-
Mambo ya Walawi 7:1Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
7 “‘Hii ndiyo sheria kuhusu dhabihu ya hatia:+ Ni dhabihu takatifu kabisa.
-
-
Mambo ya Walawi 14:2Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
2 “Hii ndiyo sheria inayomhusu mtu mwenye ukoma ambayo inapaswa kufuatwa siku ambayo utakaso wake unathibitishwa, anapopelekwa kwa kuhani.+
-
-
Mambo ya Walawi 19:20, 21Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
20 “‘Mwanamume akifanya ngono na kijakazi anayechumbiwa na mwanamume mwingine, na iwe kwamba kijakazi huyo hajakombolewa wala kuwekwa huru, wanapaswa kuadhibiwa. Hata hivyo, hawapaswi kuuawa, kwa sababu kijakazi huyo hakuwa amewekwa huru. 21 Mwanamume huyo anapaswa kumletea Yehova dhabihu yake ya hatia kwenye mlango wa hema la mkutano, kondoo dume wa dhabihu ya hatia.+
-
-
Hesabu 6:12Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
12 Ni lazima ajitenge tena kwa ajili ya Yehova na kuanza upya siku za Unadhiri wake, naye ataleta mwanakondoo dume wa mwaka mmoja kuwa dhabihu ya hatia. Hata hivyo, zile siku za awali hazitahesabiwa kwa sababu aliuchafua Unadhiri wake.
-