Wimbo wa Sulemani
7 “Miguu yako inapendeza kwelikweli katika viatu vyako,
Ewe binti unayeheshimika!
Umbo la mapaja yako ni kama mapambo,
Kazi ya mikono ya fundi.
2 Kitovu chako ni bakuli la mviringo.
Kisikose kamwe divai iliyotiwa vikolezo.
Tumbo lako ni rundo la ngano,
Lililozungukwa na mayungiyungi.
3 Matiti yako mawili ni kama paa wawili wachanga,
Mapacha wa paa.+
4 Shingo yako+ ni kama mnara wa pembe ya tembo.+
Pua yako ni kama mnara wa Lebanoni,
Unaoelekea Damasko.
5 Kichwa chako kinakuvika taji kama Karmeli,+
Mfalme ameduwazwa* na nywele zako ndefu.
6 Wewe ni mrembo kwelikweli, nawe unapendeza sana,
Ewe msichana mpendwa, unazidi vyote vinavyopendeza!
7 Kimo chako ni kama cha mtende,
Na matiti yako ni kama vishada vya tende.+
8 Nilisema, ‘Nitapanda juu ya mtende
Nishike vitawi vyake vyenye tende.’
Matiti yako na yawe kama vishada vya mizabibu,
Na pumzi yako inanukia kama matofaa,
9 Na kinywa chako* kama divai bora kabisa.”
“Na ishuke taratibu kwa ajili ya mpenzi wangu,
Itiririke taratibu juu ya midomo ya mpenzi wangu.*
10 Mimi ni wa mpenzi wangu,+
Naye ananitamani.
12 Tuamke mapema twende kwenye mashamba ya mizabibu
Tuone ikiwa mzabibu umechipuka,
Ikiwa maua yamechanua,+
Ikiwa mikomamanga imechanua.+
Huko nitakuonyesha upendo wangu.+
Mapya na pia ya zamani,
Ewe mpenzi wangu, nimekuhifadhia.