-
Kutoka 8:21, 22Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
21 Lakini usipowaruhusu watu wangu waende zao, nitakuletea nzi,* wewe, watumishi wako, na watu wako, nao wataingia katika nyumba zako; na nyumba za Misri zitajaa nzi hao, nao wataifunika hata ardhi ambayo Wamisri wamesimama juu yake. 22 Siku hiyo, hakika nitaitenga nchi ya Gosheni, wanakoishi watu wangu. Hakuna nzi yeyote atakayepatikana huko,+ na kwa jambo hilo utajua kwamba mimi, Yehova, niko humu nchini.+
-
-
Kutoka 9:6Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
6 Na kesho yake Yehova akafanya hivyo, kila aina ya mifugo ya Wamisri ikaanza kufa,+ lakini hakuna mnyama hata mmoja wa Waisraeli aliyekufa.
-
-
Kutoka 9:26Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
26 Ila tu mvua hiyo ya mawe haikunyesha katika nchi ya Gosheni, ambako Waisraeli waliishi.+
-
-
Kutoka 12:13Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
13 Ile damu itakuwa ishara inayoonyesha nyumba mtakazokuwamo; nami nitaiona damu hiyo na kupita juu yenu, na pigo halitawajia na kuwaangamiza ninyi nitakapoipiga nchi ya Misri.+
-