Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ijwbq habari 32
  • Je, Biblia Inaweza Kunisaidia Ninapovunjika Moyo?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je, Biblia Inaweza Kunisaidia Ninapovunjika Moyo?
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jibu la Biblia
  • Mungu anawasaidia namna gani wenye kuvunjika moyo?
  • Kushuka Moyo Kushuka Moyo
    Amuka!—2013
  • Vijana Wanashuka Moyo—Sababu Gani? Ni Nini Inaweza Kuwasaidia?
    Amuka!—2017
Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
ijwbq habari 32

Je, Biblia Inaweza Kunisaidia Ninapovunjika Moyo?

Jibu la Biblia

Ndiyo, kwa sababu musaada muzuri zaidi unatoka kwa “Mungu mwenye kufariji wenye huzuni.”​—2 Wakorintho 7:6, La Sainte Bible en swahili de la R.D. Congo.

Mungu anawasaidia namna gani wenye kuvunjika moyo?

  • Anawatolea Nguvu. Mungu ‘anawafariji’ ao kuwatuliza. Hilo halimaanishe kwamba anaondoa matatizo yao yote, lakini anajibu sala ya wale wanaomuomba kwa kuwapatia nguvu ya kuvumilia. (Wafilipi 4:13) Unaweza kuwa hakika kwamba iko tayari kukusikiliza, kwa sababu Biblia inasema hivi: ‘Yehova yuko karibu na wale waliovunjika moyo; naye anawaokoa wale waliopondwa roho.’ (Zaburi 34:18) Kwa hiyo, Mungu anasikia unapomuomba musaada hata ikiwa unakosa maneno ya kutumia ili kueleza namna unavyojisikia.​—Waroma 8:26, 27.

  • Anawatolea mifano mizuri. Muandikaji mumoja wa Biblia alisali hivi: “Toka shimoni, nakulilia, ee Bwana.” Alipokuwa mwenye kuvunjika moyo, mutunga-zaburi alifarijiwa alipokumbuka kwamba Mungu iko tayari kutusamehe makosa yetu. Kwa hiyo, alimuambia Mungu hivi: “Ukikumbuka zambi, nani atasimama? Lakini kwako kuna maondoleo (musamaha) ili wakutumikie kwa heshima.”​—Zaburi 130:1, 3, 4, Verbum Bible.

  • Anawatolea Tumaini. Zaidi ya kuwafariji watu sasa, Mungu anaahidi kwamba ataondoa matatizo yote yanayowafanya watu wavunjike moyo. Atakapotimiza ahadi hiyo, “mambo ya zamani [kutia ndani huzuni na kuvunjika moyo] hayatakumbukwa akilini, wala hayataingia moyoni.”​—Isaya 65:17.

Usisahau jambo hili: Hata ikiwa wanaamini kwamba Mungu anaweza kuwasaidia, Mashahidi wa Yehova wanatafuta matunzo ya kiganga ikiwa wanagonjwa. (Marko 2:17) Hata hivyo, sisi Mashahidi wa Yehova hatutie watu moyo kufuata matunzo fulani, tunajua kwamba kila mutu anapaswa kufanya uamuzi wake kuhusu jambo hilo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine