Wimbo wa Sulemani
2 “Mimi ni ua la zafarani tu la mwambao wa pwani,
Yungiyungi la mabondeni.”+
2 “Kama yungiyungi katikati ya miiba
Ndivyo alivyo mpenzi wangu kati ya mabinti.”
3 “Kama mtofaa kati ya miti ya msituni,
Ndivyo alivyo mpenzi wangu miongoni mwa wana.
Natamani sana kukaa katika kivuli chake,
Na tunda lake ni tamu kinywani mwangu.
4 Alinileta katika nyumba ya karamu,*
Na bendera aliyoweka juu yangu ilikuwa upendo.
6 Amenishika shingoni kwa mkono wake wa kushoto,
Na mkono wake wa kulia unanikumbatia.+
7 Nawaapisha, enyi mabinti wa Yerusalemu,
Kwa swala+ na paa jike wa porini:
Msijaribu kuamsha au kuchochea upendo ndani yangu mpaka utakapoamka wenyewe.+
8 Sauti ya mpenzi wangu!
Tazama! Ndiye yule anakuja,
Akipanda milima, akirukaruka juu ya vilima.
9 Mpenzi wangu ni kama swala, kama paa dume mchanga.+
Yule pale, amesimama nyuma ya ukuta wetu,
Akichungulia madirishani,
Akitazama kupitia viunzi vya madirisha.
10 Mpenzi wangu anaongea, ananiambia:
‘Inuka, mpenzi wangu,
Mrembo wangu, njoo twende zetu.
11 Angalia, majira ya baridi* yamepita.
Mvua zimekwisha na kwenda zake.
12 Maua yamechanua nchini,+
Wakati wa kupunguza matawi umefika,+
Na wimbo wa njiwa tetere unasikiwa katika nchi yetu.+
13 Mtini unaivisha tini zake za mapema;+
Mizabibu inachanua na kunukia manukato.
Inuka, mpenzi wangu, njoo.
Mrembo wangu, njoo twende zetu.
14 Ewe njiwa wangu, kwenye mapango ya miamba,+
Kwenye mashimo ya mlimani,
Acha nikuone na kusikia sauti yako,+
Kwa maana sauti yako inavutia na umbo lako linapendeza.’”+
15 “Tukamatieni mbweha,
Mbweha wadogo wanaoharibu mashamba ya mizabibu,
Kwa maana mashamba yetu ya mizabibu yamechanua.”
16 “Mpenzi wangu ni wangu mimi, na mimi ni wake.+