-
1 Samweli 2:14-16Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
14 naye aliutia kwa nguvu ndani ya beseni, chungu cha kupikia chenye mikono miwili, sufuria kubwa, au chungu cha kupikia chenye mkono mmoja. Nyama yoyote iliyoinuliwa na uma huo, ilichukuliwa na kuhani. Hivyo ndivyo walivyokuwa wakiwatendea Waisraeli wote waliokuja Shilo. 15 Pia, hata kabla ya mtu anayetoa dhabihu kuyafanya mafuta yafuke moshi,+ mtumishi wa kuhani alikuwa akija na kumwambia, “Mpe kuhani nyama akachome. Hatachukua nyama iliyochemshwa kutoka kwako, atachukua nyama mbichi tu.” 16 Mtu huyo alipomwambia, “Acha kwanza wahakikishe kwamba mafuta yamefuka moshi,+ kisha ujichukulie chochote upendacho,”* alisema: “Hapana, nipe sasa hivi; la sivyo, nitaichukua kwa nguvu!”
-