-
1 Samweli 18:6-8Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
6 Daudi na watu wengine walipokuwa wakirudi baada ya kuwaua Wafilisti, wanawake walikuwa wakitoka katika majiji yote ya Israeli wakiimba+ na kucheza dansi ili kumpokea Mfalme Sauli kwa matari,+ kwa vigelegele, na udi. 7 Wanawake hao waliokuwa wakisherehekea walikuwa wakiimba hivi:
“Sauli ameua maelfu yake,
Na Daudi makumi yake ya maelfu.”+
8 Sauli akakasirika sana,+ na wimbo huo haukumpendeza kwa kuwa alisema: “Wamempa Daudi makumi ya maelfu, lakini mimi wamenipa maelfu. Lililobaki tu ni kumpa ufalme!”+
-
-
1 Samweli 29:4, 5Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
4 Lakini wakuu wa Wafilisti wakamkasirikia vikali Akishi na kumwambia: “Mrudishe mtu huyu.+ Acha arudi mahali ulipompa. Usimruhusu ashuke kwenda pamoja nasi vitani, asije akatugeuka na kutushambulia wakati wa vita.+ Kuna njia gani bora ya mtu huyu kupata kibali cha bwana wake isipokuwa kumpelekea vichwa vya wanaume wetu? 5 Je, huyu si Daudi waliyeimba kumhusu walipocheza dansi, wakisema:
‘Sauli ameua maelfu yake,
Na Daudi makumi yake ya maelfu’?”+
-