-
Hesabu 14:28Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
28 Waambie, ‘“Kwa hakika kama ninavyoishi,” asema Yehova, “nitawatendea mambo yaleyale niliyosikia mkisema!+
-
-
Hesabu 14:35Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
35 “‘“Mimi, Yehova, nimesema. Hivi ndivyo nitakavyoutendea umati huu wa watu waovu, ambao umekusanyika pamoja dhidi yangu: Wataishia humu nyikani, naam, watafia humu.+
-
-
Hesabu 32:10-12Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
10 Yehova aliwaka hasira siku hiyo na kuapa hivi:+ 11 ‘Wanaume waliotoka Misri wenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi hawataiona nchi+ ambayo niliapa kwamba nitampa Abrahamu, Isaka, na Yakobo,+ kwa sababu hawakunifuata kwa moyo wote— 12 isipokuwa Kalebu+ mwana wa Yefune, Mkenizi, na Yoshua+ mwana wa Nuni, kwa sababu wamenifuata mimi Yehova kwa moyo wote.’+
-
-
Kumbukumbu la Torati 2:14Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
14 Tulitembea kwa miaka 38 kutoka Kadesh-barnea mpaka tulipovuka Bonde la Zeredi, mpaka kizazi chote cha wanaume wa vita kilipoangamia kutoka kambini, kama Yehova alivyokuwa amewaapia.+
-
-
Zaburi 95:11Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
11 Kwa hiyo niliapa kwa hasira yangu:
“Hawataingia katika pumziko langu.”+
-
-
Waebrania 3:11Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
11 Kwa hiyo niliapa kwa hasira yangu: ‘Hawataingia katika pumziko langu.’”+
-