuacha kutumia silaha (armes), zaidi sana silaha za nyuklia (nucléaires), za kemikali (chimiques), na za kibiolojia (biologiques).

Mipaka: Mara mingi mainchi inakatalaka kuacha kutumia silaha juu inaogopaka kama haitakuwa tena na nguvu ao uwezo wa kujitetea. Hata kama banaacha kutumikisha zile silaha zote, habawezi kumaliza sababu zenye zinafanyaka batu bapigane.

“Guvernema za mingi zenye ziliahidi kuachana na silaha ao kupunguza kuzitumia kisha mwaka wa 1991, hazikutenda kulingana na vile zilisema. Ilikuwa pia vile kuhusu, mipango yenye balikamata juu ya kupunguza mambo yenye kuhatarisha na kupunguza mikokotano yenye kuwa mu dunia yote, mambo yenye ingefanya mu dunia mukuwe amani na usalama.” —Dokima “Assurer notre avenir commun : Un programme pour le désarmement.”

Mambo yenye Biblia inasema: Batu banapaswa kuacha silaha zao na ‘kufua panga zao kuwa majembe.’ (Isaya 2:4) Lakini juu ya kumaliza vita, kuko mambo mingi yenye inaomba kufanya, juu matendo ya jeuri inaanziaka njo mu moyo ya mutu.—Matayo 15:19.

Bipande ya mapicha kwenye kuko bakubwa ya guvernema benye kuikala ku meza na banaizunguka. Bote banatia sinyatire ku dokima ya kufanana.

GUVERNEMA ZINAUNGANA JUU YA KUZUIA VITA

Kusudi: Guvernema zinaungana juu ya kusaidiana wakati maadui wanawashambulia. Banawaza kama maadui habataanzisha vita juu bakifanya vile, batakuwa njo napigana na zile guvernema zote zenye kuungana.

Mipaka: Hata kama inchi fulani inaweza kuogopa kupigana na mainchi yenye kuungana, ile haiwezi kuzuia vita. Mainchi ya mingi haitendake kila mara kulingana na mambo yenye ilisema ao kulingana na vile ilikubaliana juu ya namna na wakati ya kutenda saa maadui wanawashambulia.

“Hata kama Shirika ya Mataifa na Umoja wa Mataifa zimejikaza kusaidia guvernema ziungane, ile haisaidie tu kuzuia vita.”—Kitabu “Encyclopedia Britannica.”

Mambo yenye Biblia inasema: Kusema kweli, inakuwaka tu muzuri wakati batu mingi banatumika pamoya. (Muhubiri 4:12) Lakini, guvernema na matengenezo yenye kuwa mu dunia, haziwezi kabisa kuleta amani na usalama. “Msiwategemee wakuu wa dunia; hao ni binadamu tu, hawawezi kuokoa. Binadamu akitoa pumzi yake ya mwisho, anarudi mavumbini alimotoka; na hapo mipango yake yote hutoweka.”—Zaburi 146:3, 4, Biblia Habari Njema.

Hata kama guvernema mingi zimejikaza sana juu ya kuleta amani, mavita inaendelea tu.

Mu dunia munaendelea kuwa amani?

Kuko batu benye banasema kama mu dunia munaendelea kuwa amani kupita zamani. Banasema kama mavita ya hii masiku haikawie tu sana na haiue batu mingi saa zamani. Lakini bengine habakubaliane na ile, na banawaza kama inaomba kufikiria mambo mingi hapana tu kufikiria hesabu ya benye banakufaka ku vita.

Hata batu baseme nini, ukweli ni kama vita inagusaka batu mingi mu dunia leo, na mu njia moya ao ingine, inatugusaka siye bote.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine