-
Waamuzi 2:17Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
17 Lakini walikataa kuwasikiliza hata waamuzi hao, nao walifanya ukahaba na miungu mingine na kuiinamia. Waliacha haraka njia ambayo mababu zao walifuata, ambao walitii amri za Yehova.+ Walikataa kutii.
-
-
Zaburi 106:37-39Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
37 Waliwatoa dhabihu wana wao
Na mabinti wao kwa roho waovu.+
38 Waliendelea kumwaga damu isiyo na hatia,+
Damu ya wana wao na mabinti wao wenyewe
Ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani;+
Na nchi ikachafuliwa kwa umwagaji wa damu.
39 Wakawa wachafu kwa sababu ya kazi zao;
Walifanya ukahaba wa kiroho kwa matendo yao.+
-