-
Hesabu 29:12Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
12 “‘Na siku ya 15 ya mwezi wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu. Hampaswi kufanya kazi yoyote ngumu, nanyi mnapaswa kumfanyia Yehova sherehe kwa siku saba.+
-
-
Nehemia 8:14-18Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
14 Kisha wakaona imeandikwa katika Sheria kwamba Yehova alikuwa ameamuru kupitia Musa kwamba Waisraeli wanapaswa kukaa katika vibanda* wakati wa sherehe, mwezi wa saba,+ 15 na kwamba wanapaswa kutangaza+ katika majiji yao yote na kotekote Yerusalemu wakisema: “Nendeni katika eneo lenye milima mlete matawi ya mizeituni, ya misonobari, ya mihadasi na ya mitende, na matawi ya miti mingine yenye majani mengi ili mjenge vibanda, kama ilivyoandikwa.”
16 Basi watu wakaenda kuleta matawi hayo ili kujijengea vibanda, kila mtu juu ya paa lake, na pia katika nyua zao, na katika nyua za nyumba ya Mungu wa kweli,+ na katika uwanja wa jiji wa Lango la Maji,+ na katika uwanja wa jiji wa Lango la Efraimu.+ 17 Basi watu wote wa kutaniko waliokuwa wamerudi kutoka utekwani wakajenga vibanda nao wakakaa katika vibanda hivyo, kwa maana Waisraeli hawakuwa wamefanya hivyo tangu siku za Yoshua+ mwana wa Nuni mpaka siku hiyo, basi wakashangilia sana.+ 18 Na siku baada ya siku kitabu cha Sheria ya Mungu wa kweli kilikuwa kikisomwa,+ tangu siku ya kwanza hadi siku ya mwisho. Nao wakafanya sherehe hiyo kwa siku saba, na siku ya nane walifanya kusanyiko takatifu, kama ilivyoagizwa.+
-
-
Yohana 7:2Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
2 Hata hivyo, Sherehe ya Vibanda ya Wayahudi,+ ilikuwa imekaribia.
-